< رومیان 11 >

پس می‌گویم آیا خدا قوم خود را ردکرد؟ حاشا! زیرا که من نیز اسرائیلی ازاولاد ابراهیم از سبط بنیامین هستم. ۱ 1
Basi, nauliza: je, Mungu amewakataa watu wake? Hata kidogo! Mini binafsi ni Mwisraeli mzawa wa Abrahamu, wa kabila la Benyamini.
خدا قوم خود را که از قبل شناخته بود، رد نفرموده است. آیا نمی دانید که کتاب در الیاس چه می‌گوید، چگونه بر اسرائیل از خدا استغاثه می‌کند ۲ 2
Mungu hakuwakataa watu wake aliowateua tangu mwanzo. Mnakumbuka yasemavyo Maandiko Matakatifu juu ya Eliya wakati alipomnung'unikia Mungu kuhusu Israeli:
که «خداوندا انبیای تو را کشته و مذبحهای تو راکنده‌اند و من به تنهایی مانده‌ام و در قصد جان من نیز می‌باشند»؟ ۳ 3
“Bwana, wamewaua manabii wako na kubomoa madhabahu yako. Ni mimi tu peke yangu niliyebaki, nao wanataka kuniua?”
لکن وحی بدو چه می‌گوید؟ اینکه «هفت هزار مرد بجهت خود نگاه داشتم که به نزد بعل زانو نزده‌اند». ۴ 4
Je, Mungu alimjibu nini? Alimwambia: “Nimejiwekea elfu saba ambao hawakumwabudu Baali.”
پس همچنین در زمان حاضر نیز بقیتی بحسب اختیار فیض مانده است. ۵ 5
Basi, ndivyo ilivyo pia wakati huu wa sasa: ipo idadi ya waliobaki ambao Mungu aliwateua kwa sababu ya neema yake.
و اگر از راه فیض است دیگر از اعمال نیست وگرنه فیض دیگر فیض نیست. اما اگر از اعمال است دیگر از فیض نیست والا عمل دیگر عمل نیست. ۶ 6
Uteuzi wake unatokana na neema yake, na si kwa sababu ya matendo yao. Maana, kama uteuzi wake ungetegemea matendo ya watu, neema yake haingekuwa neema tena.
پس مقصود چیست؟ اینکه اسرائیل آنچه راکه می‌طلبد نیافته است، لکن برگزیدگان یافتند وباقی ماندگان سختدل گردیدند؛ ۷ 7
Sasa, je? Watu wa Israeli hawakukipata kile walichokuwa wanakitafuta; lakini wote walioteuliwa walikipata. Wengine walipumbazwa,
چنانکه مکتوب است که «خدا بدیشان روح خواب‌آلود دادچشمانی که نبیند و گوشهایی که نشنود تا امروز.» ۸ 8
kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: “Mungu ameifanya mioyo yao kuwa mizito, na mpaka leo hii hawawezi kuona kwa macho yao wala kusikia kwa masikio yao.”
و داود می‌گوید که «مائده ایشان برای ایشان تله و دام و سنگ مصادم و عقوبت باد؛ ۹ 9
Naye Daudi anasema: “Karamu zao na ziwe mtego wa kuwanasa, waanguke na kuadhibiwa.
چشمان ایشان تار شود تا نبینند و پشت ایشان را دائم خم گردان.» ۱۰ 10
Macho yao yatiwe giza wasiweze kuona. Migongo yao ipindike kwa taabu daima!”
پس می‌گویم آیا لغزش خوردند تا بیفتند؟ حاشا! بلکه از لغزش ایشان نجات به امت‌ها رسیدتا در ایشان غیرت پدید آورد. ۱۱ 11
Basi, nauliza: je, Wayahudi wamejikwaa hata wakaangamia kabisa? Hata kidogo! Kutokana na kosa lao ukombozi umewajia watu wa mataifa mengine, ili Wayahudi wapate kuwaonea wivu.
پس چون لغزش ایشان دولتمندی جهان گردید و نقصان ایشان دولتمندی امت‌ها، به چند مرتبه زیادترپری ایشان خواهد بود. ۱۲ 12
Kosa la Wayahudi limesababisha baraka nyingi kwa ulimwengu, na utovu wao kwa kiroho umeleta baraka nyingi kwa watu wa mataifa mengine. Basi, ni dhahiri zaidi kwamba utimilifu wao utasababisha baraka nyingi zaidi.
