< 1 Nyakati 16 >

1 Wakaleta Sanduku la Mungu na kuliweka ndani ya hema ambalo Daudi alikuwa amelisimamisha kwa ajili yake, na wakatoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani mbele za Mungu.
Ils amenèrent donc l'arche de Dieu, et la placèrent dans la tente que David lui avait dressée; et on offrit des holocaustes et des sacrifices de prospérités devant Dieu.
2 Baada ya Daudi kumaliza kutoa hizo sadaka za kuteketezwa na hizo sadaka za amani, akawabariki watu katika jina la Bwana.
Et quand David eut achevé d'offrir les holocaustes et les sacrifices de prospérités, il bénit le peuple au nom de l'Éternel.
3 Kisha akamgawia kila Mwisraeli mwanaume na mwanamke mkate, andazi la tende na andazi la zabibu kavu.
Et il distribua à tous les Israélites, hommes et femmes, à chacun un pain, une portion de viande et un gâteau de raisins.
4 Akawaweka pia baadhi ya Walawi ili wahudumu mbele ya Sanduku la Bwana kufanya maombi, kumshukuru na kumsifu Bwana, Mungu wa Israeli:
Et il établit des Lévites devant l'arche de l'Éternel, pour faire le service, pour célébrer, pour louer, et pour magnifier l'Éternel, Dieu d'Israël:
5 Asafu ndiye alikuwa mkuu wao, akisaidiwa na Zekaria, Yeieli, Shemiramothi, Yehieli, Matithia, Eliabu, Benaya, Obed-Edomu na Yeieli. Hawa ndio wangepiga zeze na vinubi, Asafu angepiga matoazi,
Asaph, le chef; Zacharie, le second après lui, Jéiel, Shémiramoth, Jéhiel, Matthithia, Éliab, Bénaja, Obed-Édom, et Jeïel, avec des instruments de musique, des lyres et des harpes; et Asaph faisait retentir les cymbales.
6 nao Benaya na Yahazieli makuhani, ndio wangepiga tarumbeta mara kwa mara mbele ya Sanduku la Agano la Mungu.
Bénaja et Jachaziel, sacrificateurs, étaient continuellement avec des trompettes devant l'arche de l'alliance de Dieu.
7 Siku ile, kitu cha kwanza Daudi alichofanya ni kumkabidhi Asafu na wenzake zaburi hii ya shukrani kwa Bwana:
Ce jour-là, pour la première fois, David chargea Asaph et ses frères de célébrer l'Éternel, comme suit:
8 Mshukuruni Bwana, liitieni jina lake; wajulisheni mataifa yale aliyoyatenda.
Célébrez l'Éternel, invoquez son nom! Faites connaître parmi les peuples ses hauts faits!
9 Mwimbieni yeye, mwimbieni yeye sifa; waambieni matendo yake yote ya ajabu.
Chantez-lui, psalmodiez-lui! Parlez de toutes ses merveilles!
10 Lishangilieni jina lake takatifu; mioyo ya wale wamtafutao Bwana na ifurahi.
Glorifiez-vous de son saint nom! Que le cœur de ceux qui cherchent l'Éternel se réjouisse!
11 Mtafuteni Bwana na nguvu zake; utafuteni uso wake siku zote.
Recherchez l'Éternel et sa force; cherchez continuellement sa face!
12 Kumbuka matendo ya ajabu aliyoyafanya, miujiza yake na hukumu alizozitamka,
Souvenez-vous des merveilles qu'il a faites, de ses miracles, et des jugements de sa bouche,
13 enyi wazao wa Israeli mtumishi wake, enyi wana wa Yakobo, wateule wake.
Vous, postérité d'Israël, son serviteur, enfants de Jacob, ses élus!
14 Yeye ndiye Bwana Mungu wetu; hukumu zake zimo duniani pote.
C'est lui, l'Éternel, qui est notre Dieu; ses jugements sont sur toute la terre.
