< Salmos 18 >

1 Amarte he, Jehová, fortaleza mía.
Nakupenda, Yahwe, nguvu yangu.
2 Jehová, roca mía, y castillo mío, y escapador mío; Dios mío, fuerte mío: confiarme he en él: escudo mío, y el cuerno de mi salud; refugio mío.
Yahwe ni mwamba wangu, ngome yangu, yeye ambaye aniwekae kweye usalama; yeye ni Mungu wangu, mwamba wangu; ninapata kimbilio kwake. Yeye ni ngao yangu, pembe ya wokovu wangu, na ngome yangu.
3 Al alabado Jehová invocaré, y seré salvo de mis enemigos.
Nitamuita Yahwe kwa sababu anastahili kusifiwa, na nitaokolewa kutoka kwa adui zangu.
4 Cercáronme dolores de muerte, y arroyos de perversidad me atemorizaron:
Kamba za mauti zilinizunguka, na mafuriko yakimbiayo yalinielemea.
5 Dolores del sepulcro me rodearon; anticipáronme lazos de muerte: (Sheol h7585)
Kamba za kuzimu zilinizunguka; mitego ya mauti ilininasa. (Sheol h7585)
6 En mi angustia llamé a Jehová, y clamé a mi Dios: él oyó desde su templo mi voz, y mi clamor entró delante de él, en sus orejas.
dhiki yangu nilimuita Yahwe; Niliita msaada kwa Mungu. Naye alisikia sauti yangu kutoka hekaluni mwake; kuita kwangu msaada kulienda mpaka uweponi mwake; na kuingia masikioni pake.
7 Y la tierra fue conmovida y tembló: y los fundamentos de los montes se estremecieron, y se removieron, porque él se enojó.
Kisha nchi ikatikisika na kutetemeka; misingi ya milima pia ilitetemeka na kutikiswa kwa sababu Mungu alikuwa amekasirika.
8 Subió humo en su nariz, y de su boca fuego quemante: carbones se encendieron de él.
Moshi ulifuka kutoka kwenye pua zake, na moto mkali ulitokea mdomoni mwake. Makaa yaliwashwa kwa moto huo.
9 Y abajó los cielos, y descendió; y oscuridad debajo de sus pies.
Yeye alizifunua mbingu na alishuka chini, na giza nene lilikuwa chini ya miguu yake.
10 Y cabalgó sobre un querubín, y voló: y voló sobre las alas del viento.
Alipanda kwenye kerubi na akaruka; alinyiririka kwenye mabawa ya upepo.
11 Puso tinieblas por su escondedero: en sus en derredores de su tabernáculo, oscuridad de aguas, nubes de los cielos.
Yahwe alilifanya giza kuwa hema likimzunguka yeye, wingu la mvua zito katika mbingu.
12 Por el resplandor de delante de él sus nubes pasaron: granizo y carbones de fuego.
Mawe ya barafu na makaa ya moto yalianguka kutoka katika mwangaza kabla yake.
13 Y tronó en los cielos Jehová, y el Altísimo dio su voz: granizo y carbones de fuego.
Yahwe aliongea katika mbingu! Sauti ya aliye juu ilisikika.
14 Y envió sus saetas y desbaratólos: y echó relámpagos, y los destruyó.
Yeye aliifyatua mishale yake na kuwatawanya adui zake; na radi nyingi zenye mwanga alizitawanya katika maeneo tofauti tofauti.
15 Y aparecieron las honduras de las aguas: y descubriéronse los cimientos del mundo por tu reprensión, o! Jehová, por el soplo del viento de tu nariz.
Ndipo mifereji ya maji ilitokea; misingi ya dunia ikadhihirishwa kwa mlio wa pigo lako, Yahwe kwa sauti ya pumzi ya pua zako.
16 Envió desde lo alto, me tomó, me sacó de las muchas aguas.
Yeye alishuka chini kutokea juu; akanishikilia mimi! Akanivuta nje ya maji yafurikayo.