زیرا به شما‌ای امت هاسخن می‌گویم پس از این‌روی که رسول امت هامی باشم خدمت خود را تمجید می‌نمایم، ۱۳ 13
Basi, sasa nawaambieni ninyi watu wa mataifa mengine: Maadamu mimi nimekuwa mtume kwa watu wa mataifa mengine, ninajivunia huduma yangu,
تاشاید ابنای جنس خود را به غیرت آورم و بعضی از ایشان را برهانم. ۱۴ 14
nipate kuwafanya wananchi wenzangu wawaonee ninyi wivu, na hivyo nipate kuwaokoa baadhi yao.
زیرا اگر رد شدن ایشان مصالحت عالم شد، باز‌یافتن ایشان چه خواهدشد؟ جز حیات از مردگان! ۱۵ 15
Maana ikiwa kukataliwa kwao kulisababisha ulimwengu upatanishwe na Mungu, itakuwaje wakati watakapokubaliwa na Mungu? Wafu watafufuka!
و چون نوبر مقدس است، همچنان خمیره و هرگاه ریشه مقدس است، همچنان شاخه‌ها. ۱۶ 16
Ikiwa kipande cha kwanza cha mkate kimewekwa wakfu, mkate wote umewekwa wakfu; mizizi ya mti ikiwa mizuri, na matawi yake huwa mazuri pia.
و چون بعضی از شاخه‌ها بریده شدند و تو که زیتون بری بودی در آنها پیوند گشتی و در ریشه وچربی زیتون شریک شدی، ۱۷ 17
Naam, baadhi ya matawi ya mzeituni bustanini yalikatwa, na mahali pake tawi la mzeituni mwitu likapandikizwa. Ninyi watu wa mataifa mengine ndio hilo tawi la mzeituni mwitu; na sasa mnashiriki nguvu na utomvu wa mzeituni bustanini.
بر شاخه‌ها فخرمکن و اگر فخر کنی تو حامل ریشه نیستی بلکه ریشه حامل تو است. ۱۸ 18
Basi, msiwadharau wale waliokatwa kama matawi! Na, hata kama kuna la kujivunia, kumbukeni kwamba si ninyi mnaoitegemeza mizizi, bali mizizi ndiyo inayowategemeza ninyi.
پس می‌گویی که «شاخه‌ها بریده شدند تا من پیوند شوم؟» ۱۹ 19
Lakini utasema: “Matawi yalikatwa kusudi mimi nipandikizwe mahali pake.”
آفرین بجهت بی‌ایمانی بریده شدند و تومحض ایمان پایدار هستی. مغرور مباش بلکه بترس! ۲۰ 20
Sawa! Yalikatwa kwa sababu ya kukosa imani, bali wewe unasimama kwa imani yako. Lakini usijivune; ila uwe na tahadhari.
زیرا اگر خدا بر شاخه های طبیعی شفقت نفرمود، بر تو نیز شفقت نخواهد کرد. ۲۱ 21
Kwa maana, ikiwa Mungu hakuwahurumia Wayahudi ambao ni kama matawi ya asili, je, unadhani atakuhurumia wewe?
پس مهربانی و سختی خدا را ملاحظه نما؛ اماسختی بر آنانی که افتادند، اما مهربانی برتو اگر درمهربانی ثابت باشی والا تو نیز بریده خواهی شد. ۲۲ 22
Kumbuka, basi, jinsi Mungu alivyo mwema na mkali. Yeye ni mkali kwa wale walioanguka, na ni mwema kwako wewe ikiwa utaendelea katika wema wake; la sivyo, nawe pia utakatwa.
و اگر ایشان نیز در بی‌ایمانی نمانند باز پیوندخواهند شد، زیرا خدا قادر است که ایشان را باردیگر بپیوندد. ۲۳ 23
Nao Wayahudi, hali kadhalika; wakiacha utovu wao wa imani, watapandikizwa tena. Maana Mungu anao uwezo wa kuwapandikiza tena.
