< Psalm 120 >

1 Ein Stufenlied. - In meiner Drangsal rufe ich zum Herrn. Er hört auf mich.
Wimbo wa kwenda juu. Katika dhiki yangu namwita Bwana, naye hunijibu.
2 Herr! Rette mich von Lügenlippen, von trügerischer Zunge!
Ee Bwana, uniokoe kutoka midomo ya uongo na ndimi za udanganyifu.
3 Wie liefert Dir die trügerische Zunge fort und fort
Atakufanyia nini, au akufanyie nini zaidi, ewe ulimi mdanganyifu?
4 geschärfte Pfeile eines Helden samt Ginsterkohlen!
Atakuadhibu kwa mishale mikali ya shujaa, kwa makaa yanayowaka ya mti wa mretemu.
5 Weh mir, daß ich bei Mesech gaste, bei Kedars Zelten weile!
Ole wangu kwa kuwa naishi Mesheki, kwamba naishi katikati ya hema za Kedari!
6 Zu lange schon weilt meine Seele bei Friedensfeinden.
Nimeishi muda mrefu mno miongoni mwa wale wanaochukia amani.
7 Ich bin so friedsam. Doch, wenn ich's auch noch so sehr beteure, sie wollen Kampf.
Mimi ni mtu wa amani; lakini ninaposema, wao wanataka vita.

< Psalm 120 >