< 1 Nyakati 9 >

1 Waisraeli wote waliorodheshwa katika koo zilizoandikwa kwenye kitabu cha wafalme wa Israeli. Watu wa Yuda walichukuliwa mateka kwenda Babeli kwa sababu ya kukosa uaminifu kwa Mungu.
Ainsi tous ceux d'Israël furent rangés par généalogie, et voilà, ils sont écrits au Livre des Rois d'Israël; et ceux de Juda furent transportés à Babylone à cause de leurs péchés.
2 Basi watu wa kwanza kurudi kukaa kwenye milki zao katika miji yao walikuwa baadhi ya Waisraeli, makuhani, Walawi na watumishi wa Hekalu.
Mais ce sont ici les premiers qui habitèrent dans leurs possessions, [et] dans leurs villes, tant d'Israël, que des Sacrificateurs, des Lévites, et des Néthiniens.
3 Wale waliotoka Yuda, Benyamini, Efraimu na Manase ambao waliishi Yerusalemu walikuwa:
Et il demeura dans Jérusalem, des enfants de Juda, des enfants de Benjamin, et des enfants d'Ephraïm et de Manassé.
4 Uthai mwana wa Amihudi, mwana wa Omri, mwana wa Imri, mwana wa Bani, wa wana wa Peresi, mwana wa Yuda.
Huthaï fils d'Hammihud, fils de Homri, fils d'Imri, fils de Bani, des enfants de Pharez, fils de Juda.
5 Wazao wa Washiloni waliorudi ni: Asaya mzaliwa wa kwanza na wanawe.
Et des Silonites, Hasaïa le premier-né, et ses fils.
6 Kwa wana wa Zera: Yeueli. Watu wa Yuda jumla yao walikuwa watu 690.
Et des enfants de Zara, Jéhuël, et ses frères, six cent quatre-vingt et dix.
7 Kwa Benyamini walikuwa: Salu mwana wa Meshulamu, mwana wa Hodavia, mwana wa Hasenua;
Et des enfants de Benjamin, Sallu fils de Mésullam, fils de Hodavia, fils de Hassenua.
8 Ibneya mwana wa Yerohamu, Ela mwana wa Uzi, mwana wa Mikri; na Meshulamu mwana wa Shefatia, mwana wa Reueli, mwana wa Ibniya.
Et Jibnéja fils de Jéroham, et Ela fils de Huzi, fils de Micri; et Mésullam fils de Saphatia, fils de Réhuël, fils de Jibnija.
9 Watu kutoka Benyamini kama walivyoorodheshwa katika koo zao jumla yao ni 956. Watu hawa wote walikuwa viongozi wa jamaa zao.
Leurs frères, selon leurs générations, furent neuf cent cinquante-six. Tous ces hommes-là furent chefs des pères, selon la maison de leurs pères.
10 Wa jamaa za makuhani walikuwa: Yedaya, Yehoyaribu na Yakini;
Et des Sacrificateurs, Jédahja, Jéhojarib, et Jakin.
11 Azaria mwana wa Hilkia, mwana wa Meshulamu, mwana wa Sadoki, mwana wa Merayothi, mwana wa Ahitubu aliyekuwa afisa kiongozi wa nyumba ya Mungu.
Et Hazaria fils de Hilkija, fils de Mésullam, fils de Tsadoc, fils de Mérajoth, fils d'Ahitub, conducteur de la maison de Dieu.
12 Adaya mwana wa Yerohamu, mwana wa Pashuri, mwana wa Malkiya; Maasai, mwana wa Adieli, mwana wa Yahzera, mwana wa Meshulamu, mwana wa Meshilemithi, mwana wa Imeri.
Et Hadaja fils de Jéroham, fils de Pashur, fils de Malkija; et Mahasaï, fils d'Hadiël, fils de Jahzéra, fils de Mésullam, fils de Mésillémith, fils d'Immer.
13 Makuhani waliokuwa viongozi wa jamaa zao walikuwa 1,760. Walikuwa watu wenye uwezo, waliowajibika kuhudumu katika nyumba ya Mungu.
Et leurs frères chefs en la maison de leurs pères, mille sept cent soixante hommes, forts et vaillants, pour faire l'œuvre du service de la maison de Dieu.
14 Jamaa za Walawi walikuwa: Shemaya, mwana wa Hashubu, mwana wa Azrikamu, mwana wa Hashabia, wa wana wa Merari.
Et les Lévites, Sémahja, fils de Hasub, fils de Hazrikam, fils de Hasabia, des enfants de Mérari,
15 Bakbakari, Hereshi, Galali na Matania mwana wa Mika, mwana wa Zikri, mwana wa Asafu.
Bakbakar, Hérès, et Galal; et Mattania fils de Mica, fils de Zicri, fils d'Asaph.
