< תהילים 18 >
למנצח לעבד יהוה לדוד אשר דבר ליהוה את דברי השירה הזאת ביום הציל יהוה אותו מכף כל איביו ומיד שאול ויאמר ארחמך יהוה חזקי׃ | 1 |
Nakupenda, Yahwe, nguvu yangu.
יהוה סלעי ומצודתי ומפלטי אלי צורי אחסה בו מגני וקרן ישעי משגבי׃ | 2 |
Yahwe ni mwamba wangu, ngome yangu, yeye ambaye aniwekae kweye usalama; yeye ni Mungu wangu, mwamba wangu; ninapata kimbilio kwake. Yeye ni ngao yangu, pembe ya wokovu wangu, na ngome yangu.
מהלל אקרא יהוה ומן איבי אושע׃ | 3 |
Nitamuita Yahwe kwa sababu anastahili kusifiwa, na nitaokolewa kutoka kwa adui zangu.
אפפוני חבלי מות ונחלי בליעל יבעתוני׃ | 4 |
Kamba za mauti zilinizunguka, na mafuriko yakimbiayo yalinielemea.
חבלי שאול סבבוני קדמוני מוקשי מות׃ (Sheol ) | 5 |
Kamba za kuzimu zilinizunguka; mitego ya mauti ilininasa. (Sheol )
בצר לי אקרא יהוה ואל אלהי אשוע ישמע מהיכלו קולי ושועתי לפניו תבוא באזניו׃ | 6 |
dhiki yangu nilimuita Yahwe; Niliita msaada kwa Mungu. Naye alisikia sauti yangu kutoka hekaluni mwake; kuita kwangu msaada kulienda mpaka uweponi mwake; na kuingia masikioni pake.
ותגעש ותרעש הארץ ומוסדי הרים ירגזו ויתגעשו כי חרה לו׃ | 7 |
Kisha nchi ikatikisika na kutetemeka; misingi ya milima pia ilitetemeka na kutikiswa kwa sababu Mungu alikuwa amekasirika.
עלה עשן באפו ואש מפיו תאכל גחלים בערו ממנו׃ | 8 |
Moshi ulifuka kutoka kwenye pua zake, na moto mkali ulitokea mdomoni mwake. Makaa yaliwashwa kwa moto huo.
ויט שמים וירד וערפל תחת רגליו׃ | 9 |
Yeye alizifunua mbingu na alishuka chini, na giza nene lilikuwa chini ya miguu yake.
וירכב על כרוב ויעף וידא על כנפי רוח׃ | 10 |
Alipanda kwenye kerubi na akaruka; alinyiririka kwenye mabawa ya upepo.
ישת חשך סתרו סביבותיו סכתו חשכת מים עבי שחקים׃ | 11 |
Yahwe alilifanya giza kuwa hema likimzunguka yeye, wingu la mvua zito katika mbingu.
מנגה נגדו עביו עברו ברד וגחלי אש׃ | 12 |
Mawe ya barafu na makaa ya moto yalianguka kutoka katika mwangaza kabla yake.
וירעם בשמים יהוה ועליון יתן קלו ברד וגחלי אש׃ | 13 |
Yahwe aliongea katika mbingu! Sauti ya aliye juu ilisikika.
וישלח חציו ויפיצם וברקים רב ויהמם׃ | 14 |
Yeye aliifyatua mishale yake na kuwatawanya adui zake; na radi nyingi zenye mwanga alizitawanya katika maeneo tofauti tofauti.
ויראו אפיקי מים ויגלו מוסדות תבל מגערתך יהוה מנשמת רוח אפך׃ | 15 |
Ndipo mifereji ya maji ilitokea; misingi ya dunia ikadhihirishwa kwa mlio wa pigo lako, Yahwe kwa sauti ya pumzi ya pua zako.
ישלח ממרום יקחני ימשני ממים רבים׃ | 16 |
Yeye alishuka chini kutokea juu; akanishikilia mimi! Akanivuta nje ya maji yafurikayo.
