< Jobs 40 >

1 Og Herren svara Job og sagde:
Bwana akamwambia Ayubu:
2 «Vil klandraren med Allvald trætta? Lat han som lastar Gud då svara!»
“Je, mwenye kushindana na Mwenyezi aweza kumsahihisha? Mwenye kumlaumu Mungu na ajibu.”
3 Då svara Job Herren og sagde:
Ndipo Ayubu akamjibu Bwana:
4 «For ring eg er; kva skal eg svara? Eg handi legg på munnen min.
“Mimi sistahili kabisa: ninawezaje kukujibu wewe? Nauweka mkono wangu juu ya kinywa changu.
5 Ein gong eg tala, no eg tegjer, tvo gong’ - eg gjer det ikkje meir.»
Nimesema mara moja, lakini sina jibu; naam, nimesema mara mbili, lakini sitasema tena.”
6 Og Herren svara Job or stormen og sagde:
Ndipo Bwana akasema na Ayubu kutoka upepo wa kisulisuli:
7 «Spenn som mann ditt beltet på, gjev meg på mine spursmål svar:
“Jikaze kama mwanaume; nitakuuliza maswali, nawe yakupasa unijibu.
8 Vil du forspille meg min rett, fordøma meg, so du fær rett?
“Je, utabatilisha hukumu yangu? Utanilaumu mimi ili kujihesabia haki mwenyewe?
9 Hev du vel slik ein arm som Gud? Kann du som han med røysti dundra?
Je, una mkono kama wa Mungu, nawe waweza kutoa sauti ya ngurumo kama yake?
10 Pryd deg med høgd og herredom, klæd deg i glans og herlegdom,
Basi jivike mwenyewe utukufu na fahari, nawe uvae heshima na enzi.
11 Lat so din vreide strøyma fram, sjå kvar ein stolt og audmyk han!
Fungulia ukali wa ghadhabu yako, mtafute kila mwenye kiburi umshushe,
12 Så kvar ein stolt og bøyg han ned, og slå til jord dei gudlause!
mwangalie kila mtu mwenye kiburi na umnyenyekeze, waponde waovu mahali wasimamapo.
13 Og gøym deim alle under jordi, bitt deira andlit fast i løynd!
Wazike wote mavumbini pamoja; wafunge nyuso zao kaburini.
14 So skal eg og lovprisa deg, som siger med di høgre vann.
Ndipo mimi mwenyewe nitakukubalia kuwa mkono wako mwenyewe wa kuume unaweza kukuokoa.
15 Sjå elvhesten! Eg hev skapt han liksom deg; som ein ukse et han gras.
“Mwangalie mnyama aitwaye Behemothi, niliyemuumba kama nilivyokuumba wewe, anayekula majani kama ngʼombe.
16 Sjå då krafti i hans lender, i bukmusklarne hans styrke!
Tazama basi nguvu alizo nazo kwenye viuno vyake, uwezo alio nao kwenye misuli ya tumbo lake!
17 Halen gjer han stiv som ceder, fast bogsenarne er tvinna.
Mkia wake hutikisika kama mwerezi; mishipa ya mapaja yake imesukwa pamoja.
18 Knokarne er koparrøyrer, beini som jarnstenger er.
Mifupa yake ni bomba za shaba, maungo yake ni kama fito za chuma.
19 Av Guds verk er han det fyrste, av sin skapar fekk han sverd.
Yeye ni wa kwanza miongoni mwa kazi za Mungu, lakini Muumba wake anaweza kumsogelea kwa upanga wake.
20 Bergi ber åt honom for, alle villdyr leikar der.
Vilima humletea yeye mazao yake, nao wanyama wote wa porini hucheza karibu naye.
21 Under lotusbusk han kviler, løyner seg i røyr og sev.
Hulala chini ya mimea ya yungiyungi, katika maficho ya matete kwenye matope.
22 Lotusbusk gjev honom skugge, piletre umkransar honom.
Hiyo mimea ya yungiyungi humficha kwenye vivuli vyake; miti mirefu karibu na kijito humzunguka.
23 Strid gjeng elvi, ei han ottast; trygg er han um so sjølve Jordan fossar imot hans gap.
Wakati mto ufurikapo, yeye hapati mshtuko wa hofu; yeye yu salama, hata kama Yordani ingefurika hadi kwenye kinywa chake.
24 Kann ein tak han so han ser det, draga snara gjenom snuten?
Je, mtu yeyote anaweza kumkamata yeye akiwa macho, au kumnasa kwa mtego na kutoboa pua yake?

< Jobs 40 >