< 1 Samweli 16 >

1 Bwana akamwambia Samweli, “Utamlilia Sauli mpaka lini, maadamu nimemkataa asiendelee kuwa mfalme juu ya Israeli? Jaza pembe yako mafuta, ushike njia uende; ninakutuma kwa Yese huko Bethlehemu. Nimemchagua mmoja wa wanawe kuwa mfalme.”
И рече Господь к Самуилу: доколе ты плачеши о Сауле, Аз же уничижих его, не царствовати во Израили? Наполни рог твой елеа и прииди, послю тя ко Иессею до Вифлеема, яко узрех в сынех его Себе царя.
2 Lakini Samweli akasema, “Nitakwendaje? Sauli atasikia juu ya jambo hili na ataniua.” Bwana akamwambia, “Chukua mtamba wa ngʼombe na useme, ‘Nimekuja kumtolea Bwana dhabihu.’
И рече Самуил: како пойду? И услышит Саул, и убиет мя. И рече Господь: юницу от волов возми в руце твои и речеши: пожрети Господеви иду:
3 Mwalike Yese aje kwenye dhabihu, nami nitakuonyesha utakalofanya. Utamtia mafuta kwa ajili yangu yule nitakayekuonyesha.”
и призовеши Иессеа и сыны его к жертве: и Аз ти покажу, яже сотвориши, и помажеши Ми, егоже ти реку.
4 Samweli akafanya kile Bwana alichosema. Alipofika Bethlehemu, wazee wa mji wakatetemeka walipomlaki. Wakauliza, “Je, umekuja kwa amani?”
И сотвори Самуил вся, елика рече ему Господь: и прииде в Вифлеем, и ужасошася старейшины града о пришествии его и реша: мир ли вход твой, о, прозорливче?
5 Samweli akajibu, “Ndiyo, kwa amani; nimekuja kumtolea Bwana dhabihu. Jiwekeni wakfu na mje kwenye dhabihu pamoja nami.” Ndipo akamweka Yese wakfu pamoja na wanawe na kuwaalika kwenye dhabihu.
И рече: мир: пожрети Господу приидох: освятитеся и возвеселитеся днесь со мною. И освяти Иессеа и сыны его, и призва я к жертве.
6 Walipofika, Samweli akamwona Eliabu, naye akafikiri, “Hakika mpakwa mafuta wa Bwana anasimama hapa mbele za Bwana.”
И бысть внегда внити им, и виде Елиава и рече: сей ли пред Господем помазанник Его?
7 Lakini Bwana akamwambia Samweli, “Usitazame sura yake wala kimo chake, kwa kuwa nimemkataa. Bwana hatazami katika vile vitu mwanadamu avitazamavyo. Mwanadamu hutazama katika sura ya nje, lakini Bwana hutazama moyoni.”
И рече Господь Самуилу: не зри на лице его, ниже на возраст величества его, яко уничижих его: понеже не тако зрит человек, яко зрит Бог: яко человек зрит на лице, Бог же зрит на сердце.
8 Kisha Yese akamwita Abinadabu na kumpitisha mbele ya Samweli. Lakini Samweli akasema, “Hata huyu Bwana hakumchagua.”
И призва Иессей Аминадава и представи его пред лице Самуила. И рече (Самуил): ниже сего избра Господь.
9 Kisha Yese akampitisha Shama, lakini Samweli akasema, “Wala huyu Bwana hakumchagua.”
И приведе Иессей Саммаа. И рече: и сего не избра Господь.
10 Yese alikuwa na wana saba aliowapitisha mbele ya Samweli, lakini Samweli akamwambia, “Bwana hajawachagua hawa.”
И приведе Иессей седмь сынов своих пред Самуила. И рече Самуил ко Иессею: не избра Господь от сих.
11 Hivyo akamuuliza Yese, “Je, hawa ndio wana pekee ulio nao?” Yese akajibu, “Bado yuko mdogo kuliko wote, lakini anachunga kondoo.” Samweli akasema, “Tuma aitwe; hatutaketi mpaka afike.”
И рече Самуил ко Иессею: не достало ли уже детей? И рече Иессей: еще есть един мал, и сей пасет на пажити. И рече Самуил ко Иессею: посли и приведи его, яко не возляжем, дондеже приидет той семо.
