< Pāvila Vēstule Galatiešiem 4 >

1 Bet Es jums saku: kamēr mantinieks vēl ir bērns, tad starp viņu un kalpu nav nekādas starpības, jebšu viņš kungs ir pār visu mantu.
Lile nisemalo ni kwamba wakati wote mrithi bado ni mtoto, hana tofauti na mtumwa, ingawa ndiye mmiliki wa mali yote.
2 Bet viņš ir apakš pārstāvētājiem un sargiem līdz tam no tēva nospriestam laikam.
Yeye huwa yuko chini ya uangalizi wa walezi na wadhamini mpaka ufike wakati uliowekwa na baba yake.
3 Tāpat arī mēs, kad bijām bērni, bijām kalpu kārtā apakš pasaules likumu sākumiem.
Vivyo hivyo na sisi, tulipokuwa bado watoto wadogo, tulikuwa utumwani chini ya taratibu za kawaida za ulimwengu.
4 Bet kad tā laika piepildīšana nāca, tad Dievs sūtīja Savu Dēlu, dzimušu no sievas un noliktu apakš bauslības,
Lakini ulipowadia utimilifu wa wakati, Mungu alimtuma Mwanawe, ambaye alizaliwa na mwanamke, akazaliwa chini ya sheria,
5 Ka Viņš tos, kas bija apakš bauslības, atpirktu, ka mēs to bērnu tiesu dabūtu.
kusudi awakomboe wale waliokuwa chini ya sheria, ili tupate kupokea zile haki kamili za kufanywa watoto wa Mungu.
6 Un kad nu jūs esat bērni, tad Dievs Sava Dēla Garu ir sūtījis jūsu sirdīs, tas sauc: Abba, Tēvs!
Kwa sababu ninyi ni watoto wa Mungu, Mungu amemtuma Roho wa Mwanawe mioyoni mwetu, anayelia, “Abba, Baba.”
7 Tad nu vairs neesi kalps, bet bērns; bet ja bērns, tad arī Dieva mantinieks caur Kristu.
Kwa hiyo, wewe si mtumwa tena, bali ni mtoto, kwa kuwa wewe ni mtoto, Mungu amekufanya wewe pia kuwa mrithi kwa kupitia Kristo.
8 Bet to brīdi, kad jūs Dievu neatzināt, jūs esat kalpojuši tiem, kas pēc būšanas nav dievi.
Zamani, mlipokuwa hammjui Mungu, mlikuwa watumwa wa viumbe ambavyo kwa asili si Mungu.
9 Un tagad, kad jūs Dievu atzīstat, bet jo vairāk, kad no Dieva esat atzīti, - kā jūs atkal griežaties pie tiem vājiem un tukšiem sākumiem un tiem atkal no jauna gribat kalpot?
Lakini sasa kwa kuwa mmemjua Mungu, au zaidi mmejulikana na Mungu, inakuwaje mnarejea tena katika zile kanuni za kwanza zenye udhaifu na upungufu? Mnataka ziwafanye tena watumwa?
10 Jūs cienījat dienas un mēnešus un laikus un gadus.
Mnaadhimisha siku maalum, miezi, nyakati na miaka!
11 Man bail jūsu dēļ, ka tik nebūšu velti pie jums strādājis.
Nina hofu juu yenu, kwamba kazi niliyofanya kwa ajili yenu inaweza kuwa nimejitaabisha bure.
12 Topiet tādi, kā es; jo arī es esmu tapis tāds, kā jūs, brāļi, es jūs lūdzu. - Jūs man neko neesat pāri darījuši.
Ndugu zangu, nawasihi mwe kama mimi, kwa sababu mimi nimekuwa kama ninyi. Hamkunitendea jambo lolote baya.
13 Bet jūs zināt, ka es pirmoreiz miesas vājības dēļ jums evaņģēliju esmu sludinājis;
Ninyi mwajua kwamba ni kwa ajili ya udhaifu wangu niliwahubiria Injili.
14 Un tā pārbaudīšana, kas jums caur manu miesu notikusi, jums nav bijusi nicināma nedz nepanesama, bet jūs mani esat uzņēmuši tā kā Dieva eņģeli, tā kā Kristu Jēzu.
Ingawa hali yangu iliwatia majaribuni, hamkunidharau wala kunidhihaki, bali mlinikaribisha kama malaika wa Mungu, kama vile Kristo Yesu.
15 Tad nu, kāda līksmība jums to brīdi bija? Jo es jums dodu liecību, ka jūs, ja tas būtu varējis būt, savas acis būtu izrāvuši un man devuši.
Ile hali ya furaha mliyokuwa nayo imekwenda wapi? Naweza kushuhudia kwamba, kama ingewezekana mngengʼoa macho yenu na kunipa mimi.
16 Vai tad es nu jūsu ienaidnieks esmu tapis, jums patiesību sacīdams?
Je, sasa nimekuwa adui yenu kwa kuwaambia kweli?