16 Obadia mwana wa Shemaya, mwana wa Galali, mwana wa Yeduthuni. Berekia mwana wa Asa, mwana wa Elikana, ambao waliishi katika vijiji vya Wanetofathi.
Et Hobadia fils de Sémathia, fils de Galal, fils de Jéduthun; et Bérécia, fils d'Asa, fils d'Elkana, qui habita dans les bourgs des Nétophatiens.
17 Mabawabu katika Hekalu la Bwana waliorudi walikuwa: Shalumu, Akubu, Talmoni, Ahimani na ndugu zao. Shalumu alikuwa mlinzi wao mkuu.
Et quant aux portiers, Sallum, Hakkub, Talmon, et Ahiman, et leurs frères; [mais] Sallum était le chef;
18 Walikuwa wamewekwa katika lango la mfalme lililokuwa upande wa mashariki, mpaka wakati huu. Hawa walikuwa mabawabu wa kutoka kwenye kambi ya Walawi.
[Et il l'a été] jusqu'à maintenant, [ayant la charge] de la porte du Roi vers l'Orient. Ceux-là furent portiers selon les familles des enfants de Lévi.
19 Shalumu mwana wa Kore, mwana wa Ebiasafu, mwana wa Kora, pamoja na mabawabu wenzake kutoka jamaa yake ya Kora waliwajibika kulinda malango ya Hema, kama vile baba zao walivyokuwa wamewajibika kulinda ingilio la Maskani ya Bwana.
Et Sallum fils de Coré, fils d'Ebiasaph, fils de Coré, et ses frères Corites, selon la maison de son père, avaient la charge de l'ouvrage du service, gardant les vaisseaux du Tabernacle, comme leurs pères en avaient gardé l'entrée au camp de l'Eternel,
20 Hapo zamani Finehasi mwana wa Eleazari alikuwa kiongozi wa mabawabu, naye Bwana alikuwa pamoja naye:
Lorsque Phinées, fils d'Eléazar, fut établi chef sur eux en la présence de l'Eternel, qui était avec lui.
21 Zekaria mwana wa Meshelemia alikuwa bawabu katika ingilio la Hema la Kukutania.
Et Zacharie fils de Mésélémia [était] le portier de l'entrée du Tabernacle d'assignation.
22 Jumla ya waliochaguliwa kuwa mabawabu katika sakafu za kupuria nafaka walikuwa watu 212. Waliandikishwa kwa koo zao kwenye vijiji vyao. Mabawabu hawa waliwekwa katika nafasi zao za kuaminiwa na Daudi pamoja na mwonaji Samweli.
Ce sont là tous ceux qui furent choisis pour être les portiers des entrées, deux cent et douze; qui furent mis selon les familles par généalogie, selon leurs bourgs, comme David et Samuël le Voyant les avaient établis dans leur office.
23 Wao na wazao wao walikuwa viongozi wa kulinda malango ya nyumba ya Bwana, nyumba iliyoitwa Hema.
Eux, [dis-je], et leurs enfants furent établis sur les portes de la maison de l'Eternel, qui est la maison du Tabernacle, pour y faire la garde.
24 Mabawabu walikuwa pande zote nne: mashariki, magharibi, kaskazini na kusini.
Les portiers devaient être vers les quatre vents; [savoir], vers l'Orient et l'Occident, vers le Septentrion et le Midi.
25 Ndugu zao katika vijiji vyao walikuwa wakija mara kwa mara na kuwasaidia katika kazi zao kwa vipindi mbalimbali vya siku saba.
Et leurs frères, qui étaient dans leurs bourgs, devaient venir avec eux de sept jours en sept jours, de temps en temps.
26 Lakini mabawabu wanne wakuu, waliokuwa Walawi, walikabidhiwa wajibu kwa ajili ya vyumba na hazina katika nyumba ya Mungu.
Car selon cet ordre, il y avait toujours quatre maîtres-portiers, Lévites, qui étaient même commis sur les chambres, et sur les trésors de la maison de Dieu.
27 Walikesha mahali walipowekwa kuizunguka nyumba ya Mungu, kwa sababu iliwapasa kuilinda. Pia walitunza funguo kwa ajili ya kufungua mlango kila siku asubuhi.
Et ils se tenaient la nuit tout autour de la maison de Dieu; car la garde leur en appartenait, et ils avaient la charge de l'ouvrir tous les matins.
28 Baadhi yao walikuwa viongozi wa kutunza vifaa vilivyotumika katika huduma ndani ya Hekalu; walivihesabu kila vilipoingizwa ndani na kila vilipotolewa.
Il y en avait aussi quelques-uns d'entr'eux commis sur les vaisseaux du service; car on les portait dans le [Temple], par compte, et on les en tirait par compte.
