< 1 Nyakati 7 >

1 Wana wa Isakari walikuwa: Tola, Pua, Yashubu na Shimroni; wote ni wanne.
Fils d'Issachar: Thola, Phua, Jasub et Siméron: quatre. —
2 Wana wa Tola walikuwa: Uzi, Refaya, Yerieli, Yahmai, Ibsamu na Shemueli waliokuwa viongozi wa jamaa zao. Wakati wa utawala wa Mfalme Daudi, wazao wa Tola walioorodheshwa kama wapiganaji katika ukoo wao walikuwa watu 22,600.
Fils de Thola: Ozi, Raphaïa, Jériel, Jémaï, Jebsem et Samuel, chefs de leurs maisons patriarcales issues de Thola, vaillants hommes, inscrits d'après leurs générations, au temps de David, au nombre de vingt-deux mille six cents. —
3 Mwana wa Uzi alikuwa: Izrahia. Wana wa Izrahia walikuwa: Mikaeli, Obadia, Yoeli na Ishia. Wote hawa watano walikuwa wakuu wao.
Fils d'Ozi: Izrahia. Fils de Izrahia: Michaël, Obadia, Johel et Jésia: en tout cinq chefs.
4 Kulingana na ukoo wa jamaa zao, walikuwa na watu hodari wa vita wapatao 36,000, kwa sababu walikuwa na wanawake na watoto wengi.
Ils avaient avec eux, selon leurs générations, selon leurs maisons patriarcales, des troupes armées pour la guerre, trente-six mille hommes; car ils avaient beaucoup de femmes et de fils.
5 Jamaa ya watu waliokuwa wapiganaji hodari kutoka koo zote za Isakari, kama ilivyoorodheshwa katika ukoo wao, jumla yao walikuwa 87,000.
Leurs frères, d'après toutes les familles d'Issachar, hommes vaillants, formaient un nombre total de quatre-vingt-sept mille, inscrits dans les généalogies.
6 Wana watatu wa Benyamini walikuwa: Bela, Bekeri na Yediaeli.
Fils de Benjamin: Béla, Béchor et Jadiel: trois. —
7 Wana wa Bela walikuwa: Esboni, Uzi, Uzieli, Yeremothi na Iri; walikuwa viongozi wa jamaa zao; wote ni watano. Watu wapiganaji walioorodheshwa katika ukoo wao walikuwa 22,034.
Fils de Béla: Esbon, Ozi, Oziel, Jérimoth et Uraï: cinq chefs de maisons patriarcales, hommes vaillants, inscrits dans les généalogies, au nombre de vingt-deux mille quatre cents. —
8 Wana wa Bekeri walikuwa: Zemira, Yoashi, Eliezeri, Elioenai, Omri, Yeremothi, Abiya, Anathothi na Alemethi. Hawa wote walikuwa wana wa Bekeri.
Fils de Béchor: Zamira, Joas, Eliézer, Elioénaï, Amri, Jérimoth, Abia, Anathoth et Almath: tous ceux-là fils de Béchor,
9 Orodha ya ukoo wao iliyoandikwa viongozi wa jamaa zao walikuwa wapiganaji 20,200.
inscrits dans les généalogies, d'après leurs générations, comme chefs de leurs maisons patriarcales, hommes vaillants, au nombre de vingt mille deux cents. —
10 Mwana wa Yediaeli alikuwa: Bilhani. Wana wa Bilhani walikuwa: Yeushi, Benyamini, Ehudi, Kenaana, Zethani, Tarshishi na Ahishahari.
Fils de Jadihel: Balan. — Fils de Balan: Jéhus, Benjamin, Aod, Chanana, Zéthan, Tarsis et Abisahar:
11 Hawa wana wote wa Yediaeli walikuwa viongozi wa jamaa zao. Kulikuwako wanaume wapiganaji 17,200 waliokuwa tayari kwenda vitani.
tous ceux là fils de Jadihel, chefs de leurs maisons patriarcales, hommes vaillants, au nombre de dix-sept mille deux cents, en état d'aller en armes à la guerre.
