< Gênesis 9 >

1 Deus abençoou Noé e seus filhos, e lhes disse: “Sejam fecundos, multipliquem-se e reabasteçam a terra”.
Kisha Mungu akambariki Nuhu na wanawe, na kuwaambia, “Zaeni, mkaongezeke, na muijaze nchi.
2 O medo de vocês e o pavor de vocês estarão sobre cada animal da terra, e sobre cada ave do céu”. Tudo o que se move ao longo da terra, e todos os peixes do mar, são entregues em suas mãos.
Hofu na utisho wenu vitakuwa juu ya kila mnyama aliye hai juu ya nchi, juu ya kila ndege wa angani, juu ya kila kitu kiendacho chini juu ya ardhi, na juu ya samaki wote wa baharini. Vimetolewa katika mikono yenu.
3 Cada coisa que se move que vive será alimento para você. Como eu lhe dei a erva verde, eu lhe dei tudo a você.
Kila kitu kiendacho kilicho hai kitakuwa chakula kwa ajili yenu. Kama nilivyo wapa mimea, sasa nawapa kila kitu.
4 Mas a carne com sua vida, ou seja, seu sangue, você não comerá.
Lakini msile nyama pamoja na uhai wake - yaani damu yake - ndani yake.
5 Certamente exigirei a prestação de contas pelo sangue de sua vida. Às mãos de cada animal, eu o requererei. Na mão do homem, mesmo na mão do irmão de cada homem, eu exigirei a vida do homem.
Lakini kwa ajili ya damu yenu, uhai uliomo katika damu yenu nitataka malipo. Kutoka katika mkono wa kila mnyama nitaitaka. Kutoka katika mkono wa kila mtu, yaani, kutoka katika mkono wa yule ambaye amemuua ndugu yake, nitataka fidia kwa ajili ya uhai wa mtu huyo.
6 Whoever derrama o sangue do homem, seu sangue será derramado pelo homem, pois Deus fez o homem à sua própria imagem.
Yeyote amwagaye damu ya mtu, kwa njia ya mtu damu yake itamwagwa, kwa sababu ilikuwa ni katika mfano wa Mungu kwamba Mungu alimuumba mtu.
7 Seja fecundo e multiplique. Aumenta abundantemente na terra, e multiplica-te nela”.
Na hivyo nanyi zaeni na kuongezeka, sambaeni katika inchi yote na muongezeke juu yake.”
8 Deus falou a Noé e a seus filhos com ele, dizendo:
Kisha Mungu akazungumza na Nuhu na wanae pamoja naye, akisema,
9 “Quanto a mim, eis que estabeleço minha aliança com você, e com seus descendentes depois de você,
“Kwa ajili yangu, sikiliza! Ninakwenda kulithibitisha agano langu pamoja nawe na uzao wenu baada yenu,
10 e com todo ser vivo que está com você: as aves, o gado e todo animal da terra com você, de todos os que saem do navio, até mesmo todo animal da terra.
na kwa kila kiumbe hai kilicho pamoja nawe, pamoja na ndege, mnyama wa kufugwa, na kila kiumbe cha nchi pamoja nawe, kuanzia kwa wote waliotoka kwenye safina, mpaka kwa kila kiumbe hai juu ya nchi.
11 Eu estabelecerei meu convênio com vocês: Toda a carne não será mais cortada pelas águas do dilúvio. Nunca mais haverá uma inundação para destruir a terra”.
Kwa sababu hii ninalithibitisha agano langu pamoja nanyi, kwamba hapatatokea kuangamizwa kwa mwenye mwili kwa njia ya maji ya gharika. Tena hapatatokea gharika ya kuangamiza nchi.”
12 Deus disse: “Este é o sinal do pacto que faço entre mim e vós e todo ser vivo que está convosco, por gerações perpétuas”:
Mungu akasema, “na hii ndiyo ishara ya agano ambalo ninafanya kati yangu na ninyi pamoja na kila kiumbe hai kilicho pamoja nanyi, kwa vizazi vyote vya baadaye:
13 Coloco meu arco-íris na nuvem, e será um sinal de um pacto entre mim e a Terra”.
Nimeweka upinde wangu wa mvua katika wingu, na itakuwa ndiyo ishara ya agano kati yangu na nchi.
