< 1 Nyakati 11 >

1 Israeli yote walimjia Daudi kwa pamoja huko Hebroni wakamwambia, “Sisi ni nyama yako na damu yako.
Then all Israel gathered together to David at Hebron, saying, "Look, we are your bone and your flesh.
2 Zamani, wakati Sauli alikuwa mfalme, wewe ndiwe uliyeiongoza Israeli vitani, naye Bwana Mungu wako alikuambia, ‘Wewe utawachunga watu wangu Israeli, na utakuwa mtawala wao.’”
In times past, even when Saul was king, it was you who led out and brought in Israel. Jehovah your God said to you, 'You shall be shepherd of my people Israel, and you shall rule over my people Israel.'"
3 Wazee wote wa Israeli walipokuwa wamewasili kwa Mfalme Daudi huko Hebroni, alifanya mapatano nao huko Hebroni mbele za Bwana, nao wakamtia Daudi mafuta awe mfalme wa Israeli, sawasawa na Bwana alivyoahidi kupitia kwa Samweli.
So all the elders of Israel came to the king to Hebron; and David made a covenant with them in Hebron before Jehovah; and they anointed David king over Israel, according to the word of Jehovah by Samuel.
4 Daudi na Waisraeli wote wakaenda Yerusalemu (ndio Yebusi). Nao Wayebusi walioishi humo
David and all Israel went to Jerusalem (that is, Jebus); and the Jebusites, the inhabitants of the land, were there.
5 wakamwambia Daudi, “Wewe hutaingia humu.” Hata hivyo, Daudi akaiteka ngome ya Sayuni, Mji wa Daudi.
The inhabitants of Jebus said to David, "You shall not come in here." Nevertheless David took the stronghold of Zion, that is, the City of David.
6 Daudi alikuwa amesema, “Yeyote aongozaye mashambulizi dhidi ya Wayebusi, atakuwa jemadari mkuu.” Yoabu mwana wa Seruya akawa wa kwanza kukwea, naye akawa mkuu.
David said, "Whoever strikes the Jebusites first shall be chief and captain." Joab the son of Zeruiah went up first, and was made chief.
7 Daudi akafanya makao yake kwenye ngome, hivyo ukaitwa Mji wa Daudi.
David lived in the stronghold; therefore they called it the City of David.
8 Akajenga mji pande zote, kuanzia kwenye mito hadi kwenye ukuta kuzunguka, wakati huo huo Yoabu akajenga sehemu zingine zilizobaki za Yerusalemu.
He built the city all around, from the Millo even around; and Joab repaired the rest of the city.
9 Daudi akazidi kuwa na nguvu zaidi na zaidi, kwa sababu Bwana Mwenye Nguvu Zote alikuwa pamoja naye.
David grew greater and greater; for Jehovah of hosts was with him.
10 Hawa ndio waliokuwa wakuu wa mashujaa wa Daudi: wao pamoja na Israeli wote wakauimarisha ufalme wake ili kuenea katika nchi yote, kama Bwana alivyoahidi.
Now these are the chief of the warriors whom David had, who gave him strong support in his kingdom, together with all Israel, to make him king, according to the word of Jehovah concerning Israel.
11 Hii ndio orodha ya mashujaa wa Daudi: Yashobeamu, Mhakmoni, alikuwa mkuu wa maafisa; yeye aliinua mkuki wake dhidi ya watu 300, ambao aliwaua katika pambano moja.
This is the number of the warriors whom David had: Jeshbaal the son of Hachmoni, leader of the Three. And he wielded his spear against eight hundred and killed them at one time.
12 Aliyefuata alikuwa Eleazari, mwana wa Dodai, Mwahohi, mmojawapo wa wale mashujaa watatu.
After him was Eleazar the son of Dodo, the Ahohite, who was one of the Three warriors.
13 Huyo alikuwa pamoja na Daudi huko Pas-Damimu, wakati Wafilisti walikusanyika huko kwa ajili ya vita. Huko ambapo kulikuwa na shamba lililokuwa limejaa shayiri, vikosi vya Israeli vikawakimbia Wafilisti.
