< 1 Samweli 2 >

1 Kisha Hana akaomba na kusema: “Moyo wangu wamshangilia Bwana, katika Bwana pembe yangu imeinuliwa juu. Kinywa changu chajisifu juu ya adui zangu, kwa kuwa naufurahia wokovu wako.
And Hannah prayed, and said, My heart is glad in the Lord, my horn is exalted through the Lord: my mouth is enlarged over my enemies; because I rejoice in thy salvation.
2 “Hakuna yeyote aliye mtakatifu kama Bwana, hakuna mwingine zaidi yako; hakuna Mwamba kama Mungu wetu.
There is none holy like the Lord; for there is none beside thee; and there is not any rock like our God.
3 “Msiendelee kusema kwa kiburi hivyo wala msiache vinywa vyenu kunena kwa kiburi, kwa kuwa Bwana ndiye Mungu ajuaye, na kwa yeye matendo hupimwa.
Talk no more so exceeding proudly; let not arrogance come out of your mouth; for a God of knowledge is the Lord, and by him are actions weighed.
4 “Pinde za mashujaa zimevunjika, lakini wale wanaojikwaa wamevikwa nguvu.
The bow of the mighty is broken, and those that stumbled are girded with strength.
5 Wale waliokuwa na chakula tele wamejikodisha wenyewe ili kupata chakula, lakini wale waliokuwa na njaa hawana njaa tena. Mwanamke yule aliyekuwa tasa amezaa watoto saba, lakini yule ambaye alikuwa na wana wengi amedhoofika.
They that were full hire themselves out for bread; and they that were hungry cease [from labor]: while the barren hath born seven, she that hath many children fadeth away.
6 “Bwana huua na huleta uhai, hushusha chini mpaka kaburini na hufufua. (Sheol h7585)
The Lord killeth, and maketh alive: he bringeth down to the grave, and bringeth up. (Sheol h7585)
7 Bwana humfanya mtu maskini naye hutajirisha, hushusha na hukweza.
The Lord maketh poor and maketh rich: he bringeth low and also lifteth up.
8 Humwinua maskini kutoka mavumbini na humwinua mhitaji kutoka lundo la majivu; huwaketisha pamoja na wakuu na kuwafanya warithi kiti cha enzi cha heshima. “Kwa kuwa misingi ya dunia ni ya Bwana; juu yake ameuweka ulimwengu.
He raiseth up out of the dust the poor, from the dunghill he lifteth up the needy, to set them among nobles, and he assigneth them the throne of glory; for the Lord's are the pillars of the earth, on which he hath set the world.
9 Yeye atailinda miguu ya watakatifu wake, lakini waovu watanyamazishwa kwenye giza. “Si kwa nguvu mtu hushinda;
He ever guardeth the feet of his pious ones, and the wicked shall be made silent in darkness; for not by strength can man prevail.
10 wale wampingao Bwana wataharibiwa kabisa. Atapiga radi dhidi yao kutoka mbinguni; Bwana ataihukumu miisho ya dunia. “Atampa nguvu mfalme wake, na kuitukuza pembe ya mpakwa mafuta wake.”
The Lord—his adversaries will be crushed; out of heaven will he thunder upon them: the Lord will judge the ends of the earth; and he will give strength unto his king, and lift up the horn of his anointed.
11 Kisha Elikana akaenda nyumbani Rama, lakini mtoto akahudumu mbele za Bwana chini ya kuhani Eli.
And Elkanah went to Ramah to his house. And the lad was ministering unto the Lord before 'Eli the priest.
12 Wana wa Eli walikuwa watu wabaya kabisa, hawakumheshimu Bwana.
And the sons of 'Eli were worthless men: they knew not the Lord.
13 Basi ilikuwa desturi ya makuhani pamoja na watu kwamba kila mara yeyote anapotoa dhabihu na huku nyama ikiwa inachemshwa, mtumishi wa kuhani angalikuja na uma wenye meno matatu mkononi mwake.
And the custom of the priests with the people was, that, when any man offered a sacrifice, the priest's servant came, while [the man] was seething the flesh, with a fork with three teeth in his hand;
14 Angeutumbukiza huo uma kwenye sufuria au birika au sufuria kubwa au chungu, naye kuhani angalijichukulia mwenyewe chochote ambacho uma ungekileta. Hivi ndivyo walivyowatendea Waisraeli wote waliokuja Shilo.