14 Quando eu trouxer uma nuvem sobre a terra, que o arco-íris será visto na nuvem,
Hata itakuwa nitakapoleta wingu juu ya nchi na upinde wa mvua ukaonekana katika wingu,
15 eu me lembrarei da minha aliança, que é entre mim e você e todo ser vivo de toda a carne, e as águas não se tornarão mais uma inundação para destruir toda a carne.
ndipo nitakumbuka agano langu, ambalo ni kati yangu na ninyi na kila kiumbe hai cha wote mwenye mwili. Maji hayatafanyika tena gharika kuharibu wote wenye mwili.
16 O arco-íris será visto na nuvem. Vou olhar para ele, para que eu possa me lembrar da aliança eterna entre Deus e cada ser vivo de toda a carne que está sobre a terra”.
Upinde wa mvua utakuwa katika mawingu na nitauona, ili kukumbuka agano la milele kati ya Mungu na kila kiumbe hai cha wote wenye mwili ambacho kiko juu ya nchi.”
17 Deus disse a Noé: “Este é o símbolo do pacto que estabeleci entre mim e toda a carne que está sobre a terra”.
Kisha Mungu akamwambia Nuhu, “Hii ni ishara ya agano ambalo nimelithibitisha kati yangu na wenye mwili wote ambao wako juu ya nchi.”
18 Os filhos de Noé que saíram do navio eram Shem, Ham e Japheth. Ham é o pai de Canaã.
Wana wa Nuhu ambao walitoka katika safina walikuwa ni Shemu, Hamu, na Yafethi. Na Hamu akamzaa kanaani.
19 Estes três eram os filhos de Noé, e destes a terra inteira foi povoada.
Watatu hawa walikuwa ndio wana wa Nuhu, na kutokea kwa hawa nchi yote ikajaa watu.
20 Noé começou a ser agricultor e plantou um vinhedo.
Nuhu akaanza kuwa mkulima, na akapanda mizabibu.
21 Ele bebeu do vinho e ficou bêbado. Ele foi descoberto dentro de sua tenda.
Akanywa sehemu ya divai na akalewa. Akawa amelala hemeani uchi.
22 Ham, o pai de Canaan, viu a nudez de seu pai, e contou aos seus dois irmãos lá fora.
Kisha Hamu, baba yake na Kanaani, akaona uchi wa baba yake na akawaambia ndugu zake wawili waliokuwa nje.
23 Shem e Japheth pegaram uma roupa e a colocaram sobre os dois ombros, entraram de costas e cobriram a nudez de seu pai. Seus rostos estavam ao contrário e não viram a nudez do pai.
Kwa hiyo Shemu na Yafethi wakachukua kanzu wakaitanda juu ya mabega yao, na wakatembea kinyumenyume na wakaufunika uchi wa baba yao. Nyuso zao zikiwa zimegeuka nyuma upande mwingine, kwa hiyo hawakuona uchi wa baba yao.
24 Noé acordou de seu vinho e sabia o que seu filho mais novo havia feito com ele.
Nuhu alipozinduka kutoka katika ulevi wake, alijua ni jambo gani mtoto wake mdogo amemfanyia.
25 Disse ele, “Canaã é amaldiçoada. Ele será um servo de servos para seus irmãos”.
Hivyo akasema, “Alaaniwe Kanaani. Na awe mtumishi kwa watumishi wa ndugu zake.”
26 Ele disse, “Bendito seja Yahweh, o Deus de Shem”. Que Canaan seja seu servo.
Akasema pia, Yahwe, Mungu wa Shemu, abarikiwe, Kanaani na awe mtumwa wake.
27 Que Deus amplie o Japheth. Deixe-o morar nas tendas de Shem. Que Canaan seja seu servo”.
Mungu na apanuwe mipaka ya Yafethi, na afanye makazi yake katika hema za Shemu. Kanaani na awe mtumwa wake.”
28 Noé viveu trezentos e cinqüenta anos após a enchente.
Baada ya gharika, Nuhu aliishi miaka miatatu na hamsini.
29 Todos os dias de Noé foram novecentos e cinqüenta anos, e então ele morreu.
Siku zote za Nuhu zilikuwa ni miaka mia tisa na hamsini, na kisha alikufa.

< Gênesis 9 >