< 1 Nyakati 7 >

1 Wana wa Isakari walikuwa: Tola, Pua, Yashubu na Shimroni; wote ni wanne.
Now the sons of Issachar were, Tola, and Puah, Jashub, and Shimron, four.
2 Wana wa Tola walikuwa: Uzi, Refaya, Yerieli, Yahmai, Ibsamu na Shemueli waliokuwa viongozi wa jamaa zao. Wakati wa utawala wa Mfalme Daudi, wazao wa Tola walioorodheshwa kama wapiganaji katika ukoo wao walikuwa watu 22,600.
And the sons of Tola; Uzzi, and Rephaiah, and Jeriel, and Jahmai, and Jibsam, and Shemuel, heads of their father’s house, that is, of Tola: they were valiant men of might in their generations; whose number was in the days of David two and twenty thousand and six hundred.
3 Mwana wa Uzi alikuwa: Izrahia. Wana wa Izrahia walikuwa: Mikaeli, Obadia, Yoeli na Ishia. Wote hawa watano walikuwa wakuu wao.
And the sons of Uzzi; Izrahiah: and the sons of Izrahiah; Michael, and Obadiah, and Joel, Ishiah, five: all of them chief men.
4 Kulingana na ukoo wa jamaa zao, walikuwa na watu hodari wa vita wapatao 36,000, kwa sababu walikuwa na wanawake na watoto wengi.
And with them, by their generations, after the house of their fathers, were bands of soldiers for war, six and thirty thousand men: for they had many wives and sons.
5 Jamaa ya watu waliokuwa wapiganaji hodari kutoka koo zote za Isakari, kama ilivyoorodheshwa katika ukoo wao, jumla yao walikuwa 87,000.
And their brethren among all the families of Issachar were valiant men of might, reckoned in all by their genealogies eighty and seven thousand.
6 Wana watatu wa Benyamini walikuwa: Bela, Bekeri na Yediaeli.
The sons of Benjamin; Bela, and Becher, and Jediael, three.
7 Wana wa Bela walikuwa: Esboni, Uzi, Uzieli, Yeremothi na Iri; walikuwa viongozi wa jamaa zao; wote ni watano. Watu wapiganaji walioorodheshwa katika ukoo wao walikuwa 22,034.
And the sons of Bela; Ezbon, and Uzzi, and Uzziel, and Jerimoth, and Iri, five; heads of the house of their fathers, mighty men of valour; and were reckoned by their genealogies twenty and two thousand and thirty and four.
8 Wana wa Bekeri walikuwa: Zemira, Yoashi, Eliezeri, Elioenai, Omri, Yeremothi, Abiya, Anathothi na Alemethi. Hawa wote walikuwa wana wa Bekeri.
And the sons of Becher; Zemira, and Joash, and Eliezer, and Elioenai, and Omri, and Jerimoth, and Abiah, and Anathoth, and Alameth. All these are the sons of Becher.
9 Orodha ya ukoo wao iliyoandikwa viongozi wa jamaa zao walikuwa wapiganaji 20,200.
And the number of them, after their genealogy by their generations, heads of the house of their fathers, mighty men of valour, was twenty thousand and two hundred.
10 Mwana wa Yediaeli alikuwa: Bilhani. Wana wa Bilhani walikuwa: Yeushi, Benyamini, Ehudi, Kenaana, Zethani, Tarshishi na Ahishahari.
The sons also of Jediael; Bilhan: and the sons of Bilhan; Jeush, and Benjamin, and Ehud, and Chenaanah, and Zethan, and Tharshish, and Ahishahar.
11 Hawa wana wote wa Yediaeli walikuwa viongozi wa jamaa zao. Kulikuwako wanaume wapiganaji 17,200 waliokuwa tayari kwenda vitani.
All these the sons of Jediael, by the heads of their fathers, mighty men of valour, were seventeen thousand and two hundred soldiers, fit to go out for war and battle.
12 Washupimu na Wahupimu walikuwa wazao wa Iri. Wahushimu walikuwa wazao wa Aheri.
Shuppim also, and Huppim, the children of Ir, and Hushim, the sons of Aher.
13 Wana wa Naftali walikuwa: Yahzieli, Guni, Yeseri na Shalumu; hao walikuwa wazao wa Bilha.
The sons of Naphtali; Jahziel, and Guni, and Jezer, and Shallum, the sons of Bilhah.
14 Wana wa Manase walikuwa: Asirieli alikuwa mzao wake kutokana na suria wake wa Kiaramu. Huyu suria akamzaa Makiri baba wa Gileadi.
The sons of Manasseh; Ashriel, whom she bore: ( but his Syrian concubine bore Machir the father of Gilead:
15 Makiri akatwaa mke kutoka miongoni mwa Wahupimu na Washupimu. Jina la dada yake aliitwa Maaka. Mwana wa pili wa Makiri aliitwa Selofehadi, ambaye alikuwa na wasichana tu.
And Machir took for a wife the sister of Huppim and Shuppim, whose sister’s name was Maachah; ) and the name of the second was Zelophehad: and Zelophehad had daughters.
16 Maaka mkewe Makiri akamzaa mwana aliyemwita Pereshi. Jina la nduguye lilikuwa Shereshi. Wana wa Pereshi walikuwa Ulamu na Rakemu.
And Maachah the wife of Machir bore a son, and she called his name Peresh; and the name of his brother was Sheresh; and his sons were Ulam and Rakem.
17 Mwana wa Ulamu alikuwa: Bedani. Hawa ndio waliokuwa wana wa Gileadi mwana wa Makiri, mwana wa Manase.
And the sons of Ulam; Bedan. These were the sons of Gilead, the son of Machir, the son of Manasseh.