And he struck it into the pan, or the kettle, or the caldron, or the pot; [and] all that the fork brought up the priest took away with it. So did they unto all the Israelites that came thither, to Shiloh.
15 Lakini hata kabla mafuta ya mnyama hayajachomwa, mtumishi wa kuhani angalikuja na kusema kwa mtu ambaye alikuwa akitoa dhabihu, “Mpe kuhani nyama akaoke, kwani hatapokea nyama iliyochemshwa kutoka kwako, ila iliyo mbichi tu.”
Even before they had yet burnt the fat, the priest's servant would come, and say to the man that sacrificed, Give flesh to roast for the priest; for he will not take from thee sodden flesh, but raw.
16 Kama mtu akimwambia, “Mafuta ya mnyama na yachomwe kwanza, ndipo uchukue chochote unachotaka,” mtumishi angalijibu, “Hapana, nipe sasa, kama huwezi nitaichukua kwa nguvu.”
And if the man said unto him, They will surely presently burn the fat, and then take whatever thy soul may long for: then would he say, No; but thou shalt give it me now; and if not, I will take it by force.
17 Hii Dhambi ya hawa vijana ilikuwa kubwa sana machoni pa Bwana, kwa kuwa waliitendea dhabihu ya Bwana kwa dharau.
And the sin of the young men was very great before the Lord; for the men despised the offering of the Lord.
18 Lakini Samweli alikuwa akihudumu mbele za Bwana, kijana akivaa kisibau cha kitani.
But Samuel was ministering before the Lord, being a lad, girded with a linen ephod.
19 Kila mwaka mama yake alimshonea joho dogo na kumchukulia wakati alipokwea pamoja na mumewe kutoa dhabihu ya mwaka.
Moreover his mother used to make him a little overcoat, and brought it to him from year to year, when she came up with her husband to offer the yearly sacrifice.
20 Eli alikuwa akiwabariki Elikana na mkewe, akisema, “Bwana na akupe watoto kwa mwanamke huyu ili kuchukua nafasi ya yule aliyekuwa amemwomba na akamtoa kwa Bwana.” Kisha wakawa wanakwenda nyumbani.
And 'Eli blessed Elkanah and his wife, and said, May the Lord give thee seed from this woman instead of the loan who is lent to the Lord. And they went back unto his place.
21 Bwana akawa mwenye neema kwa Hana, naye akapata mimba akazaa wana watatu na binti wawili. Wakati huo, kijana Samweli akaendelea kukua mbele za Bwana.
And truly the Lord visited Hannah, and she conceived, and bore three sons and two daughters. And the lad Samuel grew up before the Lord.
22 Basi Eli, ambaye alikuwa mzee sana, alisikia kuhusu kila kitu ambacho wanawe walikuwa wakiwafanyia Israeli wote na jinsi walivyokutana kimwili na wanawake waliohudumu kwenye ingilio la Hema la Kukutania.
Now 'Eli was very old, and heard all that his sons were in the habit of doing unto all Israel; and how they would lie with the women that assembled at the door of the tabernacle of the congregation.
23 Hivyo akawaambia, “Kwa nini mmefanya mambo kama haya? Nimesikia kutoka kwa watu wote juu ya haya matendo yenu maovu.
And he said unto them, Why will ye do such things? for I hear of your evil dealings from all this people.
24 Sivyo, wanangu, hii si habari nzuri ambayo ninasikia ikienea miongoni mwa watu wa Bwana.
No, my sons; for the report that I hear is not good, which the Lord's people spread abroad.
25 Kama mtu akifanya dhambi dhidi ya mtu mwenzake, mtu mwingine aweza kumwombea kwa Mungu, lakini kama mtu akimfanyia Mungu dhambi, ni nani atakayemwombea?” Hata hivyo wanawe hawakusikia maonyo ya baba yao, kwa sababu Bwana alitaka kuwaua.
If one man sin against another, the judge shall judge him; but if against the Lord a man should sin, who shall pray for him? Nevertheless would they not hearken unto the voice of their father, because the Lord desired to slay them.
26 Naye kijana Samweli akaendelea kukua katika kimo, akimpendeza Bwana na wanadamu.
And the lad Samuel was constantly growing and increasing in favor both with the Lord, and also with men.
