< 1 Samweli 22 >

1 Daudi akaondoka Gathi na kukimbilia kwenye pango la Adulamu. Ndugu zake na watu wa nyumba ya baba yake waliposikia habari hiyo, wakamwendea huko.
So David left there and escaped to the cave of Adullam. When his brothers and all his father's house heard it, they went down there to him.
2 Wale wote waliokuwa katika dhiki au waliokuwa na madeni au wale ambao hawakuridhika wakamkusanyikia Daudi, naye akawa kiongozi wao. Watu wapatao 400 walikuwa pamoja naye.
Everyone who was in distress, everyone who was in debt, and everyone who was discontented—they all gathered to him. David became captain over them. There were about four hundred men with him.
3 Kutoka huko Daudi akaenda Mispa huko Moabu na kumwambia mfalme wa Moabu, “Naomba uwaruhusu baba yangu na mama yangu waje kukaa nawe mpaka nijue nini Mungu atakachonifanyia.”
Then David went from there to Mizpah in Moab. He said to the king of Moab, “Please let my father and my mother go out with you until I know what God will do for me.”
4 Hivyo akawaacha wazazi wake wakae na mfalme wa Moabu, nao wakakaa naye muda wote ambao Daudi alikuwa ngomeni.
He left them with the king of Moab. His father and mother stayed with him the whole time that David was in his stronghold.
5 Ndipo nabii Gadi akamwambia Daudi, “Usikae ngomeni. Nenda katika nchi ya Yuda.” Hivyo Daudi akaondoka na kwenda katika msitu wa Herethi.
Then the prophet Gad said to David, “Do not stay in your stronghold. Leave and go into the land of Judah.” So David left there and went into the forest of Hereth.
6 Basi Sauli akasikia kwamba Daudi na watu wake wameonekana. Sauli akiwa na mkuki mkononi, alikuwa ameketi chini ya mti wa mkwaju kwenye kilima huko Gibea, maafisa wake wote wakiwa wamesimama kumzunguka.
Saul heard that David had been discovered, along with the men who were with him. Now Saul was sitting in Gibeah under the tamarisk tree in Ramah, with his spear in his hand, and all his servants were standing around him.
7 Sauli akawaambia, “Sikilizeni enyi watu wa Benyamini! Je, mwana wa Yese atawapa ninyi nyote mashamba na mashamba ya mizabibu? Je, atawafanya ninyi nyote majemadari wa maelfu na majemadari wa mamia?
Saul said to his servants who stood around him, “Listen now, people of Benjamin! Will the son of Jesse give every one of you fields and vineyards? Will he make you all captains of thousands and captains of hundreds,
8 Je, ndiyo sababu ninyi mkapanga hila mbaya dhidi yangu? Hakuna hata mmoja wenu ambaye ameniambia ni lini mwanangu alifanya agano na mwana wa Yese. Hapana hata mmoja wenu anayejishughulisha nami wala anayeniambia kwamba mwanangu amechochea mtumishi wangu kunivizia, kama afanyavyo leo.”
in exchange for all of you plotting against me? None of you informs me when my son makes a covenant with the son of Jesse. None of you is sorry for me. None of you informs me that my son has incited my servant David against me. Today he hides and waits for me so he may attack me.”
9 Lakini Doegi Mwedomu, ambaye alikuwa akisimama na maafisa wa Sauli, akasema, “Nilimwona mwana wa Yese akija kwa Ahimeleki mwana wa Ahitubu huko Nobu.
Then Doeg the Edomite, who stood by the servants of Saul, answered, “I saw the son of Jesse come to Nob, to Ahimelech son of Ahitub.
10 Ahimeleki akamuuliza Bwana kwa ajili yake; pia akampa vyakula na ule upanga wa Goliathi Mfilisti.”
He prayed to Yahweh that he might help him, and he gave him provisions and the sword of Goliath the Philistine.”
11 Kisha mfalme akatuma watu wamwite kuhani Ahimeleki mwana wa Ahitubu, na jamaa yote ya baba yake, waliokuwa makuhani huko Nobu, nao wote wakaja kwa mfalme.
Then the king sent someone to summon the priest Ahimelech son of Ahitub and all his father's house, the priests who were in Nob. All of them came to the king.
