< תהילים 18 >

למנצח לעבד יהוה--לדוד אשר דבר ליהוה את-דברי השירה הזאת-- ביום הציל-יהוה אותו מכף כל-איביו ומיד שאול ב ויאמר-- ארחמך יהוה חזקי 1
Nakupenda, Yahwe, nguvu yangu.
יהוה סלעי ומצודתי-- ומפלטי אלי צורי אחסה-בו מגני וקרן-ישעי משגבי 2
Yahwe ni mwamba wangu, ngome yangu, yeye ambaye aniwekae kweye usalama; yeye ni Mungu wangu, mwamba wangu; ninapata kimbilio kwake. Yeye ni ngao yangu, pembe ya wokovu wangu, na ngome yangu.
מהלל אקרא יהוה ומן-איבי אושע 3
Nitamuita Yahwe kwa sababu anastahili kusifiwa, na nitaokolewa kutoka kwa adui zangu.
אפפוני חבלי-מות ונחלי בליעל יבעתוני 4
Kamba za mauti zilinizunguka, na mafuriko yakimbiayo yalinielemea.
חבלי שאול סבבוני קדמוני מוקשי מות (Sheol h7585) 5
Kamba za kuzimu zilinizunguka; mitego ya mauti ilininasa. (Sheol h7585)
בצר-לי אקרא יהוה-- ואל-אלהי אשוע ישמע מהיכלו קולי ושועתי לפניו תבוא באזניו 6
dhiki yangu nilimuita Yahwe; Niliita msaada kwa Mungu. Naye alisikia sauti yangu kutoka hekaluni mwake; kuita kwangu msaada kulienda mpaka uweponi mwake; na kuingia masikioni pake.
ותגעש ותרעש הארץ-- ומוסדי הרים ירגזו ויתגעשו כי-חרה לו 7
Kisha nchi ikatikisika na kutetemeka; misingi ya milima pia ilitetemeka na kutikiswa kwa sababu Mungu alikuwa amekasirika.
עלה עשן באפו-- ואש-מפיו תאכל גחלים בערו ממנו 8
Moshi ulifuka kutoka kwenye pua zake, na moto mkali ulitokea mdomoni mwake. Makaa yaliwashwa kwa moto huo.
ויט שמים וירד וערפל תחת רגליו 9
Yeye alizifunua mbingu na alishuka chini, na giza nene lilikuwa chini ya miguu yake.
וירכב על-כרוב ויעף וידא על-כנפי-רוח 10
Alipanda kwenye kerubi na akaruka; alinyiririka kwenye mabawa ya upepo.
ישת חשך סתרו-- סביבותיו סכתו חשכת-מים עבי שחקים 11
Yahwe alilifanya giza kuwa hema likimzunguka yeye, wingu la mvua zito katika mbingu.
מנגה נגדו עביו עברו--ברד וגחלי-אש 12
Mawe ya barafu na makaa ya moto yalianguka kutoka katika mwangaza kabla yake.
וירעם בשמים יהוה--ועליון יתן קלו ברד וגחלי-אש 13
Yahwe aliongea katika mbingu! Sauti ya aliye juu ilisikika.
וישלח חציו ויפיצם וברקים רב ויהמם 14
Yeye aliifyatua mishale yake na kuwatawanya adui zake; na radi nyingi zenye mwanga alizitawanya katika maeneo tofauti tofauti.
ויראו אפיקי מים ויגלו מוסדות תבל מגערתך יהוה-- מנשמת רוח אפך 15
Ndipo mifereji ya maji ilitokea; misingi ya dunia ikadhihirishwa kwa mlio wa pigo lako, Yahwe kwa sauti ya pumzi ya pua zako.
ישלח ממרום יקחני ימשני ממים רבים 16
Yeye alishuka chini kutokea juu; akanishikilia mimi! Akanivuta nje ya maji yafurikayo.
יצילני מאיבי עז ומשנאי כי-אמצו ממני 17
Aliniokoa kutoka kwa maadui zangu wenye nguvu, kutoka kwa wale ambao walinichukia mimi, kwa kuwa walikuwa na nguvu sana kuliko mimi.
יקדמוני ביום-אידי ויהי-יהוה למשען לי 18
Wao walikuja kinyume na mimi katika siku ile ya dhiki yangu lakini Mungu alikuwa msaada wangu!
ויוציאני למרחב יחלצני כי חפץ בי 19
Yeye aliniweka huru katika eneo pana la wazi; yeye aliniokoa kwa sababu alipenezwa nami.
יגמלני יהוה כצדקי כבר ידי ישיב לי 20
Yahwe amenitunuku mimi kwa sababu ya haki yangu; yeye amenirejesha mimi kwa sababu mikono yangu ilikuwa misafi.
כי-שמרתי דרכי יהוה ולא-רשעתי מאלהי 21
Kwa kuwa nimezitunza njia za Yahwe na sijafanya uovu wa kumgeuka Mungu wangu.
כי כל-משפטיו לנגדי וחקתיו לא-אסיר מני 22
Kwa kuwa amri zake zote za haki zimekuwa mbele yangu; kama asemavyo, sijaenda kinyume nazo.
ואהי תמים עמו ואשתמר מעוני 23
Pia nimekuwa sina hatia mbele zake, na nimejiweka mwenyewe mbali na dhambi.
וישב-יהוה לי כצדקי כבר ידי לנגד עיניו 24
Hivyo Yahwe amenirejesha kwa sababu ya haki yangu, na kwa sababu mikono yangu ilikuwa safi mbele ya macho yake.
