< لاویان 12 >

و خداوند موسی را خطاب کرده، گفت: ۱ 1
Bwana akamwambia Mose,
«بنی‌اسرائیل را خطاب کرده، بگو: چون زنی آبستن شده، پسر نرینه‌ای بزاید، آنگاه هفت روز نجس باشد، موافق ایام طمث حیضش نجس باشد. ۲ 2
“Waambie Waisraeli: ‘Mwanamke ambaye atapata mimba na kuzaa mtoto wa kiume atakuwa najisi kwa kawaida ya ibada kwa siku saba, kama anavyokuwa najisi wakati wa siku zake za hedhi.
و در روز هشتم گوشت غلفه اومختون شود. ۳ 3
Mvulana atatahiriwa siku ya nane.
و سی و سه روز در خون تطهیرخود بماند، و هیچ‌چیز مقدس را لمس ننماید، وبه مکان مقدس داخل نشود، تا ایام طهرش تمام شود. ۴ 4
Kisha ni lazima huyo mwanamke asubiri kwa siku thelathini na tatu, ndipo atakaswe kutoka damu kwake. Hataruhusiwa kugusa kitu chochote kilicho kitakatifu au kuingia mahali patakatifu, mpaka siku za kutakaswa kwake zimetimia.
و اگر دختری بزاید، دو هفته برحسب مدت طمث خود نجس باشد، و شصت و شش روز در خون تطهیر خود بماند. ۵ 5
Kama akimzaa mtoto wa kike, mwanamke huyo atakuwa najisi kwa majuma mawili, kama wakati wake wa hedhi. Kisha atasubiri kwa siku sitini na sita, ndipo atatakaswa kutoka damu kwake.
و چون ایام طهرش برای پسر یا دختر تمام شود، بره‌ای یک ساله برای قربانی سوختنی و جوجه کبوتر یافاخته‌ای برای قربانی گناه به در خیمه اجتماع نزدکاهن بیاورد. ۶ 6
“‘Siku zake za utakaso kwa ajili ya mwana au binti zitakapotimia, mwanamke huyo atamletea kuhani kwenye ingilio la Hema la Kukutania mwana-kondoo mwenye umri wa mwaka mmoja kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa, na kinda la njiwa au hua kwa ajili ya sadaka ya dhambi.
و او آن را به حضور خداوندخواهد گذرانید، و برایش کفاره خواهد کرد، تا ازچشمه خون خود طاهر شود. این است قانون آن که بزاید، خواه پسر خواه دختر. ۷ 7
Atavitoa mbele za Bwana ili kufanya upatanisho kwa ajili yake, na kisha atakuwa safi kwa desturi ya ibada kutokana na kutokwa damu kwake. “‘Haya ndiyo masharti kwa ajili ya mwanamke atakayezaa mtoto wa kiume au wa kike.
و اگر دست اوبه قیمت بره نرسد، آنگاه دو فاخته یا دو جوجه کبوتر بگیرد، یکی برای قربانی سوختنی ودیگری برای قربانی گناه. و کاهن برای وی کفاره خواهد کرد، و طاهر خواهد شد.» ۸ 8
Kama huyo mwanamke hana uwezo wa kumpata mwana-kondoo, ataleta hua wawili au makinda mawili ya njiwa, moja kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa na mwingine kwa ajili ya sadaka ya dhambi. Kwa njia hii, kuhani atafanya upatanisho kwa ajili yake, naye atakuwa safi.’”

< لاویان 12 >