< 1 Samweli 12 >

1 Samweli akawaambia Israeli wote, “Nimesikiliza kila kitu mlichoniambia nami nimewawekea mfalme juu yenu.
Samuel said to all Israel, "Look, I have listened to your voice in all that you said to me, and have made a king over you.
2 Sasa mnaye mfalme kama kiongozi wenu. Lakini kwa habari yangu mimi ni mzee na nina mvi, nao wanangu wapo hapa pamoja nanyi. Nimekuwa kiongozi wenu tangu ujana wangu mpaka siku hii ya leo.
Now, look, the king walks before you; and I am old and gray-headed; and look, my sons are with you: and I have walked before you from my youth to this day.
3 Mimi ninasimama hapa. Shuhudieni juu yangu mbele za Bwana na mpakwa mafuta wake. Nimechukua maksai wa nani? Nimechukua punda wa nani? Ni nani nimepata kumdanganya? Ni nani nimepata kumwonea? Ni kutoka kwenye mkono wa nani nimepokea rushwa ili kunifanya nifumbe macho yangu? Kama nimefanya chochote katika hivi, mimi nitawarudishia.”
Here I am. Testify against me before Jehovah, and before his anointed. Whose ox have I taken, or whose donkey have I taken, or whom have I defrauded? Whom have I oppressed, or from whose hand have I taken a bribe, or a shoe? Testify against me, and I will restore it to you."
4 Wakajibu, “Hujatudanganya wala kutuonea. Hujapokea chochote kutoka kwenye mkono wa mtu awaye yote.”
They said, "You have not defrauded us, nor oppressed us, neither have you taken anything of any man's hand."
5 Samweli akawaambia, “Bwana ni shahidi juu yenu, pia mpakwa mafuta wake ni shahidi siku hii ya leo, kwamba hamkukuta chochote mkononi mwangu.” Wakasema, “Yeye ni shahidi.”
He said to them, "Jehovah is witness against you, and his anointed is witness this day, that you have not found anything in my hand." They said, "He is witness."
6 Kisha Samweli akawaambia watu, “Bwana ndiye alimchagua Mose na Aroni, na kuwaleta baba zenu akiwapandisha kutoka Misri.
Samuel said to the people, "It is Jehovah who appointed Moses and Aaron, and that brought your fathers up out of the land of Egypt.
7 Sasa basi, simameni hapa, kwa sababu nitakabiliana nanyi kwa ushahidi mbele za Bwana wa matendo yote ya haki yaliyofanywa na Bwana kwenu na kwa baba zenu.
Now therefore stand still, that I may plead with you before Jehovah concerning all the righteous acts of Jehovah, which he did to you and to your fathers.
8 “Baada ya Yakobo kuingia Misri, walimlilia Bwana kwa ajili ya msaada, naye Bwana akawatuma Mose na Aroni, ambao waliwatoa baba zenu kutoka Misri na kuwakalisha mahali hapa.
"When Jacob went into Egypt, and the Egyptians oppressed them, and your fathers cried to Jehovah, then Jehovah sent Moses and Aaron, who brought your fathers out of Egypt, and made them to dwell in this place.
9 “Lakini wakamsahau Bwana Mungu wao, hivyo Mungu akawauza katika mkono wa Sisera, jemadari wa jeshi la Hazori na katika mikono ya Wafilisti na mfalme wa Moabu, ambaye alipigana dhidi yao.
"But they forgot Jehovah their God; and he sold them into the hand of Sisera, captain of the army of Hazor, and into the hand of the Philistines, and into the hand of the king of Moab; and they fought against them.
10 Wakamlilia Bwana na kusema, ‘Tumetenda dhambi; tumemwacha Bwana na kutumikia Mabaali na Maashtorethi. Lakini sasa tuokoe kutoka mikono ya adui zetu, nasi tutakutumikia.’
And they cried to Jehovah, and they said, 'We have sinned, because we have forsaken Jehovah, and have served the Baals and the Ashtaroth: but now deliver us out of the hand of our enemies, and we will serve you.'
11 Ndipo Bwana akawatuma Yerub-Baali, Baraka, Yefta na Samweli, naye akawaokoa kutoka mikononi mwa adui zenu kila upande, ili ninyi mpate kukaa salama.
Jehovah sent Jerubbaal, and Barak, and Jephthah, and Samuel, and delivered you out of the hand of your enemies on every side; and you lived in safety.
