< 1 Wafalme 16 >

1 Ndipo neno la Bwana likamjia Yehu mwana wa Hanani dhidi ya Baasha, kusema:
Et la parole de l'Éternel fut adressée à Jéhu, fils de Hanani, contre Baesha, pour lui dire:
2 “Nilikuinua kutoka mavumbini na kukufanya kiongozi wa watu wangu Israeli, lakini ukaenenda katika njia za Yeroboamu na kusababisha watu wangu Israeli kutenda dhambi na kunikasirisha kwa dhambi zao.
Parce que je t'ai élevé de la poussière et que je t'ai établi conducteur de mon peuple d'Israël, et que tu as marché dans la voie de Jéroboam, et que tu as fait pécher mon peuple d'Israël, en m'irritant par leurs péchés,
3 Basi nitamwangamiza Baasha pamoja na nyumba yake, nami nitaifanya nyumba yako kama ile ya Yeroboamu mwanawe Nebati.
Voici, je m'en vais balayer Baesha et sa maison; et je rendrai ta maison semblable à la maison de Jéroboam, fils de Nébat.
4 Mbwa watawala watu wa Baasha watakaofia mjini na ndege wa angani watajilisha kwa wale watakaofia mashambani.”
Celui de la maison de Baesha qui mourra dans la ville, les chiens le mangeront; et celui des siens qui mourra dans les champs, sera mangé par les oiseaux des cieux.
5 Kwa matukio mengine ya utawala wa Baasha, aliyoyafanya na mafanikio yake, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
Le reste des actions de Baesha, et ce qu'il fit et ses exploits, cela n'est-il pas écrit au livre des Chroniques des rois d'Israël?
6 Baasha akalala na baba zake naye akazikwa huko Tirsa. Naye Ela mwanawe akawa mfalme baada yake.
Ainsi Baesha s'endormit avec ses pères, et il fut enseveli à Thirtsa; et Éla, son fils, régna à sa place.
7 Zaidi ya hayo, neno la Bwana likamjia Baasha pamoja na nyumba yake kupitia kwa nabii Yehu mwana wa Hanani, kwa sababu ya maovu yote aliyokuwa ametenda machoni pa Bwana, akamkasirisha kwa mambo aliyotenda, na kuwa kama nyumba ya Yeroboamu, na pia kwa sababu aliiangamiza.
Mais, par le prophète Jéhu, fils de Hanani, la parole de l'Éternel avait été adressée à Baesha et à sa maison, tant à cause de tout le mal qu'il avait fait devant l'Éternel, en l'irritant par l'œuvre de ses mains et en devenant comme la maison de Jéroboam, que parce qu'il l'avait détruite.
8 Katika mwaka wa ishirini na sita wa utawala wa Asa mfalme wa Yuda, Ela mwana wa Baasha akawa mfalme wa Israeli, naye akatawala huko Tirsa kwa miaka miwili.
La vingt-sixième année d'Asa, roi de Juda, Éla, fils de Baesha, commença à régner sur Israël; et il régna deux ans à Thirtsa.
9 Zimri, mmoja wa maafisa wake, aliyekuwa na amri juu ya nusu ya magari yake ya vita, akafanya hila mbaya dhidi ya Ela. Wakati huo Ela alikuwa Tirsa, akilewa katika nyumba ya Arsa, mtu aliyekuwa msimamizi wa jumba la kifalme huko Tirsa.
Et Zimri, son serviteur, capitaine de la moitié des chars, fit une conspiration contre lui, lorsqu'il était à Thirtsa, buvant et s'enivrant dans la maison d'Artsa, son maître d'hôtel, à Thirtsa.
10 Zimri akaingia, akampiga na kumuua katika mwaka wa ishirini na saba wa utawala wa Asa mfalme wa Yuda. Kisha Zimri akaingia mahali pake kuwa mfalme.
Zimri vint donc, le frappa et le tua, la vingt-septième année d'Asa, roi de Juda; et il régna à sa place.
11 Mara tu alipoanza kutawala na kuketi juu ya kiti cha ufalme, aliua jamaa yote ya Baasha. Hakumwacha mwanaume hata mmoja, akiwa ni ndugu au rafiki.
Dès qu'il fut roi et qu'il fut assis sur son trône, il frappa toute la maison de Baesha; il extermina tout ce qui lui appartenait, et ses parents, et ses amis.