زیرا اگر تو از زیتون طبیعی بری بریده شده، برخلاف طبع به زیتون نیکو پیوندگشتی، به چند مرتبه زیادتر آنانی که طبیعی‌اند درزیتون خویش پیوند خواهند شد. ۲۴ 24
Ninyi watu wa mataifa mengine, kwa asili ni kama tawi la mzeituni mwitu, lakini mmeondolewa huko, mkapandikizwa katika mzeituni bustanini mahali ambapo kwa asili si penu. Lakini, Wayahudi kwa asili ni kama mzeituni bustanini, na itakuwa jambo rahisi zaidi kwao kupandikizwa tena katika mti huohuo wao.
زیرا‌ای برادران نمی خواهم شما از این سربی خبر باشید که مبادا خود را دانا انگارید که مادامی که پری امت‌ها درنیاید، سختدلی بربعضی از اسرائیل طاری گشته است. ۲۵ 25
Ndugu zangu, napenda mjue ukweli huu uliofichika msije mkajiona wenye akili sana. Ukaidi wa Wayahudi ulikuwa ni wa muda tu, mpaka watu wa mataifa mengine watakapokuwa wamemfikia Mungu.
وهمچنین همگی اسرائیل نجات خواهند یافت، چنانکه مکتوب است که «از صهیون نجات‌دهنده‌ای ظاهر خواهد شد و بی‌دینی را ازیعقوب خواهد برداشت؛ ۲۶ 26
Hapo ndipo taifa lote la Israeli litakapookolewa, kama yesemavyo Maandiko Matakatifu: “Mkombozi atakuja kutoka Sioni, atauondoa uovu wa Yakobo.
و این است عهد من باایشان در زمانی که گناهانشان را بردارم.» ۲۷ 27
Hili ndilo agano nitakalofanya nao wakati nitakapoziondoa dhambi zao.”
نظر به انجیل بجهت شما دشمنان‌اند، لکن نظر به اختیاربه‌خاطر اجداد محبوبند. ۲۸ 28
Kwa sababu wanaikataa Habari Njema, Wayahudi wamekuwa adui wa Mungu, lakini kwa faida yenu nyinyi watu wa mataifa. Lakini, kwa kuwa waliteuliwa, bado ni rafiki wa Mungu kwa sababu ya baba zao.
زیرا که در نعمتهاودعوت خدا بازگشتن نیست. ۲۹ 29
Maana Mungu akisha wapa watu zawadi zake na kuwateua, hajuti kwamba amefanya hivyo.
زیرا همچنان‌که شما در سابق مطیع خدا نبودید و الان به‌سبب نافرمانی‌ایشان رحمت یافتید، ۳۰ 30
Hapo awali ninyi mlikuwa mmemwasi Mungu, lakini sasa mmepata huruma yake kutokana na kuasi kwao.
همچنین ایشان نیز الان نافرمان شدند تا بجهت رحمتی که بر شما است بر ایشان نیز رحم شود ۳۱ 31
Hali kadhalika, kutokana na huruma mliyojaliwa ninyi, Wayahudi wanamwasi Mungu sasa ili nao pia wapokee sasa huruma ya Mungu.
زیرا خدا همه رادر نافرمانی بسته است تا بر همه رحم فرماید. (eleēsē g1653) ۳۲ 32
Maana Mungu amewafunga watu wote katika uasi wao ili wapate kuwahurumia wote. (eleēsē g1653)
زهی عمق دولتمندی و حکمت و علم خدا! چقدر بعید از غوررسی است احکام او وفوق از کاوش است طریقهای وی! ۳۳ 33
Utajiri, hekima na elimu ya Mungu ni kuu mno! Huruma zake hazichunguziki, na njia zake hazieleweki! Kama yasemavyo Maandiko Matakatifu:
زیرا کیست که رای خداوند را دانسته باشد؟ یا که مشیر اوشده؟ ۳۴ 34
“Nani aliyepata kuyajua mawazo ya Bwana? Nani awezaye kuwa mshauri wake?
یا که سبقت جسته چیزی بدو داده تا به او باز داده شود؟ ۳۵ 35
Au, nani aliyempa yeye kitu kwanza hata aweze kulipwa tena kitu hicho?”
زیرا که از او و به او و تا او همه‌چیز است؛ و او را تا ابدالاباد جلال باد، آمین. (aiōn g165) ۳۶ 36
Kwa maana vitu vyote vyatoka kwake, vyote vipo kwa uwezo wake na kwa ajili yake. Utukufu na uwe kwake hata milele! Amina. (aiōn g165)

< رومیان 11 >