17 Me escapó de mi fuerte enemigo, y de los que me aborrecieron: aunque ellos eran más fuertes que yo.
Aliniokoa kutoka kwa maadui zangu wenye nguvu, kutoka kwa wale ambao walinichukia mimi, kwa kuwa walikuwa na nguvu sana kuliko mimi.
18 Anticipáronme en el día de mi quebrantamiento: mas Jehová me fue por bordón.
Wao walikuja kinyume na mimi katika siku ile ya dhiki yangu lakini Mungu alikuwa msaada wangu!
19 Y me sacó a anchura: me libró, porque se agradó de mí.
Yeye aliniweka huru katika eneo pana la wazi; yeye aliniokoa kwa sababu alipenezwa nami.
20 Jehová me pagará conforme a mi justicia: conforme a la limpieza de mis manos me volverá.
Yahwe amenitunuku mimi kwa sababu ya haki yangu; yeye amenirejesha mimi kwa sababu mikono yangu ilikuwa misafi.
21 Por cuanto guardé los caminos de Jehová: y no me maleé con mi Dios.
Kwa kuwa nimezitunza njia za Yahwe na sijafanya uovu wa kumgeuka Mungu wangu.
22 Porque todos sus juicios estuvieron delante de mí: y no eché de mí sus estatutos.
Kwa kuwa amri zake zote za haki zimekuwa mbele yangu; kama asemavyo, sijaenda kinyume nazo.
23 Y fui perfecto con él: y me recaté de mi maldad.
Pia nimekuwa sina hatia mbele zake, na nimejiweka mwenyewe mbali na dhambi.
24 Y pagóme Jehová conforme a mi justicia: conforme a la limpieza de mis manos delante de sus ojos.
Hivyo Yahwe amenirejesha kwa sababu ya haki yangu, na kwa sababu mikono yangu ilikuwa safi mbele ya macho yake.
25 Con el misericordioso serás misericordioso: y con el varón perfecto serás perfecto.
Kwa yeyote aliye mwaminifu, jionyeshe wenyewe kuwa mwaminifu; kwa mtu asiye na lawama, jionyeshe mwenyewe kuwa usiye na lawama.
26 Con el limpio serás limpio, y con el perverso serás perverso.
Kwa yeyote aliye msafi, jionyeshe mwenyewe safi; bali ni mjanja kwa yeyote aliye geuzwa.
27 Por tanto tú al pueblo humilde salvarás: y los ojos altivos humillarás.
Kwa kuwa wewe huwaokoa watu walio taabishwa, lakini wewe huwashusha chini wale wenye majivuno, yaani macho yaliyo jinua!
28 Por tanto tú alumbrarás mi candela: Jehová, mi Dios, alumbrará mis tinieblas,
Kwa kuwa wewe huipa mwanga taa yangu; Yahwe Mungu wangu hutia mwanga giza langu.
29 Porque contigo desharé ejércitos: y en mi Dios asaltaré muros.
Kwa kuwa kwa kupitia wewe ninaweza kuruka juu ya kiwazo kilichowekwa; kupitia Mungu ninaweza kuruka juu ya ukuta.
30 Dios, perfecto su camino: la palabra de Jehová afinada: escudo es a todos los que esperan en él.
Kama kwa Mungu: njia yake ni kamilifu. Neno la Yahwe ni safi! Yeye ni ngao kwa yeyote anaye kimbilia katika yeye.
31 Porque ¿qué Dios hay fuera de Jehová? ¿y qué fuerte fuera de nuestro Dios?
Kwa kuwa nani ni Mungu ispokuwa Yahwe? Nani ndiye mwamba ispokuwa Mungu wetu?
32 Dios, que me ciñe de fuerza; e hizo perfecto mi camino:
Ni Mungu anitiaye nguvu ndani yangu kama vile mkanda, ambaye humweka mtu mwenye lawama katika njia yake.
33 Que pone mis pies como pies de ciervas: y me hizo estar sobre mis alturas:
Yeye hunifanya miguu yangu kuwa myepesi kama mbawala na kuniweka mahali pa juu!