29 Wengine walipangiwa kutunza mapambo na vifaa vingine vya patakatifu, pamoja na unga, divai, mafuta, uvumba na vikolezo.
Il y en avait aussi qui étaient commis sur les autres ustensiles, et sur tous les vaisseaux consacrés, et sur la fleur de farine, et sur le vin, et sur l'huile, et sur l'encens, et sur les choses aromatiques.
30 Lakini baadhi ya makuhani walifanya kazi ya kuchanganya vikolezo.
Mais ceux qui faisaient les parfums des choses aromatiques, étaient des enfants des Sacrificateurs.
31 Mlawi aliyeitwa Matithia, mwana mzaliwa wa kwanza wa Shalumu, wa ukoo wa Kora, alikabidhiwa wajibu kwa ajili ya kuoka mikate ya sadaka.
Et Mattitia, d'entre les Lévites, premier-né de Sallum, Corite, avait la charge de ce qui se faisait avec les plaques.
32 Baadhi ya ndugu zao wa ukoo wa Kohathi walikuwa viongozi wa kuandaa mikate ya Wonyesho kwa ajili ya kila Sabato, mikate iliyokuwa inawekwa mezani.
Et il y en avait d'entre les enfants des Kéhathites, leurs frères, qui avaient la charge du pain de proposition pour l'apprêter chaque Sabbat.
33 Wale waliokuwa waimbaji, viongozi wa jamaa za Walawi, waliishi katika vyumba vya Hekalu, nao hawakufanya shughuli nyingine yoyote kwa sababu iliwapasa kuwajibika kwa kazi hiyo usiku na mchana.
Et d'entr'eux il y avait aussi des chantres, chefs des pères des Lévites, qui demeuraient dans les chambres, sans avoir autre charge, parce qu'ils devaient être en fonction le jour et la nuit.
34 Hawa wote walikuwa viongozi wa jamaa za Walawi, wakuu kama walivyoorodheshwa katika koo zao, nao waliishi Yerusalemu.
Ce sont là les chefs des pères des Lévites, selon leurs familles; ils furent chefs, et ils habitèrent à Jérusalem.
35 Yeieli alikuwa baba yake Gibeoni naye aliishi huko Gibeoni. Mke wake aliitwa Maaka,
Or Jéhiël, le père de Gabaon, habita à Gabaon; et le nom de sa femme était Mahaca.
36 mwanawe mzaliwa wa kwanza alikuwa Abdoni, akafuatiwa na Suri, Kishi, Baali, Neri, Nadabu,
Et son fils premier-né Habdon, puis Tsur, Kis, Bahal, Ner, Nadab,
37 Gedori, Ahio, Zekaria na Miklothi.
Guédor, Ahio, Zacharie, et Mikloth.
38 Miklothi akamzaa Shimeamu. Wao pia waliishi karibu na jamaa zao huko Yerusalemu.
Et Mikloth engendra Siméam; et ils habitèrent vis-à-vis de leurs frères à Jérusalem avec leurs frères.
39 Neri akamzaa Kishi, Kishi akamzaa Sauli. Sauli akamzaa Yonathani, Malki-Shua, Abinadabu na Esh-Baali.
Et Ner engendra Kis, et Kis engendra Saül, et Saül engendra Jonathan, Malki-suah, Abinadab et Esbahal.
40 Yonathani akamzaa Merib-Baali, naye Merib-Baali akamzaa Mika.
Et le fils de Jonathan [fut] Mérib-bahal; et Mérib-bahal engendra Mica.
41 Wana wa Mika walikuwa: Pithoni, Meleki, Tarea, na Ahazi.
Et les enfants de Mica furent, Pithon, Mélec, Tahréah, [et Achaz].
42 Ahazi akamzaa Yara, Yara akawazaa Alemethi, Azmawethi na Zimri, naye Zimri akamzaa Mosa.
Et Achaz engendra Jahra; et Jahra engendra Halemeth, Hazmaveth, et Zimri; et Zimri engendra Motsa,
43 Mosa akamzaa Binea, Binea akamzaa Refaya, na mwanawe huyo ni Eleasa, na mwanawe huyo ni Aseli.
Et Motsa engendra Binha, qui eut pour fils Réphaja, qui eut pour fils Elhasa, qui eut pour fils Atsel.
44 Aseli alikuwa na wana sita, na haya ndiyo majina yao: Azrikamu, Bokeru, Ishmaeli, Shearia, Obadia na Hanani. Hawa ndio waliokuwa wana wa Aseli.
Et Atsel eut six fils, dont les noms [sont] Hazrikam, Bocru, Ismaël, Séharia, Hobadia, et Hanan. Ce furent là les fils d'Atsel.

< 1 Nyakati 9 >