15 Hulikumbuka agano lake milele, neno ambalo aliamuru, kwa vizazi elfu,
Souvenez-vous toujours de son alliance, de sa promesse établie pour mille générations;
16 agano alilolifanya na Abrahamu, kiapo alichomwapia Isaki.
Du traité qu'il fit avec Abraham, du serment qu'il fit à Isaac,
17 Alilithibitisha kwa Yakobo kuwa amri, kwa Israeli liwe agano la milele:
Et qu'il a confirmé à Jacob, pour être un statut, à Israël, pour être une alliance éternelle,
18 “Nitakupa wewe nchi ya Kanaani kuwa sehemu utakayoirithi.”
En disant: Je te donnerai le pays de Canaan; c'est le lot de votre héritage;
19 Walipokuwa wachache kwa idadi, wachache sana na wageni ndani yake,
Lorsqu'ils n'étaient qu'une poignée de gens, peu nombreux et étrangers dans le pays,
20 walitangatanga kutoka taifa moja hadi jingine, kutoka ufalme mmoja hadi mwingine.
Allant de nation en nation et d'un royaume vers un autre peuple.
21 Hakuruhusu mtu yeyote awaonee; kwa ajili yao aliwakemea wafalme, akisema:
Il ne permit à personne de les opprimer, et il châtia des rois à cause d'eux,
22 “Msiwaguse niliowatia mafuta; msiwadhuru manabii wangu.”
Disant: Ne touchez pas à mes oints, et ne faites point de mal à mes prophètes.
23 Mwimbieni Bwana dunia yote; tangazeni wokovu wake siku baada ya siku.
Vous, toute la terre, chantez à l'Éternel; annoncez de jour en jour son salut;
24 Tangazeni utukufu wake katikati ya mataifa, matendo yake ya ajabu miongoni mwa mataifa yote.
Racontez sa gloire parmi les nations, ses merveilles parmi tous les peuples.
25 Kwa kuwa Bwana ni mkuu, mwenye kustahili kusifiwa kuliko wote; yeye ni wa kuogopwa kuliko miungu yote.
Car l'Éternel est grand, et digne de grandes louanges; il est redoutable par-dessus tous les dieux.
26 Kwa maana miungu yote ya mataifa ni sanamu, lakini Bwana aliziumba mbingu.
Car tous les dieux des peuples sont des idoles! mais l'Éternel a fait les cieux.
27 Fahari na enzi viko mbele yake; nguvu na utukufu vimo patakatifu pake.
La splendeur et la majesté sont devant lui; la force et la joie sont dans sa Demeure.
28 Mpeni Bwana, enyi jamaa za mataifa, mpeni Bwana utukufu na nguvu,
Rendez à l'Éternel, familles des peuples, rendez à l'Éternel la gloire et la force!
29 mpeni Bwana utukufu unaostahili jina lake. Leteni sadaka na mje katika nyua zake; mwabuduni Bwana katika uzuri wa utakatifu wake.
Rendez à l'Éternel la gloire due à son nom. Apportez des offrandes, et présentez-vous devant lui; prosternez-vous devant l'Éternel avec des ornements sacrés!
30 Dunia yote na itetemeke mbele zake! Ulimwengu ameuweka imara; hauwezi kusogezwa.
Tremblez devant lui, vous, toute la terre. Le monde est ferme et ne chancelle point.
31 Mbingu na zishangilie, nchi na ifurahi; semeni katikati ya mataifa, “Bwana anatawala!”
Que les cieux se réjouissent, et que la terre tressaille de joie; qu'on dise parmi les nations: L'Éternel règne!
32 Bahari na ivume, na vyote vilivyomo ndani yake; mashamba na yashangilie, na vyote vilivyomo ndani yake.
Que la mer retentisse, avec tout ce qu'elle contient; que les campagnes s'égaient, avec tout ce qui est en elles!
