< 1 Nyakati 18 >

1 Baada ya muda, Daudi akawashinda Wafilisti na kuwatiisha, naye akautwaa Gathi pamoja na vijiji vinavyouzunguka kutoka utawala wa Wafilisti.
And after this it came to pass, that David smote the Philistines, and subdued them, and took Gath and its towns out of the hand of the Philistines.
2 Pia Daudi akawashinda Wamoabu, wakawa watumishi wake, nao wakawa wanamletea ushuru.
And he smote Moab; and the Moabites became servants to David, and brought presents.
3 Zaidi ya hayo, Daudi akapigana na Hadadezeri mfalme wa Soba, hadi Hamathi, wakati alikwenda kuimarisha utawala wake katika Mto Frati.
And David smote Hadarezer king of Zobah by Hamath, as he went to establish his dominion at the river Euphrates.
4 Daudi akateka magari ya vita 1,000 miongoni mwa magari yake, waendesha hayo magari ya kukokotwa na farasi 7,000 na askari wa miguu 20,000. Daudi akakata mishipa ya miguu ya nyuma ya farasi wote wakokotao magari, ila akabakiza 100.
And David took from him a thousand chariots, and seven thousand horsemen, and twenty thousand footmen; and David houghed all the chariot horses, but reserved of them for a hundred chariots.
5 Waaramu wa Dameski, walipokuja kumsaidia Hadadezeri mfalme wa Soba, Daudi akawashambulia na kuwaua 22,000 miongoni mwao.
And when the Arameans of Damascus came to succour Hadarezer king of Zobah, David smote of the Arameans two and twenty thousand men.
6 Daudi akaweka askari walinzi katika ufalme wa Waaramu huko Dameski. Basi Waaramu wakawa watumwa wa Daudi, na kumlipa ushuru. Bwana akampa Daudi ushindi kote alipokwenda.
Then David put garrisons in Aram Damascus; and the Arameans became servants to David, and brought presents. And the LORD gave victory to David whithersoever he went.
7 Daudi akazitwaa ngao za dhahabu zilizokuwa za maafisa wa Hadadezeri na kuzileta Yerusalemu.
And David took the shields of gold that were on the servants of Hadarezer, and brought them to Jerusalem.
8 Kutoka miji ya Tibhathi na Kuni, iliyokuwa miji ya Hadadezeri, Daudi akatwaa shaba nyingi sana, ambayo Solomoni aliitumia kutengenezea ile Bahari ya shaba, zile nguzo na vifaa mbalimbali vya shaba.
And from Tibhath and from Cun, cities of Hadarezer, David took very much brass, wherewith Solomon made the brazen sea, and the pillars, and the vessels of brass.
9 Tou mfalme wa Hamathi aliposikia kwamba Daudi amelishinda jeshi lote la Hadadezeri mfalme wa Soba,
And when Tou king of Hamath heard that David had smitten all the host of Hadarezer king of Zobah,
10 akamtuma mwanawe, Hadoramu kwa Mfalme Daudi ili kumsalimu na kumpongeza kwa ushindi wake katika vita dhidi ya Mfalme Hadadezeri, kwa kuwa alikuwa amepigana vita mara nyingi na Tou. Hadoramu akamletea Daudi vifaa mbalimbali vya dhahabu, fedha na shaba.
he sent Hadoram his son to king David, to salute him, and to bless him — because he had fought against Hadarezer and smitten him; for Hadarezer had wars with Tou — and he had with him all manner of vessels of gold and silver and brass.
11 Mfalme Daudi akaviweka vifaa hivi wakfu kwa Bwana kama vile alivyokuwa amefanya kwa fedha na dhahabu aliyokuwa ameitwaa katika mataifa yote haya: Edomu na Moabu, Waamoni, Wafilisti na Waamaleki.
These also did king David dedicate unto the LORD, with the silver and the gold that he carried away from all the nations; from Edom, and from Moab, and from the children of Ammon, and from the Philistines, and from Amalek.
12 Abishai mwana wa Seruya akawaua Waedomu 18,000 katika Bonde la Chumvi.
Moreover Abishai the son of Zeruiah smote of the Edomites in the Valley of Salt eighteen thousand.
13 Akaweka kambi za askari walinzi huko Edomu, nao Waedomu wote wakawa watumishi wa Daudi. Bwana akampa Daudi ushindi kila alipokwenda.
And he put garrisons in Edom; and all the Edomites became servants to David. And the LORD gave victory to David whithersoever he went.
14 Daudi akatawala Israeli yote, akitenda lililo haki na sawa kwa watu wake wote.
And David reigned over all Israel; and he executed justice and righteousness unto all his people.
15 Yoabu mwana wa Seruya alikuwa jemadari wa jeshi; Yehoshafati mwana wa Ahiludi alikuwa mweka kumbukumbu;
And Joab the son of Zeruiah was over the host; and Jehoshaphat the son of Ahilud was recorder.
16 Sadoki mwana wa Ahitubu na Ahimeleki mwana wa Abiathari walikuwa makuhani; Shausha alikuwa mwandishi;
And Zadok the son of Ahitub, and Abimelech the son of Abiathar, were priests; and Shavsha was scribe;
17 naye Benaya mwana wa Yehoyada alikuwa msimamizi wa Wakerethi na Wapelethi; nao wana wa Daudi walikuwa maafisa wakuu katika utumishi wa mfalme.
and Beniah the son of Jehoiada was over the Cherethites and the Pelethites; and the sons of David were chief about the king.

< 1 Nyakati 18 >