< کارهای رسولان 4 >

و چون ایشان با قوم سخن می‌گفتند، کهنه وسردار سپاه هیکل و صدوقیان بر سر ایشان تاختند، ۱ 1
Wakati Petro na Yohana walipokuwa wakizungumza na watu, makuhani na mlinzi wa hekalu na masadukayo waliwaendea.
چونکه مضطرب بودند از اینکه ایشان قوم را تعلیم می‌دادند و در عیسی به قیامت ازمردگان اعلام می‌نمودند. ۲ 2
Walikuwa wameudhika sana kwa sababu Petro na Yohana walikuwa wanawafundisha watu kuhusu Yesu na kutangaza juu ya kufufuka kwake kutoka kwa wafu.
پس دست بر ایشان انداخته، تا فردا محبوس نمودند زیرا که آن، وقت عصر بود. ۳ 3
Waliwakamata na kuwaweka gerezani hadi asubuhi iliyofuata, kwani tayari ilikuwa jioni.
اما بسیاری از آنانی که کلام را شنیدند ایمان آوردند و عدد ایشان قریب به پنج هزاررسید. ۴ 4
Lakini watu wengi waliokuwa wamesikia ujumbe waliamini; na idadi ya wanaume waliokuwa wameamini walikadiliwa kuwa elfu tano.
بامدادان روسا و مشایخ و کاتبان ایشان دراورشلیم فراهم آمدند، ۵ 5
Hata ilipofika asubuhi siku iliyofuata, kwamba wakuu wao, wazee na waandishi, kwa pamoja walikusanyika Yerusalemu.
با حنای رئیس کهنه وقیافا و یوحنا و اسکندر و همه کسانی که از قبیله رئیس کهنه بودند. ۶ 6
Anasi kuhani mkuu alikuwepo, na Kayafa, na Yohana, na Iskanda, na wote waliokuwa ni ndugu wa kuhani mkuu.
و ایشان را در میان بداشتند واز ایشان پرسیدند که «شما به کدام قوت و به چه نام این کار را کرده‌اید؟» ۷ 7
Walipokuwa wamewaweka Petro na Yohana katikati yao, waliwauliza, “Kwa uwezo gani, au kwa jina gani mmefanya hili?”
آنگاه پطرس ازروح‌القدس پر شده، بدیشان گفت: «ای روسای قوم و مشایخ اسرائیل، ۸ 8
Kisha, Petro, akiwa amejaa Roho Mtakatifu, akawaambia, “Ninyi wakuu wa watu, na wazee,
اگر امروز از ما بازپرس می‌شود درباره احسانی که بدین مرد ضعیف شده، یعنی به چه سبب او صحت یافته است، ۹ 9
kama sisi siku ya leo tunahojiwa kuhusu tendo jema lililofanywa kwa mtu huyu mgonjwa - kwa namna gani mtu huyu alifanywa mzima?
جمیع شما و تمام قوم اسرائیل را معلوم باد که به نام عیسی مسیح ناصری که شما مصلوب کردید و خدا او را از مردگان برخیزانید، در او این کس به حضور شما تندرست ایستاده است. ۱۰ 10
Hebu lijulikane hilo kwenu na kwa watu wote katika Israel, kwamba kwa jina la Yesu Kristo wa Nazareti, ambaye mlimsulibisha, ambaye Mungu alimfufua kutoka kwa wafu, ni kwa njia yake kwamba mtu huyu anasimama hapa mbele yenu akiwa mwenye afya.
این است آن سنگی که شما معماران آن را رد کردید والحال سر زاویه شده است. ۱۱ 11
Yesu Kristo ni jiwe ambalo ninyi wajenzi mlilidharau, lakini ambalo limefanywa kuwa jiwe kuu la pembeni.
و در هیچ‌کس غیراز او نجات نیست زیرا که اسمی دیگر زیر آسمان به مردم عطانشده که بدان باید ما نجات یابیم.» ۱۲ 12
Hakuna wokovu katika mtu mwingine awaye yote. Kwa maana hakuna jina jingine chini ya mbingu walilopewa watu, ambalo kwa hilo tunaweza kuokolewa.”
پس چون دلیری پطرس و یوحنا را دیدندو دانستند که مردم بی‌علم و امی هستند، تعجب کردند و ایشان را شناختند که از همراهان عیسی بودند. ۱۳ 13
Sasa walipoona ujasiri wa Petro na Yohana, na wakagundua kwamba walikuwa ni watu wakawaida wasio na elimu, walishangaa, wakafahamu kwamba Petro na Yohana wamekuwa pamoja na Yesu.
