< 1 Samweli 21 >

1 Daudi akaenda Nobu, kwa Ahimeleki kuhani. Ahimeleki akatetemeka alipokutana naye, akamuuliza, “Kwa nini uko peke yako? Kwa nini hukufuatana na mtu yeyote?”
Then David came to Nob to Ahimelech the priest. Ahimelech came to meet David trembling, and said to him, "Why are you alone, and no man with you?"
2 Daudi akamjibu Ahimeleki kuhani, akisema, “Mfalme ameniagiza shughuli fulani na kuniambia, ‘Mtu yeyote asijue chochote kuhusu kazi yako wala maagizo yako!’ Kuhusu watu wangu, nimewaambia tukutane mahali fulani.
David said to the priest, "The king has commanded me a business, and has said to me, 'Let no man know anything of the business about which I send you, and what I have commanded you; and I have arranged to meet the young men at a certain place.'
3 Sasa basi, una nini mkononi? Nipatie mikate mitano au chochote unachoweza kupata.”
Now, if there are five loaves of bread under your control, give them into my hand, or whatever there is."
4 Lakini kuhani akamjibu Daudi, “Sina mkate wowote wa kawaida kwa sasa. Hata hivyo, ipo hapa mikate iliyowekwa wakfu, iwapo watu wamejitenga na wanawake.”
And the priest answered David, and said, "There is no common bread in my control, but there is holy bread. If the young men have kept themselves from women, they may eat of it."
5 Daudi akajibu, “Hakika tumejitenga na wanawake kwa siku hizi chache kama kawaida ya ninapotoka kwenda kwenye shughuli. Navyo vyombo vya wale vijana huwa ni vitakatifu hata kwenye safari ya kawaida, si zaidi sana leo vyombo vyao vitakuwa ni vitakatifu?”
And David answered the priest, and said to him, "Truly women have been kept from us as always when I set out. All the young men are holy, even when it is an ordinary mission. So how much more today will their vessels be holy?"
6 Hivyo kuhani akampa ile mikate iliyowekwa wakfu, kwa kuwa hapakuwepo mikate mingine isipokuwa hiyo ya Wonyesho iliyokuwa imeondolewa hapo mbele za Bwana na kubadilishwa na mingine yenye moto siku ile ilipoondolewa.
So the priest gave him what had been consecrated, for there was no bread there but the show bread, that had been removed before Jehovah, to put hot bread in the day when it was taken away.
7 Basi siku hiyo palikuwepo na mmoja wa watumishi wa Sauli, aliyezuiliwa mbele za Bwana; alikuwa Doegi Mwedomu, kiongozi wa wachunga wanyama wa Sauli.
Now a certain man of the servants of Saul was there that day, detained before Jehovah; and his name was Doeg the Edomite, the best of the herdsmen who belonged to Saul.
8 Daudi akamuuliza Ahimeleki, “Je, unao mkuki au upanga hapa? Sikuleta upanga wala silaha nyingine yoyote, kwa sababu shughuli ya mfalme ilikuwa ya haraka.”
David said to Ahimelech, "Isn't there here under your control spear or sword? For I have neither brought my sword nor my weapons with me, because the king's business required haste."
9 Kuhani akajibu, “Upanga wa Goliathi Mfilisti, ambaye ulimuua katika Bonde la Ela, upo hapa, umefungiwa katika kitambaa nyuma ya kisibau. Kama unauhitaji, uchukue, hakuna upanga mwingine hapa ila huo tu.” Daudi akasema, “Hakuna upanga mwingine kama huo. Nipatie huo.”
The priest said, "The sword of Goliath the Philistine, whom you killed in the Valley of Elah, look, it is here wrapped in a cloth behind an ephod. If you will take that, take it; for there is no other except that here." David said, "There is none like that. Give it to me."
10 Siku ile Daudi akamkimbia Sauli na kwenda kwa Akishi mfalme wa Gathi.
David arose, and fled that day for fear of Saul, and went to Achish the king of Gath.
11 Lakini watumishi wa Akishi wakamwambia, “Je, huyu si ndiye Daudi mfalme wa nchi? Je, huyu si ndiye yule ambaye wanaimba katika ngoma zao wakisema: “‘Sauli amewaua elfu zake, naye Daudi makumi elfu yake’?”
The servants of Achish said to him, "Isn't this David the king of the land? Did they not sing one to another about him in dances, saying, 'Saul has slain his thousands, David his ten thousands?'"
12 Daudi akayaweka maneno haya moyoni naye akamwogopa sana Akishi mfalme wa Gathi.
David laid up these words in his heart, and was very afraid of Achish the king of Gath.
13 Basi akajifanya mwendawazimu mbele yao; naye alipokuwa mikononi mwao, alitenda kama kichaa, akikwaruza kwa kutia alama juu ya milango ya lango na kuachia udelele kutiririka kwenye ndevu zake.
He changed his behavior before them, and pretended to be mad in their hands, and drummed on the doors of the gate, and let his spittle run down his beard.
14 Akishi akawaambia watumishi wake, “Tazameni mtu huyu! Ana wazimu! Kwa nini mnamleta kwangu?
Then Achish said to his servants, "Look, you see the man is mad. Why then have you brought him to me?
15 Je, mimi nimepungukiwa na wenda wazimu kiasi kwamba mmeniletea mtu huyo hapa aendelee kufanya hivi mbele yangu? Je, ilikuwa ni lazima mtu huyo aje nyumbani kwangu?”
Do I lack madmen, that you have brought this fellow to play the madman in my presence? Shall this fellow come into my house?"

< 1 Samweli 21 >