< 1 Samweli 25 >

1 Basi Samweli akafa, nao Israeli wote wakakusanyika na kumwombolezea; wakamzika nyumbani kwake huko Rama. Kisha Daudi akateremka kwenye Jangwa la Maoni.
Et Samuel mourut; et tout Israël se rassembla pour pleurer sur lui, et on l'inhuma dans la ville d'Armathem. Cependant David s'en retourna au désert de Maon.
2 Mtu mmoja huko Maoni, aliyekuwa na makao huko Karmeli, alikuwa tajiri sana. Alikuwa na mbuzi elfu moja na kondoo elfu tatu, aliokuwa akiwakata manyoya huko Karmeli.
Il y avait alors en Maon un homme d'une très grande taille, et ses troupeaux étaient sur le mont Carmel; il possédait trois mille brebis et mille chèvres; or, il était à tondre ses brebis sur le Carmel.
3 Jina la mtu huyo lilikuwa Nabali, naye mkewe aliitwa Abigaili. Alikuwa mwanamke mwenye busara na mzuri wa sura, lakini mumewe, ambaye alikuwa wa ukoo wa Kalebu, alikuwa mwenye hasira na mchoyo katika utendaji wake.
L'homme s'appelait Nabal, et sa femme Abigaïl, femme excellente par l'intelligence, et très belle de visage; mais l'homme était dur, méchant dans ses habitudes; c'était un homme grossier.
4 Daudi alipokuwa huko jangwani, akasikia kuwa Nabali alikuwa anakata kondoo manyoya.
David apprit dans le désert que Nabal, du Carmel, tondait ses brebis.
5 Basi akatuma vijana kumi na kuwaambia, “Pandeni kwa Nabali huko Karmeli, mkamsalimie kwa jina langu.
Et il envoya dix jeunes serviteurs, leur disant: Montez sur le Carmel, allez trouver Nabal et saluez-le en mon nom.
6 Mwambieni: ‘Amani iwe kwako! Amani iwe kwako pamoja na wa nyumbani mwako! Pia amani iwe pamoja na vyote ulivyo navyo!
Voici ce que vous lui direz: Bonne santé à toi pour toujours, prospérité à ta maison et à tout ce que tu possèdes.
7 “‘Nasikia kuwa huu ni wakati wa kukata kondoo manyoya. Wachunga mifugo wako walipokuwa pamoja nasi, hatukuwatendea mabaya na wakati wote waliokuwa huko Karmeli hakuna chochote chao kilipotea.
Or, voici que je viens d'apprendre que tes bergers faisaient la tonte; ce sont ceux qui étaient avec nous dans le désert; nous ne leur avons jamais fait obstacle. Nous n'avons rien exigé d'eux, aussi longtemps qu'ils ont demeuré sur le Carmel.
8 Waulize watumishi wako nao watakuambia. Kwa hiyo uwatendee wema vijana wangu, kwani tumekuja wakati wa furaha. Tafadhali wape watumishi wako na mwanao Daudi chochote kitakachokuja mkononi mwako kwa ajili yao.’”
Interroge tes serviteurs, et ils te le déclareront; pour nous, tes serviteurs aussi, puissions-nous trouver grâce à tes yeux, car nous sommes venus en un jour heureux. Donne donc à ton fils David quelque chose que tu aies sous la main.
9 Watu wa Daudi walipofika wakampa Nabali ujumbe huu kwa jina la Daudi. Kisha wakangojea.
Les serviteurs partent; ils répètent à Nabal, au nom de David, toutes les paroles que celui-ci leur a dites. Mais Nabal fit un bond en arrière,
10 Nabali akawajibu watumishi wa Daudi, “Huyu Daudi ni nani? Huyu mwana wa Yese ni nani? Watumishi wengi wanakimbia kutoka kwa bwana zao siku hizi.
Et répondant aux serviteurs de David, il dit: Qu'est-ce que David? Qu'est-ce que le fils de Jessé? Le monde est plein aujourd'hui de serviteurs qui s'échappent de la maison de leur maître.
11 Kwa nini nichukue mkate wangu, maji yangu na nyama niliyochinja kwa ajili ya wakata manyoya wangu, na kuwapa watu ambao hakuna anayejua wanakotoka?”
Oui, je vais prendre mon pain, mon vin, les victimes que j'ai sacrifiées pour mes tondeurs, et je vais les donner à des hommes qui viennent je ne sais d'où!
