< 1 Wafalme 4 >

1 Basi Mfalme Solomoni akatawala Israeli yote.
And king Solomon reigned over Israel.
2 Hawa ndio waliokuwa maafisa wake wakuu: Kuhani: Azaria mwana wa Sadoki;
And these [are] the princes which he had; Azarias son of Sadoc.
3 Elihorefu na Ahiya, wana wa Shisha: waandishi; Yehoshafati mwana wa Ahiludi: karani;
Eliaph, and Achia son of Seba, scribes; and Josaphat son of Achilud, recorder.
4 Benaya mwana wa Yehoyada: jemadari mkuu wa jeshi; Sadoki na Abiathari: makuhani;
And Banaeas son of Jodae over the host; and Sadoc and Abiathar [were] priests.
5 Azaria mwana wa Nathani: kiongozi wa maafisa wa wilaya; Zabudi mwana wa Nathani: kuhani na mshauri binafsi wa mfalme;
And Ornia the son of Nathan [was] over the officers; and Zabuth son of Nathan [was] the king's friend.
6 Ahishari: msimamizi wa jumba la kifalme; Adoniramu mwana wa Abda: msimamizi wa kazi za kulazimisha.
And Achisar was steward, and Eliac the [chief] steward; and Eliab the son of Saph [was] over the family: and Adoniram the son of Audon over the tribute.
7 Pia Solomoni alikuwa na watawala kumi na wawili wa wilaya katika Israeli yote, walioleta mahitaji kwa mfalme na kwa watu wa nyumbani kwa mfalme. Kila mmoja alitoa chakula kwa mwezi mmoja katika mwaka.
And Solomon had twelve officers over all Israel, to provide for the king and his household; each one's turn came to supply for a month in the year.
8 Majina yao ni haya: Ben-Huri: katika nchi ya vilima ya Efraimu;
And these [were] their names: Been the son of Or in the mount of Ephraim, one.
9 Ben-Dekeri: katika Makasi, Shaalbimu, Beth-Shemeshi na Elon-Bethhanani;
The son of Dacar, in Makes, and in Salabin, and Baethsamys, and Elon as far as Bethanan, one.
10 Ben-Hesedi: katika Arubothi (Soko na nchi yote ya Heferi zilikuwa zake);
The son of Esdi in Araboth; his [was] Socho, and all the land of Opher.
11 Ben-Abinadabu: katika Nafoth-Dori (alimwoa Tafathi binti Solomoni);
All Nephthador [belonged to] the son of Aminadab, Tephath daughter of Solomon was his wife, one.
12 Baana mwana wa Ahiludi: katika Taanaki na Megido, na katika Beth-Shani yote karibu na Sarethani chini ya Yezreeli, kuanzia Beth-Shani hadi Abel-Mehola kupita hadi Yokmeamu;
Bana son of Achiluth [had] Ithaanach, and Mageddo, and [his was] the whole house of San which was by Sesathan below Esrae, and from Bethsan as far as Sabelmaula, as far as Maeber Lucam, one.
13 Ben-Geberi: katika Ramoth-Gileadi (makao ya Yairi mwana wa Manase katika Gileadi ilikuwa miji yake, pamoja na wilaya ya Argobu katika Bashani na miji yake mikubwa sitini yenye kuzungukwa na kuta zenye makomeo ya shaba);
The son of Naber in Raboth Galaad, to him [fell] the lot of Ergab in Basan, sixty great cities with walls, and brazen bars, one.
14 Ahinadabu mwana wa Ido: katika Mahanaimu;
Achinadab son of Saddo, [had] Maanaim.
15 Ahimaasi: katika Naftali (alikuwa amemwoa Basemathi binti Solomoni);
Achimaas [was] in Nephthalim, and he took Basemmath daughter of Solomon to wife, one.
16 Baana mwana wa Hushai: katika Asheri na katika Bealothi;
Baana son of Chusi, in Aser and in Baaloth, one,
17 Yehoshafati mwana wa Parua: katika Isakari;
Josaphat son of Phuasud [was] in Issachar.
18 Shimei mwana wa Ela: katika Benyamini;
Semei son of Ela, in Benjamin.
