< Postanak 9 >

1 I Bog blagoslovi Noja i sinove njegove, i reèe im: raðajte se i množite se, i napunite zemlju;
Kisha Mungu akambariki Nuhu na wanawe, na kuwaambia, “Zaeni, mkaongezeke, na muijaze nchi.
2 I sve zvijeri zemaljske i sve ptice nebeske i sve što ide po zemlji i sve ribe morske neka vas se boje i straše; sve je predano u vaše ruke.
Hofu na utisho wenu vitakuwa juu ya kila mnyama aliye hai juu ya nchi, juu ya kila ndege wa angani, juu ya kila kitu kiendacho chini juu ya ardhi, na juu ya samaki wote wa baharini. Vimetolewa katika mikono yenu.
3 Što se god mièe i živi, neka vam bude za jelo, sve vam to dadoh kao zelenu travu.
Kila kitu kiendacho kilicho hai kitakuwa chakula kwa ajili yenu. Kama nilivyo wapa mimea, sasa nawapa kila kitu.
4 Ali ne jedite mesa s dušom njegovom, a to mu je krv.
Lakini msile nyama pamoja na uhai wake - yaani damu yake - ndani yake.
5 Jer æu i vašu krv, duše vaše, iskati; od svake æu je zvijeri iskati; iz ruke samoga èovjeka, iz ruke svakoga brata njegova iskaæu dušu èovjeèiju.
Lakini kwa ajili ya damu yenu, uhai uliomo katika damu yenu nitataka malipo. Kutoka katika mkono wa kila mnyama nitaitaka. Kutoka katika mkono wa kila mtu, yaani, kutoka katika mkono wa yule ambaye amemuua ndugu yake, nitataka fidia kwa ajili ya uhai wa mtu huyo.
6 Ko prolije krv èovjeèiju, njegovu æe krv proliti èovjek; jer je Bog po svojemu oblièju stvorio èovjeka.
Yeyote amwagaye damu ya mtu, kwa njia ya mtu damu yake itamwagwa, kwa sababu ilikuwa ni katika mfano wa Mungu kwamba Mungu alimuumba mtu.
7 Raðajte se dakle i množite se; narodite se veoma na zemlji i namnožite se na njoj.
Na hivyo nanyi zaeni na kuongezeka, sambaeni katika inchi yote na muongezeke juu yake.”
8 I reèe Bog Noju i sinovima njegovijem s njim, govoreæi:
Kisha Mungu akazungumza na Nuhu na wanae pamoja naye, akisema,
9 A ja evo postavljam zavjet svoj s vama i s vašim sjemenom nakon vas,
“Kwa ajili yangu, sikiliza! Ninakwenda kulithibitisha agano langu pamoja nawe na uzao wenu baada yenu,
10 I sa svijem životinjama, što su s vama od ptica, od stoke i od svega zvijerja zemaljskoga što je s vama, sa svaèim što je izašlo iz kovèega, i sa svijem zvijerjem zemaljskim.
na kwa kila kiumbe hai kilicho pamoja nawe, pamoja na ndege, mnyama wa kufugwa, na kila kiumbe cha nchi pamoja nawe, kuanzia kwa wote waliotoka kwenye safina, mpaka kwa kila kiumbe hai juu ya nchi.
11 Postavljam zavjet svoj s vama, te otsele neæe nijedno tijelo poginuti od potopa, niti æe više biti potopa da zatre zemlju.
Kwa sababu hii ninalithibitisha agano langu pamoja nanyi, kwamba hapatatokea kuangamizwa kwa mwenye mwili kwa njia ya maji ya gharika. Tena hapatatokea gharika ya kuangamiza nchi.”
12 I reèe Bog: evo znak zavjeta koji postavljam izmeðu sebe i vas i svake žive tvari, koja je s vama dovijeka:
Mungu akasema, “na hii ndiyo ishara ya agano ambalo ninafanya kati yangu na ninyi pamoja na kila kiumbe hai kilicho pamoja nanyi, kwa vizazi vyote vya baadaye:
13 Metnuo sam dugu svoju u oblake, da bude znak zavjeta izmeðu mene i zemlje.
Nimeweka upinde wangu wa mvua katika wingu, na itakuwa ndiyo ishara ya agano kati yangu na nchi.
