< 1 Wafalme 17 >

1 Basi Eliya, Mtishbi kutoka Tishbi katika Gileadi, akamwambia Ahabu, “Kama Bwana, Mungu wa Israeli, aishivyo, ambaye ninamtumikia, hapatakuwa na umande wala mvua katika miaka hii, isipokuwa kwa neno langu.”
Alors Elie Tisbite, [l'un de ceux] qui s'étaient habitués à Galaad, dit à Achab: L'Eternel le Dieu d'Israël, en la présence duquel je me tiens, est vivant, qu'il n'y aura ces années-ci ni rosée ni pluie, sinon à ma parole.
2 Kisha neno la Bwana likamjia Eliya, kusema,
Puis la parole de l'Eternel fut adressée à Elie, en disant:
3 “Ondoka hapa, elekea upande wa mashariki ukajifiche katika Kijito cha Kerithi, mashariki mwa Yordani.
Va-t'en d'ici, et tourne-toi vers l'Orient, et te cache au torrent de Kérith, qui est vis-à-vis du Jourdain.
4 Utakunywa maji kutoka kile kijito, nami nimeagiza kunguru wakulishe huko.”
Tu boiras du torrent, et j'ai commandé aux corbeaux de t'y nourrir.
5 Hivyo akafanya kile alichoambiwa na Bwana. Akaenda katika Kijito cha Kerithi, mashariki ya Yordani na akakaa huko.
Il partit donc, et fit selon la parole de l'Eternel; il s'en alla, dis-je, et demeura au torrent de Kérith, vis-à-vis du Jourdain.
6 Kunguru wakamletea mkate na nyama asubuhi na mkate na nyama jioni, naye akanywa maji kutoka kile kijito.
Et les corbeaux lui apportaient du pain et de la chair le matin, et du pain et de la chair le soir, et il buvait du torrent.
7 Baada ya muda, kile kijito kikakauka kwa sababu mvua haikuwa imenyesha katika nchi.
Mais il arriva qu'au bout de quelques jours le torrent tarit; parce qu'il n'y avait point eu de pluie au pays.
8 Kisha neno la Bwana likamjia, kusema,
Alors la parole de l'Eternel lui fut adressée, en disant:
9 “Ondoka, uende Sarepta ya Sidoni na ukae huko. Nimemwagiza mjane katika sehemu ile akupatie chakula.”
Lève-toi, [et] t'en va à Sarepta, qui est près de Sidon, et demeure-là. Voici, j'ai commandé là à une femme veuve de t'y nourrir.
10 Hivyo akaenda Sarepta. Alipofika kwenye lango la mji, mjane alikuwa huko akiokota kuni. Akamwita na kumwambia, “Naomba uniletee maji kidogo kwenye gudulia ili niweze kunywa.”
Il se leva donc, et s'en alla à Sarepta; et comme il fut arrivé à la porte de la ville, voilà, une femme veuve était là, qui amassait du bois; et il l'appela, et lui dit: Je te prie, apporte-moi un peu d'eau dans un vaisseau, et que je boive.
11 Alipokuwa anakwenda kumletea, akamwita akasema, “Tafadhali niletee pia kipande cha mkate.”
Elle s'en alla pour en prendre; et il la rappela, et lui dit: Je te prie, prends en ta main une bouchée de pain pour moi.
12 Akamjibu, “Hakika kama Bwana Mungu wako aishivyo, sina mkate wowote, isipokuwa konzi ya unga kwenye gudulia na mafuta kidogo kwenye chupa. Ninakusanya kuni chache nipeleke nyumbani na nikapike chakula kwa ajili yangu na mwanangu, ili kwamba tule, kiishe, tukafe.”
Mais elle répondit: L'Eternel ton Dieu est vivant, que je n'ai aucun gâteau; je n'ai que pleine ma main de farine dans une cruche, et un peu d'huile dans une fiole, et voici j'amasse deux bûches, puis je m'en irai, et je l'apprêterai pour moi et pour mon fils, et nous le mangerons; et après cela nous mourrons.
13 Eliya akamwambia, “Usiogope. Nenda nyumbani ukafanye kama ulivyosema. Lakini kwanza unitengenezee mimi mkate mdogo kutoka vile ulivyo navyo kisha uniletee na ndipo utayarishe chochote kwa ajili yako na mwanao.
