< Psalmi 55 >

1 Usliši, Bože, molitvu moju, i nemoj se sakriti od moljenja mojega.
Uyategee sikio maombi yangu, Mungu; nawe usijifiche mbali na kusihi kwangu.
2 Pazi, i saslušaj me; cvilim u jadu svom i uzdišem
Unitazame kwa makini na unijibu; Sina pumziko katika shida zangu
3 Od vike neprijateljske i od dosade bezbožnièke; jer dižu na me zlo, i u gnjevu gone me.
kwa sababu ya sauti ya adui zangu, kwa sababu ya ukandamizaji wa waovu; maana wananiletea matatizo na kunitesa wakiwa na hasira.
4 Srce je moje uzdrktalo u meni, i strah smrtni popade me;
Moyo wangu wasumbuka ndani yangu, na hofu ya kifo imeniangukia.
5 Strah i trepet doðe na me, i groza poduze me.
Uwoga na kutetemeka kumenijia, nayo hofu imenielemea.
6 I rekoh: ko bi mi dao krila golubinja? ja bih odleteo i poèinuo;
Nikasema, “Oh, kama tu ningekuwa na mabawa kama njiwa! Ningelipaa mbali na kupata pumziko.
7 Daleko bih pobjegao, i nastanio se u pustinji.
Tazama, ningeenda mbali; ningekaa jangwani. (Selah)
8 Pohitao bih da uteèem od vihora i od bure.
Ningefanya haraka kuja mafichoni mwako kuzikimbia dhoruba na tufani.”
9 Porazi, Gospode, i razdijeli jezike njihove, jer vidim nasilje i svaðu u gradu;
Uwaangamize, Bwana, vuruga lugha zao! Kwa maana nimeona vurugu na ugomvi katika mji.
10 Danju i noæu to hodi po zidovima njegovijem; zloèinstvo je i muka posred njega.
Mchana na usiku wao huenda kwenye kuta zake; uchafu na ufisadi uko katikati yake.
11 Usred njega je pogibao, s ulice njegove ne odlazi prijevara i lukavstvo.
Uovu uko katikati yake; ukandamizaji na uongo hauiachi mitaa yake.
12 Jer ne ruži me neprijatelj moj, to bih podnio; ne ustaje na me javni nenavidnik, od njega bih se sakrio.
Kwa maana hakuwa adui aliye nikemea, hivyo ningevumilia; wala ingekuwa ni yule aliye nichukia aliyejiinua mwenyewe dhidi yagu, hivyo ningejificha asinione.
13 Nego ti koji si mi bio to što ja sam, drug moj i znanac moj.
Lakini ulikuwa wewe, mtu sawa na mimi, mwenzangu na rafiki yangu.
14 S kojim mi bješe radost dijeliti tajnu, i u dom Božji hodih kroz sabor narodni.
Tulikuwa na ushirika mtamu pamoja; tuliingia katika nyumba ya Mungu tukiwa na umati mkubwa.
15 Neka ih ugrabi smrt, neka živi siðu u pakao, jer je zloèinstvo u stanu njihovu i u njima. (Sheol h7585)
Kifo na kiwapate ghafla; na washuke wakiwa hai kuzimuni, maana ndiko waishiko waovu, hapo hapo kati yao. (Sheol h7585)
16 Ja Boga prizivljem, i Gospod æe me spasti.
Lakini kwangu mimi, nitamwita Mungu, na Yahwe ataniokoa.
17 Veèerom i jutrom i u podne tužim i uzdišem, i èuæe glas moj;
Wakati wa jioni, asubuhi na mchana ninalalamika na kuomboleza; yeye atasikia sauti yangu.
18 Uèiniæe, te æe duša moja biti mirna od onijeh koji napadaju na me, jer ih mnogo imam.
Kwa usalama kabisa atayaokoa maisha yangu na vita dhidi yangu, kwa maana wale waliopigana nami walikuwa ni wengi.
19 Da usliši, i ukroti ih Bog, koji živi od vijeka; jer se ne mijenjaju i ne boje se Boga.
Mungu, yule unayetawala milele, atawasikia na kuwaaibisha wao. (Selah) Hawabadiliki, na hawamhofu Mungu.
20 Dižu ruke svoje na one koji su s njima u miru, i raskidaju svoju družbu.
Rafiki yangu ameinua mikono yake dhidi ya wale waliokuwa na amani naye; Hakuheshimu agano alilokuwa nalo.
21 Usta su im meka kao maslo, a na srcu im je rat. Rijeèi su im blaže od ulja, ali su goli maèevi.
Mdomo wake ulikuwa laini kama siagi, lakini moyo wake ulikuwa adui; maneno yake yalikuwa laini kuliko mafuta, lakini yalikuwa ni panga zilizochomolewa.
22 Stavi na Gospoda breme svoje, i on æe te potkrijepiti. Neæe dati dovijeka pravedniku da posrne.
Umtwike mizigo yako Yahwe, naye atakusaidia; yeye hataruhusu mtu mwenye haki kuyumbayumba.
23 Ti æeš ih, Bože, svaliti u jamu pogibli; krvopije i lukavi neæe sastaviti polovine dana svojih. A ja se u tebe uzdam.
Bali wewe, Mungu, utawaleta waovu chini kwenye shimo la uharibifu; watu wenye kiu ya kumwaga damu na waongo hawataishi hata nusu ya maisha kama wengine, lakini mimi nitakuamini wewe.

< Psalmi 55 >