< 1 Nyakati 24 >

1 Hii ndiyo migawanyo ya wana wa Aroni: Aroni alikuwa na wana wanne: Nadabu, Abihu, Eleazari na Ithamari.
Now [these are] the divisions of the sons of Aaron. The sons of Aaron; Nadab, and Abihu, Eleazar, and Ithamar.
2 Nadabu na Abihu walikufa kabla ya baba yao, nao hawakuwa na wana; kwa hiyo ndugu zao Eleazari na Ithamari wakahudumu kama makuhani.
But Nadab and Abihu died before their father, and had no children: therefore Eleazar and Ithamar executed the priests' office.
3 Akisaidiwa na Sadoki mwana wa Eleazari na Ahimeleki mwana wa Ithamari, Daudi aliwapanga wazao wa Aroni katika migawanyo kufuatana na wajibu wa huduma zao.
And David distributed them, both Zadok of the sons of Eleazar, and Ahimelech of the sons of Ithamar, according to their offices in their service.
4 Idadi kubwa ya viongozi walipatikana miongoni mwa wazao wa Eleazari, kuliko miongoni mwa wazao wa Ithamari, nao waligawanywa kwa uwiano: Viongozi kumi na sita kutoka jamaa ya wazao wa Eleazari na viongozi wanane kutoka jamaa ya wazao wa Ithamari.
And there were more chief men found of the sons of Eleazar than of the sons of Ithamar; and [thus] were they divided. Among the sons of Eleazar [there were] sixteen chief men of the house of [their] fathers, and eight among the sons of Ithamar according to the house of their fathers.
5 Waliwagawanya bila upendeleo kwa kupiga kura, kwa kuwa kulikuwa na maafisa wa mahali patakatifu na maafisa wa Mungu miongoni mwa wazao wale wa Eleazari na wale wa Ithamari.
Thus were they divided by lot, one sort with another; for the governors of the sanctuary, and governors [of the house] of God, were of the sons of Eleazar, and of the sons of Ithamar.
6 Mwandishi Shemaya mwana wa Nethaneli, Mlawi, aliorodhesha majina yao mbele ya Mfalme Daudi na maafisa: Kuhani Sadoki, Ahimeleki mwana wa Abiathari, na viongozi wa jamaa za makuhani na za Walawi: jamaa moja ikitoka upande wa Eleazari na nyingine upande wa Ithamari.
And Shemaiah the son of Nethaneel the scribe, [one] of the Levites, wrote them before the king, and the princes, and Zadok the priest, and Ahimelech the son of Abiathar, and [before] the chief of the fathers of the priests and Levites: one principal household being taken for Eleazar, and [one] taken for Ithamar.
7 Kura ya kwanza ilimwangukia Yehoyaribu, ya pili Yedaya,
Now the first lot came forth to Jehoiarib, the second to Jedaiah,
8 ya tatu Harimu, ya nne Seorimu,
The third to Harim, the fourth to Seorim,
9 ya tano Malkiya, ya sita Miyamini,
The fifth to Malchijah, the sixth to Mijamin,
10 ya saba Hakosi, ya nane Abiya,
The seventh to Hakkoz, the eighth to Abijah,
11 ya tisa Yeshua, ya kumi Shekania,
The ninth to Jeshuah, the tenth to Shecaniah,
12 ya kumi na moja Eliashibu, ya kumi na mbili Yakimu,
The eleventh to Eliashib, the twelfth to Jakim,
13 ya kumi na tatu Hupa, ya kumi na nne Yeshebeabu,
The thirteenth to Huppah, the fourteenth to Jeshebeab,
14 ya kumi na tano Bilga, ya kumi na sita Imeri,
The fifteenth to Bilgah, the sixteenth to Immer,
15 ya kumi na saba Heziri, ya kumi na nane Hapisesi,
The seventeenth to Hezer, the eighteenth to Aphses,
16 ya kumi na tisa Pethahia, ya ishirini Yehezkeli,
The nineteenth to Pethahiah, the twentieth to Jehezekel,
17 ya ishirini na moja Yakini, ya ishirini na mbili Gamuli,
The one and twentieth to Jachin, the two and twentieth to Gamul,
18 ya ishirini na tatu Delaya, ya ishirini na nne Maazia.