עם-חסיד תתחסד עם-גבר תמים תתמם 25
Kwa yeyote aliye mwaminifu, jionyeshe wenyewe kuwa mwaminifu; kwa mtu asiye na lawama, jionyeshe mwenyewe kuwa usiye na lawama.
עם-נבר תתברר ועם-עקש תתפתל 26
Kwa yeyote aliye msafi, jionyeshe mwenyewe safi; bali ni mjanja kwa yeyote aliye geuzwa.
כי-אתה עם-עני תושיע ועינים רמות תשפיל 27
Kwa kuwa wewe huwaokoa watu walio taabishwa, lakini wewe huwashusha chini wale wenye majivuno, yaani macho yaliyo jinua!
כי-אתה תאיר נרי יהוה אלהי יגיה חשכי 28
Kwa kuwa wewe huipa mwanga taa yangu; Yahwe Mungu wangu hutia mwanga giza langu.
כי-בך ארץ גדוד ובאלהי אדלג-שור 29
Kwa kuwa kwa kupitia wewe ninaweza kuruka juu ya kiwazo kilichowekwa; kupitia Mungu ninaweza kuruka juu ya ukuta.
האל תמים דרכו אמרת-יהוה צרופה מגן הוא לכל החסים בו 30
Kama kwa Mungu: njia yake ni kamilifu. Neno la Yahwe ni safi! Yeye ni ngao kwa yeyote anaye kimbilia katika yeye.
כי מי אלוה מבלעדי יהוה ומי צור זולתי אלהינו 31
Kwa kuwa nani ni Mungu ispokuwa Yahwe? Nani ndiye mwamba ispokuwa Mungu wetu?
האל המאזרני חיל ויתן תמים דרכי 32
Ni Mungu anitiaye nguvu ndani yangu kama vile mkanda, ambaye humweka mtu mwenye lawama katika njia yake.
משוה רגלי כאילות ועל במתי יעמידני 33
Yeye hunifanya miguu yangu kuwa myepesi kama mbawala na kuniweka mahali pa juu!
מלמד ידי למלחמה ונחתה קשת-נחושה זרועתי 34
Yeye hufunza viganja vyangu kwa ajili ya vita na mikono yangu kupiga upinde wa shaba.
ותתן-לי מגן ישעך וימינך תסעדני וענותך תרבני 35
Wewe umenipa mimi ngao ya wokovu. Mkono wako wa kuume umenisaidia, na neema yako imenifanya kuwa mkubwa.
תרחיב צעדי תחתי ולא מעדו קרסלי 36
Wewe umetengeneza nafasi pana kwa ajili ya miguu yangu ili miguu yangu isiteleze.
ארדוף אויבי ואשיגם ולא-אשוב עד-כלותם 37
Ninawashawishi adui zangu na kuwakamata; nami sikurudi nyuma mpaka walipo haribiwa.
אמחצם ולא-יכלו קום יפלו תחת רגלי 38
Niliwashambulia hata hawakuweza kuamka; nao wameangukia chini ya miguu yangu.
ותאזרני חיל למלחמה תכריע קמי תחתי 39
Kwa kuwa unanitia nguvu kama mshipi kwa ajili ya vita; wewe unawaweka chini yangu wale ambao wanainuka kinyume na mimi.
ואיבי נתתה לי ערף ומשנאי אצמיתם 40
Wewe ulinipa visogo vya maadui zangu; niliwaagamiza wale walio nichukia.
ישועו ואין-מושיע על-יהוה ולא ענם 41
Wao waliita msaada lakini hakuna aliye wasaidia; walimuita Yahwe, lakini hakuwaitikia.
ואשחקם כעפר על-פני-רוח כטיט חוצות אריקם 42
Niliwapiga wao katika vipande vidogo vidogo kama vile vumbi mbele ya upepo; niliwatupa nje kama udongo mtaani.
תפלטני מריבי-עם תשימני לראש גוים עם לא-ידעתי יעבדוני 43
Wewe uliniokoa mimi kutoka katika migogoro ya watu. wewe umenifanya kichwa juu ya mataifa. Watu ambao sikuwahi kuwafahamu huntumikia.
לשמע אזן ישמעו לי בני-נכר יכחשו-לי 44
Pindi tu waliposikia kuhusu mimi, wao walinitii; wageni walilazimishwa kunisujudu.
בני-נכר יבלו ויחרגו ממסגרותיהם 45
Wageni walitoka kwenye ngome yao wakitetemeka.
חי-יהוה וברוך צורי וירום אלוהי ישעי 46
Yahwe anaishi; mwamba wangu usifiwe. Ainuliwe Mungu wa wokovu wangu.
האל--הנותן נקמות לי וידבר עמים תחתי 47
Yeye ni Mungu ambaye hutelekeza visasi kwa ajili yangu, ambaye huwatiisha mataifa chini yangu.
מפלטי מאיבי אף מן-קמי תרוממני מאיש חמס תצילני 48
Nimewekwa huru kutoka kwa adui zangu! wewe uliniinua juu ya wale walioinuka kunyume na mimi! Wewe uliniokoa kutoka kwa watu wenye vurugu.
על-כן אודך בגוים יהוה ולשמך אזמרה 49
Kwa hiyo nitakushukuru wewe, Yahwe, kati ya mataifa; Nitaliimbia sifa jina lako!
מגדל ישועות מלכו ועשה חסד למשיחו--לדוד ולזרעו עד-עולם 50
Mungu hutoa ushindi mkuu kwa mfalme wake, na yeye huonyesha uaminifu wa agano lake kwa mpakwa mafuta wake, kwa Daudi na ukoo wake milele.

< תהילים 18 >