< Salmos 18 >

1 Al maestro de coro. Del servidor de Dios, de David, el cual dirigió al Señor las palabras de este cántico en el día en que le libró de las manos de todos sus enemigos y de las de Saúl. Y dijo: Te amo, Yahvé, fortaleza mía, mi peña, mi baluarte, mi libertador,
Nakupenda, Yahwe, nguvu yangu.
2 Dios mío, mi roca, mi refugio, broquel mío, cuerno de mi salud, asilo mío.
Yahwe ni mwamba wangu, ngome yangu, yeye ambaye aniwekae kweye usalama; yeye ni Mungu wangu, mwamba wangu; ninapata kimbilio kwake. Yeye ni ngao yangu, pembe ya wokovu wangu, na ngome yangu.
3 Invoco a Yahvé, el digno de alabanza, y quedo libre de mis enemigos.
Nitamuita Yahwe kwa sababu anastahili kusifiwa, na nitaokolewa kutoka kwa adui zangu.
4 Olas de muerte me rodeaban, me alarmaban los torrentes de iniquidad;
Kamba za mauti zilinizunguka, na mafuriko yakimbiayo yalinielemea.
5 las ataduras del sepulcro me envolvieron, se tendían a mis pies lazos mortales. (Sheol h7585)
Kamba za kuzimu zilinizunguka; mitego ya mauti ilininasa. (Sheol h7585)
6 En mi angustia invoqué a Yahvé, y clamé a mi Dios; y Él, desde su palacio, oyó mi voz; mi lamento llegó a sus oídos.
dhiki yangu nilimuita Yahwe; Niliita msaada kwa Mungu. Naye alisikia sauti yangu kutoka hekaluni mwake; kuita kwangu msaada kulienda mpaka uweponi mwake; na kuingia masikioni pake.
7 Se estremeció la tierra y tembló; se conmovieron los cimientos de los montes y vacilaron, porque Él ardía de furor.
Kisha nchi ikatikisika na kutetemeka; misingi ya milima pia ilitetemeka na kutikiswa kwa sababu Mungu alikuwa amekasirika.
8 Humo salió de sus narices; de su boca, fuego devorador; y despedía carbones encendidos.
Moshi ulifuka kutoka kwenye pua zake, na moto mkali ulitokea mdomoni mwake. Makaa yaliwashwa kwa moto huo.
9 Inclinó los cielos, y descendió con densas nubes bajo sus pies.
Yeye alizifunua mbingu na alishuka chini, na giza nene lilikuwa chini ya miguu yake.
10 Subió sobre un querube y voló, y era llevado sobre las alas del viento.
Alipanda kwenye kerubi na akaruka; alinyiririka kwenye mabawa ya upepo.
11 Se ocultaba bajo un velo de tinieblas; aguas tenebrosas y oscuras nubes lo rodeaban como un pabellón.
Yahwe alilifanya giza kuwa hema likimzunguka yeye, wingu la mvua zito katika mbingu.
12 Se encendieron carbones de fuego al resplandor de su rostro.
Mawe ya barafu na makaa ya moto yalianguka kutoka katika mwangaza kabla yake.
13 Tronó Yahvé desde el cielo, el Altísimo hizo resonar su voz;
Yahwe aliongea katika mbingu! Sauti ya aliye juu ilisikika.
14 y lanzó sus saetas y los dispersó; multiplicó sus rayos, y los puso en derrota.
Yeye aliifyatua mishale yake na kuwatawanya adui zake; na radi nyingi zenye mwanga alizitawanya katika maeneo tofauti tofauti.
15 Y aparecieron a la vista los lechos de los océanos; se mostraron desnudos los cimientos del orbe terráqueo, ante la amenaza de Yahvé, al resollar el soplo de su ira.
Ndipo mifereji ya maji ilitokea; misingi ya dunia ikadhihirishwa kwa mlio wa pigo lako, Yahwe kwa sauti ya pumzi ya pua zako.
16 Desde lo alto extendió su brazo y me arrebató, sacándome de entre las muchas aguas;
Yeye alishuka chini kutokea juu; akanishikilia mimi! Akanivuta nje ya maji yafurikayo.
