< Juda 1 >

1 Juda, služabnik Jezusa Kristusa in Jakobov brat, tem, ki so posvečeni po Bogu Očetu in ohranjeni v Jezusu Kristusu in poklicani:
Mimi Yuda, mtumishi wa Yesu Kristo, ndugu yake Yakobo, nawaandikia ninyi mlioitwa na Mungu na ambao mnaishi katika upendo wa Mungu Baba, na katika ulinzi wa Yesu Kristo.
2 ›Usmiljenje in mir in ljubezen naj se vam pomnožijo.‹
Nawatakieni huruma, amani na upendo kwa wingi.
3 Ljubljeni, ko sem posvetíl vso marljivost, da vam pišem o skupni rešitvi duš, je bilo zame nujno, da vam pišem in vas spodbujam, da se resno borite za vero, ki je bila enkrat [za vselej] izročena svetim.
Ndugu wapenzi, wakati nimo katika jitihada ya kuwaandikieni juu ya ule wokovu tunaoshiriki sote, nimeona lazima ya kuwaandikieni na kuwahimizeni mwendelee kupigana kwa ajili ya imani ambayo Mungu amewajalia watu wake mara moja tu kwa wakati wote.
4 Kajti ne-sluteč so se prikradli določeni ljudje, ki so bili že od davno odrejeni za to obsodbo, brezbožni ljudje, ki milost našega Boga sprevračajo v opolzkost in zanikajo edinega Gospoda Boga in našega Gospoda Jezusa Kristusa.
Maana watu wasiomcha Mungu wamepata kujiingiza kwa siri miongoni mwetu, watu ambao, kwa faida ya maisha yao mabaya, wanaupotosha ujumbe wa neema ya Mungu wetu na kumkana Yesu Kristo aliye peke yake kiongozi na Bwana wetu. Maandiko Matakatifu yalikwisha bashiri tangu awali hukumu inayowangojea watu hao.
5 Hočem vas torej spomniti, čeprav ste nekoč to vedeli, da je Gospod, ki je ljudi rešil iz egiptovske dežele, potem uničil te, ki niso verovali.
Nataka kuwakumbusheni mambo fulani ambayo mmekwisha yajua: kumbukeni jinsi Bwana alivyowaokoa watu wa Israeli na kuwatoa katika nchi ya Misri, lakini baadaye aliwaangamiza wale ambao hawakuamini.
6 In angele, ki niso obdržali svojega prvega stanja, temveč so zapustili svoje prebivališče, je ohranil v večnih verigah pod temo, do sodbe vélikega dne. (aïdios g126)
Na, malaika ambao hawakuridhika na cheo chao, wakayaacha makao yao ya asili, Mungu amewafunga gizani kwa minyororo ya milele wahukumiwe Siku ile kuu. (aïdios g126)
7 Celó kakor so Sódoma in Gomóra in na podoben način mesta okoli njiju, ki so same sebe predajala v prešuštvo in hodila za tujim mesom, postavljena kot zgled, trpeč maščevanje večnega ognja. (aiōnios g166)
Kumbukeni pia Sodoma na Gomora, na miji ya kandokando yake; wenyeji wake walifanya kama wale malaika; walifanya uzinzi na mambo yaliyo kinyume cha maumbile, wakapewa hukumu ya moto wa milele, iwe onyo kwa watu wote. (aiōnios g166)
8 Podobno tudi ti umazani sanjači omadežujejo meso, prezirajo gospostvo in hudobno govorijo o dostojanstvih.
Hivyo ndivyo pia walivyo watu hawa. ndoto zao huwaongoza katika kuichafua miili yao wenyewe, kuyadharau mamlaka ya Mungu na kuvitukana viumbe vitukufu vya huko juu.
9 Vendarle si nadangel Mihael, ko se je pričkal s hudičem in prerekal glede Mojzesovega telesa, ni drznil zoper njega udrihati obtožbe, temveč je rekel: »Gospod te ošteje.«
Hata Mikaeli, malaika mkuu, hakufanya hivyo. Katika ule ubishi kati yake na Ibilisi waliobishana juu ya mwili wa Mose, Mikaeli hakuthubutu kumhukumu Ibilisi kwa matusi; ila alisema: “Bwana mwenyewe na akukaripie.”
10 Toda ti govorijo hudobno o teh stvareh, ki jih ne poznajo; toda kar naravno vedo kot brezčutne živali, v teh stvareh sami sebe kvarijo.
Lakini watu hawa hutukana chochote wasichokielewa; mambo yaleyale wanayoyajua kwa silika kama vile wanyama wanayoyajua ndiyo yanayowaangamiza.
11 Gorje jim! Kajti odšli so na Kajnovo pot in lakomno tekli za Bileámovo zmoto po nagrado in propadli v Korahovem uporu.
Ole wao! Watu hao wamefuata mwenendo uleule wa Kaini. Kwa ajili ya fedha, wamejiingiza katika mkosi uleule wa Baalamu. Wameasi kama Kora alivyoasi na wameangamizwa kama yeye alivyoangamizwa.