He was with David at Pas Dammim, and there the Philistines were gathered together to battle, where there was a plot of ground full of barley; and the people fled from before the Philistines.
14 Lakini Eleazari na Daudi wakasimama imara katikati ya lile shamba, nao wakalishindania na wakawaua Wafilisti. Naye Bwana akawapa ushindi mkubwa.
And he took his stand in the midst of the plot, and defended it, and killed the Philistines; and Jehovah saved them by a great victory.
15 Wakuu watatu miongoni mwa wale thelathini, walimwendea Daudi katika mwamba huko kwenye pango la Adulamu, wakati kikundi cha Wafilisti kilikuwa kimepiga kambi katika Bonde la Warefai.
And three of the Thirty chief men went down to the rock to David, into the cave of Adullam; and the army of the Philistines were camped in the Valley of Rephaim.
16 Wakati huo Daudi alikuwa katika ngome, na kambi ya Wafilisti ilikuwa huko Bethlehemu.
David was then in the stronghold, and the garrison of the Philistines was then in Bethlehem.
17 Daudi akatamani maji, akasema, “Laiti mtu angenipatia maji ya kunywa kutoka kisima kilichoko karibu na lango la Bethlehemu!”
And David had a craving and said, "Oh that one would give me water to drink of the well of Bethlehem, which is by the gate."
18 Kwa hivyo wale watatu, wakapita katikati ya safu za Wafilisti, wakachota maji kutoka kwa kisima kilicho karibu na lango la Bethlehemu, wakamletea Daudi. Lakini yeye akakataa kuyanywa. Badala yake, aliyamimina mbele za Bwana.
The Three broke through the army of the Philistines, and drew water out of the well of Bethlehem, that was by the gate, and took it, and brought it to David: but David would not drink of it, but poured it out to Jehovah,
19 Akasema, “Mungu apishie mbali kwamba nifanye hivi! Je kweli, niinywe damu ya watu hawa waliohatarisha maisha yao?” Kwa sababu walihatarisha maisha yao kuyaleta yale maji, Daudi hakukubali kuyanywa. Huo ndio uliokuwa ujasiri wa wale mashujaa watatu.
and said, "My God forbid it me, that I should do this. Shall I drink the blood of these men who have put their lives in jeopardy?" For they risked their lives to bring it. Therefore he would not drink it. The Three warriors did these things.
20 Abishai, ndugu yake Yoabu ndiye alikuwa kiongozi wa hao Watatu. Aliinua mkuki wake dhidi ya watu 300, ambao aliwaua, kwa hiyo naye akawa na sifa kama hao Watatu.
And Abishai, the brother of Joab, was leader of the Thirty. And he wielded his spear against three hundred and killed them, and had a name beside the Three.
21 Alitunukiwa heshima maradufu ya wale Watatu, akawa jemadari wao, ingawa hakuhesabiwa miongoni mwao.
He was the most illustrious of the Thirty, and he became their leader. However, he did not attain to the Three.
22 Benaya, mwana wa Yehoyada alikuwa mpiganaji hodari kutoka Kabseeli ambaye alifanya mambo makubwa ya ujasiri. Aliwaua mashujaa wawili waliokuwa hodari kuliko wote wa Moabu. Pia alishuka shimoni kulipokuwa na theluji na kumuua simba.
Benaiah the son of Jehoiada was a valiant man of Kabzeel, who performed great deeds. He killed the two of Ariel of Moab. He also went down and killed a lion in the midst of a pit in time of snow.
23 Alimuua Mmisri aliyekuwa na urefu kama dhiraa tano. Ingawa Mmisri alikuwa na mkuki kama mti wa mfumaji mkononi mwake, Benaya alimwendea na rungu. Akamnyangʼanya Mmisri mkuki wake na kumuua nao.
He killed an Egyptian, a man of great stature, seven feet five inches tall; and in the Egyptian's hand was a spear like a weaver's beam; and he went down to him with a staff, and grabbed the spear out of the Egyptian's hand, and killed him with his own spear.
24 Haya yalikuwa mambo ya ushujaa ya Benaya mwana wa Yehoyada; naye pia alikuwa maarufu kama wale mashujaa watatu.
Benaiah the son of Jehoiada did these things, and had a name among the Three warriors.
