< امثال 21 >

دل پادشاه مثل نهرهای آب در دست خداوند است، آن را به هر سو که بخواهد برمی گرداند. ۱ 1
Moyo wa mfalme ni mfereji wa maji katika mkono wa Yehova; anaugeuza popote anakopenda.
هر راه انسان در نظر خودش راست است، اماخداوند دلها را می‌آزماید. ۲ 2
Kila njia ya mtu ni sawa katika macho yake mwenyewe, lakini ni Yehova anayeipima mioyo.
عدالت و انصاف را بجا آوردن، نزد خداونداز قربانی‌ها پسندیده تر است. ۳ 3
Kutenda haki na adili hukubaliwa zaidi na Yehova kuliko sadaka.
چشمان بلند و دل متکبر و چراغ شریران، گناه است. ۴ 4
Macho ya kiburi na moyo wa majivuno- taa ya waovu- ni dhambi.
فکرهای مرد زرنگ تمام به فراخی می‌انجامد، اما هر‌که عجول باشد برای احتیاج تعجیل می‌کند. ۵ 5
Mipango ya mwenye juhudi huelekea kwenye mafanikio tu, bali kila mtu anayetenda kwa haraka huelekea umasikini.
تحصیل گنجها به زبان دروغگو، بخاری است بر هوا شده برای جویندگان موت. ۶ 6
Kujipatia utajiri kwa ulimi wa uongo ni mvuke unaopita upesi na mtego ambao unafisha.
ظلم شریران ایشان را به هلاکت می‌اندازد، زیرا که از بجا آوردن انصاف ابا می‌نمایند. ۷ 7
Vurugu ya waovu itawaburuta mbali, maana wanakataa kutenda haki.
طریق مردی که زیر بار (گناه ) باشد بسیار کج است، اما اعمال مرد طاهر، مستقیم است. ۸ 8
Njia ya mwenye hatia ni ukatiri, bali mwenye usafi hutenda yaliyo ya haki.
در زاویه پشت بام ساکن شدن بهتر است، ازساکن بودن با زن ستیزه گر در خانه مشترک. ۹ 9
Bora kuishi kwenye kona ya juu darini kuliko katika nyumba pamoja na mke mgonvi.
جان شریر مشتاق شرارت است، و برهمسایه خود ترحم نمی کند. ۱۰ 10
Hamu ya mwovu ni uchu wa mabaya; jirani yake haoni ukarimu katika macho yake.
چون استهزاکننده سیاست یابد جاهلان حکمت می‌آموزند، و چون مرد حکیم تربیت یابد معرفت را تحصیل می‌نماید. ۱۱ 11
Mwenye dhihaka anapoadhibiwa mjinga hupata busara, na mtu mwenye busara anapofundishwa, anaongeza maarifa.
مرد عادل در خانه شریر تامل می‌کند که چگونه اشرار به تباهی واژگون می‌شوند. ۱۲ 12
Atendaye haki huilinda nyumba ya mwovu; huwashusha waovu kwenye uharibifu.
هر‌که گوش خود را از فریاد فقیر می‌بندد، او نیز فریاد خواهد کرد و مستجاب نخواهد شد. ۱۳ 13
Anayeziba masikio yake kwenye kilio cha masikini, pia atalia, lakini hatajibiwa.
هدیه‌ای در خفا خشم را فرو می‌نشاند، ورشوه‌ای در بغل، غضب سخت را. ۱۴ 14
Zawadi ya siri hutuliza hasira na zawadi ya kificho hutuliza ghadhabu kuu.
انصاف کردن خرمی عادلان است، اما باعث پریشانی بدکاران می‌باشد. ۱۵ 15
Haki ikitendeka, huleta furaha kwa mwenye kutenda wema, lakini huleta hofu kubwa kwa watenda mabaya.
