< Второзаконие 29 >

1 Сия словеса завета, яже завеща Господь Моисею уставити сыном Израилевым в земли Моавли, кроме завета, егоже завеща им в Хориве.
Haya ni maneno ambayo Yahwe alimuamuru Musa kuwaambia watu wa Israeli katika nchi ya Moabu, maneno ambayo yaliongezwa katika agano alilolifanya pamoja nao kule Horebu.
2 И призва Моисей вся сыны Израилевы и рече к ним: вы видесте вся, елика сотвори Господь в земли Египетстей пред вами фараону и всем слугам его и всей земли его,
Musa aliwaita Waisraeli wote na kuwaambia, “Mmeona kila kitu ambacho Yahwe alifanya mbele ya macho yenu katika nchi ya Misri kwa Farao, kwa watumishi wake wote, na kwa nchi yake yote –
3 искушения великая, яже видеста очи твои, знамения и чудеса великая оная, руку крепкую и мышцу высокую:
mateso makubwa ambayo macho yenu yaliona, ishara, pamoja na ile miujiza mikubwa.
4 и не даде Господь Бог вам сердца разумети и очес видети и ушес слышати, даже до дне сего:
Lakini mpaka leo Yahwe hajawapatia moyo wa kufahamu, macho ya kuona, au masikio ya kusikia.
5 и водил вас четыредесять лет по пустыни: не обетшаша ризы вашя, и сапози ваши не сотрошася на ногах ваших:
Nimewaongoza kwa miaka arobaini jangwani; mavazi yenu hayakuchakaa juu yenu, na ndala zenu hazikuchakaa miguuni mwenu.
6 хлеба не ядосте, вина и сикера не писте, да познаете, яко Сей Господь Бог ваш:
Hamkula mkate wowote, na wala hamkunywa divai yoyote au kinywaji chochote chenye ulevi, ili kwamba muweze kujua kuwa mimi ni Yahwe Mungu wenu.
7 и приидосте до сего места: и изыде Сион царь Есевонский и Ог царь Васанский во сретение нам на брань,
Mlipokuja mahali hapa, Sihoni, mfalme wa Heshboni, na Ogu, mfalme wa Bashani, walikuja dhidi yetu kutupiga, na tukawapiga.
8 и поразихом их на брани, и прияхом землю их: и дах ю во жребий Рувиму и Гаду и полуплемени Манассиину.
Tulichukua ardhi yao na kuwapa kama urithi Wareubeni, kwa Wagadi, na kwa nusu ya kabila ya Manase.
9 И сохраните творити вся словеса завета сего творити я, да разумеете вся, елика сотворите.
Kwa hiyo shikilia maneno ya agano hili na kuyatenda, ili ufanikiwe katika kila kitu ufanyacho.
10 Вы стасте вси днесь пред Господем Богом вашим, племеноначалницы ваши и старейшины ваши, и судии ваши и писмовводители ваши, всяк муж Израилтеск,
Nyie wote, mnasimama leo, mbele ya Yahwe Mungu wenu; machifu wenu, makabila yenu, wazee wenu, na maafisa wenu – wanaume wote wa Israeli,
11 и жены вашя и чада ваша, пришлец иже посреде полка вашего, от древосечца вашего даже до водоносца вашего,
watoto wenu, wake zenu, na wageni ambao wamo miongoni wa kambi yenu, kutoka kwa yule anayekata mbao zenu mpaka kwa yule atekaye maji.
12 еже прейти в завет Господа Бога вашего и в клятвы Его, елика завещает Господь Бог твой к тебе днесь:
Mpo hapa ili kwamba muingie katika agano la Yahwe Mungu wenu na katika kiapo ambacho Yahwe Mungu wako anafanya na wewe leo,
13 да поставит тя Себе в люди, и Той будет тебе Бог, якоже тебе рече и якоже клятся отцем твоим, Аврааму и Исааку и Иакову.
ili kwamba awafanye leo kuwa watu wake, na kwamba aweze kuwa Mungu kwa ajili yako, kama alivyonena kwako, na kama alivyoapa kwa mababu zako, kwa Abrahamu, kwa Isaka na kwa Yakobo.
14 И не вам единем аз завет сей и клятву сию завещаваю,
Kwa maana ninafanya agano hili na kiapo hiki sio na wewe tu –
15 но и зде сущым с вами днесь, пред Господем Богом вашим, и не сущым с вами зде днесь.
pamoja kila mtu aliyesimama hapa pamoja nasi leo mbele ya Yahwe Mungu wetu – bali na wale ambao hawapo pamoja nasi leo pia.
16 Яко вы весте, како жихом в земли Египетстей и како проидохом посреде языков, ихже преидосте,
Unajua jinsi tulivyoishi katika nchi ya Misri, na jinsi tulivyopenya miongoni mwa mataifa ambao uliwapita.
17 и видесте мерзости их и кумиры их, древо и камение, сребро и злато, яже суть у них.
