< 1 Samweli 22 >

1 Daudi akaondoka Gathi na kukimbilia kwenye pango la Adulamu. Ndugu zake na watu wa nyumba ya baba yake waliposikia habari hiyo, wakamwendea huko.
Or, David partit de là, et se sauva dans la caverne d'Adullam; et ses frères et toute la maison de son père l'apprirent, et descendirent là vers lui.
2 Wale wote waliokuwa katika dhiki au waliokuwa na madeni au wale ambao hawakuridhika wakamkusanyikia Daudi, naye akawa kiongozi wao. Watu wapatao 400 walikuwa pamoja naye.
Et tous ceux aussi qui étaient mal dans leurs affaires, et tous ceux qui avaient des créanciers, et tous ceux qui avaient le cœur plein d'amertume, s'assemblèrent vers lui, et il fut leur chef; il y eut ainsi avec lui environ quatre cents hommes.
3 Kutoka huko Daudi akaenda Mispa huko Moabu na kumwambia mfalme wa Moabu, “Naomba uwaruhusu baba yangu na mama yangu waje kukaa nawe mpaka nijue nini Mungu atakachonifanyia.”
Puis David s'en alla de là à Mitspé de Moab. Et il dit au roi de Moab: Je te prie, que mon père et ma mère se retirent chez vous, jusqu'à ce que je sache ce que Dieu fera de moi.
4 Hivyo akawaacha wazazi wake wakae na mfalme wa Moabu, nao wakakaa naye muda wote ambao Daudi alikuwa ngomeni.
Et il les amena devant le roi de Moab, et ils demeurèrent avec lui tout le temps que David fut dans cette forteresse.
5 Ndipo nabii Gadi akamwambia Daudi, “Usikae ngomeni. Nenda katika nchi ya Yuda.” Hivyo Daudi akaondoka na kwenda katika msitu wa Herethi.
Or, Gad, le prophète, dit à David: Ne demeure point dans cette forteresse; va-t'en, et entre au pays de Juda. David s'en alla donc, et vint dans la forêt de Héreth.
6 Basi Sauli akasikia kwamba Daudi na watu wake wameonekana. Sauli akiwa na mkuki mkononi, alikuwa ameketi chini ya mti wa mkwaju kwenye kilima huko Gibea, maafisa wake wote wakiwa wamesimama kumzunguka.
Et Saül apprit qu'on avait découvert David, et les gens qui étaient avec lui. Or, Saül était assis sous un tamarin sur la hauteur, à Guibea, sa lance à la main; et tous ses serviteurs se tenaient devant lui.
7 Sauli akawaambia, “Sikilizeni enyi watu wa Benyamini! Je, mwana wa Yese atawapa ninyi nyote mashamba na mashamba ya mizabibu? Je, atawafanya ninyi nyote majemadari wa maelfu na majemadari wa mamia?
Et Saül dit à ses serviteurs, qui se tenaient devant lui: Écoutez, Benjamites; le fils d'Isaï vous donnera-t-il, à tous, des champs et des vignes? vous établira-t-il tous chefs de milliers et de centaines?
8 Je, ndiyo sababu ninyi mkapanga hila mbaya dhidi yangu? Hakuna hata mmoja wenu ambaye ameniambia ni lini mwanangu alifanya agano na mwana wa Yese. Hapana hata mmoja wenu anayejishughulisha nami wala anayeniambia kwamba mwanangu amechochea mtumishi wangu kunivizia, kama afanyavyo leo.”
Que vous ayez tous conspiré contre moi, et que nul ne m'avertisse que mon fils a fait alliance avec le fils d'Isaï, et que personne de vous ne soit touché de mon état, et ne m'avertisse que mon fils a soulevé mon serviteur contre moi, pour me dresser des embûches, comme il le fait aujourd'hui.
9 Lakini Doegi Mwedomu, ambaye alikuwa akisimama na maafisa wa Sauli, akasema, “Nilimwona mwana wa Yese akija kwa Ahimeleki mwana wa Ahitubu huko Nobu.
Alors Doëg, l'Iduméen, qui était le chef des serviteurs de Saül, répondit et dit: J'ai vu le fils d'Isaï venir à Nob, vers Achimélec, fils d'Achitub,
10 Ahimeleki akamuuliza Bwana kwa ajili yake; pia akampa vyakula na ule upanga wa Goliathi Mfilisti.”
Qui a consulté l'Éternel pour lui, et lui a donné des vivres; il lui a aussi donné l'épée de Goliath, le Philistin.
11 Kisha mfalme akatuma watu wamwite kuhani Ahimeleki mwana wa Ahitubu, na jamaa yote ya baba yake, waliokuwa makuhani huko Nobu, nao wote wakaja kwa mfalme.
Alors le roi envoya appeler Achimélec, fils d'Achitub, le sacrificateur, et toute la famille de son père, les sacrificateurs qui étaient à Nob; et ils vinrent tous vers le roi.
12 Sauli akasema, “Sikiliza sasa, mwana wa Ahitubu.” Akajibu, “Naam, bwana wangu.”
Et Saül dit: Écoute, fils d'Achitub. Et il répondit: Me voici, mon seigneur.
