< 1 Wafalme 14 >

1 Wakati ule Abiya mwana wa Yeroboamu akaugua,
En ce temps-là, Abija, fils de Jéroboam, devint malade.
2 naye Yeroboamu akamwambia mke wake, “Nenda ukajibadilishe, ili watu wasijue kwamba wewe ni mke wa Yeroboamu. Kisha uende Shilo. Nabii Ahiya yuko huko, yule aliyeniambia kuwa nitakuwa mfalme juu ya watu hawa.
Et Jéroboam dit à sa femme: Lève-toi maintenant, et déguise-toi, qu'on ne reconnaisse pas que tu es la femme de Jéroboam, et va-t'en à Silo; là est Achija, le prophète; c'est lui qui a dit que je serais roi sur ce peuple.
3 Chukua mikate kumi, maandazi kadhaa na gudulia la asali na umwendee. Atakuambia kitakachotokea kwa kijana.”
Et prends en ta main dix pains, des gâteaux, et un vase de miel, et entre chez lui; il te déclarera ce qui doit arriver à l'enfant.
4 Basi mke wa Yeroboamu akafanya kama alivyosema mumewe, akaenda kwenye nyumba ya Ahiya huko Shilo. Wakati huu Ahiya alikuwa kipofu naye alishindwa kuona kwa sababu ya umri wake.
Et la femme de Jéroboam fit ainsi; elle se leva, et s'en alla à Silo, et elle entra dans la maison d'Achija. Or, Achija ne pouvait voir, car ses yeux étaient obscurcis par la vieillesse.
5 Lakini Bwana alikuwa amemwambia Ahiya, “Mke wa Yeroboamu anakuja kukuuliza kuhusu mwanawe, kwa kuwa ni mgonjwa, nawe utamjibu hivi na hivi. Atakapowasili, atajifanya kuwa ni mtu mwingine.”
Mais l'Éternel avait dit à Achija: Voici la femme de Jéroboam qui vient pour s'enquérir de toi touchant son fils, parce qu'il est malade. Tu lui diras telles et telles choses. Quand elle entrera, elle fera semblant d'être quelque autre.
6 Hivyo Ahiya aliposikia kishindo cha hatua zake mlangoni, akasema, “Karibu ndani, mke wa Yeroboamu. Kwa nini kujibadilisha? Nimetumwa kwako nikiwa na habari mbaya.
Aussitôt donc qu'Achija eut entendu le bruit de ses pas, comme elle entrait par la porte, il dit: Entre, femme de Jéroboam; pourquoi fais-tu semblant d'être quelque autre? J'ai mission de t'annoncer des choses dures.
7 Nenda, ukamwambie Yeroboamu kwamba hivi ndivyo asemavyo Bwana, Mungu wa Israeli: ‘Nilikuinua miongoni mwa watu na kukufanya kiongozi juu ya watu wangu Israeli.
Va, dis à Jéroboam: Ainsi a dit l'Éternel, le Dieu d'Israël: Parce que je t'ai élevé du milieu du peuple et que je t'ai établi pour conducteur de mon peuple d'Israël;
8 Nikararua ufalme kutoka kwa nyumba ya Daudi na kukupa wewe, lakini hukuwa kama mtumishi wangu Daudi, ambaye aliyashika maagizo yangu na kunifuata kwa moyo wake wote, akifanya tu lile lililokuwa sawa machoni pangu.
Et que j'ai déchiré le royaume de la maison de David, et te l'ai donné; mais que tu n'as point été comme David, mon serviteur, qui a gardé mes commandements et marché après moi de tout son cœur, ne faisant que ce qui est droit devant moi;
9 Umefanya maovu mengi kuliko wote waliokutangulia. Umejitengenezea miungu mingine, sanamu za chuma, umenighadhibisha na kunitupa nyuma yako.
Et que tu as fait plus mal que tous ceux qui ont été avant toi; que tu t'en es allé et t'es fait d'autres dieux et des images de fonte, pour m'irriter, et que tu m'as rejeté derrière ton dos;
10 “‘Kwa sababu ya hili, nitaleta maafa juu ya nyumba ya Yeroboamu. Nitakatilia mbali kutoka kwa Yeroboamu kila mzaliwa wa mwisho wa kiume katika Israeli, mtumwa au mtu huru. Nitachoma nyumba ya Yeroboamu mpaka iteketee yote kama mtu achomaye kinyesi.
