< 1 Wafalme 5 >

1 Hiramu mfalme wa Tiro aliposikia kuwa Solomoni ametiwa mafuta awe mfalme mahali pa Daudi baba yake, akatuma wajumbe kwa Solomoni, kwa sababu Hiramu siku zote alikuwa na uhusiano mzuri wa kirafiki na Daudi.
Da Kong Hiram af Tyrus hørte, at Salomo var salvet til Konge i stedet for sin Fader, sendte han nogle af sine Folk til ham; thi Hiram havde altid været Davids Ven.
2 Solomoni akapeleka ujumbe huu kwa Hiramu:
Og Salomo sendte Hiram følgende Bud:
3 “Unajua kwamba kwa sababu ya vita vilivyopiganwa dhidi ya baba yangu Daudi kutoka pande zote, hakuweza kujenga Hekalu kwa ajili ya Jina la Bwana Mungu wake, hadi Bwana alipowaweka adui zake chini ya miguu yake.
"Du ved, at min Fader David ikke kunde bygge HERREN sin Guds Navn et Hus for de Kriges Skyld, man fra alle Sider påførte ham, indtil HERREN lagde hans Fjender under hans Fødder.
4 Lakini sasa Bwana Mungu wangu amenipa utulivu kila upande hakuna adui wala maafa.
Men nu har HERREN min Gud skaffet mig Ro til alle Sider; der findes ingen Modstandere, og der er ingen Fare på Færde.
5 Kwa hiyo, ninakusudia kujenga Hekalu kwa ajili ya Jina la Bwana, Mungu wangu, kama Bwana alivyomwambia baba yangu Daudi, wakati aliposema, ‘Mwanao nitakayemweka kwenye kiti cha ufalme mahali pako, ndiye atajenga Hekalu kwa ajili ya Jina langu.’
Se, derfor har jeg i Sinde at bygge HERREN min Guds Navn et Hus efter HERRENs Ord til min Fader David: Din Søn, som jeg sætter på din Trone i dit Sted, han skal bygge Huset for mit Navn.
6 “Hivyo toa amri ili mierezi ya Lebanoni ikatwe kwa ajili yangu. Watu wangu watafanya kazi na watu wako, nami nitawalipa watu wako kwa ujira wowote utakaoupanga. Unajua kwamba hatuna mtu yeyote mwenye ustadi katika kukata miti kama Wasidoni.”
Giv derfor Ordre til, at der fældes Cedre til mig på Libanon. Mine Folk skal arbejde sammen med dine, og jeg vil give dineFolk den Løn, du kræver; thi du ved jo, at der ikke findes nogen hos os, der kan fælde Træer som Zidonierne!"
7 Hiramu aliposikia ujumbe wa Solomoni, akafurahishwa sana akasema, “Ahimidiwe Bwana leo, kwa kuwa amempa Daudi mwana mwenye hekima kutawala juu ya taifa hili kubwa.”
Da Hiram modtog dette Bud fra Salomo, glædede det ham meget, og han sagde: "Lovet være HERREN i dag, fordi han har givet David en viis Søn til at herske over dette store Folk!"
8 Hiramu akatuma neno kwa Solomoni: “Nimepokea ujumbe ulionipelekea na nitafanya yote unayohitaji katika kukupatia magogo ya mierezi na misunobari.
Og Hiram sendte Salomo følgende Svar: "Jeg har modtaget det Bud, du sendte mig, og jeg skal opfylde alt, hvad du ønsker med Hensyn til Ceder- og Cyprestræer;
9 Watu wangu watayakokota kutoka Lebanoni hadi kwenye bahari, nami nitayafunga mafungu mafungu yaelee juu ya maji hadi utakapoelekeza. Huko nitayatenganisha, nawe utaweza kuyachukua. Wewe utakidhi haja yangu kwa kunipatia chakula kwa ajili ya watu wa nyumbani mwangu.”
mine Folk skal bringe dem fra Libanon ned til Havet, og så skal jeg lade dem samle til Tømmerflåder på Havet og sende dem til det Sted, du anviser mig; der skal jeg lade dem skille ad, så at du kan lade dem hente. Men du vil da også opfylde mit Ønske og sende Fødevarer til mit Hof!"
10 Kwa njia hii Hiramu akampa Solomoni miti yote ya mierezi na magogo ya misunobari kama alivyohitaji,
Så sendte Hiram Salomo alt, hvad han ønskede af Ceder- og Cyprestræer;
11 naye Solomoni akampa Hiramu kori 20,000 za ngano kama chakula kwa ajili ya watu wa nyumbani mwake, pamoja na mafuta safi ya zeituni yaliyokamuliwa bathi 20,000. Solomoni aliendelea kumfanyia Hiramu hivyo mwaka baada ya mwaka.
og Salomo sendte Hiram 20 000 Kor Hvede til Underhold for hans Hof og 20 Kor Olie af knuste Oliven. Så meget sendte Salomo Hiram År efter År.
12 Bwana akampa Solomoni hekima, kama alivyomwahidi. Palikuwepo na uhusiano wa amani kati ya Hiramu na Solomoni, na wote wawili wakafanya mkataba.
Og HERREN gav Salomo Visdom, som han havde lovet ham; og der var Fred mellem Hiram og Salomo, og de sluttede Pagt med hinanden.
13 Mfalme Solomoni akakusanya wafanyakazi 30,000 kutoka Israeli yote.
Kong Salomo udskrev nu Hoveriarbejdere overalt i Israel, og Hoveriarbejderne udgjorde 30 000 Mand.
14 Akawapeleka Lebanoni kwa zamu za watu 10,000 kwa mwezi, hivyo walikaa Lebanoni kwa mwezi mmoja na miezi miwili nyumbani. Adoniramu ndiye alikuwa kiongozi wa shokoa.
Dem sendte han så til Libanon, et Hold på 10 000 om Måneden, således at de var en Måned på Libanon og to Måneder hjemme. Adoniram havd Tilsyn med Hoveriarbejderne.
15 Solomoni alikuwa na wachukuzi wa mizigo 70,000 na wachonga mawe 80,000 huko vilimani,
Salomo havde 70 000 Lastdragere og 80 000 Stenhuggere i Bjergene
16 pamoja na wasimamizi 3,300 ambao walisimamia kazi hiyo na kuwaongoza wafanyakazi.
foruden Overfogeder, der ledede Arbejdet, 3 300 Mand, som havde Opsyn med Folkene, der arbejdede.
17 Kwa amri ya mfalme walitoa kwenye machimbo ya mawe, mawe makubwa, yaliyo bora kwa kujengea msingi wa nyumba yaliyochongwa kwa ajili ya Hekalu.
På Kongens Bud brød de store Stenblokke, kostbare Sten til Templets Grundvold, Kvadersten;
18 Mafundi wa Solomoni, wa Hiramu na watu wa Gebali walikata na kuandaa mbao na mawe kwa ajili ya ujenzi wa Hekalu.
og Salomos og Hiroms Bygmestre og Folkene fra Gebal huggede dem til, og de gjorde Træstammerne og Stenene i Stand til Templets Opførelse.

< 1 Wafalme 5 >