12 Watu wa Daudi wakageuka na kurudi. Walipofika, wakaarifu kila neno.
Les serviteurs reprirent donc le chemin par lequel ils étaient venus, et ils arrivèrent, et ils rapportèrent cette réponse à David.
13 Daudi akawaambia watu wake, “Jifungeni panga zenu!” Basi wakajifunga panga zao, naye Daudi akajifunga upanga wake. Watu kama mia nne hivi wakapanda pamoja na Daudi, na watu mia mbili wakabaki na vifaa.
Alors, David dit à ses gens: Que chacun de vous ceigne son épée. Et environ quatre cents hommes s'en allèrent avec David; il en resta deux cents auprès des bagages.
14 Mmoja wa watumishi akamwambia Abigaili, mkewe Nabali: “Daudi alituma wajumbe kutoka jangwani kumpa bwana wetu salamu zake, lakini akawavurumishia matukano.
Et l'un des serviteurs de Nabal parla à sa femme Abigaïl, disant: Voilà que David a envoyé du désert des messagers pour bénir notre maître, et il leur a tourné le dos.
15 Hata hivyo watu hawa walikuwa wema sana kwetu. Hawakututendea mabaya, na wakati wote tulipokuwa nje huko mashambani karibu nao, hatukupotewa na kitu chochote.
Ce sont des hommes très bienveillants pour nous; ils ne nous ont point fait obstacle, ils n'ont rien exigé de nous, durant tout le temps que nous avons passé près d'eux.
16 Usiku na mchana walikuwa ukuta wakituzunguka wakati wote tulipokuwa tukichunga kondoo zetu karibu nao.
Et, tandis que nous étions aux champs, ils étaient pour nous comme un retranchement, nuit et jour, durant tout le temps que nous avons été près d'eux paissant nos troupeaux.
17 Sasa fikiri juu ya jambo hili na uone unaweza kufanya nini, kwa sababu maafa yanakaribia juu ya bwana wetu na nyumba yake yote. Yeye ni mtu mwovu kiasi kwamba hakuna mtu awezaye kuzungumza naye.”
Et maintenant réfléchis, vois ce que tu as à faire; car le malheur fond sur notre maître et sa maison; lui-même est un fils de pestilence, et il n'y a pas à lui parler.
18 Abigaili akafanya haraka, akachukua mikate mia mbili, viriba viwili vya divai, kondoo watano waliochinjwa vipimo vitano vya bisi, vishada mia moja vya zabibu kavu, mikate mia mbili ya tini, akavipakia juu ya punda.
Et Abigaïl se hâta; elle prit deux cents pains, deux vases pleins de vin, cinq brebis apprêtées, cinq éphi de fleur de farine, un gomor de raisins secs, deux cents cabas de figues, et elle les chargea sur des ânes.
19 Kisha akawaambia watumishi wake, “Tangulieni; mimi nitakuja nyuma yenu.” Lakini hakumwambia Nabali mumewe.
Puis, elle dit à ses serviteurs: Partez devant moi; voilà que je vous suis. Mais elle ne dit rien à son mari.
20 Ikawa alipokuwa amepanda punda wake kwenye bonde la mlima, tazama, Daudi na watu wake wakawa wanateremka kumwelekea, naye akakutana nao.
Or, tandis qu'elle cheminait sur son ânesse et qu'elle descendait cachée par les plis de la montagne, David et ses gens montaient par le même chemin, de sorte qu'elle les rencontra.
21 Daudi alikuwa amesema, “Ilikuwa ni kazi bure kuchunga kwangu kote mali za huyu mtu huko jangwani hivi kwamba hakuna chochote chake kilichopotea. Yeye amenilipa baya kwa ajili ya wema.
Et David disait: J'ai gardé équitablement dans le désert un homme injuste et tout ce qui lui appartenait, je n'ai jamais ordonné qu'on lui en prît la moindre chose, et il m'a rendu le mal pour le bien.
22 Bwana na amshughulikie Daudi, tena kwa ukali, ikiwa kesho asubuhi nitambakizia mwanaume hata mmoja aliye hai miongoni mwa watu wake wote!”
Que le Seigneur punisse David et le punisse encore, si de tout ce qui est à Nabal je laisse jusqu'à demain matin quelque chose en vie, ne fût-ce qu'un chien.