יצילני מאיבי עז ומשנאי כי אמצו ממני׃ | 17 |
Aliniokoa kutoka kwa maadui zangu wenye nguvu, kutoka kwa wale ambao walinichukia mimi, kwa kuwa walikuwa na nguvu sana kuliko mimi.
יקדמוני ביום אידי ויהי יהוה למשען לי׃ | 18 |
Wao walikuja kinyume na mimi katika siku ile ya dhiki yangu lakini Mungu alikuwa msaada wangu!
ויוציאני למרחב יחלצני כי חפץ בי׃ | 19 |
Yeye aliniweka huru katika eneo pana la wazi; yeye aliniokoa kwa sababu alipenezwa nami.
יגמלני יהוה כצדקי כבר ידי ישיב לי׃ | 20 |
Yahwe amenitunuku mimi kwa sababu ya haki yangu; yeye amenirejesha mimi kwa sababu mikono yangu ilikuwa misafi.
כי שמרתי דרכי יהוה ולא רשעתי מאלהי׃ | 21 |
Kwa kuwa nimezitunza njia za Yahwe na sijafanya uovu wa kumgeuka Mungu wangu.
כי כל משפטיו לנגדי וחקתיו לא אסיר מני׃ | 22 |
Kwa kuwa amri zake zote za haki zimekuwa mbele yangu; kama asemavyo, sijaenda kinyume nazo.
ואהי תמים עמו ואשתמר מעוני׃ | 23 |
Pia nimekuwa sina hatia mbele zake, na nimejiweka mwenyewe mbali na dhambi.
וישב יהוה לי כצדקי כבר ידי לנגד עיניו׃ | 24 |
Hivyo Yahwe amenirejesha kwa sababu ya haki yangu, na kwa sababu mikono yangu ilikuwa safi mbele ya macho yake.
עם חסיד תתחסד עם גבר תמים תתמם׃ | 25 |
Kwa yeyote aliye mwaminifu, jionyeshe wenyewe kuwa mwaminifu; kwa mtu asiye na lawama, jionyeshe mwenyewe kuwa usiye na lawama.
עם נבר תתברר ועם עקש תתפתל׃ | 26 |
Kwa yeyote aliye msafi, jionyeshe mwenyewe safi; bali ni mjanja kwa yeyote aliye geuzwa.
כי אתה עם עני תושיע ועינים רמות תשפיל׃ | 27 |
Kwa kuwa wewe huwaokoa watu walio taabishwa, lakini wewe huwashusha chini wale wenye majivuno, yaani macho yaliyo jinua!
כי אתה תאיר נרי יהוה אלהי יגיה חשכי׃ | 28 |
Kwa kuwa wewe huipa mwanga taa yangu; Yahwe Mungu wangu hutia mwanga giza langu.
כי בך ארץ גדוד ובאלהי אדלג שור׃ | 29 |
Kwa kuwa kwa kupitia wewe ninaweza kuruka juu ya kiwazo kilichowekwa; kupitia Mungu ninaweza kuruka juu ya ukuta.
האל תמים דרכו אמרת יהוה צרופה מגן הוא לכל החסים בו׃ | 30 |
Kama kwa Mungu: njia yake ni kamilifu. Neno la Yahwe ni safi! Yeye ni ngao kwa yeyote anaye kimbilia katika yeye.
כי מי אלוה מבלעדי יהוה ומי צור זולתי אלהינו׃ | 31 |
Kwa kuwa nani ni Mungu ispokuwa Yahwe? Nani ndiye mwamba ispokuwa Mungu wetu?
האל המאזרני חיל ויתן תמים דרכי׃ | 32 |
Ni Mungu anitiaye nguvu ndani yangu kama vile mkanda, ambaye humweka mtu mwenye lawama katika njia yake.