34 Que enseña mis manos para la batalla; y el arco de acero será quebrado con mis brazos.
Yeye hufunza viganja vyangu kwa ajili ya vita na mikono yangu kupiga upinde wa shaba.
35 Y me diste el escudo de tu salud; y tu diestra me sustentará, y tu mansedumbre me multiplicará.
Wewe umenipa mimi ngao ya wokovu. Mkono wako wa kuume umenisaidia, na neema yako imenifanya kuwa mkubwa.
36 Ensancharás mi paso debajo de mí, y no titubearán mis rodillas.
Wewe umetengeneza nafasi pana kwa ajili ya miguu yangu ili miguu yangu isiteleze.
37 Perseguiré mis enemigos, y alcanzarles he; y no volveré hasta acabarles.
Ninawashawishi adui zangu na kuwakamata; nami sikurudi nyuma mpaka walipo haribiwa.
38 Herírles he, y no podrán levantarse: caerán debajo de mis pies.
Niliwashambulia hata hawakuweza kuamka; nao wameangukia chini ya miguu yangu.
39 Y ceñísteme de fortaleza para la pelea: agobiaste mis enemigos debajo de mí.
Kwa kuwa unanitia nguvu kama mshipi kwa ajili ya vita; wewe unawaweka chini yangu wale ambao wanainuka kinyume na mimi.
40 Y dísteme la cerviz de mis enemigos: y a los que me aborrecían, destruí.
Wewe ulinipa visogo vya maadui zangu; niliwaagamiza wale walio nichukia.
41 Clamaron, y no hubo quien salvase: a Jehová, mas no les oyó.
Wao waliita msaada lakini hakuna aliye wasaidia; walimuita Yahwe, lakini hakuwaitikia.
42 Y los molí como polvo delante del viento: como a lodo de las calles los esparcí.
Niliwapiga wao katika vipande vidogo vidogo kama vile vumbi mbele ya upepo; niliwatupa nje kama udongo mtaani.
43 Librásteme de contiendas de pueblo: pusísteme por cabecera de gentes; pueblo que no conocí, me sirvió.
Wewe uliniokoa mimi kutoka katika migogoro ya watu. wewe umenifanya kichwa juu ya mataifa. Watu ambao sikuwahi kuwafahamu huntumikia.
44 A oída de oreja me obedeció: los hombres extraños me mintieron.
Pindi tu waliposikia kuhusu mimi, wao walinitii; wageni walilazimishwa kunisujudu.
45 Los hombres extraños se cayeron: y tuvieron miedo desde sus encerramientos.
Wageni walitoka kwenye ngome yao wakitetemeka.
46 Viva Jehová, y bendito sea mi fuerte: y sea ensalzado el Dios de mi salud.
Yahwe anaishi; mwamba wangu usifiwe. Ainuliwe Mungu wa wokovu wangu.
47 El Dios que me da las venganzas, y sujetó pueblos debajo de mí.
Yeye ni Mungu ambaye hutelekeza visasi kwa ajili yangu, ambaye huwatiisha mataifa chini yangu.
48 Mi librador de mis enemigos: también me hiciste superior de mis adversarios: de varón violento me libraste.
Nimewekwa huru kutoka kwa adui zangu! wewe uliniinua juu ya wale walioinuka kunyume na mimi! Wewe uliniokoa kutoka kwa watu wenye vurugu.
49 Por tanto yo te confesaré entre las gentes, o! Jehová, y cantaré a tu nombre.
Kwa hiyo nitakushukuru wewe, Yahwe, kati ya mataifa; Nitaliimbia sifa jina lako!
50 Que engrandece las saludes de su rey, y que hace misericordia a su ungido David, y a su simiente para siempre.
Mungu hutoa ushindi mkuu kwa mfalme wake, na yeye huonyesha uaminifu wa agano lake kwa mpakwa mafuta wake, kwa Daudi na ukoo wake milele.

< Salmos 18 >