23 Abigaili alipomwona Daudi, akashuka haraka kwenye punda wake, akainama kifudifudi uso wake mpaka nchi mbele ya Daudi.
Et Abigaïl vit David; aussitôt, elle sauta de son ânesse, elle tomba devant David la face contre terre, et resta prosternée
24 Akamwangukia miguuni pake na kusema: “Bwana wangu, kosa hili na liwe juu yangu mwenyewe. Tafadhali mruhusu mtumishi wako aseme nawe. Sikia kile mtumishi wako atakachosema.
A ses pieds, disant: Ne fais retomber sur moi que ma propre iniquité, seigneur; que ta servante te parle; écoute les paroles de ta servante;
25 Bwana wangu na asimjali huyo mtu mwovu Nabali. Yeye anafanana na jina lake; jina lake ni Mpumbavu, nao upumbavu huenda pamoja naye. Lakini kwangu mimi, mtumishi wako, sikuwaona hao watu waliotumwa na bwana wangu.
Que mon seigneur ne fasse pas attention à cet homme de pestilence; car il est bien ce que son nom indique; il se nomme Nabal (fou), et la folie est avec lui. Mais moi, ta servante, je n'ai point vu les serviteurs de mon seigneur, que tu avais envoyés.
26 “Basi sasa, kwa kuwa Bwana amekuzuia, wewe bwana wangu, kutokumwaga damu na kutolipiza kisasi kwa mikono yako mwenyewe, hakika kama Bwana aishivyo na kama uishivyo, maadui zako na wote wanaokusudia kumdhuru bwana wangu wawe kama Nabali.
Maintenant, mon seigneur, vive le Seigneur et vive ton âme! D'autant plus que ton Seigneur t'a empêché de verser le sang innocent et de te venger par ta main. Puissent ressembler à Nabal tes ennemis et ceux qui veulent nuire à mon seigneur.
27 Nayo zawadi hii ambayo mtumishi wako amemletea bwana wangu, wapewe watu wanaofuatana nawe.
Accepte donc cette bénédiction que ta servante a apportée à mon seigneur; tu la distribueras aux serviteurs qui accompagnent mon seigneur.
28 Tafadhali samehe kosa la mtumishi wako, kwa kuwa Bwana kwa hakika ataifanya imara nyumba ya ufalme kwa bwana wangu, kwa sababu anapigana vita vya Bwana.
Détourne de ta servante la peine de l'iniquité, car le Seigneur, pour mon seigneur, édifiera certainement une maison sûre; le Seigneur combat pour mon seigneur en toutes ses batailles, et jamais le malheur ne se trouvera avec toi.
29 Hata ingawa yuko mtu anayekufuatia kuuondoa uhai wako, usiruhusu baya lolote kuonekana kwako siku zote za maisha yako, uhai wa bwana wangu utafungwa salama kwenye furushi la walio hai na Bwana Mungu wako. Lakini uhai wa adui zako atavurumishwa kama vile jiwe kutoka kwenye kombeo.
Et si un homme s'élève qui te poursuive, et en veuille à ta vie, l'âme de mon seigneur sera maintenue dans les liens de la vie par la volonté du Seigneur Dieu, et tu feras tournoyer la vie de tes adversaires, comme au milieu d'une fronde.
30 Bwana atakapokuwa ameshamtendea bwana wangu kila kitu chema alichoahidi kumhusu yeye na kumweka kuwa kiongozi wa Israeli,
Et lorsque le Seigneur aura fait à mon seigneur tout le bien qu'il lui a promis, il te donnera la mission de régner sur Israël.
31 bwana wangu hatakuwa na dhamiri inayolemewa na mzigo kwa kumwaga damu kusiko na sababu, au kujilipizia kisasi yeye mwenyewe. Bwana atakapomletea bwana wangu mafanikio, umkumbuke mtumishi wako.”
Et mon seigneur n'aura point commis le péché et l'abomination de verser, sans cause, le sang innocent ni de se venger par sa main; et le Seigneur sera bienveillant pour mon seigneur; et tu te souviendras de ta servante, tu seras bienveillant pour elle.
32 Daudi akamwambia Abigaili, “Ahimidiwe Bwana, Mungu wa Israeli aliyekutuma kunilaki leo.
Et David dit à Abigaïl: Béni soit le Seigneur Dieu d'Israël, qui t'a envoyée aujourd'hui au-devant de moi.
33 Ubarikiwe kwa uamuzi wako mzuri na kwa kunizuia nisimwage damu leo na kulipiza kisasi kwa mikono yangu.
Bénie sois ta résolution; bénie sois-tu toi-même, qui m'as empêché aujourd'hui de verser le sang innocent et de me venger par ma main.