12 Washupimu na Wahupimu walikuwa wazao wa Iri. Wahushimu walikuwa wazao wa Aheri.
Sepham et Hapham, fils d'Hir: Hasim, fils d'Aher.
13 Wana wa Naftali walikuwa: Yahzieli, Guni, Yeseri na Shalumu; hao walikuwa wazao wa Bilha.
Fils de Nephthali: Jasiel, Guni, Jéser et Sellum, fils de Bala.
14 Wana wa Manase walikuwa: Asirieli alikuwa mzao wake kutokana na suria wake wa Kiaramu. Huyu suria akamzaa Makiri baba wa Gileadi.
Fils de Manassé: Esriel. Sa concubine syrienne enfanta Machir, père de Galaad. —
15 Makiri akatwaa mke kutoka miongoni mwa Wahupimu na Washupimu. Jina la dada yake aliitwa Maaka. Mwana wa pili wa Makiri aliitwa Selofehadi, ambaye alikuwa na wasichana tu.
Machir prit une femme de Happhim et de Saphan; le nom de sa sœur était Maacha. Le nom du second fils était Salphaad, et Salphaad eut des filles.
16 Maaka mkewe Makiri akamzaa mwana aliyemwita Pereshi. Jina la nduguye lilikuwa Shereshi. Wana wa Pereshi walikuwa Ulamu na Rakemu.
Maacha, femme de Machir, enfanta un fils, et l'appela du nom de Pharès; le nom de son frère était Sarès, et ses fils étaient Ulam et Récen. —
17 Mwana wa Ulamu alikuwa: Bedani. Hawa ndio waliokuwa wana wa Gileadi mwana wa Makiri, mwana wa Manase.
Fils d'Ulam: Badan. — Ce sont là les fils de Galaad, fils de Machir, fils de Manassé. —
18 Dada yake aliyeitwa Hamolekethi aliwazaa Ish-Hodi, Abiezeri na Mahla.
Sa sœur Hammoléketh enfanta Ischod, Abiézer et Mohola. —
19 Wana wa Shemida walikuwa: Ahiani, Shekemu, Liki na Aniamu.
Les fils de Sémida étaient: Ahin, Séchem, Léci et Aniam.
20 Wana wa Efraimu walikuwa: Shuthela, ambaye alimzaa Beredi, Beredi akamzaa Tahathi, Tahathi akazaa Eleada, Eleada akamzaa Tahathi,
Fils d'Ephraïm: Suthala; Bared, son fils; Thahath, son fils; Elada, son fils; Thahath, son fils;
21 Tahathi akamzaa Zabadi, na Zabadi akamzaa Shuthela. Ezeri na Eleadi waliuawa na wenyeji wa Gathi walipokuwa wamekwenda huko kuwanyangʼanya mifugo yao.
Zabad, son fils; Suthala, son fils; Ezer et Elad, que tuèrent les hommes de Geth nés dans le pays, parce qu'ils étaient descendus pour prendre leurs troupeaux.
22 Baba yao Efraimu akawaombolezea kwa siku nyingi, na jamaa zake wakaja kumfariji.
Ephraïm, leur père, fut longtemps dans le deuil, et ses frères vinrent pour le consoler.
23 Kisha akakutana kimwili na mke wake tena, naye akachukua mimba, akamzalia mwana. Akamwita Beria, kwa sababu ya misiba iliyoipata nyumba yake.
Et il alla vers sa femme, et elle conçut et enfanta un fils; il l'appela du nom de Béria, parce qu'on était dans le malheur en sa maison.
24 Beria alikuwa na binti jina lake Sheera. Huyu ndiye aliijenga miji ya Beth-Horoni ya Juu na Beth-Horoni ya Chini, pamoja na Uzen-Sheera.
Sa fille était Sara, qui bâtit Bethoron le Bas et Bethoron le Haut, et Ozen-Sara.