و چون آن شخص را که شفا یافته بود باایشان ایستاده دیدند، نتوانستند به ضد ایشان چیزی گویند. ۱۴ 14
Kwa sababu walimwona yule mtu aliyeponywa amesimama pamoja nao, hawakuwa na kitu cha kusema dhidi ya hili.
پس حکم کردند که ایشان ازمجلس بیرون روند و با یکدیگر مشورت کرده، گفتند ۱۵ 15
Lakini walipokuwa wamekwisha kuwaamuru mitume waondoke mbele ya mkutano wa baraza, walizungumza wao kwa wao.
که «با این دو شخص چه کنیم؟ زیرا که برجمیع سکنه اورشلیم واضح شد که معجزه‌ای آشکار از ایشان صادر گردید و نمی توانیم انکار کرد. ۱۶ 16
Walisema, tutawafanyaje watu hawa? Ni kweli kwamba muujiza wa ajabu umefanyika kupitia wao unajulikana na kila mmoja anayeishi Yerusalemu; hatuwezi kulikataa hilo.
لیکن تا بیشتر در میان قوم شیوع نیابد، ایشان را سخت تهدید کنیم که دیگر با هیچ‌کس این اسم را به زبان نیاورند.» ۱۷ 17
Lakini, ili kwamba jambo hili lisienee miongoni mwa watu, hebu tuwaonye wasinene tena kwa mtu yeyote kwa jina hili.
پس ایشان راخواسته قدغن کردند که هرگز نام عیسی را بر زبان نیاورند و تعلیم ندهند. ۱۸ 18
Waliwaita Petro na Yohana ndani na kuwaamuru kamwe wasinene wala kufundisha kwa jina la Yesu.
اما پطرس و یوحنا درجواب ایشان گفتند: «اگر نزد خدا صواب است که اطاعت شما را بر اطاعت خدا ترجیح دهیم حکم کنید. ۱۹ 19
Lakini Petro na Yohana walijibu na kuwaambia, “Kama ni sahihi machoni pa Mungu kuwatii ninyi kuliko Mungu, hukumuni wenyewe.
زیرا که ما را امکان آن نیست که آنچه دیده و شنیده‌ایم، نگوییم.» ۲۰ 20
Maana sisi hatuwezi kuacha kuyanena mambo ambayo tumeyaona na kuyasikia.”
و چون ایشان رازیاد تهدید نموده بودند، آزاد ساختند چونکه راهی نیافتند که ایشان را معذب سازند به‌سبب قوم زیرا همه به واسطه آن ماجرا خدا را تمجیدمی نمودند، ۲۱ 21
Baada ya kuwaonya sana Petro na Yohana, waliwaacha waende. Hawakuweza kupata sababu yoyote ya kuwaadhibu, kwa sababu watu wote walikuwa wakimsifu Mungu kwa kile kilichokuwa kimetendeka.
زیرا آن شخص که معجزه شفا دراو پدید گشت، بیشتر از چهل ساله بود. ۲۲ 22
Mtu aliyekuwa amepokea muujiza wa uponyaji alipata kuwa na umri zaidi ya miaka arobaini.
و چون رهایی یافتند، نزد رفقای خودرفتند و ایشان را از آنچه روسای کهنه و مشایخ بدیشان گفته بودند، مطلع ساختند. ۲۳ 23
Baada ya kuwaacha huru, Petro na Yohana walikuja kwa watu wao na kuwataarifu yote ambayo makuhani wakuu na wazee walikuwa wamewaambia.
چون این راشنیدند، آواز خود را به یکدل به خدا بلند کرده، گفتند: «خداوندا، تو آن خدا هستی که آسمان وزمین و دریا و آنچه در آنها است آفریدی، ۲۴ 24
Walipoyasikia, walipaza sauti zao kwa pamoja kwa Mungu na kusema, “Bwana, wewe uliyeumba mbingu na dunia na bahari na kila kitu ndani yake,
که بوسیله روح‌القدس به زبان پدر ما و بنده خودداود گفتی “چرا امت‌ها هنگامه می‌کنند و قومها به باطل می‌اندیشند؛ ۲۵ 25
wewe ambaye, kwa Roho Mtakatifu, kwa kinywa cha baba yetu Daudi, mtumishi wako, ulisema, “Kwanini watu wa mataifa wamefanya ghasia, na watu wametafakari mambo yasiyofaa?