34 La sivyo, hakika kama Bwana, Mungu wa Israeli, aishivyo, ambaye amenizuia nisiwadhuru, kama usingekuja haraka kunilaki, hakuna hata mwanaume mmoja wa Nabali angeachwa hai kufikia mapambazuko.”
Mais, vive le Seigneur Dieu; vivant d'Israël, qui m'empêche aujourd'hui de te maltraiter! sans ton empressement à venir à ma rencontre, j'avais dit: de ne laisserai rien en vie chez Nabal jusqu'à demain matin.
35 Ndipo Daudi akapokea kutoka mkononi mwake kile alichokuwa amemletea, naye akasema, “Nenda nyumbani kwako kwa amani; nimesikia maneno yako na kukujalia ombi lako.”
David prit de ses mains tout ce qu'elle lui avait apporté, et il lui dit: Retourne en paix à ta demeure. Vois, je t'ai accordé ce que tu m'as demandé, et je me suis réjoui de ta présence.
36 Abigaili alipokwenda kwa Nabali, alikuwa ndani ya nyumba yake akifanya karamu kama ile ya mfalme. Naye alikuwa ana furaha nyingi, akiwa amelewa sana. Kwa hiyo Abigaili hakumwambia mumewe kitu chochote mpaka asubuhi yake.
Abigaïl rentra donc chez Nabal, et il y avait en sa maison un festin comme un festin de roi; Nabal montrait la joie de son cœur; il était complètement ivre. Jusqu'aux lueurs du matin, sa femme ne lui dit aucune chose, grande ni petite.
37 Basi asubuhi, Nabali alipokuwa amelevuka, mkewe akamwambia mambo yote, nao moyo wake ukazimia, akawa kama jiwe.
Le jour parut; comme Nabal avait cuvé son vin, elle lui raconta tout; aussitôt le cœur lui manqua et lui-même fut comme une pierre.
38 Baada ya siku kumi, Bwana akampiga Nabali, naye akafa.
Il passa en cet état dix jours; puis, le Seigneur l'ayant frappé, il expira.
39 Daudi aliposikia kwamba Nabali amekufa, akasema, “Ahimidiwe Bwana, ambaye amenitetea shauri langu dhidi ya Nabali kwa kuwa alinitendea kwa dharau. Amemzuia mtumishi wake asitende mabaya na Bwana ameuleta ubaya wa Nabali juu ya kichwa chake mwenyewe.” Kisha Daudi akatuma ujumbe kwa Abigaili kumwomba awe mke wake.
David l'apprit, et il dit: Béni soit le Seigneur, qui a jugé l'outrage que j'avais reçu de Nabal, et qui a sauvé son serviteur des mains des méchants, et qui a fait retomber l'iniquité de Nabal sur sa tête. Ensuite, David envoya chez Abigaïl, et lui fit parler pour la prendre en mariage.
40 Watumishi wa Daudi wakaenda mpaka Karmeli na kumwambia Abigaili, wakisema, “Daudi ametutuma kwako kukuchukua uwe mkewe.”
Les serviteurs de David arrivèrent au Carmel chez Abigaïl, et ils lui parlèrent, disant: David nous a envoyés vers toi afin de te prendre pour sa femme.
41 Akainama chini uso wake mpaka ardhini, akasema, “Mjakazi wako yuko hapa, tayari kuwatumikia na kuwanawisha miguu watumishi wa bwana wangu.”
A ces mots, elle se leva et elle se prosterna la face contre terre, et elle dit: Voici ta servante, emploie-la comme une esclave à laver les pieds de tes serviteurs.
42 Abigaili akainuka kwa haraka, akapanda punda wake, akihudumiwa na wajakazi wake watano, akaenda pamoja na wajumbe wa Daudi, naye akawa mkewe.
Abigaïl se releva, elle monta sur une ânesse, cinq jeunes filles l'accompagnèrent; elle suivit les serviteurs de David, et elle fut sa femme.
43 Pia Daudi alikuwa amemwoa Ahinoamu wa Yezreeli, wote wawili wakawa wake zake.
David avait déjà épousé Achinaam de Jezraël; toutes les deux étaient ses femmes;
44 Lakini Sauli alikuwa amemwoza Mikali binti yake, aliyekuwa mkewe Daudi, kwa Palti mwana wa Laishi, kutoka Galimu.
Et Saül avait donné sa fille Michol, la femme de David, à Phalti, fils d'Amis de Rhomma.

< 1 Samweli 25 >