< جامعه 9 >

زیرا که جمیع این مطالب را در دل خود نهادم و این همه را غور نمودم که عادلان وحکیمان و اعمال ایشان در دست خداست. خواه محبت و خواه نفرت، انسان آن را نمی فهمد. همه‌چیز پیش روی ایشان است. ۱ 1
Kwa hiyo niliyatafakari yote haya nikafikia uamuzi kwamba waadilifu na wenye hekima na yale wanayoyafanya yako mikononi mwa Mungu, lakini hakuna mtu ajuaye kama anangojewa na upendo au chuki.
همه‌چیز برای همه کس مساوی است. برای عادلان و شریران یک واقعه است؛ برای خوبان و طاهران و نجسان؛ برای آنکه ذبح می‌کند و برای آنکه ذبح نمی کندواقعه یکی است. چنانکه نیکانند همچنان گناهکارانند؛ و آنکه قسم می‌خورد و آنکه از قسم خوردن می‌ترسد مساوی‌اند. ۲ 2
Wote wanayo hatima inayofanana, mwadilifu na mwovu, mwema na mbaya, aliye safi na aliye najisi, wale wanaotoa dhabihu na wale wasiotoa. Kama ilivyo kwa mtu mwema, ndivyo ilivyo kwa mtu mwenye dhambi; kama ilivyo kwa wale wanaoapa, ndivyo ilivyo kwa wale wasioapa.
در تمامی اعمالی که زیر آفتاب کرده می‌شود، از همه بدتر این است که یک واقعه برهمه می‌شود و اینکه دل بنی آدم از شرارت پراست و مادامی که زنده هستند، دیوانگی در دل ایشان است و بعد از آن به مردگان می‌پیوندند. ۳ 3
Huu ni ubaya ulio katika kila kitu kinachotendeka chini ya jua: Mwisho unaofanana huwapata wote. Zaidi ya hayo, mioyo ya watu, imejaa ubaya na kuna wazimu mioyoni mwao wangali hai, hatimaye huungana na waliokufa.
زیرا برای آنکه با تمامی زندگان می‌پیوندد، امیدهست چونکه سگ زنده از شیر مرده بهتر است. ۴ 4
Yeyote aliye miongoni mwa walio hai analo tumaini, hata mbwa hai ni bora kuliko simba aliyekufa!
زانرو که زندگان می‌دانند که باید بمیرند، امامردگان هیچ نمی دانند و برای ایشان دیگر اجرت نیست چونکه ذکر ایشان فراموش می‌شود. ۵ 5
Kwa maana walio hai wanajua kwamba watakufa, lakini wafu hawajui chochote, hawana tuzo zaidi, hata kumbukumbu yao imesahaulika.
هم محبت و هم نفرت و حسد ایشان، حال نابود شده است و دیگر تا به ابد برای ایشان از هر‌آنچه زیرآفتاب کرده می‌شود، نصیبی نخواهد بود. ۶ 6
Upendo wao, chuki yao na wivu wao vimetoweka tangu kitambo, kamwe hawatakuwa tena na sehemu katika lolote linalotendeka chini ya jua.
پس رفته، نان خود را به شادی بخور وشراب خود را به خوشدلی بنوش چونکه خدااعمال تو را قبل از این قبول فرموده است. ۷ 7
Nenda, kula chakula chako kwa furaha, unywe divai yako kwa moyo wa shangwe, kwa maana sasa Mungu anakubali unachofanya.
لباس تو همیشه سفید باشد و بر سر تو روغن کم نشود. ۸ 8
Daima uvae nguo nyeupe na daima upake kichwa chako mafuta.
جمیع روزهای عمر باطل خود را که او تو را درزیر آفتاب بدهد با زنی که دوست می‌داری درجمیع روزهای بطالت خود خوش بگذران. زیراکه از حیات خود و از زحمتی که زیر آفتاب می‌کشی نصیب تو همین است. ۹ 9
Furahia maisha na mke wako, umpendaye, siku zote za maisha ya ubatili uliyopewa na Mungu chini ya jua, siku zote za ubatili. Kwa maana hili ndilo fungu lako katika maisha na katika kazi yako ya taabu chini ya jua.
