< 1 Samweli 20 >

1 Kisha Daudi akakimbia kutoka Nayothi huko Rama akamwendea Yonathani na kumuuliza, “Kwani nimefanya nini? Kosa langu ni nini? Nimemkosea baba yako kwa jinsi gani, hata kwamba anajaribu kuuondoa uhai wangu?”
David, s'enfuyant de Najoth, qui est près de Rama, vint trouver Jonathan, et dit en sa présence: Qu'ai-je fait, quelle est mon iniquité, et quel est mon péché devant ton père, qu'il cherche ma vie?
2 Yonathani akajibu, “La hasha! Hutakufa! Tazama, baba yangu hafanyi kitu chochote, kikubwa au kidogo, bila kuniambia mimi. Kwa nini anifiche hili? Sivyo ilivyo!”
Et il lui dit: A Dieu ne plaise! tu ne mourras point. Voici, mon père ne fait aucune chose, ni grande ni petite, qu'il ne me la communique, et pourquoi mon père me cacherait-il celle-ci? Cela n'est pas.
3 Lakini Daudi akaapa na kusema, “Baba yako anajua kabisa kwamba nimepata kibali mbele yako, naye amesema moyoni mwake, ‘Yonathani sharti asilijue hili, la sivyo atahuzunika.’ Lakini kweli kama Bwana aishivyo na kama uishivyo, kuna hatua moja tu kati yangu na mauti.”
Alors David, jurant, dit encore: Ton père sait certainement que je suis dans tes bonnes grâces, et il aura dit: Que Jonathan ne le sache pas, de peur qu'il n'en soit affligé. Mais, certainement, comme l'Éternel est vivant, et comme ton âme vit, il n'y a qu'un pas entre moi et la mort.
4 Yonathani akamwambia Daudi, “Chochote unachotaka nifanye, nitakufanyia.”
Alors Jonathan dit à David: Que désires-tu que je fasse? et je le ferai pour toi.
5 Basi Daudi akamwambia, “Angalia, kesho ni sikukuu ya Mwezi Mwandamo, nami inanipasa kula chakula pamoja na mfalme; lakini niache niende kujificha shambani mpaka kesho kutwa.
Et David dit à Jonathan: Voici, c'est demain la nouvelle lune, et je devrais m'asseoir avec le roi pour manger; mais laisse-moi aller, et je me cacherai aux champs jusqu'au soir du troisième jour.
6 Kama baba yako akiona ya kuwa sipo, mwambie, ‘Daudi aliniomba sana ruhusa kuwahi Bethlehemu, mji wake wa nyumbani, kwa sababu dhabihu ya mwaka inafanywa huko kwa ajili ya ukoo wake wote.’
Si ton père vient à s'informer de moi, tu répondras: David m'a demandé instamment la permission d'aller en hâte à Bethléhem, sa ville, parce que toute sa famille y fait un sacrifice annuel.
7 Kama akisema, ‘Ni vyema sana,’ basi mtumishi wako yu salama. Lakini kama akikasirika, unaweza kuwa na hakika kwamba anakusudia kunidhuru.
S'il dit ainsi: C'est bon! tout va bien pour ton serviteur; mais s'il se met en colère, sache que le mal est résolu de sa part.
8 Lakini kwa habari yako wewe, mtende wema mtumishi wako, kwa sababu mmeingia kwenye agano pamoja naye mbele za Bwana. Kama nina hatia, basi niue wewe mwenyewe! Kwa nini unikabidhi kwa baba yako?”
Fais donc cette grâce à ton serviteur, puisque tu as fait entrer ton serviteur en alliance avec toi au nom de l'Éternel. Mais s'il y a quelque iniquité en moi, fais-moi mourir toi-même; car pourquoi me mènerais-tu à ton père?
9 Yonathani akasema, “La hasha! Kama ningekuwa na kidokezo kidogo kwamba baba yangu amekusudia kukudhuru wewe, je, nisingekuambia?”
Et Jonathan lui dit: Loin de toi cette pensée! car si j'apprenais que mon père a résolu d'amener la ruine sur toi, ne te le ferais-je pas savoir?