17 me libró de mi feroz enemigo, de adversarios más poderosos que yo.
Aliniokoa kutoka kwa maadui zangu wenye nguvu, kutoka kwa wale ambao walinichukia mimi, kwa kuwa walikuwa na nguvu sana kuliko mimi.
18 Se echaron sobre mí en el día de mi infortunio; pero salió Yahvé en mi defensa,
Wao walikuja kinyume na mimi katika siku ile ya dhiki yangu lakini Mungu alikuwa msaada wangu!
19 y me trajo a la anchura; me salvó porque me ama.
Yeye aliniweka huru katika eneo pana la wazi; yeye aliniokoa kwa sababu alipenezwa nami.
20 Yahvé me ha retribuido conforme a mi rectitud; me remunera según la limpieza de mis manos.
Yahwe amenitunuku mimi kwa sababu ya haki yangu; yeye amenirejesha mimi kwa sababu mikono yangu ilikuwa misafi.
21 Porque seguí los caminos de Yahvé, y no me rebelé contra mi Dios;
Kwa kuwa nimezitunza njia za Yahwe na sijafanya uovu wa kumgeuka Mungu wangu.
22 porque mantuve ante mis ojos todos sus mandamientos y nunca aparté de mí sus estatutos.
Kwa kuwa amri zake zote za haki zimekuwa mbele yangu; kama asemavyo, sijaenda kinyume nazo.
23 Fui íntegro para con Él, y me cuidé de mi maldad.
Pia nimekuwa sina hatia mbele zake, na nimejiweka mwenyewe mbali na dhambi.
24 Yahvé me ha retribuido conforme a mi rectitud; según la limpieza de mis manos ante sus ojos.
Hivyo Yahwe amenirejesha kwa sababu ya haki yangu, na kwa sababu mikono yangu ilikuwa safi mbele ya macho yake.
25 Tú eres misericordioso con el misericordioso; con el varón recto, eres recto.
Kwa yeyote aliye mwaminifu, jionyeshe wenyewe kuwa mwaminifu; kwa mtu asiye na lawama, jionyeshe mwenyewe kuwa usiye na lawama.
26 Con el sincero, eres sincero; y con el doble, te haces astuto.
Kwa yeyote aliye msafi, jionyeshe mwenyewe safi; bali ni mjanja kwa yeyote aliye geuzwa.
27 Tú salvas al pueblo oprimido, y humillas los ojos altaneros.
Kwa kuwa wewe huwaokoa watu walio taabishwa, lakini wewe huwashusha chini wale wenye majivuno, yaani macho yaliyo jinua!
28 Eres Tú quien mantiene encendida mi lámpara, oh Yahvé; Tú, Dios mío, disipas mis tinieblas.
Kwa kuwa wewe huipa mwanga taa yangu; Yahwe Mungu wangu hutia mwanga giza langu.
29 Fiado en Ti embestiré a un ejército; con mi Dios saltaré murallas.
Kwa kuwa kwa kupitia wewe ninaweza kuruka juu ya kiwazo kilichowekwa; kupitia Mungu ninaweza kuruka juu ya ukuta.
30 ¡El Dios mío!... Su conducta es perfecta, Su palabra acrisolada. Él mismo es el escudo de cuantos lo buscan como refugio.
Kama kwa Mungu: njia yake ni kamilifu. Neno la Yahwe ni safi! Yeye ni ngao kwa yeyote anaye kimbilia katika yeye.
31 Pues ¿quién es Dios fuera de Yahvé? o ¿qué roca hay si no es el Dios nuestro?
Kwa kuwa nani ni Mungu ispokuwa Yahwe? Nani ndiye mwamba ispokuwa Mungu wetu?
32 Aquel Dios que me ciñó de fortaleza e hizo inmaculado mi camino.
Ni Mungu anitiaye nguvu ndani yangu kama vile mkanda, ambaye humweka mtu mwenye lawama katika njia yake.
33 El que volvió mis pies veloces como los del ciervo, y me afirmó sobre las cumbres.
Yeye hunifanya miguu yangu kuwa myepesi kama mbawala na kuniweka mahali pa juu!
