< Sprueche 9 >

1 Die Weisheit hatte sich ein Haus gebaut und sieben Säulensitze machen lassen.
Hekima amejenga nyumba yake; amechonga nguzo zake saba.
2 Sie schlachtete ihr Vieh und mischte ihren Wein und deckte ihre Tische.
Ameandaa nyama na kuchanganya divai yake; pia ameandaa meza yake.
3 Sie sandte ihre Mägde aus, um auf erhöhten Plätzen in der Stadt zu rufen:
Amewatuma watumishi wake wa kike, naye huita kutoka mahali pa juu sana pa mji.
4 "Wer immer töricht ist, der pflege hier der Einkehr!" Wem's an Verstand gebricht, zu dem sag ich:
Anawaambia wale wasio na akili, “Wote ambao ni wajinga na waje hapa!
5 "Kommt her, genießt von meiner Speise und trinkt den Wein, den ich gemischt!
Njooni, mle chakula changu na mnywe divai niliyoichanganya.
6 Laßt von der Torheit, daß ihr lebet, und schlagt den Weg der Einsicht ein!"
Acheni njia zenu za ujinga nanyi mtaishi; tembeeni katika njia ya ufahamu.
7 Wer einen Spötter schilt, der holt sich selber Schande, wer einen Frevler tadelt, eigene Schmach.
“Yeyote anayemkosoa mwenye mzaha hukaribisha matukano; yeyote anayekemea mtu mwovu hupatwa na matusi.
8 So tadle nicht den Spötter, daß er dich nicht hasse! Doch tadle einen Weisen, dieser wird dich lieben!
Usimkemee mwenye mzaha la sivyo atakuchukia; mkemee mwenye hekima naye atakupenda.
9 Belehre einen Weisen! Und er wird noch weiser. Den Frommen lehr! Er mehrt sein Wissen.
Mfundishe mtu mwenye hekima naye atakuwa na hekima zaidi; mfundishe mtu mwadilifu naye atazidi kufundishika.
10 Der Weisheit Anfang ist die Furcht des Herrn; den Heiligen erkennen, das heißt Einsicht.
“Kumcha Bwana ndicho chanzo cha hekima, na kumjua Aliye Mtakatifu ni ufahamu.
11 "Durch mich ja werden deiner Tage viele; die Lebensjahre werden dir sich mehren.
Kwa maana kwa msaada wangu siku zako zitakuwa nyingi, na miaka itaongezwa katika maisha yako.
12 Bist du jetzt weise, bist du weise dir zum Besten; bist du ein Spötter, hast du es allein zu tragen."
Kama wewe una hekima, hekima yako itakupa tuzo; kama wewe ni mtu wa mzaha, wewe mwenyewe ndiwe utateseka.”
13 Das Weib der Torheit schwatzt nur dummes Zeug; unwissend ist es.
Mwanamke aitwaye Mpumbavu ana kelele; hana adabu na hana maarifa.
14 Sie sitzt an ihres Hauses Pforte, auf einem Sessel, fern dem Herzen ihrer Stadt,
Huketi kwenye mlango wa nyumba yake, juu ya kiti katika mahali pa juu sana pa mji,
15 um denen zuzurufen, die des Weges ziehen und auf den Pfaden fürbaß schreiten:
akiita wale wapitao karibu, waendao moja kwa moja kwenye njia yao.
16 "Wer immer töricht ist, der pflege hier der Einkehr!" Wem's an Verstand gebricht, zu dem möcht ich jetzt sagen:
Anawaambia wale wasio na akili, “Wote ambao ni wajinga na waje hapa ndani!”
17 "Gestohlen Wasser, das ist fein; verboten Brot - ein süßes Brot!"
“Maji yaliyoibiwa ni matamu; chakula kinacholiwa sirini ni kitamu!”
18 Und er weiß nicht, daß dort die Schatten hausen, daß ihre Gäste in der Hölle Abgrund kommen. (Sheol h7585)
Lakini hawajui hata kidogo kuwa wafu wako humo, kwamba wageni wake huyo mwanamke wako katika vilindi vya kuzimu. (Sheol h7585)

< Sprueche 9 >