< Psalm 63 >

1 Ein Lied, von David, als er in der Wüste Juda war. Dich such ich, Gott, mein Gott; nach Dir lechzt meine Seele; nach Dir sehnt sich mein Fleisch. Wie in dem dürren, trocknen, wasserlosen Lande,
Mungu, wewe ni Mungu wangu! Ninakutafuta wewe kwa bidii, moyo wangu unakiu yako, mwili wangu unakutamani sana wewe, katika ukame na nchi iliyochoka mahali ambapo hakuna maji.
2 so schau ich aus nach Dir, um Deine Pracht zu sehen und Deine Majestät im Heiligtum.
Hivyo nimekutafuta wewe katika watu watakatifu kuona nguvu zako na utukufu wako.
3 Denn köstlicher ist Deine Huld als Leben. Dich preisen meine Lippen.
Kwa sababu uaminifu wa agano lako ni bora kuliko uhai, midomo yangu itakusifu wewe.
4 So preise ich Dich lebenslang; in Deinem Namen will ich regen meine Hände.
Hivyo nitakutukuza wewe niwapo hai; kwa jina lako nitainua mikono yangu juu.
5 Gleichwie von Fett und Öl wird meine Seele satt; mit Jubellippen singt mein Mund,
Itakuwa kana kwamba nilikula mlo wa mafuta na wenye kunona, kwa midomo ya furaha kinywa changu kitakusifu wewe,
6 wenn ich auf meinem Lager Dein gedenke, in mitternächtiger Stunde sinne über Dich,
nikufikiripo kitandani mwangu na kukutafakari wewe wakati wa saa za usiku.
7 Du möchtest Schutz mir sein, daß ich im Schatten Deiner Flügel jauchze.
Kwa maana umekuwa msaada wangu, na katika uvuli wa mbawa zako ninafurahia.
8 An Dir hängt meine Seele; ich klammere mich an Deine Rechte.
Ninashikamana nawe; mkono wako wa kuume unanisaidia.
9 Die meine Seele gerne in der Wüste wüßten, sie mögen in der Erde Tiefe fahren!
Lakini wale watafutao kuuharibu uhai wangu wataenda chini kwenye sehemu ya chini kabisa ya nchi;
10 Die sie dem Untergange überliefern wollen, die mögen der Schakale Beute werden!
watakabidhiwa kwa wale ambao mikono yao hutumia upanga, nao watakuwa chakula cha mbweha.
11 Der König aber freue sich in Gott, und wer ihm Treue schwört, der jauchze! Der Lügner Mund wird zugestopft.
Bali mfalme atashangilia katika Mungu; yeyote anaye apa kupitia yeye atajivunia yeye, lakini vinywa ya wale wasemao uongo watanyamazishwa.

< Psalm 63 >