12 Ti so madeži na vaših dobrodelnih pojedinah, ko se zabavajo z vami in se hranijo brez strahu. Oblaki so brez vode, ki jih vetrovi nosijo okoli; drevesa, katerih sad vene, brez sadu, dvakrat mrtva, izruvana s koreninami;
Kwa makelele yao yasiyo na adabu, watu hao ni kama madoa machafu katika mikutano yenu ya karamu ya Bwana. Hujipendelea wao wenyewe tu, na wako kama mawingu yanayopeperushwa huko na huko na upepo bila ya kuleta mvua. Wao ni kama miti isiyozaa matunda hata wakati wa majira yake, wamekufa kabisa.
13 besneči morski valovi, ki se penijo od svoje lastne sramote; blodeče zvezde, ki jim je za vedno prihranjena črna temà. (aiōn g165)
Watu hao ni kama mawimbi makali ya bahari, na matendo yao ya aibu yanaonekana dhahiri kama vile mapovu ya mawimbi. Wao ni kama nyota zinazotangatanga, ambao Mungu amewawekea mahali pao milele katika giza kuu. (aiōn g165)
14 In tudi Henoh, sedmi od Adama, je prerokoval o njih, rekoč: ›Glej, Gospod prihaja z deset tisoči svojih svetih,
Henoki, ambaye ni babu wa saba tangu Adamu, alibashiri hivi juu ya watu hawa: “Sikilizeni! Bwana atakuja pamoja na maelfu ya malaika wake watakatifu
15 da izvrši sodbo nad vsemi in da prepriča vse, ki so med njimi brezbožni, o vseh njihovih brezbožnih dejanjih, ki so jih brezbožno zagrešili in o vseh njihovih trdih govorih, ki so jih brezbožni grešniki govorili zoper njega.‹
kutoa hukumu juu ya binadamu wote, kuwahukumu wote kwa ajili ya matendo yao yote maovu waliyotenda na kwa ajili ya maneno yote mabaya ambayo watu waovu walimkashifu nayo.”
16 To so godrnjači, pritoževalci, ki hodijo za svojimi lastnimi poželenji; in njihova usta govorijo velike napihnjene besede, ker zaradi koristi občudujejo človeško zunanjost.
Watu hawa wananung'unika daima na kuwalaumu watu wengine. Hufuata tamaa zao mbaya, hujigamba na kuwasifu watu wengine mno kusudi wafaulu katika mipango yao.
17 Toda ljubljeni, spominjajte se besed, ki so vam jih prej govorili apostoli našega Gospoda Jezusa Kristusa,
Lakini ninyi wapenzi wangu, kumbukeni yale mliyoambiwa hapo awali ni mitume wa Bwana wetu Yesu Kristo.
18 kako so vam povedali, da bodo v poslednjem času zasmehovalci, ki naj bi hodili za svojimi lastnimi brezbožnimi poželenji.
Waliwaambieni: “Siku za mwisho zitakapofika, watatokea watu watakaowadhihaki ninyi, watu wafuatao tamaa zao mbaya.”
19 Ti so tisti, ki se oddvojijo, čutni, ki nimajo Duha.
Hao ndio watu wanaosababisha mafarakano, watu wanaotawaliwa na tamaa zao za kidunia, watu wasio na Roho wa Mungu.
20 Toda vi, ljubljeni, se izgrajujte v svoji najsvetejši veri, moleč v Svetem Duhu,
Lakini ninyi, wapenzi wangu, endeleeni kujijenga kikamilifu katika imani yenu takatifu. Salini kwa nguvu ya Roho Mtakatifu,
21 ohranite se v Božji ljubezni, pričakujte usmiljenje našega Gospoda Jezusa Kristusa, za večno življenje. (aiōnios g166)
na kubaki katika upendo wa Mungu, mkiwa mnamngojea Bwana wetu Yesu Kristo awapeni uzima wa milele kwa huruma yake. (aiōnios g166)
22 In do nekaterih imejte sočutje, s tem da delate razliko;
Muwe na huruma kwa watu walio na mashaka;
23 druge pa rešite s strahom in jih potegnite iz ognja; in sovražite celó obleko, omadeževano z mesom.
waokoeni kwa kuwanyakua kutoka motoni; na kwa wengine muwe na huruma pamoja na hofu, lakini chukieni hata mavazi yao ambayo yamechafuliwa na tamaa zao mbaya.
24 Torej njemu, ki vas je zmožen varovati pred padcem in vas s silno radostjo predstaviti brezhibne pred prisotnost svoje slave,
Kwake yeye awezaye kuwalinda msije mkaanguka, na kuwaleta ninyi bila hatia mpaka mbele ya utukufu wake,
25 edinemu modremu Bogu, našemu Odrešeniku, bodi slava in veličanstvo, gospostvo in oblast, tako sedaj kot na veke. Amen. (aiōn g165)
kwake yeye aliye peke yake Mungu, Mkombozi wetu, uwe utukufu, ukuu, nguvu na mamlaka kwa njia ya Kristo Bwana wetu, tangu zama zote, sasa na hata milele! Amina. (aiōn g165)

< Juda 1 >