< 1 Nyakati 24 >

1 Hii ndiyo migawanyo ya wana wa Aroni: Aroni alikuwa na wana wanne: Nadabu, Abihu, Eleazari na Ithamari.
The work groups based on Aaron's descendants were these: Nadab, Abihu, Eleazar and Ithamar.
2 Nadabu na Abihu walikufa kabla ya baba yao, nao hawakuwa na wana; kwa hiyo ndugu zao Eleazari na Ithamari wakahudumu kama makuhani.
Nadab and Abihu died before their father died. They had no children, so Eleazar and Ithamar served as priests.
3 Akisaidiwa na Sadoki mwana wa Eleazari na Ahimeleki mwana wa Ithamari, Daudi aliwapanga wazao wa Aroni katika migawanyo kufuatana na wajibu wa huduma zao.
David, together with Zadok, a descendant of Eleazar, and Ahimelech, a descendant of Ithamar, divided them into groups for their work as priests.
4 Idadi kubwa ya viongozi walipatikana miongoni mwa wazao wa Eleazari, kuliko miongoni mwa wazao wa Ithamari, nao waligawanywa kwa uwiano: Viongozi kumi na sita kutoka jamaa ya wazao wa Eleazari na viongozi wanane kutoka jamaa ya wazao wa Ithamari.
There were more leading men among Eleazar's descendants than among Ithamar's descendants, so they divided Eleazar's descendants into sixteen groups. They did this by heads of clans and by Ithamar's descendants. These divisions were eight in number, corresponding to their clans.
5 Waliwagawanya bila upendeleo kwa kupiga kura, kwa kuwa kulikuwa na maafisa wa mahali patakatifu na maafisa wa Mungu miongoni mwa wazao wale wa Eleazari na wale wa Ithamari.
They divided them impartially by lot, for there were holy officials and officials of God, from both Eleazar's descendants and Ithamar's descendants.
6 Mwandishi Shemaya mwana wa Nethaneli, Mlawi, aliorodhesha majina yao mbele ya Mfalme Daudi na maafisa: Kuhani Sadoki, Ahimeleki mwana wa Abiathari, na viongozi wa jamaa za makuhani na za Walawi: jamaa moja ikitoka upande wa Eleazari na nyingine upande wa Ithamari.
Shemaiah son of Nethanel the scribe, a Levite, wrote down their names in the presence of the king, the officials, Zadok the priest, Ahimelech son of Abiathar, and the leaders of the priestly and Levite families. One clan was drawn by lot from Eleazar's descendants, and then the next would be drawn from Ithamar's descendants.
7 Kura ya kwanza ilimwangukia Yehoyaribu, ya pili Yedaya,
The first lot went to Jehoiarib, the second to Jedaiah,
8 ya tatu Harimu, ya nne Seorimu,
the third to Harim, the fourth to Seorim,
9 ya tano Malkiya, ya sita Miyamini,
the fifth to Malchijah, the sixth to Mijamin,
10 ya saba Hakosi, ya nane Abiya,
the seventh to Hakkoz, the eighth to Abijah,
11 ya tisa Yeshua, ya kumi Shekania,
the ninth to Jeshua, the tenth to Shecaniah,
12 ya kumi na moja Eliashibu, ya kumi na mbili Yakimu,
the eleventh to Eliashib, the twelfth to Jakim,
13 ya kumi na tatu Hupa, ya kumi na nne Yeshebeabu,
the thirteenth to Huppah, the fourteenth to Jeshebeab,
14 ya kumi na tano Bilga, ya kumi na sita Imeri,
the fifteenth to Bilgah, the sixteenth to Immer,
15 ya kumi na saba Heziri, ya kumi na nane Hapisesi,
the seventeenth to Hezir, the eighteenth to Happizzez,
16 ya kumi na tisa Pethahia, ya ishirini Yehezkeli,
the nineteenth to Pethahiah, the twentieth to Jehezkel,
17 ya ishirini na moja Yakini, ya ishirini na mbili Gamuli,
the twenty-first to Jakin, the twenty-second to Gamul,
18 ya ishirini na tatu Delaya, ya ishirini na nne Maazia.
the twenty-third to Delaiah, and the twenty-fourth to Maaziah.
19 Huu ulikuwa ndio utaratibu wao uliokubalika wa kuhudumu walipoingia katika Hekalu la Bwana kulingana na masharti waliyoelekezwa na Aroni baba yao, kama Bwana, Mungu wa Israeli, alivyokuwa amemwamuru.
This was the order of their service, when they came into Yahweh's house, following the procedure given to them by Aaron their ancestor, as Yahweh, the God of Israel, had instructed him.
20 Kuhusu wazao wa Lawi waliobaki: Kutoka kwa wana wa Amramu: alikuwa Shubaeli; kutoka kwa wana wa Shubaeli: alikuwa Yedeya.
These were the rest of the descendants of Levi: Of the sons of Amram, Shubael; of the sons of Shubael, Jehdeiah.
21 Kwa wa Rehabia, kutoka kwa wanawe: Ishia alikuwa wa kwanza.
As for Rehabiah, the sons of Rehabiah: Ishijah the leader.
22 Kutoka kwa Waishari: alikuwa Shelomithi, kutoka kwa wana wa Shelomithi: alikuwa Yahathi.
From the Izharites: Shelomoth; from the sons of Shelomoth: Jahath.
23 Wana wa Hebroni: Yeria alikuwa mkuu, Amaria wa pili, Yahazieli wa tatu, na Yekameamu wa nne.
The sons of Hebron: Jeriah the leader, Amariah the second, Jahaziel the third, and Jekameam the fourth.
24 Mwana wa Uzieli: alikuwa Mika; kutoka kwa wana wa Mika: alikuwa Shamiri.
The son of Uzziel: Micah; from the sons of Micah: Shamir.
25 Ndugu yake Mika: alikuwa Ishia; na kutoka kwa wana wa Ishia: alikuwa Zekaria.
The brother of Micah: Ishijah. From the sons of Ishijah: Zechariah.
26 Wana wa Merari: walikuwa Mahli na Mushi. Mwana wa Yaazia: alikuwa Beno.
The sons of Merari: Mahli and Mushi; from the son of Jaaziah: Beno.
27 Wana wa Merari: kutoka kwa Yaazia: ni Beno, Shohamu, Zakuri na Ibri.
The sons of Merari from Jaaziah: Beno, Shoham, Zaccur, and Ibri.
28 Kutoka kwa Mahli: alikuwa Eleazari, ambaye hakuwa na wana.
From Mahli: Eleazar, who had no sons.
29 Kutoka kwa Kishi: mwana wa Kishi: alikuwa Yerameeli.
From Kish: The son of Kish: Jerahmeel.
30 Nao wana wa Mushi: walikuwa Mahli, Ederi na Yeremothi. Hawa walikuwa Walawi kulingana na jamaa zao.
The sons of Mushi: Mahli, Eder, and Jerimoth. These were the Levites, listed by their families.
31 Pia walipiga kura kama vile ndugu zao wazao wa Aroni walivyofanya, mbele ya Mfalme Daudi, Sadoki, Ahimeleki na mbele ya viongozi wa jamaa ya makuhani na ya Walawi. Jamaa za ndugu wakubwa zilitendewa sawasawa na zile za ndugu wadogo.
These men who were the head of each father's house and each of their younger brothers, cast lots in the presence of King David, and Zadok and Ahimelech, along with the leaders of the families of the priests and Levites. They cast lots just as Aaron's descendants had done.

< 1 Nyakati 24 >