< دوم تواریخ 22 >

و ساکنان اورشلیم پسر کهترش اخزیارا در جایش به پادشاهی نصب کردند، زیرا گروهی که با عربان بر اردو هجوم آورده بودند، همه پسران بزرگش را کشته بودند. پس اخزیا ابن یهورام پادشاه یهودا سلطنت کرد. ۱ 1
Watu wa Yerusalemu wakamfanya Ahazia, mdogo wa wote wa wana wa Yerohamu, kuwa mfalme mahali pa baba yake, kwa sababu washambuliaji wa ghafula waliokuwa wameingia kambini pamoja na Waarabu, walikuwa wamewaua wana wakubwa wote wa Yehoramu. Kwa hiyo Ahazia mwana wa Yehoramu mfalme wa Yuda akaanza kutawala.
واخزیا چهل و دو ساله بود که پادشاه شد و یک سال در اورشلیم سلطنت کرد و اسم مادرش عتلیادختر عمری بود. ۲ 2
Ahazia alikuwa na umri wa miaka ishirini na miwili alipoanza kutawala, naye akatawala katika Yerusalemu kwa mwaka mmoja. Mama yake aliitwa Athalia, mjukuu wa Omri.
و او نیز به طریق های خاندان اخاب سلوک نمود زیرا که مادرش ناصح او بود تا اعمال زشت بکند. ۳ 3
Ahazia naye akaenenda katika njia za nyumba ya Ahabu, kwa sababu mama yake alimshawishi katika kutenda maovu.
و مثل خاندان اخاب آنچه در نظر خداوند ناپسند بود، بجا آورد زیرا که ایشان بعد از وفات پدرش، برای هلاکتش ناصح او بودند. ۴ 4
Akafanya yaliyo maovu machoni pa Bwana kama walivyokuwa wamefanya nyumba ya Ahabu, kwa kuwa baada ya kufa kwa baba yake nyumba ya Ahabu ndio waliokuwa washauri wake, kwa uangamivu wake.
پس برحسب مشورت ایشان رفتارنموده، با یهورام بن اخاب پادشاه اسرائیل نیزبرای جنگ با حزائیل پادشاه ارام به راموت جلعاد رفت و ارامیان یورام را مجروح نمودند. ۵ 5
Pia akafuata shauri lao alipokwenda pamoja na Yoramu mwana wa Ahabu mfalme wa Israeli kupigana na Hazaeli mfalme wa Aramu huko Ramoth-Gileadi. Waaramu wakamjeruhi Yoramu.
پس به یزرعیل مراجعت کرد تا از جراحاتی که در محاربه با حزائیل پادشاه ارام در رامه یافته بود، شفا یابد. و عزریا ابن یهورام پادشاه یهودا برای عیادت یهورام بن اخاب به یزرعیل فرود آمد زیراکه بیمار بود. ۶ 6
Hivyo akarudi Yezreeli ili apate kuuguza majeraha aliyojeruhiwa huko Ramothi alipopigana na Hazaeli mfalme wa Aramu. Ndipo Ahazia mwana wa Yehoramu, mfalme wa Yuda, akashuka kwenda Yezreeli kumtazama Yoramu mwana wa Ahabu, kwa sababu alikuwa amejeruhiwa.
و هلاکت اخزیا در اینکه نزد یورام رفت، ازجانب خدا بود زیرا چون به آنجا رسید، با یهورام به مقابله ییهو ابن نمشی که خداوند او را برای هلاک ساختن خاندان اخاب مسح کرده بود، بیرون رفت. ۷ 7
Mungu alikuwa ameamuru kwamba kuanguka kwa Ahazia kungetokea atakapokwenda kumwona Yoramu. Ahazia alipowasili, wakatoka pamoja na Yoramu ili kwenda kukutana na Yehu mwana wa Nimshi, ambaye Bwana alikuwa amemtia mafuta kuangamiza nyumba ya Ahabu.
و چون ییهو قصاص بر خاندان اخاب می‌رسانید، بعضی از سروران یهودا وپسران برادران اخزیا را که ملازمان اخزیا بودندیافته، ایشان را کشت. ۸ 8
Yehu alipokuwa anatekeleza hukumu juu ya nyumba ya Ahabu, akawakuta wakuu wa Yuda na wana wa jamaa ya Ahazia waliokuwa wanamhudumia Ahazia, naye akawaua.
و اخزیا را طلبید و او رادر حالتی که در سامره پنهان شده بود، دستگیرنموده، نزد ییهو آوردند و او را به قتل رسانیده، دفن کردند زیرا گفتند: «پسر یهوشافاط است که خداوند را به تمامی دل خود طلبید.» پس، ازخاندان اخزیا، کسی‌که قادر بر سلطنت باشد، نماند. ۹ 9
Ndipo akaenda kumsaka Ahazia, nao watu wake wakamkamata alipokuwa amejificha huko Samaria. Akaletwa kwa Yehu, naye Yehu akamuua. Wakamzika kwani walisema, “Alikuwa mwana wa Yehoshafati, ambaye alimtafuta Bwana kwa moyo wake wote.” Hivyo hapakuwa na mtu mwenye uwezo katika nyumba ya Ahazia aliyeweza kushika ufalme.
پس چون عتلیا مادر اخزیا دید که پسرش کشته شده است، برخاست و تمامی اولادپادشاهان از خاندان یهودا را هلاک کرد. ۱۰ 10
Wakati Athalia mamaye Ahazia alipoona kuwa mwanawe amekufa, akainuka na kuiangamiza jamaa yote ya mfalme ya nyumba ya Yuda.
لیکن یهوشبعه، دختر پادشاه، یوآش پسر اخزیا را گرفت و او را از میان پسران پادشاه که مقتول شدند دزدیده، او را با دایه‌اش در اطاق خوابگاه گذاشت و یهوشبعه، دختر یهورام پادشاه، زن یهویاداع کاهن که خواهر اخزیا بود، او را از عتلیاپنهان کرد که او را نکشت. ۱۱ 11
Lakini Yehosheba, binti wa Mfalme Yehoramu, akamtwaa Yoashi mwana wa Ahazia kwa siri kutoka miongoni mwa wana wa mfalme waliokuwa karibu kuuawa. Akamweka Yoashi pamoja na yaya wake ndani ya chumba cha kulala. Kwa kuwa Yehosheba, aliyekuwa binti wa Mfalme Yehoramu, na pia alikuwa mke wa kuhani Yehoyada, alikuwa dada yake Ahazia, akamficha huyo mtoto ili Athalia asimuue.
و او نزد ایشان درخانه خدا مدت شش سال پنهان ماند. و عتلیا برزمین سلطنت می‌کرد. ۱۲ 12
Alibaki amefichwa pamoja nao katika Hekalu la Mungu kwa muda wa miaka sita wakati Athalia alikuwa akitawala nchi.

< دوم تواریخ 22 >