< ایّوب 1 >

در زمین عوص، مردی بود که ایوب نام داشت و آن مرد کامل و راست و خداترس بود و از بدی اجتناب می‌نمود. ۱ 1
Katika nchi ya Usi paliishi mtu ambaye aliitwa Ayubu. Mtu huyu alikuwa hana hatia, naye alikuwa mkamilifu; alimcha Mungu na kuepukana na uovu.
و برای او، هفت پسر و سه دختر زاییده شدند. ۲ 2
Alikuwa na wana saba na binti watatu,
و اموال او هفت هزار گوسفند و سه هزار شتر و پانصد جفت گاو وپانصد الاغ ماده بود و نوکران بسیار کثیر داشت وآن مرد از تمامی بنی مشرق بزرگتر بود. ۳ 3
naye alikuwa na kondoo elfu saba, ngamia elfu tatu, jozi mia tano za maksai, na punda mia tano, tena alikuwa na idadi kubwa ya watumishi. Alikuwa mtu mkuu sana miongoni mwa watu wa Mashariki.
و پسرانش می‌رفتند و در خانه هر یکی ازایشان، در روزش مهمانی می‌کردند و فرستاده، سه خواهر خود را دعوت می‌نمودند تا با ایشان اکل و شرب بنمایند. ۴ 4
Wanawe walikuwa na desturi ya kufanya karamu katika nyumba zao kwa zamu, nao wangewaalika umbu zao watatu ili kula na kunywa pamoja nao.
و واقع می‌شد که چون دوره روزهای مهمانی‌ایشان بسر می‌رفت، ایوب فرستاده، ایشان را تقدیس می‌نمود و بامدادان برخاسته، قربانی های سوختنی، به شماره همه ایشان می‌گذرانید، زیرا ایوب می‌گفت: «شایدپسران من گناه کرده، خدا را در دل خود ترک نموده باشند» و ایوب همیشه چنین می‌کرد. ۵ 5
Wakati kipindi cha karamu kilimalizika, Ayubu angetuma waitwe na kuwafanyia utakaso. Angetoa dhabihu ya sadaka ya kuteketezwa kwa ajili ya kila mmoja wao asubuhi na mapema, akifikiri, “Pengine wanangu wametenda dhambi na kumlaani Mungu mioyoni mwao.” Hii ilikuwa ndiyo desturi ya kawaida ya Ayubu.
و روزی واقع شد که پسران خدا آمدند تا به حضور خداوند حاضر شوند و شیطان نیز در میان ایشان آمد. ۶ 6
Siku moja wana wa Mungu walikwenda kujionyesha mbele za Bwana. Shetani naye akaja pamoja nao.
و خداوند به شیطان گفت: «از کجاآمدی؟» شیطان در جواب خداوند گفت: «ازتردد کردن در زمین و سیر کردن در آن.» ۷ 7
Bwana akamwambia Shetani, “Umetoka wapi?” Shetani akamjibu Bwana, “Natoka kuzunguka pote duniani, nikitembea huku na huko humo.”
خداوندبه شیطان گفت: «آیا در بنده من ایوب تفکر کردی که مثل او در زمین نیست؟ مرد کامل وراست و خداترس که از گناه اجتناب می‌کند.» ۸ 8
Ndipo Bwana akamwambia Shetani, “Je, umemwangalia huyo mtumishi wangu Ayubu? Hakuna mtu mwingine duniani aliye kama yeye, asiye na hatia, ni mnyofu, mwenye kumcha Mungu, na kuepukana na uovu.”
شیطان در جواب خداوند گفت: «آیا ایوب مجان از خدا می‌ترسد؟ ۹ 9
Shetani akamjibu Bwana, “Je, Ayubu anamcha Mungu bure?
آیا تو گرد او و گردخانه او و گرد همه اموال او، به هر طرف حصارنکشیدی و اعمال دست او را برکت ندادی ومواشی او در زمین منتشر نشد؟ ۱۰ 10
Je, wewe hukumjengea boma pande zote yeye na wa nyumbani mwake pamoja na kila kitu alicho nacho? Kazi za mikono yake umezibariki na hivyo makundi yake ya kondoo na mbuzi pamoja na ya wanyama yameenea katika nchi nzima.
لیکن الان دست خود را دراز کن و تمامی مایملک او رالمس نما و پیش روی تو، تو را ترک خواهدنمود.» ۱۱ 11
Lakini nyoosha mkono wako na kupiga kila kitu alicho nacho, naye kwa hakika atakulaani mbele za uso wako.”