13 Sauli akamwambia, “Kwa nini umepanga shauri baya dhidi yangu, wewe na mwana wa Yese, ukampa vyakula na upanga, tena hukumuuliza Mungu kwa ajili yake, na kwa sababu hiyo ameasi dhidi yangu na kunivizia, kama afanyavyo leo?”
Alors Saül lui dit: Pourquoi avez-vous conspiré contre moi, toi et le fils d'Isaï, quand tu lui as donné du pain et une épée, et que tu as consulté Dieu pour lui, afin qu'il s'élevât contre moi, pour me dresser des embûches, comme il le fait aujourd'hui?
14 Ahimeleki akamjibu mfalme, “Ni nani miongoni mwa watumishi wako wote aliye mwaminifu kama Daudi, mkwewe mfalme, kiongozi wa walinzi wako na anayeheshimika sana katika watu wa nyumbani mwako?
Et Achimélec répondit au roi, et dit: Et qui donc, entre tous tes serviteurs, est aussi fidèle que David, gendre du roi, qui est parti sur ton ordre, et qui est honoré dans ta maison?
15 Je, siku hiyo ilikuwa ndiyo ya kwanza kumwomba Mungu kwa ajili yake? La hasha! Mfalme na usiwashutumu watumishi wako wala yeyote wa jamaa ya baba yake, kwa kuwa mtumishi wako hafahamu lolote kabisa kuhusu jambo hili lote.”
Ai-je commencé aujourd'hui à consulter Dieu pour lui? Loin de moi cette pensée! Que le roi n'impute rien à son serviteur, ni à toute la maison de mon père; car ton serviteur ne sait de tout ceci aucune chose, ni petite ni grande.
16 Lakini mfalme akasema, “Ahimeleki, hakika utakufa, wewe na jamaa yote ya baba yako.”
Et le roi dit: Certainement, tu mourras, Achimélec, toi et toute la famille de ton père!
17 Ndipo mfalme akawaamuru walinzi wake waliokuwa kando yake: “Geukeni na kuwaua makuhani wa Bwana, kwa sababu nao pia wamejiunga na Daudi. Walijua kuwa alikuwa anakimbia, wala hawakuniambia.” Lakini maafisa wa mfalme hawakuwa radhi kuinua mkono kuwaua makuhani wa Bwana.
Alors le roi dit aux archers qui se tenaient devant lui: Tournez-vous, et faites mourir les sacrificateurs de l'Éternel; parce qu'ils ont aussi prêté la main à David, qu'ils ont bien su qu'il s'enfuyait, et ne m'en ont point averti. Mais les serviteurs du roi ne voulurent point porter la main ni se jeter sur les sacrificateurs de l'Éternel.
18 Kisha mfalme akamwagiza Doegi, “Wewe geuka ukawaue makuhani.” Hivyo basi Doegi Mwedomu, akageuka na kuwaua. Siku ile aliwaua watu themanini na watano wavaao visibau vya kitani.
Alors le roi dit à Doëg: Tourne-toi, et jette-toi sur les sacrificateurs. Et Doëg, l'Iduméen, se tourna, et se jeta sur les sacrificateurs, et tua, en ce jour-là, quatre-vingt-cinq hommes portant l'éphod de lin;
19 Pia akaupiga Nobu kwa upanga, mji wa makuhani, wakiwemo wanaume na wanawake, watoto wadogo na wale wanyonyao, ngʼombe wake, punda na kondoo.
Et il fit passer Nob, ville des sacrificateurs, au fil de l'épée, les hommes et les femmes, les enfants et les nourrissons; les bœufs aussi, les ânes, et le menu bétail, au fil de l'épée.
20 Lakini Abiathari, mwana wa Ahimeleki, mwana wa Ahitubu, akatoroka, akakimbia na kujiunga na Daudi.
Toutefois, un des fils d'Achi-mélec, fils d'Achitub, qui s'appelait Abiathar, se sauva et s'enfuit auprès de David.
21 Akamwambia Daudi kuwa Sauli amewaua makuhani wa Bwana.
Et Abiathar rapporta à David, que Saül avait tué les sacrificateurs de l'Éternel.
22 Kisha Daudi akamwambia Abiathari: “Siku ile, wakati Doegi Mwedomu alipokuwa pale, nilijua atahakikisha amemwambia Sauli. Mimi ninawajibika kwa vifo vya jamaa ya baba yako yote.
Et David dit à Abiathar: Je compris bien, ce jour-là, puisque Doëg, l'Iduméen, s'y trouvait, qu'il ne manquerait point de le rapporter à Saül. Je suis cause de la mort de toutes les personnes de la famille de ton père;
23 Kaa pamoja nami; usiogope. Mtu anayeutafuta uhai wako anautafuta uhai wangu pia. Ukiwa pamoja nami utakuwa salama.”
Demeure avec moi; ne crains rien; car celui qui cherche ma vie, cherche la tienne; tu seras bien gardé avec moi.

< 1 Samweli 22 >