25 Beria akamzaa pia Refa, naye Refa akamzaa Reshefu, Reshefu akamzaa Tela, Tela akamzaa Tahani,
Rapha, son fils, et Réseph; Thalé, son fils; Taan, son fils;
26 Tahani akamzaa Ladani, Ladani akamzaa Amihudi, Amihudi akamzaa Elishama,
Laadan, son fils; Ammiud, son fils; Elisama, son fils;
27 Elishama akamzaa Nuni, Nuni akamzaa Yoshua.
Nun, son fils; Josué, son fils. —
28 Nchi zao na makazi yao yalijumuisha Betheli na vijiji vilivyouzunguka, Naarani ilikuwa upande wa mashariki, Gezeri pamoja na vijiji vyake upande wa magharibi, pia Shekemu na vijiji vyake hadi kufikia Aya na vijiji vyake.
Leurs possessions et leurs habitations étaient: Béthel et les villes de sa dépendance; à l'orient, Noran; à l'occident, Gézer et les villes de sa dépendance, Sichem et les villes de sa dépendance, jusqu'à Aza et aux villes de sa dépendance.
29 Katika mipaka ya Manase walikuwepo Beth-Shani, Taanaki, Megido na Dori pamoja na vijiji vyake. Wana wa Yosefu mwana wa Israeli waliishi katika miji hii.
Entre les mains des fils de Manassé étaient encore Bethsan et les villes de sa dépendance, Thanach et les villes de sa dépendance, Mageddo et les villes de sa dépendance, Dor et les villes de sa dépendance. Ce fut dans ces villes qu'habitèrent les fils de Joseph, fils d'Israël.
30 Wana wa Asheri walikuwa: Imna, Ishva, Ishvi na Beria. Dada yao alikuwa Sera.
Fils d'Aser: Jemma, Jésua, Jessui, Baria, et Sara, leur sœur. —
31 Wana wa Beria walikuwa: Heberi na Malkieli, aliyekuwa baba yake Birzaithi.
Fils de Baria: Héber et Melchiel, qui fut père de Barsaïth.
32 Heberi akawazaa Yafleti, Shomeri na Hothamu, na Shua dada yao.
Héber engendra Jéphlat, Somer, Hotham, et Suaa, leur sœur. —
33 Wana wa Yafleti walikuwa: Pasaki, Bimhali na Ashvathi. Hawa walikuwa wana wa Yafleti.
Fils de Jéphlat: Phosech, Chamaal et Asoth: ce sont là les fils de Jéphlat. —
34 Wana wa Shemeri walikuwa: Ahi, Roga, Yehuba na Aramu.
Fils de Somer: Ahi, Roaga, Haba et Aram. —
35 Wana wa Helemu ndugu yake walikuwa: Sofa, Imna, Sheleshi na Amali.
Fils de Hélem, son frère: Supha, Jemna, Sellès et Amal. —
36 Wana wa Sofa walikuwa: Sua, Harneferi, Shuali, Beri, Imra,
Fils de Supha: Sué, Harnapher, Sual, Béri, Jamra,
37 Bezeri, Hodu, Shama, Shilsha, Ithrani na Beera.
Bosor, Hod, Samma, Salusa, Jéthran et Béra. —
38 Wana wa Yetheri walikuwa: Yefune, Pispa na Ara.
Fils de Jéther: Jéphoné, Phaspha et Ara. —
39 Wana wa Ula walikuwa: Ara, Hanieli na Risia.
Fils d'Olla: Arée, Haniel et Résia. —
40 Hawa wote ndio waliokuwa wazao wa Asheri, viongozi wa jamaa zao, watu bora, mashujaa walio hodari na viongozi maarufu. Idadi ya watu waliokuwa tayari kwa vita, kama ilivyoorodheshwa katika ukoo wao, walikuwa 26,000.
Tous ceux-là étaient fils d'Aser, chefs de maisons patriarcales, hommes d'élite et vaillants, chefs des princes, inscrits au nombre de vingt-six mille hommes en état d'aller en armes à la guerre.

< 1 Nyakati 7 >