< 1 Nyakati 24 >

1 Hii ndiyo migawanyo ya wana wa Aroni: Aroni alikuwa na wana wanne: Nadabu, Abihu, Eleazari na Ithamari.
These were the divisions of the sons of Aaron. The sons of Aaron: Nadab and Abihu, Eleazar and Ithamar.
2 Nadabu na Abihu walikufa kabla ya baba yao, nao hawakuwa na wana; kwa hiyo ndugu zao Eleazari na Ithamari wakahudumu kama makuhani.
But Nadab and Abihu died before their father, and had no children: therefore Eleazar and Ithamar executed the priest's office.
3 Akisaidiwa na Sadoki mwana wa Eleazari na Ahimeleki mwana wa Ithamari, Daudi aliwapanga wazao wa Aroni katika migawanyo kufuatana na wajibu wa huduma zao.
David with Zadok of the sons of Eleazar, and Ahimelech of the sons of Ithamar, divided them according to their ordering in their service.
4 Idadi kubwa ya viongozi walipatikana miongoni mwa wazao wa Eleazari, kuliko miongoni mwa wazao wa Ithamari, nao waligawanywa kwa uwiano: Viongozi kumi na sita kutoka jamaa ya wazao wa Eleazari na viongozi wanane kutoka jamaa ya wazao wa Ithamari.
There were more chief men found among the sons of Eleazar than of the sons of Ithamar; so they were divided like this: of the sons of Eleazar there were sixteen heads according to their ancestral houses, and eight according to their ancestral houses among the sons of Ithamar.
5 Waliwagawanya bila upendeleo kwa kupiga kura, kwa kuwa kulikuwa na maafisa wa mahali patakatifu na maafisa wa Mungu miongoni mwa wazao wale wa Eleazari na wale wa Ithamari.
And thus were they divided impartially by drawing lots; for there were officiers of the sanctuary, and officiers of God, both of the descendants of Eleazar, and of the descendants of Ithamar.
6 Mwandishi Shemaya mwana wa Nethaneli, Mlawi, aliorodhesha majina yao mbele ya Mfalme Daudi na maafisa: Kuhani Sadoki, Ahimeleki mwana wa Abiathari, na viongozi wa jamaa za makuhani na za Walawi: jamaa moja ikitoka upande wa Eleazari na nyingine upande wa Ithamari.
And Shemaiah the son of Nethanel the scribe, who was of the Levites, wrote them in the presence of the king, and the officiers, and Zadok the priest, and Ahimelech the son of Abiathar, and the heads of the ancestral houses of the priests and of the Levites; one fathers' house being taken for Eleazar and one being taken for Ithamar.
7 Kura ya kwanza ilimwangukia Yehoyaribu, ya pili Yedaya,
Now the first lot came forth to Jehoiarib, the second to Jedaiah,
8 ya tatu Harimu, ya nne Seorimu,
the third to Harim, the fourth to Seorim,
9 ya tano Malkiya, ya sita Miyamini,
the fifth to Malchijah, the sixth to Mijamin,
10 ya saba Hakosi, ya nane Abiya,
the seventh to Hakkoz, the eighth to Abijah,
11 ya tisa Yeshua, ya kumi Shekania,
the ninth to Jeshua, the tenth to Shecaniah,
12 ya kumi na moja Eliashibu, ya kumi na mbili Yakimu,
the eleventh to Eliashib, the twelfth to Jakim,
13 ya kumi na tatu Hupa, ya kumi na nne Yeshebeabu,
the thirteenth to Huppah, the fourteenth to Jeshbaal,
14 ya kumi na tano Bilga, ya kumi na sita Imeri,
the fifteenth to Bilgah, the sixteenth to Immer,
15 ya kumi na saba Heziri, ya kumi na nane Hapisesi,
the seventeenth to Hezir, the eighteenth to Happizzez,
16 ya kumi na tisa Pethahia, ya ishirini Yehezkeli,
the nineteenth to Pethahiah, the twentieth to Jehezkel,
17 ya ishirini na moja Yakini, ya ishirini na mbili Gamuli,
the twenty-first to Jakin, the twenty-second to Gamul,
18 ya ishirini na tatu Delaya, ya ishirini na nne Maazia.
the twenty-third to Delaiah, the twenty-fourth to Maaziah.
19 Huu ulikuwa ndio utaratibu wao uliokubalika wa kuhudumu walipoingia katika Hekalu la Bwana kulingana na masharti waliyoelekezwa na Aroni baba yao, kama Bwana, Mungu wa Israeli, alivyokuwa amemwamuru.
This was their ordering in their service, to come into the house of the LORD according to the ordinance given to them by Aaron their father, as the LORD, the God of Israel, had commanded him.
20 Kuhusu wazao wa Lawi waliobaki: Kutoka kwa wana wa Amramu: alikuwa Shubaeli; kutoka kwa wana wa Shubaeli: alikuwa Yedeya.
Of the rest of the sons of Levi: of the sons of Amram, Shubael; of the sons of Shubael, Jehdeiah.
21 Kwa wa Rehabia, kutoka kwa wanawe: Ishia alikuwa wa kwanza.
Of Rehabiah: of the sons of Rehabiah, Isshiah the chief.
22 Kutoka kwa Waishari: alikuwa Shelomithi, kutoka kwa wana wa Shelomithi: alikuwa Yahathi.
Of the Izharites, Shelomoth; of the sons of Shelomoth, Jahath.
23 Wana wa Hebroni: Yeria alikuwa mkuu, Amaria wa pili, Yahazieli wa tatu, na Yekameamu wa nne.
The sons of Hebron: Jeriah, Amariah the second, Jahaziel the third, Jekameam the fourth.
24 Mwana wa Uzieli: alikuwa Mika; kutoka kwa wana wa Mika: alikuwa Shamiri.
The sons of Uzziel, Micah; of the sons of Micah, Shamir.
25 Ndugu yake Mika: alikuwa Ishia; na kutoka kwa wana wa Ishia: alikuwa Zekaria.
The brother of Micah, Isshiah; of the sons of Isshiah, Zechariah.
26 Wana wa Merari: walikuwa Mahli na Mushi. Mwana wa Yaazia: alikuwa Beno.
The sons of Merari: Mahli and Mushi; of his sons: Jaaziah his son.
27 Wana wa Merari: kutoka kwa Yaazia: ni Beno, Shohamu, Zakuri na Ibri.
The sons of Merari by Jaaziah his son: Shoham, and Zakkur, and Ibri.
28 Kutoka kwa Mahli: alikuwa Eleazari, ambaye hakuwa na wana.
Of Mahli: Eleazar, who had no sons.
29 Kutoka kwa Kishi: mwana wa Kishi: alikuwa Yerameeli.
Of Kish; the sons of Kish: Jerahmeel.
30 Nao wana wa Mushi: walikuwa Mahli, Ederi na Yeremothi. Hawa walikuwa Walawi kulingana na jamaa zao.
The sons of Mushi: Mahli, and Eder, and Jerimoth. These were the sons of the Levites after their fathers' houses.
31 Pia walipiga kura kama vile ndugu zao wazao wa Aroni walivyofanya, mbele ya Mfalme Daudi, Sadoki, Ahimeleki na mbele ya viongozi wa jamaa ya makuhani na ya Walawi. Jamaa za ndugu wakubwa zilitendewa sawasawa na zile za ndugu wadogo.
These likewise cast lots even as their kinsmen the descendants of Aaron in the presence of David the king, and Zadok, and Ahimelech, and the heads of the ancestral houses of the priests and of the Levites; the ancestral houses of the chief even as those of his younger brother.

< 1 Nyakati 24 >