< Efésios 3 >

1 Por esta causa eu, Paulo, sou o prisioneiro de Jesus Christo por vós, os gentios;
Kutokana na hayo, mimi Paulo, mfungwa wa Kristo Yesu kwa ajili yenu, namwomba Mungu.
2 Se é que tendes ouvido a dispensação da graça de Deus, que para comvosco me foi dada;
Bila shaka mmekwisha sikia kwamba Mungu, kwa neema yake, alinikabidhi kazi hii niifanye kwa faida yenu.
3 Como me foi este mysterio manifestado pela revelação (como acima em poucas palavras vos escrevi;
Mimi nilijulishwa kwa njia ya ufunuo mpango wake uliofichika. (Nimeandika kwa ufupi juu ya jambo hili,
4 Pelo que, lendo, podeis entender a minha sciencia n'este mysterio de Christo),
nanyi mkiyasoma maneno yangu mtaweza kujua jinsi ninavyoielewa siri hiyo ya Kristo.)
5 O qual n'outros seculos não foi manifestado aos filhos dos homens, como agora é revelado pelo Espirito aos seus sanctos apostolos e prophetas;
Zamani watu hawakujulishwa siri hiyo; lakini sasa Mungu amewajulisha mitume na manabii wake watakatifu kwa njia ya Roho.
6 A saber, que os gentios são coherdeiros, e de um mesmo corpo, e participantes da sua promessa em Christo pelo evangelho;
Siri yenyewe ni hii: kwa njia ya Habari Njema watu wa mataifa mengine wanapata sehemu yao pamoja na Wayahudi katika zile baraka za Mungu; wao ni viungo vya mwili uleule, na wanashiriki ahadi ileile aliyofanya Mungu kwa njia ya Kristo Yesu.
7 Do qual sou feito ministro, pelo dom da graça de Deus, que me foi dado segundo a operação do seu poder.
Mimi nimefanywa kuwa mtumishi wa Habari Njema kwa neema ya pekee aliyonijalia Mungu kwa uwezo wake mkuu.
8 A mim, o minimo de todos os sanctos, me foi dada esta graça de annunciar entre os gentios, por meio do evangelho, as riquezas incomprehensiveis de Christo,
Mimi ni mdogo kuliko watu wote wa Mungu; lakini amenijalia neema yake, ili niwahubirie watu wa mataifa utajiri wake Kristo usiopimika,
9 E mostrar a todos qual seja a communhão do mysterio, que desde todos os seculos esteve occulto em Deus, que por Christo Jesus creou todas as coisas; (aiōn g165)
tena niwaangazie watu wote waone jinsi mpango wa Mungu uliofichika unavyotekelezwa. Mungu aliye Muumba wa vitu vyote alificha siri hiyo yake tangu milele, (aiōn g165)
10 Para que agora pela egreja a multiforme sabedoria de Deus seja manifestada aos principados e potestades nos céus,
kusudi, sasa kwa njia ya kanisa, wakuu na wenye enzi wa mbinguni wapate kuitambua hekima ya Mungu iliyo ya namna nyingi.
11 Segundo o eterno proposito que fez em Christo Jesus nosso Senhor: (aiōn g165)
Mungu alifanya jambo hilo kufuatana na azimio lake la milele ambalo amelifanya kwa njia ya Kristo Bwana wetu. (aiōn g165)
12 No qual temos ousadia e accesso com confiança, pela fé n'elle.
Basi, katika kuungana na Kristo, na kwa njia ya imani katika Kristo, sisi tunathubutu kumkaribia Mungu kwa uhodari.
13 Portanto vos peço que não desfalleçaes nas minhas tribulações por vós, que são a vossa gloria
Kwa hiyo, nawaombeni msife moyo kwa sababu ya mateso ninayopata kwa ajili yenu, maana hayo ni kwa ajili ya utukufu wenu.
14 Por causa d'isto me ponho de joelhos perante o Pae de nosso Senhor Jesus Christo,
Kwa sababu hiyo, nampigia magoti Baba,
15 Do qual toda a familia nos céus e na terra toma o nome.
aliye asili ya jamaa zote duniani na mbinguni.
16 Para que, segundo as riquezas da sua gloria, vos conceda que sejaes corroborados com poder pelo seu Espirito no homem interior;
Namwomba Mungu, kadiri ya utajiri wa utukufu wake, awajalieni kwa uwezo wa Roho wake, nguvu ya kuwa imara ndani yenu,
17 Para que Christo habite pela fé nos vossos corações; para que, estando arraigados e fundados em amor,
naye Kristo akae mioyoni mwenu kwa imani. Namwomba mpate kuwa na mzizi na msingi katika mapendo
18 Possaes perfeitamente comprehender, com todos os sanctos, qual seja a largura, e o comprimento, e a altura, e a profundidade,
kusudi muweze kufahamu pamoja na watu wote wa Mungu jinsi upendo wa Kristo ueneavyo kwa mapana na marefu, kwa kimo na kina.
19 E conhecer o amor de Christo, que excede todo o entendimento, para que sejaes cheios de toda a plenitude de Deus.
Naam, mpate kujua upendo wa Kristo upitao elimu yote, mjazwe kabisa utimilifu wote wa Mungu.
20 Ora, áquelle que é poderoso para fazer tudo muito mais abundantemente do que pedimos ou pensamos, segundo o poder que em nós opéra,
Kwake yeye ambaye kwa nguvu yake ifanyayo kazi ndani yetu, aweza kufanya mambo makuu zaidi ya yale tuwezayo kuomba au kufikiria;
21 A esse gloria na egreja, por Jesus Christo, em todas as geracões, para todo o sempre. Amen. (aiōn g165)
kwake Mungu uwe utukufu katika kanisa na katika Kristo Yesu, nyakati zote, milele na milele! Amina. (aiōn g165)

< Efésios 3 >