12 Hivyo Zimri akaangamiza jamaa yote ya Baasha, kulingana na neno la Bwana lililonenwa dhidi ya Baasha kupitia nabii Yehu:
Ainsi Zimri détruisit toute la maison de Baesha, selon la parole que l'Éternel avait prononcée contre Baesha, par Jéhu, le prophète;
13 kwa sababu ya dhambi zote Baasha na mwanawe Ela walizokuwa wametenda na wakasababisha Israeli kuzitenda, basi wakamkasirisha Bwana, Mungu wa Israeli kwa sanamu zao zisizofaa.
A cause de tous les péchés de Baesha et des péchés d'Éla, son fils, qu'ils avaient commis et fait commettre à Israël, irritant l'Éternel, le Dieu d'Israël, par leurs idoles.
14 Kwa matukio mengine ya utawala wa Ela, na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
Le reste des actions d'Éla, tout ce qu'il fit, n'est-il pas écrit au livre des Chroniques des rois d'Israël?
15 Katika mwaka wa ishirini na saba wa utawala wa Asa mfalme wa Yuda, Zimri akatawala huko Tirsa siku saba. Jeshi lilikuwa limepiga kambi karibu na Gibethoni, mji wa Wafilisti.
La vingt-septième année d'Asa, roi de Juda, Zimri régna sept jours à Thirtsa. Or, le peuple était campé contre Guibbéthon qui était aux Philistins.
16 Wakati Waisraeli waliokuwa kambini waliposikia kuwa Zimri alikuwa amefanya hila mbaya dhidi ya mfalme na kumuua, wakamtangaza Omri, jemadari wa jeshi, kuwa mfalme wa Israeli siku iyo hiyo huko kambini.
Et le peuple qui était campé là entendit qu'on disait: Zimri a fait une conspiration, et même il a tué le roi; et, en ce même jour, tout Israël établit dans le camp pour roi, Omri, capitaine de l'armée d'Israël.
17 Ndipo Omri na Waisraeli wote pamoja naye wakaondoka Gibethoni na kuizingira Tirsa.
Et Omri et tout Israël avec lui montèrent de Guibbéthon, et ils assiégèrent Thirtsa.
18 Wakati Zimri alipoona kuwa mji umechukuliwa, alikwenda ndani ya ngome ya jumba la kifalme na kulichoma moto jumba la kifalme na kujiteketeza ndani yake. Kwa hiyo akafa,
Mais quand Zimri vit que la ville était prise, il monta au lieu le plus haut de la maison royale, et il brûla sur lui la maison royale, et mourut,
19 kwa sababu ya dhambi alizofanya, akitenda maovu machoni pa Bwana na kuenenda katika njia za Yeroboamu na katika dhambi alizofanya na kusababisha Israeli kuzifanya.
A cause des péchés qu'il avait commis, en faisant ce qui est mal aux yeux de l'Éternel, en imitant la conduite de Jéroboam et le péché qu'il avait fait commettre à Israël.
20 Kwa matukio mengine ya utawala wa Zimri, na uasi alioutenda, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
Quant au reste des actions de Zimri, et la conspiration qu'il trama, n'est-ce pas écrit au livre des Chroniques des rois d'Israël?
21 Ndipo watu wa Israeli wakagawanyika katika makundi mawili, nusu wakamuunga mkono Tibni mwana wa Ginathi ili awe mfalme na nusu nyingine wakamuunga mkono Omri.
Alors le peuple d'Israël se divisa en deux partis: la moitié du peuple suivait Thibni, fils de Guinath, pour le faire roi, et l'autre moitié suivait Omri.
22 Lakini wafuasi wa Omri wakajionyesha wenye nguvu kuliko wale wa Tibni mwana wa Ginathi. Hivyo Tibni akafa na Omri akawa mfalme.
Mais le peuple qui suivait Omri fut plus fort que le peuple qui suivait Thibni, fils de Guinath; et Thibni mourut, et Omri régna.
23 Katika mwaka wa thelathini na moja wa utawala wa Asa mfalme wa Yuda, Omri akawa mfalme wa Israeli, naye akatawala kwa miaka kumi na miwili, sita kati ya hiyo katika Tirsa.