33 Kisha miti ya msituni itaimba, itaimba kwa furaha mbele za Bwana, kwa maana anakuja kuihukumu dunia.
Que les arbres des forêts chantent de joie devant l'Éternel! Car il vient pour juger la terre.
34 Mshukuruni Bwana kwa kuwa ni mwema; upendo wake wadumu milele.
Célébrez l'Éternel, car il est bon, car sa miséricorde demeure à toujours!
35 Mlilieni, “Ee Mungu Mwokozi wetu, tuokoe. Tukusanye tena na utukomboe kutoka kwa mataifa, ili tuweze kulishukuru jina lako takatifu, na kushangilia katika sifa zako.”
Dites: Sauve-nous, Dieu de notre salut! Rassemble-nous, et nous retire d'entre les nations, afin que nous célébrions ton saint nom, et que nous nous glorifiions dans tes louanges.
36 Atukuzwe Bwana, Mungu wa Israeli, tangu milele na hata milele. Nao watu wote wakasema, “Amen,” na “Msifuni Bwana.”
Béni soit l'Éternel, le Dieu d'Israël, de siècle en siècle! Et tout le peuple dit: Amen, et loua l'Éternel.
37 Daudi akamwacha Asafu na wenzake mbele ya Sanduku la Agano la Bwana ili wahudumu humo mara kwa mara, kulingana na mahitaji ya kila siku.
Puis David laissa là, devant l'arche de l'alliance de l'Éternel, Asaph et ses frères, pour faire continuellement le service, devant l'arche, chaque chose à son jour;
38 Pia akamwacha Obed-Edomu pamoja na wenzake sitini na wanane wahudumu pamoja nao. Obed-Edomu mwana wa Yeduthuni na pia Hosa walikuwa mabawabu wa lango.
Et Obed-Édom et Hosa, avec leurs frères, au nombre de soixante-huit, Obed-Édom, fils de Jédithun, et Hosa, pour portiers;
39 Daudi akamwacha kuhani Sadoki pamoja na makuhani wenzake mbele ya hema ya ibada ya Bwana katika mahali pa juu pa kuabudia huko Gibeoni
Et il établit Tsadok le sacrificateur, et ses frères les sacrificateurs, devant la Demeure de l'Éternel, sur le haut lieu qui était à Gabaon,
40 ili kutoa sadaka za kuteketezwa kwa Bwana kwenye madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa mara kwa mara, asubuhi na jioni, sawasawa na kila kitu kilichoandikwa katika sheria ya Bwana ambayo alikuwa amempa Israeli.
Pour offrir continuellement des holocaustes à l'Éternel sur l'autel des holocaustes, le matin et le soir, et selon tout ce qui est écrit dans la loi de l'Éternel, qu'il a prescrite à Israël.
41 Waliohudumu pamoja nao walikuwa Hemani, Yeduthuni na wale wote waliochaguliwa na kutajwa kwa jina kumpa Bwana shukrani, “Kwa maana fadhili zake zadumu milele.”
Avec eux étaient Héman et Jéduthun, et les autres qui furent choisis, et désignés par leurs noms, pour louer l'Éternel; car sa miséricorde dure éternellement.
42 Hemani na Yeduthuni walikuwa na wajibu wa kupiga tarumbeta, matoazi na kutumia vyombo vingine kwa ajili ya nyimbo za sifa kwa Mungu. Wana wa Yeduthuni waliwekwa langoni.
Héman et Jéduthun étaient avec eux, avec des trompettes et des cymbales pour ceux qui les faisaient retentir, et des instruments pour les cantiques de Dieu. Les fils de Jéduthum étaient portiers.
43 Kisha watu wote wakaondoka, kila mmoja akarudi nyumbani kwake, naye Daudi akarudi nyumbani kuibariki jamaa yake.
Puis tout le peuple s'en alla, chacun dans sa maison; David aussi s'en retourna pour bénir sa maison.

< 1 Nyakati 16 >