هر‌که از طریق تعقل گمراه شود، درجماعت مردگان ساکن خواهد گشت. ۱۶ 16
Yule anayezurura kutoka kwenye njia ya ufahamu, atapumzika kwenye kusanyiko la wafu.
هر‌که عیش را دوست دارد محتاج خواهدشد، و هر‌که شراب و روغن را دوست دارددولتمند نخواهد گردید. ۱۷ 17
Anayependa raha atakuwa masikini; anayependa divai na mafuta hawezi kuwa tajiri.
شریران فدیه عادلان می‌شوند وخیانتکاران به عوض راستان. ۱۸ 18
Mtu mbaya ni fidia kwa yule atendaye haki, na mdanganyifu ni fidia kwa waaminifu.
در زمین بایر ساکن بودن بهتر است از بودن با زن ستیزه گر و جنگجوی. ۱۹ 19
Bora kuishi jangwani kuliko kuishi pamoja na mwanamke ambaye huchochea sana ugomvi na malalamiko.
در منزل حکیمان خزانه مرغوب و روغن است، اما مرد احمق آنها را تلف می‌کند. ۲۰ 20
Hazina yenye thamani na mafuta vipo nyumbani kwa mwenye busara, bali mtu mpumbavu huviharibu.
هر‌که عدالت و رحمت را متابعت کند، حیات و عدالت و جلال خواهد یافت. ۲۱ 21
Mtu atendaye haki na mwema -huyu mtu hupata uzima, haki na heshima.
مرد حکیم به شهر جباران برخواهد آمد، وقلعه اعتماد ایشان را به زیر می‌اندازد. ۲۲ 22
Mtu mwenye busara huupima mji wa mashujaa, na huiangusha ngome wanayoitumaini.
هر‌که دهان و زبان خویش را نگاه دارد، جان خود را از تنگیها محافظت می‌نماید. ۲۳ 23
Anayelinda kinywa chake na ulimi wake hujilinda mwenyewe na taabu.
مرد متکبر و مغرور مسمی به استهزاکننده می‌شود، و به افزونی تکبر عمل می‌کند. ۲۴ 24
Mtu mwenye kiburi na maringo- “Dhihaka” ndilo jina lake - hutenda kwa majivuno na kujidai.
شهوت مرد کاهل او را می‌کشد، زیرا که دستهایش از کار کردن ابا می‌نماید. ۲۵ 25
Shauku ya mtu mvivu itamuua, maana mikono yake hukataa kufanya kazi.
هستند که همه اوقات به شدت حریص می‌باشند، اما مرد عادل بذل می‌کند و امساک نمی نماید. ۲۶ 26
Kwa siku nzima hupatwa na uchu na uchu zaidi, lakini atendaye haki hutoa na wala hazuii.
قربانی های شریران مکروه است، پس چندمرتبه زیاده هنگامی که به عوض بدی آنها رامی گذرانند. ۲۷ 27
Sadaka ya mwovu ni chukizo; huwa ni chukizo zaidi anapoileta kwa nia mbaya.
شاهد دروغگو هلاک می‌شود، اما کسی‌که استماع نماید به راستی تکلم خواهد کرد. ۲۸ 28
Shahidi wa uongo ataangamia, bali anayesikiliza ataongea kwa muda wote.
مرد شریر روی خود را بی‌حیا می‌سازد، ومرد راست، طریق خویش را مستحکم می‌کند. ۲۹ 29
Mtu mwovu huufanya uso wake kuwa mgumu, bali mtu mwadilifu ni thabiti juu ya njia zake.
حکمتی نیست و نه فطانتی و نه مشورتی که به ضد خداوند به‌کار آید. ۳۰ 30
Hakuna hekima, hakuna ufahamu, na hakuna shauri linaloweza kusimama kinyume na Yehova.
اسب برای روز جنگ مهیا است، اما نصرت از جانب خداوند است. ۳۱ 31
Farasi hutayarishwa kwa siku ya mapigano, lakini ushindi hupatikana kwa Yehova.

< امثال 21 >