The three and twentieth to Delaiah, the four and twentieth to Maaziah.
19 Huu ulikuwa ndio utaratibu wao uliokubalika wa kuhudumu walipoingia katika Hekalu la Bwana kulingana na masharti waliyoelekezwa na Aroni baba yao, kama Bwana, Mungu wa Israeli, alivyokuwa amemwamuru.
These [were] the orderings of them in their service to come into the house of the LORD, according to their manner, under Aaron their father, as the LORD God of Israel had commanded him.
20 Kuhusu wazao wa Lawi waliobaki: Kutoka kwa wana wa Amramu: alikuwa Shubaeli; kutoka kwa wana wa Shubaeli: alikuwa Yedeya.
And the rest of the sons of Levi [were these]: Of the sons of Amram; Shubael: of the sons of Shubael; Jehdeiah.
21 Kwa wa Rehabia, kutoka kwa wanawe: Ishia alikuwa wa kwanza.
Concerning Rehabiah: of the sons of Rehabiah, the first [was] Isshiah.
22 Kutoka kwa Waishari: alikuwa Shelomithi, kutoka kwa wana wa Shelomithi: alikuwa Yahathi.
Of the Izharites; Shelomoth: of the sons of Shelomoth; Jahath.
23 Wana wa Hebroni: Yeria alikuwa mkuu, Amaria wa pili, Yahazieli wa tatu, na Yekameamu wa nne.
And the sons [of Hebron]; Jeriah [the first], Amariah the second, Jehaziel the third, Jekameam the fourth.
24 Mwana wa Uzieli: alikuwa Mika; kutoka kwa wana wa Mika: alikuwa Shamiri.
[Of] the sons of Uzziel; Michah: of the sons of Michah; Shamir.
25 Ndugu yake Mika: alikuwa Ishia; na kutoka kwa wana wa Ishia: alikuwa Zekaria.
The brother of Michah [was] Isshiah: of the sons of Isshiah; Zechariah.
26 Wana wa Merari: walikuwa Mahli na Mushi. Mwana wa Yaazia: alikuwa Beno.
The sons of Merari [were] Mahli, and Mushi: the sons of Jaaziah; Beno.
27 Wana wa Merari: kutoka kwa Yaazia: ni Beno, Shohamu, Zakuri na Ibri.
The sons of Merari by Jaaziah; Beno, and Shoham, and Zaccur, and Ibri.
28 Kutoka kwa Mahli: alikuwa Eleazari, ambaye hakuwa na wana.
Of Mahli [came] Eleazar, who had no sons.
29 Kutoka kwa Kishi: mwana wa Kishi: alikuwa Yerameeli.
Concerning Kish: the son of Kish [was] Jerahmeel.
30 Nao wana wa Mushi: walikuwa Mahli, Ederi na Yeremothi. Hawa walikuwa Walawi kulingana na jamaa zao.
The sons also of Mushi; Mahli, and Eder, and Jerimoth. These [were] the sons of the Levites after the house of their fathers.
31 Pia walipiga kura kama vile ndugu zao wazao wa Aroni walivyofanya, mbele ya Mfalme Daudi, Sadoki, Ahimeleki na mbele ya viongozi wa jamaa ya makuhani na ya Walawi. Jamaa za ndugu wakubwa zilitendewa sawasawa na zile za ndugu wadogo.
These likewise cast lots over against their brethren the sons of Aaron in the presence of David the king, and Zadok, and Ahimelech, and the chief of the fathers of the priests and Levites, even the principal fathers over against their younger brethren.

< 1 Nyakati 24 >