12 “Lakini mlipomwona yule Nahashi mfalme wa Waamoni anakuja dhidi yenu, mliniambia, ‘Hapana, tunataka mfalme atutawale,’ hata ingawa Bwana Mungu wenu alikuwa mfalme wenu.
"When you saw that Nahash the king of the people of Ammon came against you, you said to me, 'No, but a king shall reign over us;' when Jehovah your God was your king.
13 Sasa huyu hapa ndiye mfalme mliyemchagua, yule mliyeomba; tazameni, Bwana amemweka mfalme juu yenu.
Now therefore see the king whom you have chosen, and whom you have asked for: and look, Jehovah has set a king over you.
14 Kama mkimcha Bwana na kumtumikia na kumtii nanyi msipoasi dhidi ya amri zake, ninyi pamoja na mfalme anayetawala juu yenu mkimfuata Bwana, Mungu wenu, mambo yatakuwa mema kwenu!
If you will fear Jehovah, and serve him, and listen to his voice, and not rebel against the commandment of Jehovah, and both you and also the king who reigns over you are followers of Jehovah your God, then he will rescue you.
15 Lakini kama hamkumtii Bwana, nanyi kama mkiasi dhidi ya amri zake, mkono wake utakuwa dhidi yenu, kama ulivyokuwa dhidi ya baba zenu.
But if you will not listen to the voice of Jehovah, but rebel against the commandment of Jehovah, then the hand of Jehovah will be against you, and against your king to destroy you.
16 “Sasa basi, simameni kimya mkaone jambo hili kubwa ambalo Bwana anakwenda kulifanya mbele ya macho yenu!
"Now therefore stand still and see this great thing, which Jehovah will do before your eyes.
17 Je, sasa si mavuno ya ngano? Nitamwomba Bwana ili alete ngurumo na mvua. Nanyi mtatambua jambo hili lilivyo baya mlilolifanya mbele za macho ya Bwana mlipoomba mfalme.”
Isn't it wheat harvest today? I will call to Jehovah, that he may send thunder and rain; and you shall know and see that your wickedness is great, which you have done in the sight of Jehovah, in asking for a king."
18 Kisha Samweli akamwomba Bwana, na siku ile ile Bwana akatuma ngurumo na mvua. Hivyo watu wote wakamwogopa sana Bwana na Samweli.
So Samuel called to Jehovah; and Jehovah sent thunder and rain that day: and all the people greatly feared Jehovah and Samuel.
19 Watu wote wakamwambia Samweli, “Mwombe Bwana Mungu wako kwa ajili ya watumishi wako, ili tusije tukafa, kwa kuwa tumeongeza uovu juu ya dhambi zetu nyingine kwa kuomba mfalme.”
All the people said to Samuel, "Pray for your servants to Jehovah your God, that we not die; for we have added to all our sins this evil, to ask us a king."
20 Samweli akajibu, “Msiogope, mmefanya uovu huu wote; hata hivyo msimwache Bwana, bali mtumikieni Bwana kwa moyo wenu wote.
Samuel said to the people, "Do not be afraid. You have indeed done all this evil; yet do not turn aside from following Jehovah, but serve Jehovah with all your heart.
21 Msigeukie sanamu zisizofaa. Haziwezi kuwatendea jema, wala haziwezi kuwaokoa kwa sababu hazina maana.
Do not turn aside to go after vain things which can't profit nor deliver, for they are vain.
22 Kwa ajili ya jina lake kuu Bwana hatawakataa watu wake, kwa sababu ilimpendeza Bwana kuwafanya kuwa wake mwenyewe.
For Jehovah will not forsake his people for his great name's sake, because it has pleased Jehovah to make you a people to himself.
23 Kwa habari yangu, iwe mbali nami kutenda dhambi dhidi ya Bwana kwa kushindwa kuwaombea. Mimi nitawafundisha njia iliyo njema na ya kunyooka.
Moreover as for me, far be it from me that I should sin against Jehovah in ceasing to pray for you: but I will instruct you in the good and the right way.
24 Lakini hakikisheni mnamcha Bwana na kumtumikia kwa uaminifu kwa moyo wenu wote; tafakarini mambo makubwa aliyoyatenda kwa ajili yenu.
Only fear Jehovah, and serve him in truth with all your heart; for consider what great things he has done for you.
25 Hata hivyo mkiendelea kufanya uovu, ninyi na mfalme wenu mtafutiliwa mbali!”
But if you shall still do wickedly, you shall be swept away, both you and your king."

< 1 Samweli 12 >