خداوند به شیطان گفت: «اینک همه اموالش در دست تو است، لیکن دستت را بر خوداو دراز مکن.» پس شیطان از حضور خداوندبیرون رفت. ۱۲ 12
Bwana akamwambia Shetani, “Vema sana, kwa hiyo, kila kitu alicho nacho kiko mikononi mwako, lakini juu ya huyo mtu mwenyewe usimguse hata kwa kidole.” Ndipo Shetani akatoka mbele za Bwana.
و روزی واقع شد که پسران و دخترانش درخانه برادر بزرگ خود می‌خوردند و شراب می‌نوشیدند. ۱۳ 13
Siku moja watoto wa Ayubu walipokuwa wakifanya karamu wakila na kunywa divai katika nyumba ya ndugu yao mkubwa,
و رسولی نزد ایوب آمده، گفت: «گاوان شیار می‌کردند و ماده الاغان نزد آنهامی چریدند. ۱۴ 14
akaja mjumbe kwa Ayubu na kusema, “Maksai walikuwa wakilima na punda walikuwa wakilisha karibu nao,
و سابیان بر آنها حمله آورده، بردند و جوانان را به دم شمشیر کشتند و من به تنهایی رهایی یافتم تا تو را خبر دهم.» ۱۵ 15
Waseba wakawashambulia na kuchukua mifugo. Kisha wakawaua watumishi kwa upanga, nami ndimi peke yangu niliyenusurika kukuletea habari!”
و اوهنوز سخن می‌گفت که دیگری آمده، گفت: «آتش خدا از آسمان افتاد و گله و جوانان راسوزانیده، آنها را هلاک ساخت و من به تنهایی رهایی یافتم تا تو را خبر دهم.» ۱۶ 16
Alipokuwa bado ananena, mjumbe mwingine akaja na kusema, “Moto wa Mungu ulishuka kutoka mbinguni na kuteketeza kondoo na watumishi, nami ndimi peke yangu niliyenusurika kukuletea habari!”
و او هنوزسخن می‌گفت که دیگری آمده، گفت: «کلدانیان سه فرقه شدند و بر شتران هجوم آورده، آنها را بردند و جوانان را به دم شمشیر کشتند و من به تنهایی رهایی یافتم تا تو را خبر دهم.» ۱۷ 17
Alipokuwa bado ananena, mjumbe mwingine akaja na kusema, “Wakaldayo waliunda vikosi vitatu vya uvamizi na kuwaangukia ngamia wako na kuwachukua wakaondoka nao. Wakawaua watumishi kwa upanga, nami ndimi peke yangu niliyenusurika kukuletea habari.”
و اوهنوز سخن می‌گفت که دیگری آمده، گفت: «پسران و دخترانت در خانه برادر بزرگ خودمی خوردند و شراب می‌نوشیدند ۱۸ 18
Alipokuwa bado ananena, mjumbe mwingine akaja na kusema, “Wana wako na binti zako walipokuwa wakifanya karamu, wakila na kunywa divai katika nyumba ya ndugu yao mkubwa,
که اینک بادشدیدی از طرف بیابان آمده، چهار گوشه خانه رازد و بر جوانان افتاد که مردند و من به تنهایی رهایی یافتم تا تو را خبر دهم.» ۱۹ 19
ghafula upepo wenye nguvu ukavuma kutoka jangwani, nao ukaipiga nyumba hiyo pembe zake nne. Ikawaangukia hao watoto nao wamekufa, nami ndimi peke yangu niliyenusurika kukuletea habari!”
آنگاه ایوب برخاسته، جامه خود را درید وسر خود را تراشید و به زمین افتاده، سجده کرد ۲۰ 20
Ndipo Ayubu akasimama, akararua joho lake na kunyoa nywele zake. Kisha akaanguka chini katika kuabudu
و گفت: «برهنه از رحم مادر خود بیرون آمدم وبرهنه به آنجا خواهم برگشت؛ خداوند داد وخداوند گرفت و نام خداوند متبارک باد.» ۲۱ 21
na kusema: “Nilitoka tumboni mwa mama yangu uchi, nami nitaondoka uchi, Bwana alinipa, naye Bwana ameviondoa, jina la Bwana litukuzwe.”
دراین همه، ایوب گناه نکرد و به خدا جهالت نسبت نداد. ۲۲ 22
Katika mambo haya yote, Ayubu hakutenda dhambi kwa kumlaumu Mungu kwa kufanya ubaya.

< ایّوب 1 >