12 Basi akatuma aitwe naye akaletwa. Alikuwa mwekundu, mwenye sura nzuri na umbo la kupendeza. Ndipo Bwana akasema, “Inuka na umtie mafuta, huyu ndiye.”
И посла, и введе его: и той чермен, добрыма очима, и благ взором Господеви. И рече Господь к Самуилу: востани и помажи Давида, яко сей благ есть.
13 Basi Samweli akachukua ile pembe ya mafuta na kumtia mafuta mbele ya ndugu zake, kuanzia siku ile na kuendelea Roho wa Bwana akaja juu ya Daudi kwa nguvu. Kisha Samweli akaenda zake Rama.
И прия Самуил рог со елеем и помаза его посреде братии его. И ношашеся Дух Господень над Давидом от того дне и потом. И воста Самуил и отиде во Армафем.
14 Basi Roho wa Bwana alikuwa ameondoka kwa Sauli, nayo roho mbaya ikaachiwa nafasi na Bwana ili imtese.
И Дух Господень отступи от Саула, и давляше его дух лукавый от Господа.
15 Watumishi wa Sauli wakamwambia, “Angalia, roho mbaya imeachiwa nafasi na Bwana nayo inakutesa.
И реша отроцы Сауловы к нему: се, ныне дух лукавый от Господа давит тя:
16 Basi bwana wetu na aamuru watumishi wake walioko hapa kutafuta mtu ambaye anaweza kupiga kinubi. Atakipiga kinubi wakati roho mbaya iliyoachiwa nafasi na Mungu ikujiapo, nawe utajisikia vizuri.”
да рекут раби твои ныне пред тобою, и взыщут господину нашему мужа знающа пети в гусли: и внегда будет дух лукавый на тебе, и тогда да поет в гусли своя, и благо ти будет, и упокоит тя.
17 Basi Sauli akawaambia watumishi wake, “Mtafuteni mtu apigaye kinubi vizuri mkamlete kwangu.”
И рече Саул ко отроком своим: посмотрите ми мужа добре поюща и введите его ко мне.
18 Mmoja wa watumishi wake akajibu, “Nimemwona mwana wa Yese Mbethlehemu ambaye anajua kupiga kinubi. Yeye ni mtu hodari na shujaa wa vita. Ni mwenye busara katika kunena, mtu mzuri wa umbo. Bwana yu pamoja naye.”
И отвеща един от отрок его и рече: се, видех сына Иессеова из Вифлеема, и той весть пение, и муж разумен, и борец, и мудр в словеси, и муж благ видом, и Господь с ним.
19 Ndipo Sauli akatuma wajumbe kwa Yese na kumwambia, “Nitumie mwanao Daudi, ambaye anachunga kondoo.”
И посла Саул вестники ко Иессею, глаголя: отпусти ко мне Давида сына твоего, иже у стада твоего.
20 Kwa hiyo Yese akamchukua punda aliyepakizwa mikate, kiriba cha divai na mwana-mbuzi, na kuvipeleka vitu hivyo kwa Sauli pamoja na Daudi mwanawe.
И взя Иессей бремя хлебов и мех вина и козля от коз едино, и посла к Саулу рукою Давида сына своего.
21 Daudi akafika kwa Sauli na kuingia kwenye kazi yake. Sauli akampenda sana, naye Daudi akawa mmoja wa wabeba silaha wake.
И вниде Давид к Саулу, и предстояше пред ним, и возлюби его зело Саул, и бысть ему носяй оружие его.
22 Basi Sauli akatuma ujumbe kwa Yese, akisema, “Mruhusu Daudi abaki katika utumishi wangu, kwa kuwa ninapendezwa naye.”
И посла Саул ко Иессею, глаголя: да предстоит Давид предо мною, яко обрете благодать пред очима моима.
23 Kila mara roho mbaya iliyoachiwa nafasi na Mungu ilipomjia Sauli, Daudi alichukua kinubi chake na kupiga. Ndipo Sauli angetulizwa na kujisikia vizuri, nayo ile roho mbaya ingemwacha.
И бысть внегда быти духу лукаву на Сауле, и взимаше Давид гусли и играше рукою своею, и отдыхаше Саул, и благо ему бяше, и отступаше от него дух лукавый.

< 1 Samweli 16 >