Mmeona sanamu zao zinazokera zilizotengenezwa kwa mbao na mawe, fedha na dhahabu, ambazo zilikuwa miongoni mwenu.
18 Еда кто есть в вас муж или жена, или отечество или племя, егоже сердце уклонися от Господа Бога вашего, ити еже служити богом языков оных? Еда кий есть в вас корень горе прорастающь в желчи и горести?
Hakikisha hakuna kati yenu mwanamume, mwanamke, ukoo, au kabila ambaye moyo wake unamuacha Yahwe Mungu wetu leo, ili kwenda na kuabudu miungu ya mataifa hayo. Hakikisha hakuna kati yenu mzizi utakaozaa nyongo na pakanga.
19 И будет аще услышит словеса клятвы сея и похвалится в сердцы своем, глаголя: преподобно мне да будет, яко в прельщении сердца моего пойду, да не погубит грешник безгрешнаго (с собою):
Wakati mtu huyo anaposikia maneno ya laana hii, atajifariji moyoni mwake na kusema, “Nitakuwa na amani, ingawa natembea katika ukaidi wa moyo wangu”. Hii itaangamiza ubichi pamoja na ukavu.
20 не восхощет Бог милостив быти ему, но тогда разгорится гнев Господень и ревность Его на человека того: и прилепятся ему вся клятвы завета сего, писанныя в книзе закона сего: и потребит Господь имя его от поднебесныя,
Yahwe hatamsamehe, lakini badala yake, hasira ya Yahwe na wivu wake utambanika mtu huyo, na laana zote zilizoandikwa katika kitabu hiki vitakuwa juu yake, na Yahwe ataliondoa jina lake kutoka mbinguni.
21 и отлучит его Господь на злая от всех сынов Израилевых, по всем клятвам завета написаннаго в книзе закона сего.
Yahwe atamuweka kando kwa ajili ya maafa kutoka katika makabila yote ya Israeli, kwa kuzingatia laana zote za agano ambazo zimeandikwa katika kitabu hiki cha sheria.
22 И речет род ин, сынове ваши, иже востанут по вас, и чуждый иже приидет от земли далекия, и узрят язвы земли оныя и недуги ея, яже посла Господь на ню,
Kizazi kifuatacho, watoto wako watakaoinuka baada yako, na mgeni atakayekuja kutoka nchi ya mbali, watazungumza watakapoona mapigo juu ya nchi hii na magonjwa ambayo Yahwe ameyafanya yawe –
23 жупел и соль сожженную: вся земля ея не насеется, ни прозябнет, ниже возникнет на ней всяк злак: якоже опровержеся Содом и Гоморр, Адама и Севоим, яже опроверже Господь в ярости и гневе Своем.
na watakapoona kuwa nchi yote imekuwa salfa na chumvi ichomayo, ambapo hakuna kitu kipandwacho au kuzaa matunda, ambapo hapaoti mmea wowote, kama anguko la Sodoma na Gomora, Adma na Seboimu, ambayo Yahwe aliangamiza katika ghadhabu na hasira yake –
24 И рекут вси языцы: почто сотвори Господь сице земли сей? Кая ярость гнева великая сия?
watasema kwa pamoja na mataifa mengine, “Kwa nini Yahwe amefanya hili katika nchi hii? Joto ya hasira hii kali inamaanisha nini?”
25 И рекут: яко оставиша завет Господа Бога отец своих, егоже завеща отцем их, егда изведе их от земли Египетския,
Kisha watu watasema, “Ni kwa sababu walitelekeza agano la Yahwe, Mungu wa mababu zao, alilofanya nao alipowatoa kutoka Misri,
26 и шедше послужиша богом иным, и поклонишася им, ихже не ведяху, и не даде им ничтоже ни един:
na kwa sababu waliondoka na kutumikia miungu mingine na kuzisujudu, miungu ambayo hawakujiua na ambayo hakuwapatia.
27 и разгневася яростию Господь на землю ту, еже навести на ню по всем клятвам завета, писанным в книгах закона сего:
Kwa hiyo hasira ya Yahwe imewaka dhidi ya nchi hii, ili kuleta juu yake laana zote zilizoandikwa katika kitabu hiki.
28 и изят их Господь от земли их яростию и гневом, и прогневанием великим зело, и изверже их в землю ину якоже ныне.
Yahwe amewang’oa kutoka nchini kwao kwa hasira, kwa ghadhanu, na kwa ghadhabu kali, na kuwatupa katika nchi nyingine, leo.
29 Тайная Господеви Богу нашему, нам же явленная и чадом нашым во веки, творити вся словеса закона сего.
Mambo ya siri ni ya Yahwe Mungu wetu pekee; lakini mambo yaliyofichuliwa ni ya kwetu milele pamoja na wazawa wetu, ili tufanye maneno yote ya sheria hii.

< Второзаконие 29 >