A cause de cela, voici, je vais faire venir du mal sur la maison de Jéroboam; je retrancherai ce qui appartient à Jéroboam, jusqu'à un seul homme, tant ce qui est serré que ce qui est abandonné en Israël; et je raclerai la maison de Jéroboam comme on racle le fumier, jusqu'à ce qu'il n'en reste plus.
11 Mbwa watawala wale walio wa nyumba ya Yeroboamu watakaofia ndani ya mji na ndege wa angani watajilisha kwa wale watakaofia mashambani. Bwana amesema!’
Celui de la maison de Jéroboam qui mourra dans la ville, les chiens le mangeront; et celui qui mourra aux champs sera mangé par les oiseaux des cieux; car l'Éternel a parlé.
12 “Kukuhusu wewe, rudi nyumbani. Wakati utakapotia mguu katika mji wako, kijana atakufa.
Toi donc, lève-toi et va-t'en en ta maison; aussitôt que tes pieds entreront dans la ville, l'enfant mourra.
13 Israeli yote itamwombolezea na kumzika. Kwa sababu ni yeye pekee wa nyumba ya Yeroboamu atakayezikwa, kwa sababu ni yeye peke yake ndani ya nyumba ya Yeroboamu ambaye Bwana, Mungu wa Israeli, ameona kitu chema kwake.
Et tout Israël mènera deuil sur lui et l'ensevelira; car lui seul, de la maison de Jéroboam, entrera au tombeau; parce que l'Éternel, le Dieu d'Israël, a trouvé quelque chose de bon en lui seul, de toute la maison de Jéroboam.
14 “Bwana atajiinulia mwenyewe mfalme juu ya Israeli ambaye ataikatilia mbali jamaa ya Yeroboamu. Siku ndiyo hii! Nini? Naam, hata sasa hivi.
Et l'Éternel établira sur Israël un roi qui, en ce jour-là, retranchera la maison de Jéroboam. Et quoi? Même dans peu.
15 Naye Bwana ataipiga Israeli, hata iwe kama unyasi unaosukwasukwa juu ya maji. Ataingʼoa Israeli kutoka nchi hii nzuri aliyowapa baba zao na kuwatawanya ngʼambo ya Mto Frati, kwa sababu wamemghadhibisha Bwana kwa kutengeneza nguzo za Ashera
Et l'Éternel frappera Israël, comme quand le roseau est agité dans l'eau; et il arrachera Israël de dessus ce bon pays qu'il a donné à leurs pères; et il les dispersera au delà du fleuve, parce qu'ils se sont fait des emblèmes d'Ashéra, irritant l'Éternel.
16 Naye atawaacha Israeli kwa ajili ya makosa ya Yeroboamu aliyoyatenda na kusababisha Israeli kuyatenda.”
Et il livrera Israël, à cause des péchés que Jéroboam a commis et qu'il a fait commettre à Israël.
17 Kisha mke wa Yeroboamu akainuka, akaondoka kwenda Tirsa. Mara alipokanyaga kizingiti cha mlango, kijana akafa.
Alors la femme de Jéroboam se leva et s'en alla; et elle vint à Thirtsa. Et comme elle mettait le pied sur le seuil de la maison, le jeune garçon mourut;
18 Wakamzika na Israeli yote ikamwombolezea, kama Bwana alivyokuwa amesema kupitia mtumishi wake, nabii Ahiya.
Et on l'ensevelit, et tout Israël mena deuil sur lui, selon la parole que l'Éternel avait prononcée par son serviteur Achija, le prophète.
19 Matukio mengine ya utawala wa Yeroboamu, vita vyake na jinsi alivyotawala, vimeandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli.
Quant au reste des actions de Jéroboam, comment il fit la guerre et comment il régna, voici, cela est écrit au livre des Chroniques des rois d'Israël.
20 Yeroboamu akawatawala kwa miaka ishirini na miwili, kisha akalala na baba zake. Naye Nadabu mwanawe akawa mfalme baada yake.