Et Elie lui dit: Ne crains point; va, fais comme tu dis; mais fais m'en premièrement un petit gâteau, et apporte-le-moi, et puis tu en feras pour toi et pour ton fils.
14 Kwa kuwa hivi ndivyo asemavyo Bwana, Mungu wa Israeli: ‘Lile gudulia la unga halitakwisha wala ile chupa ya mafuta haitakauka hadi siku ile Bwana atakapoleta mvua juu ya nchi.’”
Car ainsi a dit l'Eternel le Dieu d'Israël: La farine qui est dans la cruche, ne défaudra point, et l'huile qui est dans la fiole ne défaudra point, jusqu'à ce que l'Eternel donne de la pluie sur la terre.
15 Akaondoka na kufanya kama Eliya alivyomwambia. Kwa hiyo kukawa na chakula kila siku kwa ajili ya Eliya, yule mwanamke na jamaa yake.
Elle s'en alla donc, et fit selon la parole d'Elie; et elle mangea, lui, et la famille de cette femme durant plusieurs jours.
16 Kwa kuwa lile gudulia la unga halikwisha na ile chupa ya mafuta haikukauka, sawasawa na lile neno la Bwana alilosema Eliya.
La farine de la cruche ne manqua point, et l'huile de la fiole ne tarit point, selon la parole que l'Eternel avait proférée par le moyen d'Elie.
17 Baada ya muda, mwana wa yule mwanamke mwenye nyumba akaugua. Hali yake ikaendelea kuwa mbaya sana, na hatimaye akaacha kupumua.
Après ces choses il arriva que le fils de la femme, maîtresse de la maison, devint malade; et la maladie fut si forte, qu'il expira.
18 Akamwambia Eliya, “Una nini dhidi yangu, ewe mtu wa Mungu? Umekuja ili kukumbushia dhambi yangu na kusababisha kifo cha mwanangu?”
Et elle dit à Elie: Qu'y a-t-il entre moi et toi, homme de Dieu? Es-tu venu chez moi pour rappeler en mémoire mon iniquité, et pour faire mourir mon fils?
19 Eliya akamjibu, “Nipe mwanao.” Eliya akampokea kutoka kifuani mwake, akambeba mpaka chumba cha juu alipokuwa anaishi, akamlaza kitandani mwake.
Et il lui dit: Donne-moi ton fils; et il le prit du sein de cette femme, et le porta dans la chambre haute où il demeurait, et le coucha sur son lit.
20 Kisha akamlilia Bwana, akasema “Ee Bwana Mungu wangu, je, pia umeleta msiba juu ya mjane huyu ninayeishi pamoja naye, kwa kusababisha mwanawe kufa?”
Puis il cria à l'Eternel, et dit: Eternel mon Dieu! as-tu donc tellement affligé cette veuve avec laquelle je demeure, que tu lui aies fait mourir son fils?
21 Kisha akajinyoosha juu ya kijana mara tatu na kumlilia Bwana, akisema, “Ee Bwana Mungu wangu, nakuomba roho ya huyu kijana imrudie!”
Et il s'étendit tout de son long sur l'enfant par trois fois, et cria à l'Eternel, et dit: Eternel mon Dieu! je te prie que l'âme de cet enfant r'entre dans lui.
22 Bwana akasikia kilio cha Eliya, na roho ya kijana ikamrudia, naye akafufuka.
Et l'Eternel exauça la voix d'Elie, et l'âme de l'enfant r'entra dans lui, et il recouvra la vie.
23 Eliya akamtwaa kijana na kumbeba kutoka chumbani mwake akamshusha kumpeleka kwenye nyumba. Akampa mama yake na kusema, “Tazama, mwanao yu hai!”
Et Elie prit l'enfant, et le fit descendre de la chambre haute dans la maison, et le donna à sa mère, en lui disant: Regarde, ton fils vit.
24 Ndipo yule mwanamke akamwambia Eliya, “Sasa ninajua kwamba wewe ni mtu wa Mungu, na kwamba neno la Bwana kutoka kinywani mwako ni kweli.”
Et la femme dit à Elie: Je connais maintenant, que tu es un homme de Dieu, et que la parole de l'Eternel, qui est dans ta bouche, est la vérité.

< 1 Wafalme 17 >