< Psalm 73 >

1 Ein Lied, von Asaph. - Gewiß! Das höchste Gut für Israel ist Gott, für die, die reinen Herzens sind.
Hakika Mungu ni mwema kwa Israeli, kwa wale walio na moyo safi.
2 Ich wäre fast mit meinem Fuß gestrauchelt; fast hätte einen Fehltritt ich getan.
Lakini kwangu mimi, kidogo tu miguu yangu iteleze; miguu yangu karibu iteleze kutoka kwangu
3 Denn ich beneidete die Übermütigen und gaffte bei der Frevler Wohlergehen.
kwa sababu niliwaonea wivu wenye kiburi nilipoona mafanikio ya waovu.
4 Denn ihre Sklaven brauchen keine Fesseln, und kerngesund ist ihr Gesinde.
Kwa maana hawana maumivu hadi kufa kwao, lakini wana nguvu na wameshiba.
5 Sie teilen nicht der Menschen Leid und werden nicht wie andere geplagt.
Wako huru dhidi ya mizigo ya watu wengine; nao hawateswi kama watu wengine.
6 Drum ist ihr Halsgeschmeide Übermut; Gewalttat heißt das Kleid, das sie umhüllt.
Kiburi kinawapamba kama mkufu kwenye shingo zao; jeuri huwavika kama vazi.
7 Ihr Auge quillt aus Fett hervor; ausschweifend sind des Herzens Süchte.
Katika upofu wa jinsi hii dhambi huja; mawazo maovu hupita mioyoni mwao.
8 Sie reden boshaft, voller Hohn, und drohen mit Gewalt von oben her.
Wao hudhihaki na kuongea kwa namna ya uovu; kwa kiburi chao hutishia mateso.
9 Mit ihrem Munde tasten sie den Himmel an, und ihre Zunge herrscht durchs ganze Land-
Wameweka vinywa vyao dhidi ya mbingu, na ndimi zao hutanga tanga duniani.
10 "Fürwahr! Dahin hat er sein Volk gebracht, daß sie nicht Wasser zur Genüge fanden."
Kwa hiyo watu wake huwageukia na maji yaliyojaa hukaushwa.
11 Sie sprechen: "Ach, wie weiß denn Gott? Gibt's denn ein Wissen bei dem Höchsten?"
Nao husema, “Mungu anajuaje? Yako maarifa kwake yeye aliye juu?”
12 Ja, diese sind so frevelhaft und glücklich in der Welt, vermehren sie ihr Hab und Gut.
Fahamu: watu hawa ni waovu; mara zote hawajali, wakifanyika matajiri na matajiri.
13 So hielt ich denn vergeblich rein mein Herz und wusch in Unschuld meine Hände?
Hakika nimeutunza moyo wangu bure na nimenawa mikono yangu pasipo kukosa.
14 Den ganzen Tag bin ich geplagt, und meine Züchtigung ist jeden Morgen da.
Maana mchana kutwa nimeteswa na kuadhibiwa kila asubuhi.
15 Nähm ich mir aber vor, also zu sprechen: "So geht es dem Geschlechte Deiner Kinder", so wär's von mir vermessen.
Kama ningesema, “Ningesema mambo haya,” kumbe nigewasaliti kizazi hiki cha watoto wenu.
16 Wenn ich's nachsinnend will verstehen, da wird's in meinen Augen erst ein Jammer,
Ingawa nilijaribu kuyaelewa mambo haya, yalikuwa ni magumu sana kwangu.
17 bis ich in Gottes heilige Pläne dringe. Da erst begreife ich ihr Ziel:
Ndipo nilipoingia patakatifu pa Mungu na kuelewa hatma yao.
18 Du stellst sie auf gar schlüpferigen Boden, daß Du sie ins Verderben stürzest.
Hakika wewe huwaweka penye utelezi; huwaangusha mpaka palipoharibika.
19 Wie plötzlich gehen sie zugrunde! Wie schrecklich werden sie dahingerafft, vertilgt!
Jinsi gani wamekuwa ukiwa kwa muda mfupi! Wamefika mwisho nao wamemaliza kwa utisho.
20 Wie beim Erwachen einen Traum der Wachende verachtet, so tust Du's, Herr, mit ihrem Schatten.
Wao ni kama ndoto wakati wa mtu kuamka; Bwana, utakapo inuka, utazidharau ndoto zao.
21 Wenn voll von Bitternis das Herz mir wäre, und schnitte durch die Nieren mir der Schmerz,
Maana moyo wangu ulipata uchungu, nami nilijeruhiwa sana.
22 dann wäre ich ein Tier, ganz unverständig, ein unvernünftig Tier vor Dir.
Nilikuwa mjinga na sijui neno; nilikuwa kama mnyama tu mbele yako.
23 Doch immer bleibe ich Dir treu, wenn Du mich bei der Rechten fassest
Lakini mimi nipo pamoja nawe daima; umenishika mkono wa kuume.
24 und leitest mich nach Deinem Rat und nimmst zuletzt mich noch zu Besserm mit.
Utaniongoza kwa shauri lako na baadaye utanipokea katika utukufu.
25 Wen habe ich im Himmel? Und wenn ich Dich besitze, brauche ich auf dieser Welt nichts mehr.
Ni nani niliye naye mbinguni isipokuwa wewe? Hakuna nimtamaniye duniani isipokuwa wewe.
26 Vergeht mein Fleisch, mein Herz, so bleibt doch meines Herzens Hort, mein Anteil Gott in Ewigkeit.
Mwili wangu na moyo wangu huwa dhaifu, bali Mungu ndiye nguvu ya moyo wangu daima.
27 Wer sich von Dir entfernt, kommt um. Jedweden tilgst Du, der Dir Treue kündigt.
Wale walio mbali nawe wataangamia; utawaangamiza wote wasio waaminifu kwako.
28 Für mich ist's Seligkeit, mich Gott zu nahen. Ich setze meine Hoffnung auf den Herrn, den Herrn, daß ich verkünden kann, was immer Du verheißen hast.
Lakini mimi, linipasalo kufanya ni kumkaribia Mungu. Nimemfanya Bwana Yahwe kimbilio langu. Nami nitayatangaza matendo yako yote.

< Psalm 73 >