10 Daudi akamuuliza, “Je, nani atakayeniambia kama baba yako atakujibu kwa ukali?”
Et David répondit à Jonathan: Qui me fera savoir si ton père te répond quelque chose de fâcheux?
11 Yonathani akamwambia, “Njoo, twende shambani.” Basi wakaenda huko pamoja.
Et Jonathan dit à David: Viens, et sortons aux champs. Et ils sortirent tous deux aux champs.
12 Kisha Yonathani akamwambia Daudi, “Ninakuahidi kwa jina la Bwana, Mungu wa Israeli, hakika nitamchunguza baba yangu wakati kama huu kesho kutwa! Kama ameweka utaratibu wa kufaa kukuhusu wewe, je, sitakutumia ujumbe na kukufahamisha?
Alors Jonathan dit à David: Aussi vrai que l'Éternel est Dieu d'Israël, je sonderai mon père vers cette heure-ci, demain ou après-demain; et voici, s'il est favorable à David, et qu'alors je n'envoie pas vers toi et ne te le fasse pas savoir,
13 Lakini ikiwa baba yangu amenuia kukudhuru, Bwana na anishughulikie kwa ukali, iwapo sitakufahamisha na kukuaga uende salama. Bwana na awe pamoja nawe kama alivyokuwa pamoja na baba yangu.
Que l'Éternel traite Jonathan avec la dernière rigueur! Que s'il plaît à mon père de te faire du mal, je te le ferai savoir aussi; et je te laisserai aller, et tu t'en iras en paix; et que l'Éternel soit avec toi comme il a été avec mon père!
14 Lakini nitendee wema usiokoma kama ule wa Bwana siku zote za maisha yangu, ili nisije nikauawa,
Mais aussi, si je suis encore vivant, n'useras-tu pas envers moi de la bonté de l'Éternel, en sorte que je ne meure point,
15 wala usiuondoe wema wako kwa jamaa yangu, hata kama ni wakati ule Bwana atakapokuwa amekatilia mbali kila adui wa Daudi kutoka kwenye uso wa dunia.”
Et que tu ne retires point ta bonté de ma maison, à jamais, non pas même quand l'Éternel aura retranché tous les ennemis de David de dessus la face de la terre?
16 Basi Yonathani akafanya agano na nyumba ya Daudi, akisema: “Bwana na awaangamize adui za Daudi.”
Et Jonathan traita alliance avec la maison de David, et dit: Que l'Éternel tire vengeance des ennemis de David!
17 Naye Yonathani akamtaka Daudi athibitishe tena kiapo chake cha kumpenda, kwa sababu Yonathani alimpenda Daudi kama nafsi yake mwenyewe.
Jonathan fit encore jurer David par l'amour qu'il lui portait; car il l'aimait autant que son âme.
18 Kisha Yonathani akamwambia Daudi, “Kesho ni sikukuu ya Mwezi Mwandamo. Itajulikana kwamba haupo kwa kuwa kiti chako kitakuwa hakina mtu.
Et Jonathan lui dit: C'est demain la nouvelle lune, et on s'enquerra de toi; car ta place sera vide;
19 Kesho kutwa, inapokaribia jioni, nenda mahali pale ulipojificha wakati tatizo hili lilipoanza na usubiri karibu na jiwe la Ezeli.
Mais, après-demain, tu descendras promptement, et tu viendras vers le lieu où tu t'étais caché, le jour de cette affaire, et tu demeureras auprès de la pierre d'Ézel;
20 Nitapiga mishale mitatu kando yake, kama kwamba nilikwenda kulenga shabaha.
Et je tirerai trois flèches à côté, comme si je tirais à quelque but;
21 Kisha nitamtuma mvulana na kumwambia, ‘Nenda ukaitafute mishale.’ Kama nikimwambia, ‘Tazama mishale iko upande huu wako! Uilete hapa,’ basi uje, kwa sababu hakika kama Bwana aishivyo, wewe ni salama, hakuna hatari.