19 Geberi mwana wa Uri: katika Gileadi (nchi ya Sihoni mfalme wa Waamori na nchi ya Ogu mfalme wa Bashani). Naye alikuwa ndiye mtawala pekee katika eneo hilo.
Gaber son of Adai in the land of Gad, [the land] of Seon king of Esebon, and of Og king of Basan, and one officer in the land of Juda.
20 Watu wa Yuda na Israeli walikuwa wengi kama mchanga wa pwani; walikula, wakanywa na kufurahi.
And thus the officers provided king Solomon: and [they execute] every one in his month all the orders for the table of the king, they omit nothing.
21 Mfalme Solomoni akatawala katika falme zote kuanzia Mto Frati hadi nchi ya Wafilisti, hadi kwenye mpaka wa Misri. Nchi hizi zilileta ushuru na zilikuwa chini ya Solomoni, siku zote za maisha yake.
And they carried the barley and the straw for the horses and the chariots to the place where the king might be, each according to his charge.
22 Mahitaji ya Solomoni ya kila siku yalikuwa kori thelathini za unga laini, kori sitini za unga wa kawaida.
And these [were] the requisite supplies for Solomon: in one day thirty measures of fine flour, and sixty measures of fine pounded meal,
23 Ngʼombe kumi wa zizini, ngʼombe ishirini wa malisho, kondoo na mbuzi mia moja, pamoja na ayala, paa, kulungu na kuku wazuri sana.
and ten choice calves, and twenty pastured oxen, and a hundred sheep, besides stags, and choice fatted does.
24 Kwa kuwa Solomoni alitawala falme zote magharibi ya mto, kuanzia Tifsa hadi Gaza, naye akawa na amani pande zote.
For he had dominion on this side the river, and he was at peace on all sides round about.
25 Wakati wa maisha ya Solomoni Yuda na Israeli, kuanzia Dani mpaka Beer-Sheba, wakaishi salama kila mtu chini ya mzabibu wake na chini ya mtini wake.
26 Solomoni alikuwa na mabanda 4,000 ya magari ya vita, na farasi 12,000.
27 Maafisa wa eneo hilo, kila mmoja katika mwezi wake, walileta mahitaji kwa ajili ya Mfalme Solomoni na wote waliokula mezani mwa mfalme. Walihakikisha kuwa hakuna chochote kilichopungua.
28 Pia walileta sehemu walizopangiwa za shayiri na majani kwa ajili ya farasi wavutao magari na farasi wengine mahali palipostahili.
29 Mungu akampa Solomoni hekima na akili kubwa, pia ufahamu mpana usiopimika kama mchanga ulioko pwani ya bahari.
And the Lord gave understanding to Solomon, and very much wisdom, and enlargement of heart, as the sand on the seashore.
30 Hekima ya Solomoni ilikuwa kubwa kuliko hekima ya watu wote wa Mashariki na kubwa kuliko hekima yote ya Misri.
And Solomon abounded greatly beyond the wisdom of all the ancients, and beyond all the wise men of Egypt.
31 Alikuwa na hekima kuliko kila mwandishi, akiwemo Ethani Mwezrahi: kuliko Hemani, Kalkoli na Darda, wana wa Maholi. Umaarufu wake ukaenea kwa mataifa yote yaliyomzunguka.
And he was wiser than all [other] men: and he was wiser than Gaethan the Zarite, and [than] Aenan, and [than] Chalcad and Darala the son of Mal.
32 Akanena mithali 3,000 na nyimbo zake zilikuwa 1,005.
And Solomon spoke three thousand proverbs, and his songs were five thousand.
33 Akaelezea maisha ya mimea kuanzia mwerezi wa Lebanoni hadi hisopo iotayo ukutani. Pia akafundisha kuhusu wanyama na ndege, wanyama wenye damu baridi, wakiwemo samaki.
And he spoke of trees, from the cedar in Libanus even to the hyssop which comes out through the wall: he spoke also of cattle, and of birds, and of reptiles, and of fishes.
34 Watu wa mataifa yote wakaja kusikiliza hekima ya Solomoni, waliotumwa na wafalme wote wa ulimwengu, waliokuwa wamesikia juu ya hekima yake.
And all the nations came to hear the wisdom of Solomon, and [ambassadors] from all the kings of the earth, as many as heard of his wisdom.

< 1 Wafalme 4 >