18 Dada yake aliyeitwa Hamolekethi aliwazaa Ish-Hodi, Abiezeri na Mahla.
And his sister Hammoleketh bore Ishod, and Abiezer, and Mahalah.
19 Wana wa Shemida walikuwa: Ahiani, Shekemu, Liki na Aniamu.
And the sons of Shemida were, Ahian, and Shechem, and Likhi, and Aniam.
20 Wana wa Efraimu walikuwa: Shuthela, ambaye alimzaa Beredi, Beredi akamzaa Tahathi, Tahathi akazaa Eleada, Eleada akamzaa Tahathi,
And the sons of Ephraim; Shuthelah, and Bered his son, and Tahath his son, and Eladah his son, and Tahath his son,
21 Tahathi akamzaa Zabadi, na Zabadi akamzaa Shuthela. Ezeri na Eleadi waliuawa na wenyeji wa Gathi walipokuwa wamekwenda huko kuwanyangʼanya mifugo yao.
And Zabad his son, and Shuthelah his son, and Ezer, and Elead, whom the men of Gath that were born in that land slew, because they came down to take away their cattle.
22 Baba yao Efraimu akawaombolezea kwa siku nyingi, na jamaa zake wakaja kumfariji.
And Ephraim their father mourned many days, and his brethren came to comfort him.
23 Kisha akakutana kimwili na mke wake tena, naye akachukua mimba, akamzalia mwana. Akamwita Beria, kwa sababu ya misiba iliyoipata nyumba yake.
And when he went in to his wife, she conceived, and bore a son, and he called his name Beriah, because it went evil with his house.
24 Beria alikuwa na binti jina lake Sheera. Huyu ndiye aliijenga miji ya Beth-Horoni ya Juu na Beth-Horoni ya Chini, pamoja na Uzen-Sheera.
(And his daughter was Sherah, who built Bethhoron the lower, and the upper, and Uzzensherah.)
25 Beria akamzaa pia Refa, naye Refa akamzaa Reshefu, Reshefu akamzaa Tela, Tela akamzaa Tahani,
And Rephah was his son, also Resheph, and Telah his son, and Tahan his son,
26 Tahani akamzaa Ladani, Ladani akamzaa Amihudi, Amihudi akamzaa Elishama,
Laadan his son, Ammihud his son, Elishama his son,
27 Elishama akamzaa Nuni, Nuni akamzaa Yoshua.
Non his son, Jehoshua his son.
28 Nchi zao na makazi yao yalijumuisha Betheli na vijiji vilivyouzunguka, Naarani ilikuwa upande wa mashariki, Gezeri pamoja na vijiji vyake upande wa magharibi, pia Shekemu na vijiji vyake hadi kufikia Aya na vijiji vyake.
And their possessions and habitations were, Bethel and its towns, and eastward Naaran, and westward Gezer, with its towns, Shechem also and its towns, to Gaza and its towns:
29 Katika mipaka ya Manase walikuwepo Beth-Shani, Taanaki, Megido na Dori pamoja na vijiji vyake. Wana wa Yosefu mwana wa Israeli waliishi katika miji hii.
And by the borders of the children of Manasseh, Bethshean and its towns, Taanach and its towns, Megiddo and its towns, Dor and its towns. In these dwelt the children of Joseph the son of Israel.
30 Wana wa Asheri walikuwa: Imna, Ishva, Ishvi na Beria. Dada yao alikuwa Sera.
The sons of Asher; Imnah, and Isuah, and Ishuai, and Beriah, and Serah their sister.
31 Wana wa Beria walikuwa: Heberi na Malkieli, aliyekuwa baba yake Birzaithi.
And the sons of Beriah; Heber, and Malchiel, who is the father of Birzavith.
32 Heberi akawazaa Yafleti, Shomeri na Hothamu, na Shua dada yao.
And Heber begat Japhlet, and Shomer, and Hotham, and Shua their sister.
33 Wana wa Yafleti walikuwa: Pasaki, Bimhali na Ashvathi. Hawa walikuwa wana wa Yafleti.
And the sons of Japhlet; Pasach, and Bimhal, and Ashvath. These are the children of Japhlet.
34 Wana wa Shemeri walikuwa: Ahi, Roga, Yehuba na Aramu.
And the sons of Shamer; Ahi, and Rohgah, Jehubbah, and Aram.
35 Wana wa Helemu ndugu yake walikuwa: Sofa, Imna, Sheleshi na Amali.
And the sons of his brother Helem; Zophah, and Imna, and Shelesh, and Amal.
36 Wana wa Sofa walikuwa: Sua, Harneferi, Shuali, Beri, Imra,
The sons of Zophah; Suah, and Harnepher, and Shual, and Beri, and Imrah,
37 Bezeri, Hodu, Shama, Shilsha, Ithrani na Beera.
Bezer, and Hod, and Shamma, and Shilshah, and Ithran, and Beera.
38 Wana wa Yetheri walikuwa: Yefune, Pispa na Ara.
And the sons of Jether; Jephunneh, and Pispah, and Ara.
39 Wana wa Ula walikuwa: Ara, Hanieli na Risia.
And the sons of Ulla; Arah, and Haniel, and Rezia.
40 Hawa wote ndio waliokuwa wazao wa Asheri, viongozi wa jamaa zao, watu bora, mashujaa walio hodari na viongozi maarufu. Idadi ya watu waliokuwa tayari kwa vita, kama ilivyoorodheshwa katika ukoo wao, walikuwa 26,000.
All these were the children of Asher, heads of their father’s house, choice and mighty men of valour, chief of the princes. And the number throughout the genealogy of them that were fit for war and for battle was twenty and six thousand men.

< 1 Nyakati 7 >