سلاطین زمین برخاستند وحکام با هم مشورت کردند، برخلاف خداوند وبرخلاف مسیحش.” ۲۶ 26
Wafalme wa dunia wamejipanga pamoja, na watawala wamekusanyika kwa pamoja dhidi ya Bwana na dhidi ya masihi wake.”
زیرا که فی الواقع بر بنده قدوس تو عیسی که او را مسح کردی، هیرودیس و پنطیوس پیلاطس با امت‌ها و قومهای اسرائیل با هم جمع شدند، ۲۷ 27
Ni hakika, wote Herode na Pontio Pilato, pamoja na watu wa mataifa na watu wa Israeli, walikusanyika kwa pamoja katika mji huu dhidi ya mtumishi wako mtakatifu Yesu, ambaye ulimpaka mafuta.
تا آنچه را که دست و رای تو از قبل مقدر فرموده بود، به‌جا آورند. ۲۸ 28
Walikusanyika kwa pamoja kufanya yote ambayo mkono wako na mapenzi yako yaliyaamuru tangu awali kabla hayajatokea.
و الان ای خداوند، به تهدیدات ایشان نظر کن و غلامان خود را عطا فرما تا به دلیری تمام به کلام تو سخن گویند، ۲۹ 29
Sasa, Bwana, yaangalie matisho yao, na ukawajaalie watumishi wako kulinena neno lako kwa ujasiri wote. Ili
به دراز کردن دست خود، بجهت شفادادن و جاری کردن آیات و معجزات به نام بنده قدوس خود عیسی.» ۳۰ 30
kwamba unaponyosha mkono wako kuponya, ishara na maajabu viweze kutokea kupitia jina la mtumishi wako mtakatifu Yesu.”
و چون ایشان دعا کرده بودند، مکانی که درآن جمع بودند به حرکت آمد و همه به روح‌القدس پر شده، کلام خدا را به دلیری می‌گفتند. ۳۱ 31
Walipomaliza kuomba, eneo ambalo walikusanyika kwa pamoja likatikiswa, na wote wakajazwa na Roho Mtakatifu, na walinena neno la Mungu kwa ujasili.
و جمله مومنین را یک دل و یک جان بود، بحدی که هیچ‌کس چیزی از اموال خودرا از آن خود نمی دانست، بلکه همه‌چیز رامشترک می‌داشتند. ۳۲ 32
Idadi kubwa ya wale walioamini walikuwa na moyo mmoja na roho moja: na hakuna hata mmoja wao aliyesema kwamba chochote alichomiliki kilikuwa cha kwake mwenyewe; badala yake walikuwa na vitu vyote shirika.
و رسولان به قوت عظیم به قیامت عیسی خداوند شهادت می‌دادند و فیضی عظیم برهمگی ایشان بود. ۳۳ 33
Kwa nguvu kubwa mitume walikuwa wakiutangaza ushuhuda wao kuhusu ufufuo wa Bwana Yesu, na neema kubwa ilikuwa juu yao wote.
زیرا هیچ‌کس از آن گروه محتاج نبود زیرا هر‌که صاحب زمین یا خانه بود، آنها را فروختند و قیمت مبیعات را آورده، ۳۴ 34
Hapakuwa na mtu yeyote miongoni mwao aliyepungukiwa na mahitaji, kwa sababu watu wote waliokuwa na hati za viwanja au nyumba, waliviuza na kuleta pesa ya vitu waliyokuwa wameuza
به قدمهای رسولان می‌نهادند و به هر یک بقدراحتیاجش تقسیم می‌نمودند. ۳۵ 35
na kuviweka chini ya miguu ya mitume. Na mgawanyo ulifanywa kwa kila muumini, kulingana na kila mmoja alivyokuwa na hitaji.
و یوسف که رسولان او را برنابا یعنی ابن الوعظ لقب دادند، مردی از سبط لاوی و از طایفه قپرسی، ۳۶ 36
Yusufu, mlawi, mtu kutoka Kipro, alipewa jina la Barnabasi na mitume (hiyo ikitafasiriwa, ni mwana wa faraja).
زمینی را که داشت فروخته، قیمت آن را آورد و پیش قدمهای رسولان گذارد. ۳۷ 37
Akiwa na shamba, aliliuza na akaleta fedha, akaziweka chini ya miguu ya mitume.

< کارهای رسولان 4 >