< 1 Nyakati 21 >

1 Shetani akainuka dhidi ya Israeli na kumshawishi Daudi ahesabu watu wa Israeli.
Or Satan s'éleva contre Israël, et incita David à faire le dénombrement d'Israël.
2 Kwa hiyo Daudi akamwambia Yoabu na majemadari wa jeshi, “Nendeni mkawahesabu Waisraeli kuanzia Beer-Sheba mpaka Dani. Kisha nileteeni taarifa ili kwamba niweze kufahamu wako wangapi.”
Et David dit à Joab et aux chefs du peuple: Allez, faites le dénombrement d'Israël, depuis Béer-Shéba jusqu'à Dan, et rapportez-le-moi, afin que j'en sache le nombre.
3 Yoabu akajibu, “Bwana na aongeze jeshi lake mara mia na zaidi. Mfalme bwana wangu, kwani hawa wote si raiya wa bwana wangu? Kwa nini bwana wangu unataka kufanya hivi? Kwa nini kuleta hatia juu ya Israeli?”
Mais Joab répondit: Que l'Éternel veuille augmenter son peuple cent fois autant qu'il est! O roi mon seigneur, ne sont-ils pas tous serviteurs de mon seigneur? Pourquoi mon seigneur cherche-t-il cela? Et pourquoi Israël en serait-il coupable?
4 Hata hivyo, neno la mfalme likawa na nguvu juu ya Yoabu; kwa hiyo Yoabu akaondoka na kuzunguka Israeli yote kisha akarudi Yerusalemu.
Cependant la parole du roi prévalut sur Joab; et Joab partit, et parcourut tout Israël; puis il revint à Jérusalem.
5 Yoabu akampa Daudi jumla ya idadi ya watu wanaoweza kupigana. Katika Israeli kulikuwa na watu 1,100,000 ambao wangeweza kutumia upanga na katika Yuda watu 470,000.
Et Joab donna à David le rôle du dénombrement du peuple, et il se trouva de tout Israël onze cent mille hommes tirant l'épée; et de Juda quatre cent soixante et dix mille hommes tirant l'épée;
6 Lakini Yoabu hakuwahesabu Walawi na Wabenyamini, kwa sababu alichukizwa sana na amri ya mfalme.
Il ne recensa point parmi eux Lévi et Benjamin; car l'ordre du roi était une abomination pour Joab.
7 Amri hii ilikuwa mbaya machoni pa Mungu pia; hivyo akaiadhibu Israeli.
Or cette affaire déplut à Dieu, qui frappa Israël.
8 Kisha Daudi akamwambia Mungu, “Nimetenda dhambi kubwa kwa kufanya jambo hili. Sasa, ninakusihi, ondoa hatia ya mtumishi wako. Nimefanya jambo la kipumbavu sana.”
Et David dit à Dieu: J'ai commis un grand péché en faisant cela! Et maintenant, fais passer, je te prie, l'iniquité de ton serviteur; car j'ai agi très follement.
9 Bwana akamwambia Gadi, mwonaji wa Daudi,
Alors l'Éternel parla à Gad, le Voyant de David, en disant:
10 “Nenda ukamwambie Daudi, hivi ndivyo asemavyo Bwana: ‘Ninakupa wewe uchaguzi wa mambo matatu. Nichagulie mojawapo nitakalotenda dhidi yako.’”
Va, parle à David, et dis-lui: Ainsi a dit l'Éternel: J'ai trois choses à te proposer; choisis l'une d'elles, afin que je te la fasse.
11 Kwa hiyo Gadi akamwendea Daudi akamwambia, “Hili ndilo Bwana asemalo: ‘Chagua:
Gad vint donc vers David, et lui dit: Ainsi a dit l'Éternel:
12 miaka mitatu ya njaa, au miezi mitatu ya kushindwa na adui zako, ukipatwa na upanga wao, au siku tatu za upanga wa Bwana, yaani, siku tatu za tauni katika nchi na malaika wa Bwana akiangamiza kila mahali katika Israeli.’ Sasa basi, amua jinsi nitakavyomjibu yeye aliyenituma.”