17 Tie iekarst jūsu dēļ, kā nav labi, bet tie jūs grib novērst, lai jūs atkal iekarstu viņu dēļ.
Hao wana shauku ya kuwapata lakini si kwa kusudi zuri. Wanachotaka ni kuwatenga mbali nasi, ili ninyi mpate kuwaonea wao shauku.
18 Bet labi ir vienmēr iekarst laba dēļ un ne tad vien, kad es esmu klāt pie jums.
Ni vizuri wakati wote kuwa na shauku kwa ajili ya kusudi zuri, si wakati nikiwa pamoja nanyi tu.
19 Mani bērniņi, ko es atkal dzemdēju ar sāpēm, tiekams Kristus iekš jums nāk redzams,
Watoto wangu wapendwa, ambao kwa mara nyingine ninawaonea utungu, ninatamani kwamba Kristo aumbike ndani yenu.
20 Es gan vēlētos, tagad pie jums būt un citādā balsī runāt; jo man jūsu dēļ padoma pietrūkst.
Natamani kama ningekuwa pamoja nanyi sasa, pengine ningebadilisha sauti yangu. Kwa maana nina wasiwasi kwa ajili yenu.
21 Sakiet man, jūs, kas apakš bauslības gribat būt, vai jūs bauslību neesat dzirdējuši?
Niambieni, ninyi mnaotaka kuwa chini ya sheria, je, hamjui sheria inavyosema?
22 Jo ir rakstīts, ka Ābrahāmam bijuši divi dēli, viens no tās kalpones un otrs no tās svabadās.
Kwa maana imeandikwa kwamba Abrahamu alikuwa na wana wawili, mmoja wa mwanamke mtumwa na wa pili wa mwanamke huru.
23 Bet kas no tās kalpones bija, tas ir piedzimis pēc miesas; un kas no tās svabadās, tas caur to apsolīšanu.
Lakini, mtoto wa mwanamke mtumwa alizaliwa kwa mapenzi ya mwili, na yule mwingine wa mwanamke huru alizaliwa kutokana na ahadi ya Mungu.
24 Šie vārdi pēc līdzības saprotami. Šīs ir tās divas derības; viena no Sina kalna, kas uz kalpošanu dzemdē, tā ir tā Hāgare.
Mambo haya yanaweza kuchukuliwa kama mfano. Kwa maana hao wanawake wawili ni mfano wa maagano mawili: Agano la kwanza, ni lile lililofanyika katika Mlima Sinai, lizaalo watoto wa utumwa. Hili ndilo huyo Hagari.
25 Jo Hāgare ir tas Sina kalns Arābijā - un līdzinājās tai tagadējai Jeruzālemei, kas kalpo ar saviem bērniem.
Basi Hagari anawakilisha Mlima Sinai ulioko Arabuni, na unafanana na Yerusalemu ya sasa ambayo iko utumwani pamoja na watoto wake.
26 Bet tā Jeruzāleme, kas ir augšā, ir tā svabadā, tā ir mūsu visu māte.
Lakini Yerusalemu wa juu ni huru, nayo ndiye mama yetu.
27 Jo ir rakstīts: priecājies, neauglīgā, tu, kas neesi dzemdējusi, izsaucies un gavilē tu, kas bērnu sāpes necieti; jo tai tukšai ir daudz bērnu, vairāk nekā tai, kas ir apprecēta.
Kwa maana imeandikwa: “Furahi, ewe mwanamke tasa, wewe usiyezaa; paza sauti, na kuimba kwa furaha, wewe usiyepatwa na utungu wa kuzaa; kwa maana watoto wa mwanamke aliyeachwa ukiwa ni wengi kuliko wa mwanamke mwenye mume.”
28 Bet mēs, brāļi, esam apsolīšanas bērni, tā kā Īzaks.
Basi, sisi ndugu zangu, ni kama Isaki, tu watoto wa ahadi.
29 Bet itin kā to brīdi tas, kas bija piedzimis pēc miesas, vajāja to, kas bija piedzimis pēc Gara, tāpat arī tagad.
Lakini, kama vile ilivyokuwa siku zile yule aliyezaliwa kwa mwili alivyomchokoza yule aliyezaliwa kwa Roho, ndivyo ilivyo hata sasa.
30 Bet ko tas raksts saka? Izmet to kalponi un viņas dēlu; jo tam kalpones dēlam nebūs mantot ar tās svabadās dēlu.
Lakini Maandiko yasemaje? “Mwondoe mwanamke mtumwa pamoja na mwanawe, kwa sababu mwana wa mwanamke mtumwa kamwe hatarithi pamoja na mwana wa aliye huru.”
31 Tāpēc, brāļi, mēs neesam tās kalpones bērni, bet tās svabadās.
Kwa hiyo ndugu zangu, sisi si watoto wa mwanamke mtumwa, bali wa yule aliye huru.

< Pāvila Vēstule Galatiešiem 4 >