14 Pa kad oblake navuèem na zemlju, vidjeæe se duga u oblacima,
Hata itakuwa nitakapoleta wingu juu ya nchi na upinde wa mvua ukaonekana katika wingu,
15 I opomenuæu se zavjeta svojega koji je izmeðu mene i vas i svake duše žive u svakom tijelu, i neæe više biti od vode potopa da zatre svako tijelo.
ndipo nitakumbuka agano langu, ambalo ni kati yangu na ninyi na kila kiumbe hai cha wote mwenye mwili. Maji hayatafanyika tena gharika kuharibu wote wenye mwili.
16 Duga æe biti u oblacima, pa æu je pogledati, i opomenuæu se vjeènoga zavjeta izmeðu Boga i svake duše žive u svakom tijelu koje je na zemlji.
Upinde wa mvua utakuwa katika mawingu na nitauona, ili kukumbuka agano la milele kati ya Mungu na kila kiumbe hai cha wote wenye mwili ambacho kiko juu ya nchi.”
17 I reèe Bog Noju: to je znak zavjeta koji sam uèinio izmeðu sebe i svakoga tijela na zemlji.
Kisha Mungu akamwambia Nuhu, “Hii ni ishara ya agano ambalo nimelithibitisha kati yangu na wenye mwili wote ambao wako juu ya nchi.”
18 A bijahu sinovi Nojevi koji izidoše iz kovèega: Sim i Ham i Jafet; a Ham je otac Hanancima.
Wana wa Nuhu ambao walitoka katika safina walikuwa ni Shemu, Hamu, na Yafethi. Na Hamu akamzaa kanaani.
19 To su tri sina Nojeva, i od njih se naseli sva zemlja.
Watatu hawa walikuwa ndio wana wa Nuhu, na kutokea kwa hawa nchi yote ikajaa watu.
20 A Noje poèe raditi zemlju, i posadi vinograd.
Nuhu akaanza kuwa mkulima, na akapanda mizabibu.
21 I napiv se vina opi se, i otkri se nasred šatora svojega.
Akanywa sehemu ya divai na akalewa. Akawa amelala hemeani uchi.
22 A Ham, otac Hanancima, vidje golotinju oca svojega, i kaza obojici braæe svoje na polju.
Kisha Hamu, baba yake na Kanaani, akaona uchi wa baba yake na akawaambia ndugu zake wawili waliokuwa nje.
23 A Sim i Jafet uzeše haljinu, i ogrnuše je obojica na ramena svoja, i iduæi natraške pokriše njom golotinju oca svojega, licem natrag okrenuvši se da ne vide golotinje oca svojega.
Kwa hiyo Shemu na Yafethi wakachukua kanzu wakaitanda juu ya mabega yao, na wakatembea kinyumenyume na wakaufunika uchi wa baba yao. Nyuso zao zikiwa zimegeuka nyuma upande mwingine, kwa hiyo hawakuona uchi wa baba yao.
24 A kad se Noje probudi od vina, dozna šta mu je uèinio mlaði sin,
Nuhu alipozinduka kutoka katika ulevi wake, alijua ni jambo gani mtoto wake mdogo amemfanyia.
25 I reèe: proklet da je Hanan, i da bude sluga slugama braæe svoje!
Hivyo akasema, “Alaaniwe Kanaani. Na awe mtumishi kwa watumishi wa ndugu zake.”
26 I još reèe: blagosloven da je Gospod Bog Simov, i Hanan da mu bude sluga!
Akasema pia, Yahwe, Mungu wa Shemu, abarikiwe, Kanaani na awe mtumwa wake.
27 Bog da raširi Jafeta da živi u šatorima Simovijem, a Hanan da im bude sluga!
Mungu na apanuwe mipaka ya Yafethi, na afanye makazi yake katika hema za Shemu. Kanaani na awe mtumwa wake.”
28 I poživje Noje poslije potopa trista i pedeset godina.
Baada ya gharika, Nuhu aliishi miaka miatatu na hamsini.
29 A svega poživje Noje devet stotina i pedeset godina; i umrije.
Siku zote za Nuhu zilikuwa ni miaka mia tisa na hamsini, na kisha alikufa.

< Postanak 9 >