Accepte, ou trois années de famine, ou trois mois de défaites devant tes adversaires, atteint par l'épée de tes ennemis, ou pendant trois jours l'épée de l'Éternel et la peste dans le pays, et l'ange de l'Éternel exerçant la destruction dans tout le territoire d'Israël. Vois maintenant ce que je dois répondre à celui qui m'envoie.
13 Daudi akamwambia Gadi, “Ninayo mahangaiko makubwa. Mimi na nianguke mikononi mwa Bwana kwa maana rehema zake ni kuu mno, lakini usiniache niangukie mikononi mwa wanadamu.”
Et David répondit à Gad: Je suis dans une grande angoisse. Que je tombe, je te prie, entre les mains de l'Éternel; car ses compassions sont en très grand nombre; et que je ne tombe pas entre les mains des hommes!
14 Basi Bwana akatuma tauni katika Israeli, watu 70,000 wa Israeli wakafa.
Alors l'Éternel envoya la peste sur Israël, et il tomba soixante et dix mille hommes d'Israël.
15 Mungu akapeleka malaika kuangamiza Yerusalemu. Lakini malaika alipokuwa akifanya hivyo, Bwana akaona na akahuzunika kwa sababu ya maafa, akamwambia yule malaika aliyekuwa anaangamiza watu, “Yatosha! Rudisha mkono wako.” Wakati huo malaika wa Bwana alikuwa amesimama katika sakafu ya kupuria nafaka ya Arauna Myebusi.
Dieu envoya aussi un ange à Jérusalem pour la ravager. Et comme il ravageait, l'Éternel regarda, et se repentit de ce mal, et il dit à l'ange qui ravageait: Assez! Retire maintenant ta main. Or l'ange de l'Éternel se tenait près de l'aire d'Ornan, le Jébusien.
16 Daudi akayainua macho yake akamwona huyo malaika wa Bwana akiwa amesimama katikati ya mbingu na dunia, naye ameunyoosha upanga wake juu ya Yerusalemu tayari kuangamiza. Kisha Daudi na wazee, waliokuwa wamevaa nguo za gunia, wakaanguka kifudifudi.
Et David leva les yeux et vit l'ange de l'Éternel se tenant entre la terre et le ciel, ayant en sa main son épée nue étendue sur Jérusalem. Et David et les anciens, couverts de sacs, tombèrent sur leurs faces.
17 Daudi akamwambia Mungu, “Je, si mimi ndiye niliyeamuru watu wahesabiwe? Mimi ndiye niliyetenda dhambi na kukosa. Hawa ni kondoo tu. Wamefanya nini? Ee Bwana, Mungu wangu, mkono wako na uwe juu yangu mimi na jamaa yangu, lakini usiache tauni hii iendelee juu ya watu wako.”
Et David dit à Dieu: N'est-ce pas moi qui ai commandé qu'on fît le dénombrement du peuple? C'est moi qui ai péché et qui ai très mal agi; mais ces brebis, qu'ont-elles fait? Éternel, mon Dieu! que ta main soit sur moi, je te prie, et sur la maison de mon père, mais qu'elle ne soit pas sur ton peuple, pour le frapper!
18 Kisha malaika wa Bwana akamwamuru Gadi amwambie Daudi apande na kumjengea Bwana madhabahu kwenye sakafu ya kupuria nafaka ya Arauna Myebusi.
Et l'ange de l'Éternel dit à Gad de dire à David, qu'il montât pour dresser un autel à l'Éternel, dans l'aire d'Ornan, le Jébusien.
19 Kwa hiyo Daudi akakwea, akalitii lile neno ambalo Gadi alikuwa amelisema katika jina la Bwana.
David monta donc, selon la parole que Gad avait dite au nom de l'Éternel.
20 Arauna alipokuwa akipura ngano, akageuka akamwona yule malaika. Wanawe wanne waliokuwa pamoja naye wakajificha, yeye akaendelea kupura ngano.
