< مزامیر 19 >

برای سالار مغنیان. مزمور داود آسمان جلال خدا را بیان می‌کند وفلک از عمل دستهایش خبر می‌دهد. ۱ 1
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Mbingu zinatangaza utukufu wa Mungu, anga zahubiri kazi ya mikono yake.
روز سخن می‌راند تا روز و شب معرفت را اعلان می‌کند تا شب. ۲ 2
Siku baada ya siku zinatoa habari, usiku baada ya usiku zinatangaza maarifa.
سخن نیست و کلامی نی و آوازآنها شنیده نمی شود. ۳ 3
Hakuna msemo wala lugha, ambapo sauti zao hazisikiki.
قانون آنها در تمام جهان بیرون رفت و بیان آنها تا اقصای ربع مسکون. ۴ 4
Sauti yao imeenea duniani pote, nayo maneno yao yameenea hadi miisho ya ulimwengu. Katika mbingu amepiga hema kwa ajili ya jua,
خیمه‌ای برای آفتاب در آنها قرار داد؛ و او مثل داماد از حجله خود بیرون می‌آید و مثل پهلوان ازدویدن در میدان شادی می‌کند. ۵ 5
linafanana na bwana arusi akitoka chumbani mwake, kama shujaa afurahiavyo kukamilisha kushindana kwake.
خروجش ازکرانه آسمان است و مدارش تا به کرانه دیگر؛ وهیچ‌چیز از حرارتش مستور نیست. ۶ 6
Huchomoza upande mmoja wa mbingu, na kufanya mzunguko wake hadi upande mwingine. Hakuna kilichojificha joto lake.
شریعت خداوند کامل است و جان رابرمی گرداند؛ شهادات خداوند امین است و جاهل را حکیم می‌گرداند. ۷ 7
Sheria ya Bwana ni kamilifu, ikihuisha nafsi. Shuhuda za Bwana ni za kuaminika, zikimpa mjinga hekima.
فرایض خداوند راست است و دل را شاد می‌سازد. امر خداوند پاک است و چشم را روشن می‌کند. ۸ 8
Maagizo ya Bwana ni kamili, nayo hufurahisha moyo. Amri za Bwana huangaza, zatia nuru machoni.
ترس خداوند طاهراست و ثابت تا ابدالاباد. احکام خداوند حق وتمام عدل است. ۹ 9
Kumcha Bwana ni utakatifu, nako kwadumu milele. Amri za Bwana ni za hakika, nazo zina haki.
از طلا مرغوب تر و از زرخالص بسیار. از شهد شیرینتر و از قطرات شانه عسل. ۱۰ 10
Ni za thamani kuliko dhahabu, kuliko dhahabu iliyo safi sana, ni tamu kuliko asali, kuliko asali kutoka kwenye sega.
بنده تو نیز از آنها متنبه می‌شود، و درحفظ آنها ثواب عظیمی است. ۱۱ 11
Kwa hizo mtumishi wako anaonywa, katika kuzishika kuna thawabu kubwa.
کیست که سهوهای خود را بداند؟ مرا ازخطایای مخفی‌ام طاهر ساز. ۱۲ 12
Ni nani awezaye kutambua makosa yake? Nisamehe makosa yangu nisiyoyajua.
بنده ات را نیز ازاعمال متکبرانه باز دار تا بر من مسلط نشود؛ آنگاه بی‌عیب و از گناه عظیم مبرا خواهم بود. ۱۳ 13
Mlinde mtumishi wako na dhambi za makusudi, nazo zisinitawale. Ndipo nitakapokuwa sina lawama, wala sitakuwa na hatia ya kosa kubwa.
سخنان زبانم و تفکر دلم منظور نظر تو باشد، ای خداوند که صخره من و نجات‌دهنده من هستی! ۱۴ 14
Maneno ya kinywa changu na mawazo ya moyo wangu, yapate kibali mbele zako, Ee Bwana, Mwamba wangu na Mkombozi wangu.

< مزامیر 19 >