12 Sauli akasema, “Sikiliza sasa, mwana wa Ahitubu.” Akajibu, “Naam, bwana wangu.”
Saul said, “Listen now, son of Ahitub.” He answered, “Here I am, my master.”
13 Sauli akamwambia, “Kwa nini umepanga shauri baya dhidi yangu, wewe na mwana wa Yese, ukampa vyakula na upanga, tena hukumuuliza Mungu kwa ajili yake, na kwa sababu hiyo ameasi dhidi yangu na kunivizia, kama afanyavyo leo?”
Saul said to him, “Why have you plotted against me, you and the son of Jesse, in that you have given him bread, and a sword, and have prayed to God that he might help him, so that he might rise up against me, to hide in secret, as he does today?”
14 Ahimeleki akamjibu mfalme, “Ni nani miongoni mwa watumishi wako wote aliye mwaminifu kama Daudi, mkwewe mfalme, kiongozi wa walinzi wako na anayeheshimika sana katika watu wa nyumbani mwako?
Then Ahimelech answered the king and said, “Who among all your servants is so faithful as David, who is the king's son-in-law and is over your bodyguard, and is honored in your house?
15 Je, siku hiyo ilikuwa ndiyo ya kwanza kumwomba Mungu kwa ajili yake? La hasha! Mfalme na usiwashutumu watumishi wako wala yeyote wa jamaa ya baba yake, kwa kuwa mtumishi wako hafahamu lolote kabisa kuhusu jambo hili lote.”
Is today the first time I have prayed to God to help him? Far be it from me! Do not let the king impute anything to his servant or to all the house of my father. For your servant knows nothing of this whole matter.”
16 Lakini mfalme akasema, “Ahimeleki, hakika utakufa, wewe na jamaa yote ya baba yako.”
The king replied, “You will surely die, Ahimelech, you and all your father's house.”
17 Ndipo mfalme akawaamuru walinzi wake waliokuwa kando yake: “Geukeni na kuwaua makuhani wa Bwana, kwa sababu nao pia wamejiunga na Daudi. Walijua kuwa alikuwa anakimbia, wala hawakuniambia.” Lakini maafisa wa mfalme hawakuwa radhi kuinua mkono kuwaua makuhani wa Bwana.
The king said to the guard that stood around him, “Turn and kill the priests of Yahweh. Because their hand also is with David, and because they knew that he fled, but did not reveal it to me.” But the servants of the king would not put out their hand to kill the priests of Yahweh.
18 Kisha mfalme akamwagiza Doegi, “Wewe geuka ukawaue makuhani.” Hivyo basi Doegi Mwedomu, akageuka na kuwaua. Siku ile aliwaua watu themanini na watano wavaao visibau vya kitani.
Then the king said to Doeg, “Turn and kill the priests.” So Doeg the Edomite turned and attacked the priests; he killed eighty-five persons who wore a linen ephod that day.
19 Pia akaupiga Nobu kwa upanga, mji wa makuhani, wakiwemo wanaume na wanawake, watoto wadogo na wale wanyonyao, ngʼombe wake, punda na kondoo.
He also put to the sword Nob, the city of the priests; both men and women, children and infants, and oxen and donkeys and sheep he put to the sword.
20 Lakini Abiathari, mwana wa Ahimeleki, mwana wa Ahitubu, akatoroka, akakimbia na kujiunga na Daudi.
But one of the sons of Ahimelech son of Ahitub, named Abiathar, escaped and fled after David.
21 Akamwambia Daudi kuwa Sauli amewaua makuhani wa Bwana.
Abiathar told David that Saul had killed Yahweh's priests.
22 Kisha Daudi akamwambia Abiathari: “Siku ile, wakati Doegi Mwedomu alipokuwa pale, nilijua atahakikisha amemwambia Sauli. Mimi ninawajibika kwa vifo vya jamaa ya baba yako yote.
David said to Abiathar, “I knew on that day, when Doeg the Edomite was there, that he would surely tell Saul. I am responsible for every death in your father's family!
23 Kaa pamoja nami; usiogope. Mtu anayeutafuta uhai wako anautafuta uhai wangu pia. Ukiwa pamoja nami utakuwa salama.”
Stay with me and do not be afraid. For the one who seeks your life seeks mine as well. You will be safe with me.”

< 1 Samweli 22 >