La trente et unième année d'Asa, roi de Juda, Omri commença à régner sur Israël; et il régna douze ans. Il régna six ans à Thirtsa.
24 Alinunua kilima cha Samaria kutoka kwa Shemeri kwa talanta mbili za fedha na akajenga mji juu ya hicho kilima, akiuita Samaria, kutokana na Shemeri, jina la mmiliki wa kwanza wa kilima hicho.
Puis il acheta de Shémer la montagne de Samarie, pour deux talents d'argent; et il bâtit sur cette montagne. Et il nomma la ville qu'il bâtit Samarie, du nom de Shémer, seigneur de la montagne.
25 Lakini Omri akatenda maovu machoni pa Bwana na kutenda dhambi kuliko wote waliomtangulia.
Et Omri fit ce qui est mal aux yeux de l'Éternel; il fit pis que tous ceux qui avaient été avant lui.
26 Akaenenda katika njia zote za Yeroboamu mwana wa Nebati na katika dhambi zake, ambazo alisababisha Israeli kutenda, hivyo basi wakamkasirisha Bwana, Mungu wa Israeli kwa sanamu zao zisizofaa.
Il imita toute la conduite de Jéroboam, fils de Nébat, et le péché qu'il avait fait commettre aux Israélites, irritant l'Éternel, le Dieu d'Israël, par leurs idoles.
27 Kwa matukio mengine ya utawala wa Omri, yale aliyofanya na vitu alivyovifanikisha, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
Le reste des actions d'Omri, tout ce qu'il fit et ses exploits, cela n'est-il pas écrit au livre des Chroniques des rois d'Israël?
28 Omri akalala pamoja na baba zake na akazikwa huko Samaria. Ahabu mwanawe akatawala mahali pake.
Et Omri s'endormit avec ses pères, et fut enseveli à Samarie; et Achab, son fils, régna à sa place.
29 Katika mwaka wa thelathini na nane wa utawala wa Asa mfalme wa Yuda, Ahabu mwana wa Omri akawa mfalme wa Israeli, naye akatawala Israeli akiwa Samaria kwa miaka ishirini na miwili.
Achab, fils d'Omri, commença à régner sur Israël la trente-huitième année d'Asa, roi de Juda. Et Achab, fils d'Omri, régna sur Israël, à Samarie, vingt-deux ans.
30 Ahabu mwana wa Omri akafanya maovu zaidi machoni mwa Bwana kuliko yeyote aliyewatangulia.
Et Achab, fils d'Omri, fit ce qui est mal aux yeux de l'Éternel, plus que tous ceux qui avaient été avant lui.
31 Kama vile haikutosha kuishi kama Yeroboamu mwana wa Nebati, akamwoa Yezebeli binti wa Ethbaali, mfalme wa Wasidoni, naye akaanza kumtumikia Baali na kumwabudu.
Et comme si c'eût été peu de chose pour lui d'imiter les péchés de Jéroboam, fils de Nébat, il prit pour femme Jésabel, fille d'Ethbaal, roi des Sidoniens; puis il alla et servit Baal, et se prosterna devant lui.
32 Akajenga madhabahu kwa ajili ya Baali katika hekalu la Baali lile alilolijenga huko Samaria.
Et il dressa un autel à Baal dans la maison de Baal, qu'il bâtit à Samarie.
33 Pia Ahabu akatengeneza nguzo ya Ashera na kufanya mengi ili kumkasirisha Bwana, Mungu wa Israeli, kuliko walivyofanya wafalme wote wa Israeli waliomtangulia.
Et Achab fit aussi une idole d'Ashéra. Et Achab fit plus encore que tous les rois d'Israël qui avaient été avant lui, pour irriter l'Éternel, le Dieu d'Israël.
34 Katika wakati wa Ahabu, Hieli, Mbetheli, akaijenga upya Yeriko. Aliweka misingi yake kwa gharama ya mzaliwa wake wa kwanza Abiramu, na kuweka malango yake kwa gharama ya mwanawe mdogo Segubu, kulingana na neno la Bwana alilosema kupitia Yoshua mwana wa Nuni.
De son temps, Hiel de Béthel bâtit Jérico. Il la fonda sur Abiram, son aîné, et il en posa les portes sur Ségub, son dernier-né, selon la parole que l'Éternel avait prononcée par Josué, fils de Nun.

< 1 Wafalme 16 >