Or Ornan, s'étant retourné, avait vu l'ange, et ses quatre fils s'étaient cachés avec lui. Ornan foulait du froment.
21 Kisha Daudi akakaribia, Arauna alipotazama na kumwona, akaondoka kwenye uwanja wa kupuria nafaka akamsujudia Daudi akiuinamisha uso wake ardhini.
Et David vint vers Ornan; et Ornan regarda, et, ayant vu David, il sortit de l'aire, et se prosterna devant David, le visage contre terre.
22 Daudi akamwambia, “Nipatie huu uwanja wako wa kupuria nafaka ili niweze kujenga madhabahu ya Bwana tauni ipate kukomeshwa katika watu. Niuzie kwa bei yake kamili.”
Alors David dit à Ornan: Donne-moi la place de cette aire, et j'y bâtirai un autel à l'Éternel; donne-la-moi pour le prix qu'elle vaut, afin que cette plaie soit arrêtée de dessus le peuple.
23 Arauna akamwambia Daudi, “Uchukue huo uwanja. Mfalme bwana wangu na afanye lolote analopenda. Tazama, nitatoa maksai kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa, vifaa vya kupuria kuwa kuni, pamoja na ngano kwa ajili ya dhabihu ya nafaka. Natoa hivi vyote.”
Mais Ornan dit à David: Prends-la, et que le roi mon seigneur fasse ce qui lui semblera bon. Voici, je donne les bœufs pour les holocaustes, les instruments à fouler le blé, au lieu de bois, et le froment pour l'offrande; je donne tout cela.
24 Lakini Mfalme Daudi akamjibu Arauna, “La hasha! Lakini ninasisitiza kwamba nitalipa bei yake kamili. Sitachukua kilicho chako kwa ajili ya Bwana au kutoa sadaka ya kuteketezwa ambayo hainigharimu chochote.”
Le roi David dit à Ornan: Non, mais je veux l'acheter ce que cela vaut; car je ne présenterai point à l'Éternel ce qui est à toi, et je n'offrirai point un holocauste qui ne me coûte rien.
25 Basi Daudi akamlipa Arauna shekeli za dhahabu 600 kwa ajili ya ule uwanja.
David donna donc à Ornan pour cette place, en sicles d'or, le poids de six cents sicles.
26 Kisha Daudi akamjengea Bwana madhabahu mahali hapo, na kutoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani. Akamwita Bwana naye Bwana akajibu maombi yake kwa moto toka mbinguni juu ya madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa.
Et David bâtit là un autel à l'Éternel, offrit des holocaustes et des sacrifices de prospérités, et invoqua l'Éternel, qui lui répondit par le feu qui descendit du ciel sur l'autel de l'holocauste.
27 Kisha Bwana akanena na yule malaika, naye akarudisha upanga wake katika ala yake.
Alors l'Éternel parla à l'ange, qui remit son épée dans le fourreau.
28 Wakati huo, Daudi alipoona kwamba Bwana amemjibu kule kwenye uwanja wa kupuria nafaka wa Arauna Myebusi, akatoa dhabihu huko.
En ce temps-là, David, voyant que l'Éternel l'avait exaucé dans l'aire d'Ornan, le Jébusien, y offrait des sacrifices.
29 Maskani ya Bwana ambayo Mose aliitengeneza kule jangwani, pamoja na madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa kwa wakati huo vilikuwa viko mahali pa juu pa kuabudia huko Gibeoni.
Mais la Demeure de l'Éternel, que Moïse avait faite au désert, et l'autel des holocaustes, étaient, en ce temps-là, sur le haut lieu de Gabaon.
30 Lakini Daudi hakuthubutu kuisogelea ili kumuuliza Mungu, kwa sababu aliuogopa upanga wa yule malaika wa Bwana.
Et David ne put pas aller devant cet autel pour chercher Dieu, parce qu'il était épouvanté à cause de l'épée de l'ange de l'Éternel.

< 1 Nyakati 21 >