Or, le temps que régna Jéroboam fut de vingt-deux ans; puis il s'endormit avec ses pères, et Nadab son fils régna à sa place.
21 Rehoboamu mwana wa Solomoni alikuwa mfalme wa Yuda. Alikuwa na umri wa miaka arobaini na moja alipoanza kutawala, naye akatawala miaka kumi na saba huko Yerusalemu, mji ambao Bwana alikuwa ameuchagua kutoka makabila yote ya Israeli ili apate kuliweka humo Jina lake. Mama yake aliitwa Naama, ambaye alikuwa Mwamoni.
Or Roboam, fils de Salomon, régna en Juda. Il avait quarante et un ans quand il commença à régner, et il régna dix-sept ans à Jérusalem, la ville que l'Éternel avait choisie d'entre toutes les tribus d'Israël, pour y mettre son nom. Sa mère s'appelait Naama, l'Ammonite.
22 Yuda wakatenda maovu machoni pa Bwana. Kwa dhambi walizotenda wakachochea hasira yake yenye wivu zaidi kuliko baba zao walivyofanya.
Et Juda fit ce qui est mal aux yeux de l'Éternel; et, par les péchés qu'ils commirent, ils émurent sa jalousie plus que leurs pères n'avaient jamais fait.
23 Pia wakajijengea mahali pa juu pa kuabudia miungu, mawe ya kuabudiwa na nguzo za Ashera juu ya kila kilima kilichoinuka na kila mti uliotanda.
Car ils se bâtirent aussi des hauts lieux, avec des statues et des emblèmes d'Ashéra, sur toutes les hautes collines et sous tous les arbres verts.
24 Walikuwepo hata wanaume mahanithi wa mahali pa ibada za sanamu katika nchi; watu wakajiingiza katika kutenda machukizo ya mataifa ambayo Bwana aliyafukuza mbele ya Waisraeli.
Il y eut même des prostitués dans le pays; ils imitèrent toutes les abominations des nations que l'Éternel avait chassées devant les enfants d'Israël.
25 Katika mwaka wa tano wa utawala wa Mfalme Rehoboamu, Shishaki mfalme wa Misri akashambulia Yerusalemu.
Or, il arriva la cinquième année du roi Roboam, que Shishak, roi d'Égypte, monta contre Jérusalem;
26 Akachukua hazina za Hekalu la Bwana na hazina za jumba la kifalme. Akachukua kila kitu, pamoja na zile ngao zote za dhahabu ambazo Solomoni alikuwa amezitengeneza.
Il prit les trésors de la maison de l'Éternel, et les trésors de la maison royale; il prit tout; il prit aussi tous les boucliers d'or que Salomon avait faits.
27 Kwa hiyo Mfalme Rehoboamu akatengeneza ngao za shaba badala ya zile za dhahabu na kuzikabidhi kwa majemadari wa ulinzi wa zamu kwenye ingilio la jumba la mfalme.
Et le roi Roboam fit des boucliers d'airain à la place de ceux-là et les mit entre les mains des chefs des coureurs, qui gardaient la porte de la maison du roi.
28 Kila wakati mfalme alipokwenda katika Hekalu la Bwana, walinzi walizichukua hizo ngao, na baadaye walizirudisha kwenye chumba cha ulinzi.
Et, quand le roi entrait dans la maison de l'Éternel, les coureurs les portaient; puis ils les rapportaient dans la chambre des coureurs.
29 Kwa matukio mengine ya utawala wa Rehoboamu na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
Quant au reste des actions de Roboam et tout ce qu'il fit, n'est-ce pas écrit au livre des Chroniques des rois de Juda?
30 Kulikuwa na vita vinavyoendelea kati ya Rehoboamu na Yeroboamu.
Or, il y eut toujours guerre entre Roboam et Jéroboam.
31 Naye Rehoboamu akalala na baba zake, na akazikwa pamoja nao katika Mji wa Daudi. Mama yake aliitwa Naama, ambaye alikuwa Mwamoni. Naye Abiya mwanawe akawa mfalme baada yake.
Et Roboam s'endormit avec ses pères; et il fut enseveli avec eux dans la cité de David. Sa mère s'appelait Naama, l'Ammonite; et Abijam, son fils, régna à sa place.

< 1 Wafalme 14 >