هر‌چه دستت به جهت عمل نمودن بیابد، همان را با توانایی خود به عمل آور چونکه در عالم اموات که به آن می‌روی نه کار و نه تدبیر و نه علم و نه حکمت است. (Sheol h7585) ۱۰ 10
Lolote mkono wako upatalo kufanya, fanya kwa nguvu zako zote, kwa kuwa huko kuzimu, unakokwenda, hakuna kufanya kazi wala mipango wala maarifa wala hekima. (Sheol h7585)
برگشتم و زیر آفتاب دیدم که مسابقت برای تیزروان و جنگ برای شجاعان و نان نیز برای حکیمان و دولت برای فهیمان و نعمت برای عالمان نیست، زیرا که برای جمیع ایشان وقتی واتفاقی واقع می‌شود. ۱۱ 11
Nimeona kitu kingine tena chini ya jua: Si wenye mbio washindao mashindano au wenye nguvu washindao vita, wala si wenye hekima wapatao chakula au wenye akili nyingi wapatao mali, wala wenye elimu wapatao upendeleo, lakini fursa huwapata wote.
و چونکه انسان نیز وقت خود را نمی داند، پس مثل ماهیانی که در تورسخت گرفتار و گنجشکانی که در دام گرفته می‌شوند، همچنان بنی آدم به وقت نامساعد هرگاه آن بر ایشان ناگهان بیفتد گرفتار می‌گردند. ۱۲ 12
Zaidi ya hayo, hakuna mwanadamu ajuaye wakati saa yake itakapokuja: Kama vile samaki wavuliwavyo katika wavu mkatili, au ndege wanaswavyo kwenye mtego, vivyo hivyo wanadamu hunaswa na nyakati mbaya zinazowaangukia bila kutazamia.
و نیز این حکم را در زیر آفتاب دیدم و آن نزد من عظیم بود: ۱۳ 13
Pia niliona chini ya jua mfano huu wa hekima ambao ulinivutia sana:
شهری کوچک بود که مردان در آن قلیل العدد بودند و پادشاهی بزرگ بر آن آمده، آن را محاصره نمود و سنگرهای عظیم برپاکرد. ۱۴ 14
Palikuwa na mji mdogo uliokuwa na watu wachache ndani yake. Mfalme mwenye nguvu akainuka dhidi yake, akauzunguka akaweka jeshi kubwa dhidi yake.
و در آن شهر مردی فقیر حکیم یافت شد، که شهر را به حکمت خود رهانید، اما کسی آن مرد فقیر را بیاد نیاورد. ۱۵ 15
Katika mji huo kulikuwepo mtu mmoja maskini lakini mwenye hekima, naye akauokoa ule mji kwa hekima yake. Lakini hakuna aliyemkumbuka yule maskini.
آنگاه من گفتم حکمت از شجاعت بهتر است، هر‌چند حکمت این فقیررا خوار شمردند و سخنانش را نشنیدند. ۱۶ 16
Kwa hiyo, nikasema, “Hekima ni bora kuliko nguvu.” Lakini hekima ya maskini imedharauliwa, wala hakuna anayesikiliza maneno yake.
سخنان حکیمان که به آرامی گفته شود، ازفریاد حاکمی که در میان احمقان باشد زیاده مسموع می‌گردد. ۱۷ 17
Maneno ya utulivu ya mwenye hekima husikiwa kuliko makelele ya mtawala wa wapumbavu.
حکمت از اسلحه جنگ بهتر است. اما یک خطاکار نیکویی بسیار را فاسدتواند نمود. ۱۸ 18
Hekima ni bora kuliko silaha za vita, lakini mwenye dhambi mmoja huharibu mema mengi.

< جامعه 9 >