25 Yeye aliheshimiwa zaidi ya wale Thelathini, lakini hakujumuishwa miongoni mwa wale Watatu: Daudi akamweka kuwa kiongozi wa walinzi wake.
Look, he was more honored than the Thirty, but he did not attain to the Three. And David set him over his guard.
26 Wale watu mashujaa walikuwa: Asaheli nduguye Yoabu, Elhanani mwana wa Dodo kutoka Bethlehemu,
Also the warriors of the armies: Asahel the brother of Joab, Elhanan the son of Dodo of Bethlehem,
27 Shamothi Mharori, Helesi Mpeloni,
Shammah the Harodite, Elika the Harodite, Helez the Paltite,
28 Ira mwana wa Ikeshi kutoka Tekoa, Abiezeri kutoka Anathothi,
Ira the son of Ikkesh the Tekoite, Abiezer the Anathothite,
29 Sibekai Mhushathi, Ilai Mwahohi,
Sibbekai the Hushathite, Zalmon the Ahohite,
30 Maharai Mnetofathi, Heledi mwana wa Baana, Mnetofathi,
Maharai the Netophathite, Heled the son of Baanah the Netophathite,
31 Itai mwana wa Ribai kutoka Gibea ya Benyamini, Benaya Mpirathoni,
Ithai the son of Ribai of Gibeah of the people of Benjamin, Benaiah the Pirathonite,
32 Hurai kutoka mabonde ya Gaashi, Abieli Mwaribathi,
Hiddai of Nahale Gaash, Abiel the Arbathite,
33 Azmawethi Mbaharumi, Eliaba Mshaalboni,
Azmaveth the Bahurimite, Eliahba the Shaalbinite,
34 wana wa Hashemu Mgiloni, Yonathani mwana wa Shagee Mharari,
Jashen the Gizonite, Jonathan the son of Shamma the Hararite,
35 Ahiamu mwana wa Sakari Mharari, Elifale mwana wa Uru,
Ahiam the son of Sakar the Hararite, Eliphelet the son of Ahasbai the Maacathite,
36 Heferi Mmekerathi, Ahiya Mpeloni,
Eliam the son of Ahithophel the Gilonite,
37 Hezro Mkarmeli, Naarai mwana wa Ezbai,
Hezrai the Carmelite, Paarai the Archite,
38 Yoeli nduguye Nathani, Mibhari mwana wa Hagri,
Igal the son of Nathan, from the elite troops of the Hagrites,
39 Seleki Mwamoni, Naharai Mbeerothi, mbeba silaha wa Yoabu mwana wa Seruya,
Zelek the Ammonite, Naharai the Beerothite, the armor bearer of Joab the son of Zeruiah,
40 Ira Mwithiri, Garebu Mwithiri,
Ira the Jattirite, Gareb the Jattirite,
41 Uria Mhiti, Zabadi mwana wa Alai,
Uriah the Hethite, Zabad the son of Ahlai,
42 Adina mwana wa Shiza Mreubeni, ambaye alikuwa mkuu wa Wareubeni, akiwa pamoja na watu thelathini,
Adina the son of Shiza the Reubenite, a chief of the Reubenites, and thirty with him,
43 Hanani mwana wa Maaka, Yoshafati Mmithni,
Hanan the son of Maacah, and Joshaphat the Mithnite,
44 Uzia Mwashterathi, Shama na Yeieli wana wa Hothamu Mwaroeri,
Uzzia the Ashterathite, Shama and Jeiel the sons of Hotham the Aroerite,
45 Yediaeli mwana wa Shimri, nduguye Yoha Mtizi,
Jediael the son of Shimri, and Joha his brother, the Tizite,
46 Elieli Mmahawi, Yeribai na Yoshavia wana wa Elnaamu, Ithma Mmoabu,
Eliel the Mahavite, and Jeribai, and Joshaviah, the sons of Elnaam, and Ithmah the Moabite,
47 Elieli, na Obedi na Yaasieli Mmesobai.
Eliel, and Obed, and Jaasiel the Mezobaiah.

< 1 Nyakati 11 >