< 1 Nyakati 14 >

1 Basi Hiramu mfalme wa Tiro akawatuma wajumbe kwa Daudi, wakiwa na magogo ya mierezi, waashi na maseremala ili kumjengea jumba la kifalme.
Et Hiram Roi de Tyr envoya des messagers à David, et du bois de cèdre, et des maçons, et des charpentiers, pour lui bâtir une maison.
2 Naye Daudi akatambua kwamba Bwana amemwimarisha kuwa mfalme juu ya Israeli na kwamba ufalme wake umetukuzwa kwa ajili ya Israeli, watu wake.
Alors David connut que l'Eternel l'avait affermi Roi sur Israël, parce que son règne avait été fort élevé, pour l'amour de son peuple d'Israël.
3 Huko Yerusalemu Daudi akaoa wake wengine zaidi na akawa baba wa wana na mabinti wengi.
Et David prit encore des femmes à Jérusalem, et il engendra encore des fils et des filles.
4 Haya ndiyo majina ya watoto waliozaliwa kwake huko: Shamua, Shobabu, Nathani, Solomoni,
Et ce sont ici les noms des enfants qu'il eut à Jérusalem, Sammuah, Sobab, Nathan, Salomon,
5 Ibihari, Elishua, Elpeleti,
Jibhar, Elisuah, Elpélet,
6 Noga, Nefegi, Yafia,
Nogah, Népheg, Japhiah,
7 Elishama, Beeliada na Elifeleti.
Elisamah, Béël-jadah, et Eliphelet.
8 Wafilisti waliposikia kuwa Daudi ametiwa mafuta kuwa mfalme wa Israeli yote, wakapanda na jeshi lao lote kwenda kumsaka, lakini Daudi akapata habari hizo, naye akatoka ili kwenda kukabiliana nao.
Or quand les Philistins eurent su que David avait été oint pour Roi sur tout Israël, ils montèrent tous pour chercher David; et David l'ayant appris, sortit au devant d'eux.
9 Basi Wafilisti walikuwa wameingia na kushambulia Bonde la Warefai,
Et les Philistins vinrent, et se répandirent dans la vallée des Réphaïms.
10 Hivyo Daudi akamuuliza Mungu: “Je, niende kuwashambulia hao Wafilisti? Je, utawatia mikononi mwangu?” Bwana akamjibu, “Nenda, nitawatia mikononi mwako.”
Et David consulta Dieu, en disant: Monterai-je contre les Philistins, et les livreras-tu entre mes mains? Et l'Eternel lui répondit: Monte, et je les livrerai entre tes mains.
11 Hivyo Daudi pamoja na watu wake wakakwea mpaka Baal-Perasimu, akawashinda huko. Akasema, “Kama maji yafurikavyo, Mungu amewafurikia adui zangu kwa kutumia mkono wangu.” Kwa hiyo mahali pale pakaitwa Baal-Perasimu.
Alors ils montèrent à Bahal-pératsim, et David les battit là; et il dit: Dieu a fait écouler mes ennemis par ma main, comme un débordement d'eaux; c'est pourquoi on nomma ce lieu-là Bahal-pératsim.
12 Wafilisti walikuwa wameacha miungu yao huko, Daudi akaamuru iteketezwe kwa moto.
Et ils laissèrent là leurs dieux; et David commanda qu'on les brûlât au feu.
13 Kwa mara nyingine Wafilisti wakavamia lile bonde;
Et les Philistins se répandirent encore une autre fois dans cette même vallée.
14 hivyo Daudi akamuuliza Mungu tena, naye Mungu akamjibu, “Usiwapandie moja kwa moja, bali wazungukie na uwashambulie kutoka mbele ya hiyo miti ya miforosadi.
Et David consulta encore Dieu; et Dieu lui répondit: Tu ne monteras point vers eux, mais tu tournoieras autour d'eux, et tu iras contr'eux vis-à-vis des mûriers.
15 Mara usikiapo sauti ya kwenda juu ya hiyo miti ya miforosadi, hapo ndipo utoke upigane vita, kwa sababu hiyo itaonyesha kwamba Mungu amekutangulia ili kupiga jeshi la Wafilisti.”
Et sitôt que tu auras entendu aux sommets des mûriers un bruit [comme de gens] qui marchent, tu sortiras alors au combat; car Dieu sera sorti devant toi pour frapper le camp des Philistins.
16 Kwa hiyo Daudi akafanya kama alivyoagizwa na Mungu, wakalipiga jeshi la Wafilisti kuanzia Gibeoni hadi Gezeri.
David donc fit selon ce que Dieu lui avait commandé; et on frappa le camp des Philistins, depuis Gabaon jusqu'à Guézer.
17 Hivyo umaarufu wa Daudi ukaenea katika kila nchi, naye Bwana akayafanya mataifa yote kumwogopa Daudi.
Ainsi la renommée de David se répandit par tous ces pays-là; et l'Eternel remplit de frayeur toutes ces nations-là, [au seul nom de David].

< 1 Nyakati 14 >