Et voici, j'enverrai un jeune homme, en lui disant: Va, trouve les flèches. Si je dis à ce garçon: Voici, les flèches sont de ce côté-ci de toi, prends-les; alors viens, tout va bien pour toi, et il n'y a rien à craindre: l'Éternel est vivant
22 Lakini kama nikimwambia huyo mvulana, ‘Angalia, mishale iko mbele yako,’ basi inakupasa uondoke, kwa sababu Bwana amekuruhusu uende zako.
Mais si je dis au jeune garçon: Voici, les flèches sont au-delà de toi; alors va-t'en, car l'Éternel te renvoie.
23 Kuhusu yale tuliyozungumza wewe na mimi: kumbuka, Bwana ndiye shahidi kati yako wewe na mimi milele.”
Mais quant à la parole que nous nous sommes donnée, toi et moi, voici, l'Éternel est témoin entre moi et toi, à jamais.
24 Basi Daudi akajificha shambani, na sikukuu ya Mwezi Mwandamo ilipowadia, mfalme akaketi ili ale.
David se cacha donc aux champs. Et la nouvelle lune étant venue, le roi s'assit pour prendre son repas.
25 Akaketi mahali pake pa kawaida karibu na ukuta, kuelekeana na Yonathani, naye Abneri akaketi karibu na Mfalme Sauli, lakini kiti cha Daudi kilikuwa wazi.
Et le roi s'assit sur son siège, comme les autres fois, sur le siège contre la muraille; et Jonathan se leva, et Abner s'assit à côté de Saül, mais la place de David était vide.
26 Sauli hakusema chochote siku ile kwa kuwa alifikiri, “Kuna kitu cha lazima kimetokea kwa Daudi ambacho kimemfanya najisi asihudhurie karamuni, hakika yeye yu najisi.”
Et Saül n'en dit rien ce jour-là; car il se disait: Il lui est arrivé quelque chose, qui fait qu'il n'est pas pur; certainement il n'est pas pur.
27 Lakini siku iliyofuata, siku ya pili ya mwezi, kiti cha Daudi kilikuwa wazi tena. Kisha Sauli akamwambia mwanawe Yonathani, “Kwa nini mwana wa Yese hajaja chakulani jana wala leo?”
Mais le lendemain de la nouvelle lune, le second jour, la place de David fut encore vide; et Saül dit à Jonathan, son fils: Pourquoi le fils d'Isaï n'est-il point venu manger ni hier ni aujourd'hui?
28 Yonathani akamjibu, “Daudi alinisihi sana nimpe ruhusa aende Bethlehemu.
Et Jonathan répondit à Saül: David m'a demandé instamment la permission d'aller jusqu'à Bethléhem;
29 Alisema, ‘Niruhusu niende, kwa sababu jamaa yetu wana dhabihu mjini, na ndugu yangu ameniagiza niwepo huko. Kama nimepata kibali mbele yako, niruhusu niende kuona ndugu zangu.’ Hii ndiyo sababu hakuja mezani pa mfalme.”
Et il a dit: Laisse-moi aller, je te prie; car nous avons un sacrifice de famille dans la ville, et mon frère m'a recommandé de m'y trouver; maintenant donc, si j'ai trouvé grâce à tes yeux, que j'y aille, je te prie, afin de voir mes frères. C'est pour cela qu'il n'est point venu à la table du roi.
30 Hasira ya Sauli ikawaka dhidi ya Yonathani na kumwambia, “Wewe mwana wa mwanamke mkaidi na mwasi! Je, sijui kuwa umekuwa upande wa mwana wa Yese kwa aibu yako mwenyewe na kwa aibu ya mama yako aliyekuzaa?
Alors la colère de Saül s'embrasa contre Jonathan, et il lui dit: Fils pervers et rebelle, ne sais-je pas bien que tu as choisi le fils d'Isaï, à ta honte, et à la honte de ta mère?
31 Maadamu mwana wa Yese angali anaishi katika dunia hii wewe wala ufalme wako hautasimama. Sasa tuma aitwe umlete kwangu, kwa kuwa ni lazima afe!”
Car tant que le fils d'Isaï vivra sur la terre, tu ne seras jamais stable, ni toi, ni ton royaume; maintenant donc envoie-le chercher, et amène-le-moi; car il est digne de mort.
