< 2 Samuel 22 >

1 Und David redete zu Jehova die Worte dieses Liedes an dem Tage, da Jehova ihn aus der Hand aller seiner Feinde und aus der Hand Sauls errettet hatte; und er sprach:
Daudi alimwimbia Bwana maneno ya wimbo huu wakati Bwana alipomwokoa mikononi mwa adui zake wote, na pia mkononi mwa Sauli.
2 Jehova ist mein Fels und meine Burg und mein Erretter.
Akasema: “Bwana ni mwamba wangu, ngome yangu na mwokozi wangu,
3 Gott ist mein Fels, auf ihn werde ich trauen, mein Schild und das Horn meines Heils, meine hohe Feste und meine Zuflucht. Mein Retter, von Gewalttat wirst du mich retten!
Mungu wangu ni mwamba wangu, ambaye kwake ninakimbilia, ngao yangu na pembe ya wokovu wangu. Yeye ni ngome yangu, kimbilio langu na mwokozi wangu, huniokoa kutoka kwa watu wenye jeuri.
4 Ich werde Jehova anrufen, der zu loben ist, und ich werde gerettet werden von meinen Feinden.
Ninamwita Bwana, anayestahili kusifiwa, nami ninaokolewa kutoka kwa adui zangu.
5 Denn mich umfingen die Wogen des Todes, die Ströme Belials erschreckten mich;
“Mawimbi ya mauti yalinizunguka, mafuriko ya maangamizi yalinilemea.
6 die Bande des Scheols umringten mich, es ereilten mich die Fallstricke des Todes. (Sheol h7585)
Kamba za kuzimu zilinizunguka, mitego ya mauti ilinikabili. (Sheol h7585)
7 In meiner Bedrängnis rief ich zu Jehova, und ich rief zu meinem Gott; und er hörte aus seinem Tempel meine Stimme, und mein Schrei kam in seine Ohren.
Katika shida yangu nalimwita Bwana, nilimlilia Mungu wangu. Kutoka Hekaluni mwake alisikia sauti yangu, kilio changu kikafika masikioni mwake.
8 Da wankte und bebte die Erde; die Grundfesten des Himmels zitterten und wankten, weil er entbrannt war.
“Dunia ilitetemeka na kutikisika, misingi ya mbingu ikatikisika, vilitetemeka kwa sababu alikuwa amekasirika.
9 Rauch stieg auf von seiner Nase, und Feuer fraß aus seinem Munde; glühende Kohlen brannten aus ihm.
Moshi ukapanda kutoka puani mwake, moto uteketezao ukatoka kinywani mwake, makaa ya moto yawakayo yakatoka ndani mwake.
10 Und er neigte die Himmel und fuhr hernieder, und Dunkel war unter seinen Füßen.
Akazipasua mbingu akashuka chini, mawingu meusi yalikuwa chini ya miguu yake.
11 Und er fuhr auf einem Cherub und flog daher, und er erschien auf den Fittichen des Windes.
Alipanda juu ya kerubi akaruka, akapaa juu kwa mbawa za upepo.
12 Und Finsternis machte er rings um sich her zum Gezelt, Sammlung der Wasser, dichtes Himmelsgewölk.
Alifanya giza hema lake la kujifunika: mawingu meusi ya mvua ya angani.
13 Aus dem Glanze vor ihm brannten feurige Kohlen.
Kutokana na mwanga wa uwepo wake mawingu yalisogea, ikanyesha mvua ya mawe na umeme wa radi.
14 Es donnerte Jehova vom Himmel her, und der Höchste ließ seine Stimme erschallen.
Bwana alinguruma kutoka mbinguni, sauti ya Aliye Juu Sana ilisikika.
15 Und er schoß Pfeile und zerstreute sie, seinen Blitz, und verwirrte sie.
Aliipiga mishale na kutawanya adui, umeme wa radi na kuwafukuza.
16 Da wurden gesehen die Betten des Meeres, aufgedeckt die Grundfesten des Erdkreises durch das Schelten Jehovas, vor dem Schnauben des Hauches seiner Nase.
Mabonde ya bahari yalifunuliwa, na misingi ya dunia ikawa wazi kwa kukaripia kwake Bwana, kwa uvumi wa pumzi kutoka puani mwake.