27 Basi mtu wa Mungu akaja kwa Eli na kumwambia, “Hivi ndivyo asemavyo Bwana: ‘Je, sikujifunua waziwazi kwa nyumba ya baba yako wakati walikuwa huko Misri chini ya Farao?
And there came a man of God unto 'Eli, and said unto him, Thus hath said the Lord, Did I [not] appear unto the house of thy father, when they were in Egypt, in Pharaoh's house?
28 Nilimchagua baba yako kati ya makabila yote ya Israeli kuwa kuhani wangu, kukwea kwenye madhabahu yangu, kufukiza uvumba na kuvaa kisibau mbele yangu. Pia niliwapa nyumba ya baba yako sadaka zote zilizotolewa kwa moto na Waisraeli.
And did I [not] choose him out of all the tribes of Israel to me as a priest, to offer upon my altar, to burn incense, to wear an ephod before me? and did I [not] give unto the house of thy father all the fire-offerings of the children of Israel?
29 Kwa nini unadharau dhabihu zangu na sadaka zile nilizoziamuru kwa ajili ya makao yangu? Kwa nini unawaheshimu wanao kuliko mimi kwa kujinenepesha wenyewe kwa kula sehemu zilizo bora za kila sadaka zinazotolewa na watu wangu wa Israeli?’
Wherefore kick ye at my sacrifice and at my meat-offering, which I have commanded in [my] habitation? and [why] honoredst thou thy sons above me, to fatten yourselves with the first of every offering of Israel my people?
30 “Kwa hiyo, Bwana, Mungu wa Israeli asema: ‘Niliahidi kuwa nyumba yako na nyumba ya baba yako wangehudumu mbele zangu milele.’ Lakini sasa Bwana anasema: ‘Jambo hili na liwe mbali nami! Wale wanaoniheshimu nitawaheshimu, wale wanaonidharau mimi watadharauliwa.
Therefore saith the Lord the God of Israel, I had indeed said, Thy house, and the house of thy father, should walk before me for ever; but now, saith the Lord, Be it far from me; for those that honor me will I honor, and those that despise me shall be lightly esteemed.
31 Wakati unakuja nitakapozipunguza nguvu zenu na nguvu ya nyumba ya baba yenu, ili pasiwepo mtu katika mbari yenu atakayeishi kuuona uzee
Behold, days are coming, that I will hew off thy arm, and the arm of thy father's house, so that there shall not be an old man in thy house.
32 nanyi mtaona huzuni katika makao yangu. Ingawa Israeli watafanyiwa mema, katika mbari yenu kamwe hapatakuwepo mtu atakayeishi hadi kuwa mzee.
And thou shalt behold a rival in my habitation, in all that by which he will do good for Israel: and there shall not be an old man in thy house in all times.
33 Kila mmoja wenu ambaye sitamkatilia mbali kutoka madhabahuni pangu atabakizwa tu kupofusha macho yenu kwa machozi na kuihuzunisha mioyo yenu, nao wazao wenu wote watakufa watakapokuwa wamefikia umri wa kustawi.
And yet I will not cut off the men descended from thee from my altar, to consume thy eyes, and to grieve thy soul: and all the increase of thy house shall die as [vigorous] men.
34 “‘Kile kitakachotokea kwa wanao wawili, Hofni na Finehasi, kitakuwa ishara kwako. Wote wawili watakufa katika siku moja.
And this shall be unto thee the sign, that shall happen on thy two sons, on Chophni and Phinehas: On one day shall they, both of them, die.
35 Mimi mwenyewe nitajiinulia kuhani mwaminifu, ambaye atafanya sawasawa na kile kilichoko moyoni mwangu na akilini mwangu. Nitaifanya nyumba yake kuwa imara, naye atahudumu mbele ya mpakwa mafuta wangu daima.
And I will raise up to me a faithful priest, who shall do in accordance with what is in my heart and in my mind; and I will build for him an enduring house; and he shall walk before my anointed in all times.
36 Kisha kila mmoja aliyeachwa katika mbari yenu atakuja na kusujudu mbele yake kwa ajili ya kipande cha fedha na ganda la mkate akisema, “Niteue katika baadhi ya ofisi ya ukuhani ili niweze kupata chakula.”’”
And it shall come to pass, that whoever is left in thy house shall come to bow down to him for a gera of silver and a loaf of bread, and shall say, Attach me, I pray thee, unto one of the priestly offices, that I may eat a piece of bread.

< 1 Samweli 2 >