32 Yonathani akamuuliza baba yake, “Kwa nini auawe? Kwani amefanya nini?”
Et Jonathan répondit à Saül, son père, et lui dit: Pourquoi le ferait-on mourir? Qu'a-t-il fait?
33 Lakini Sauli akamtupia Yonathani mkuki wake kwa nguvu ili amuue. Hapo ndipo Yonathani alipotambua kwamba baba yake alikusudia kumuua Daudi.
Mais Saül brandit sa lance contre lui pour le frapper. Alors Jonathan connut que son père avait résolu de faire mourir David.
34 Yonathani akainuka kutoka mezani kwa hasira kali. Siku ile ya pili ya mwezi hakula chakula, kwa kuwa alikuwa amehuzunishwa na vitendo vya aibu ambavyo baba yake alikuwa anamtendea Daudi.
Et Jonathan se leva de la table tout en colère, et ne prit point son repas le second jour de la nouvelle lune; car il était affligé à cause de David, parce que son père l'avait outragé.
35 Kesho yake asubuhi Yonathani alikwenda shambani kukutana na Daudi. Alikuwa amefuatana na mvulana mdogo,
Et le matin venu, Jonathan sortit aux champs, au lieu convenu avec David; et il amena avec lui un petit garçon;
36 naye Yonathani akamwambia yule mvulana, “Kimbia ukatafute mishale nitakayorusha.” Mvulana alipokuwa akikimbia, akarusha mishale mbele yake.
Et il dit à ce garçon: Cours, trouve donc les flèches que je vais tirer. Le garçon courut, et Jonathan tira une flèche au-delà de lui.
37 Yule mvulana alipofika mahali pale ambapo mshale wa Yonathani ulipokuwa umeanguka, Yonathani akamwita, “Je, mshale hauko mbele yako?”
Quand le garçon vint jusqu'au lieu où était la flèche que Jonathan avait tirée, Jonathan cria après lui, et lui dit: La flèche n'est-elle pas au-delà de toi?
38 Yonathani akampigia kelele, “Harakisha, nenda haraka! Usisimame!” Mvulana akaokota mshale na kurudi kwa bwana wake.
Et Jonathan cria après le garçon: Vite, hâte-toi, ne t'arrête pas! Et le garçon de Jonathan ramassa la flèche, et vint vers son maître.
39 (Mvulana hakujua chochote juu ya hayo yote; Yonathani na Daudi tu ndio waliojua.)
Mais le garçon ne savait rien; il n'y avait que David et Jonathan qui connussent l'affaire.
40 Basi Yonathani akampa yule mvulana silaha zake na kumwambia, “Nenda, zirudishe mjini.”
Et Jonathan donna ses armes au garçon qu'il avait avec lui, et lui dit: Va, porte-les à la ville.
41 Baada ya mvulana kwenda, Daudi akainuka kutoka upande wa kusini wa lile jiwe, naye akasujudu uso wake mpaka nchi mara tatu mbele ya Yonathani. Kisha kila mmoja akambusu mwenzake, wakalia pamoja. Lakini Daudi akalia zaidi.
Le garçon partit; et David se leva du côté du Midi, se jeta le visage contre terre, et se prosterna trois fois; puis ils s'embrassèrent l'un l'autre, et pleurèrent tous deux, et même David pleura extrêmement.
42 Yonathani akamwambia Daudi, “Nenda kwa amani, kwa kuwa tumeapiana kiapo cha urafiki kati yetu kwa jina la Bwana, tukisema, ‘Bwana ndiye shahidi kati yako na mimi, na kati ya wazao wako na wazao wangu milele.’” Kisha Daudi akaondoka, naye Yonathani akarudi mjini.
Et Jonathan dit David: Va en paix, selon ce que nous avons juré tous deux, au nom de l'Éternel, en disant: L'Éternel sera entre moi et toi, et entre ma postérité et ta postérité, à jamais. David se leva donc et s'en alla, et Jonathan rentra dans la ville.

< 1 Samweli 20 >