17 Er streckte seine Hand aus von der Höhe, er nahm mich, er zog mich aus großen Wassern;
“Alinyoosha mkono kutoka juu na kunishika; alinitoa kutoka kilindi cha maji makuu.
18 Er errettete mich von meinem starken Feinde, von meinen Hassern; denn sie waren mächtiger als ich.
Aliniokoa kutoka adui wangu mwenye nguvu nyingi, kutoka adui zangu waliokuwa na nguvu nyingi kuliko mimi.
19 Sie ereilten mich am Tage meines Unglücks, aber Jehova ward mir zur Stütze.
Walinikabili siku ya msiba wangu, lakini Bwana alikuwa msaada wangu.
20 Und er führte mich heraus ins Weite, er befreite mich, weil er Lust an mir hatte.
Alinileta nje mahali penye nafasi tele, akaniokoa kwa kuwa alipendezwa nami.
21 Jehova vergalt mir nach meiner Gerechtigkeit, nach der Reinheit meiner Hände erstattete er mir.
“Bwana alinitendea sawasawa na uadilifu wangu; sawasawa na usafi wa mikono yangu amenilipa.
22 Denn ich habe bewahrt die Wege Jehovas, und bin von meinem Gott nicht frevelhaft abgewichen.
Kwa maana nimezishika njia za Bwana; sijatenda ubaya nikamwacha Mungu wangu.
23 Denn alle seine Rechte waren vor mir, und seine Satzungen, ich bin nicht davon gewichen;
Sheria zake zote zi mbele yangu, wala sijayaacha maagizo yake.
24 Und ich war vollkommen gegen ihn und hütete mich vor meiner Ungerechtigkeit.
Nimekuwa sina hatia mbele zake, nami nimejilinda nisitende dhambi.
25 Und Jehova erstattete mir nach meiner Gerechtigkeit, nach meiner Reinheit vor seinen Augen.
Bwana amenilipa sawasawa na uadilifu wangu, sawasawa na usafi wangu machoni pake.
26 Gegen den Gütigen erzeigst du dich gütig, gegen den vollkommenen Mann erzeigst du dich vollkommen;
“Kwa yeye aliye mwaminifu unajionyesha kuwa mwaminifu, kwa asiye na hatia unajionyesha kutokuwa na hatia,
27 gegen den Reinen erzeigst du dich rein, und gegen den Verkehrten erzeigst du dich entgegenstreitend.
kwa aliye mtakatifu unajionyesha kuwa mtakatifu, lakini kwa aliyepotoka unajionyesha kuwa mkaidi.
28 Und du wirst retten das elende Volk; aber deine Augen sind wider die Hoffärtigen, die du erniedrigen wirst.
Wewe huwaokoa wanyenyekevu, lakini macho yako ni juu ya wenye kiburi ili uwashushe.
29 Denn du bist meine Leuchte, Jehova; und Jehova erhellt meine Finsternis.
Wewe ni taa yangu, Ee Bwana. Bwana hulifanya giza langu kuwa mwanga.
30 Denn mit dir werde ich gegen eine Schar anrennen, mit meinem Gott werde ich eine Mauer überspringen.
Kwa msaada wako naweza kushinda jeshi, nikiwa pamoja na Mungu wangu nitaweza kuruka ukuta.
31 Gott, sein Weg ist vollkommen; Jehovas Wort ist geläutert; ein Schild ist er allen, die auf ihn trauen.
“Kuhusu Mungu, njia yake ni kamilifu; neno la Bwana halina dosari. Yeye ni ngao kwa wote wanaokimbilia kwake.
32 Denn wer ist Gott, außer Jehova, und wer ein Fels, außer unserem Gott?
Kwa maana ni nani aliye Mungu zaidi ya Bwana? Ni nani aliye Mwamba isipokuwa Mungu wetu?
33 Gott ist meine starke Feste, und er lenkt vollkommen meinen Weg.
Mungu ndiye anivikaye nguvu na kufanya njia yangu kuwa kamilifu.