משוה רגלי כאילות ועל במתי יעמידני׃ | 33 |
Yeye hunifanya miguu yangu kuwa myepesi kama mbawala na kuniweka mahali pa juu!
מלמד ידי למלחמה ונחתה קשת נחושה זרועתי׃ | 34 |
Yeye hufunza viganja vyangu kwa ajili ya vita na mikono yangu kupiga upinde wa shaba.
ותתן לי מגן ישעך וימינך תסעדני וענותך תרבני׃ | 35 |
Wewe umenipa mimi ngao ya wokovu. Mkono wako wa kuume umenisaidia, na neema yako imenifanya kuwa mkubwa.
תרחיב צעדי תחתי ולא מעדו קרסלי׃ | 36 |
Wewe umetengeneza nafasi pana kwa ajili ya miguu yangu ili miguu yangu isiteleze.
ארדוף אויבי ואשיגם ולא אשוב עד כלותם׃ | 37 |
Ninawashawishi adui zangu na kuwakamata; nami sikurudi nyuma mpaka walipo haribiwa.
אמחצם ולא יכלו קום יפלו תחת רגלי׃ | 38 |
Niliwashambulia hata hawakuweza kuamka; nao wameangukia chini ya miguu yangu.
ותאזרני חיל למלחמה תכריע קמי תחתי׃ | 39 |
Kwa kuwa unanitia nguvu kama mshipi kwa ajili ya vita; wewe unawaweka chini yangu wale ambao wanainuka kinyume na mimi.
ואיבי נתתה לי ערף ומשנאי אצמיתם׃ | 40 |
Wewe ulinipa visogo vya maadui zangu; niliwaagamiza wale walio nichukia.
ישועו ואין מושיע על יהוה ולא ענם׃ | 41 |
Wao waliita msaada lakini hakuna aliye wasaidia; walimuita Yahwe, lakini hakuwaitikia.
ואשחקם כעפר על פני רוח כטיט חוצות אריקם׃ | 42 |
Niliwapiga wao katika vipande vidogo vidogo kama vile vumbi mbele ya upepo; niliwatupa nje kama udongo mtaani.
תפלטני מריבי עם תשימני לראש גוים עם לא ידעתי יעבדוני׃ | 43 |
Wewe uliniokoa mimi kutoka katika migogoro ya watu. wewe umenifanya kichwa juu ya mataifa. Watu ambao sikuwahi kuwafahamu huntumikia.
לשמע אזן ישמעו לי בני נכר יכחשו לי׃ | 44 |
Pindi tu waliposikia kuhusu mimi, wao walinitii; wageni walilazimishwa kunisujudu.
בני נכר יבלו ויחרגו ממסגרותיהם׃ | 45 |
Wageni walitoka kwenye ngome yao wakitetemeka.
חי יהוה וברוך צורי וירום אלוהי ישעי׃ | 46 |
Yahwe anaishi; mwamba wangu usifiwe. Ainuliwe Mungu wa wokovu wangu.
האל הנותן נקמות לי וידבר עמים תחתי׃ | 47 |
Yeye ni Mungu ambaye hutelekeza visasi kwa ajili yangu, ambaye huwatiisha mataifa chini yangu.
מפלטי מאיבי אף מן קמי תרוממני מאיש חמס תצילני׃ | 48 |
Nimewekwa huru kutoka kwa adui zangu! wewe uliniinua juu ya wale walioinuka kunyume na mimi! Wewe uliniokoa kutoka kwa watu wenye vurugu.
על כן אודך בגוים יהוה ולשמך אזמרה׃ | 49 |
Kwa hiyo nitakushukuru wewe, Yahwe, kati ya mataifa; Nitaliimbia sifa jina lako!
מגדל ישועות מלכו ועשה חסד למשיחו לדוד ולזרעו עד עולם׃ | 50 |
Mungu hutoa ushindi mkuu kwa mfalme wake, na yeye huonyesha uaminifu wa agano lake kwa mpakwa mafuta wake, kwa Daudi na ukoo wake milele.