34 El que adiestró mis manos para la pelea, y mi brazo para tender el arco de bronce.
Yeye hufunza viganja vyangu kwa ajili ya vita na mikono yangu kupiga upinde wa shaba.
35 Tú me diste por broquel tu auxilio, me sostuvo tu diestra; tu solicitud me ha engrandecido.
Wewe umenipa mimi ngao ya wokovu. Mkono wako wa kuume umenisaidia, na neema yako imenifanya kuwa mkubwa.
36 Ensanchaste el camino a mis pasos, y mis pies no flaquearon.
Wewe umetengeneza nafasi pana kwa ajili ya miguu yangu ili miguu yangu isiteleze.
37 Perseguía a mis enemigos y los alcanzaba; y no me volvía hasta desbaratarlos.
Ninawashawishi adui zangu na kuwakamata; nami sikurudi nyuma mpaka walipo haribiwa.
38 Los destrozaba y no podían levantarse; caían bajo mis pies.
Niliwashambulia hata hawakuweza kuamka; nao wameangukia chini ya miguu yangu.
39 Tú me revestías de valor para el combate, sujetabas a mi cetro a los que me resistían.
Kwa kuwa unanitia nguvu kama mshipi kwa ajili ya vita; wewe unawaweka chini yangu wale ambao wanainuka kinyume na mimi.
40 Ponías en fuga a mis enemigos, dispersabas a cuantos me aborrecían.
Wewe ulinipa visogo vya maadui zangu; niliwaagamiza wale walio nichukia.
41 Vociferaban, mas no había quien los auxiliase; (clamaban) a Yahvé mas Él no los oía.
Wao waliita msaada lakini hakuna aliye wasaidia; walimuita Yahwe, lakini hakuwaitikia.
42 Y yo los dispersaba como polvo que el viento dispersa; los pisoteaba como el lodo de las calles.
Niliwapiga wao katika vipande vidogo vidogo kama vile vumbi mbele ya upepo; niliwatupa nje kama udongo mtaani.
43 Me libraste de las contiendas del pueblo, me has hecho cabeza de las naciones; un pueblo que no conocía me sirve;
Wewe uliniokoa mimi kutoka katika migogoro ya watu. wewe umenifanya kichwa juu ya mataifa. Watu ambao sikuwahi kuwafahamu huntumikia.
44 con atento oído me obedecen; los extraños me adulan.
Pindi tu waliposikia kuhusu mimi, wao walinitii; wageni walilazimishwa kunisujudu.
45 Los extranjeros palidecen, y abandonan, temblando, sus fortalezas.
Wageni walitoka kwenye ngome yao wakitetemeka.
46 ¡Vive Yahvé! ¡Bendita sea mi Roca! ¡Sea ensalzado el Dios mi Salvador!
Yahwe anaishi; mwamba wangu usifiwe. Ainuliwe Mungu wa wokovu wangu.
47 Aquel Dios que me otorgó la venganza, que sujetó a mí las naciones;
Yeye ni Mungu ambaye hutelekeza visasi kwa ajili yangu, ambaye huwatiisha mataifa chini yangu.
48 que me libró de mis enemigos, que me encumbró sobre mis opositores, y me salvó de las manos del hombre violento.
Nimewekwa huru kutoka kwa adui zangu! wewe uliniinua juu ya wale walioinuka kunyume na mimi! Wewe uliniokoa kutoka kwa watu wenye vurugu.
49 Por eso te alabaré entre las naciones, oh Yahvé; cantaré himnos a tu Nombre.
Kwa hiyo nitakushukuru wewe, Yahwe, kati ya mataifa; Nitaliimbia sifa jina lako!
50 Él da grandes victorias a su rey, y usa de misericordia con su ungido, con David y su linaje, por toda la eternidad.
Mungu hutoa ushindi mkuu kwa mfalme wake, na yeye huonyesha uaminifu wa agano lake kwa mpakwa mafuta wake, kwa Daudi na ukoo wake milele.

< Salmos 18 >