34 Er macht meine Füße denen der Hindinnen gleich, und stellt mich hin auf meine Höhen.
Huifanya miguu yangu kama miguu ya kulungu, huniwezesha kusimama mahali palipo juu.
35 Er lehrt meine Hände den Streit, und meine Arme spannen den ehernen Bogen.
Huifundisha mikono yangu kupigana vita; mikono yangu inaweza kupinda upinde wa shaba.
36 Und du gabst mir den Schild deines Heils, und deine Herablassung machte mich groß.
Hunipa ngao yako ya ushindi, unajishusha chini ili kuniinua.
37 Du machtest Raum meinen Schritten unter mir, und meine Knöchel haben nicht gewankt.
Huyapanua mapito yangu, ili miguu yangu isiteleze.
38 Meinen Feinden jagte ich nach und vertilgte sie; und ich kehrte nicht um, bis sie aufgerieben waren.
“Niliwafuatia adui zangu na nikawaseta, sikurudi nyuma mpaka walipoangamizwa.
39 Und ich rieb sie auf und zerschmetterte sie; und sie standen nicht wieder auf, und sie fielen unter meine Füße.
Niliwaseta kabisa, nao hawakuweza kuinuka tena; walianguka chini ya miguu yangu.
40 Und du umgürtetest mich mit Kraft zum Streit, beugtest unter mich, die wider mich aufstanden.
Ulinivika nguvu kwa ajili ya kupigana vita; uliwafanya adui zangu wasujudu miguuni pangu.
41 Und du gabst mir den Rücken meiner Feinde; meine Hasser, ich vernichtete sie.
Uliwafanya adui zangu wageuke na kukimbia, nami nikawaangamiza adui zangu.
42 Sie blickten umher, und kein Retter war da zu Jehova, und er antwortete ihnen nicht.
Walipiga yowe, lakini hapakuwepo na yeyote wa kuwaokoa; walimlilia Bwana, lakini hakuwajibu.
43 Und ich zermalmte sie wie Staub der Erde; wie Straßenkot zertrat, zerstampfte ich sie.
Niliwaponda kama mavumbi ya nchi; niliwaponda na kuwakanyaga kama tope barabarani.
44 Und du errettetest mich aus den Streitigkeiten meines Volkes; du bewahrtest mich auf zum Haupte der Nationen; ein Volk, das ich nicht kannte, dient mir.
“Umeniokoa kutokana na mashambulizi ya watu wangu; umenihifadhi mimi kama kiongozi wa mataifa. Watu ambao sikuwajua wananitumikia,
45 Die Söhne der Fremde unterwarfen sich mir mit Schmeichelei; beim Hören des Ohres gehorchten sie mir.
nao wageni huja wakininyenyekea, mara wanisikiapo, hunitii.
46 Die Söhne der Fremde sanken hin und zitterten hervor aus ihren Schlössern.
Wote wanalegea, wanatoka katika ngome zao wakitetemeka.
47 Jehova lebt, und gepriesen sei mein Fels! Und erhoben werde der Gott, der Fels meines Heils!
“Bwana yu hai! Sifa ni kwa Mwamba wangu! Atukuzwe Mungu, Mwamba, Mwokozi wangu!
48 Der Gott, der mir Rache gab und die Völker unter mich niederwarf;
Yeye ndiye Mungu anilipiziaye kisasi, ayawekaye mataifa chini yangu,
49 und der mich herausführte aus der Mitte meiner Feinde. Ja, du erhöhtest mich über die, welche wider mich aufstanden, von dem Manne der Gewalttat befreitest du mich.
aniwekaye huru toka kwa adui zangu. Uliniinua juu ya adui zangu; uliniokoa toka kwa watu wajeuri.
50 Darum, Jehova, will ich dich preisen unter den Nationen und Psalmen singen deinem Namen,
Kwa hiyo nitakusifu, Ee Bwana, katikati ya mataifa; nitaliimbia sifa jina lako.
51 Dich, der groß macht die Rettungen seines Königs, und Güte erweist seinem Gesalbten, David und seinem Samen ewiglich.
Humpa mfalme wake ushindi mkuu; huonyesha fadhili zake kwa mpakwa mafuta wake, kwa Daudi na wazao wake milele.”

< 2 Samuel 22 >