< Éphésiens 3 >

1 C'est à cause de cela que moi, Paul, je suis le prisonnier de Jésus-Christ pour vous, les Païens.
Kutokana na hayo, mimi Paulo, mfungwa wa Kristo Yesu kwa ajili yenu, namwomba Mungu.
2 — En effet, vous avez dû apprendre la dispensation de Dieu à mon égard et la grâce qu'il m'a confiée en votre faveur;
Bila shaka mmekwisha sikia kwamba Mungu, kwa neema yake, alinikabidhi kazi hii niifanye kwa faida yenu.
3 comment, par révélation, j'ai eu connaissance du mystère que je viens de vous exposer en quelques mots.
Mimi nilijulishwa kwa njia ya ufunuo mpango wake uliofichika. (Nimeandika kwa ufupi juu ya jambo hili,
4 Vous pouvez comprendre, en les lisant, l'intelligence que j'ai du mystère de Christ,
nanyi mkiyasoma maneno yangu mtaweza kujua jinsi ninavyoielewa siri hiyo ya Kristo.)
5 mystère qui n'a pas été manifesté en d'autres âges aux enfants des hommes, comme il a été révélé maintenant, par l'Esprit, à ses saints apôtres et prophètes.
Zamani watu hawakujulishwa siri hiyo; lakini sasa Mungu amewajulisha mitume na manabii wake watakatifu kwa njia ya Roho.
6 Ce mystère, c'est que les Païens sont cohéritiers, membres du même corps, participant avec nous à la promesse qui a été faite en Jésus-Christ par l'Évangile;
Siri yenyewe ni hii: kwa njia ya Habari Njema watu wa mataifa mengine wanapata sehemu yao pamoja na Wayahudi katika zile baraka za Mungu; wao ni viungo vya mwili uleule, na wanashiriki ahadi ileile aliyofanya Mungu kwa njia ya Kristo Yesu.
7 et je suis devenu ministre de cet Evangile en vertu du don de la grâce de Dieu, qui m'a été accordée par l'efficacité de sa puissance.
Mimi nimefanywa kuwa mtumishi wa Habari Njema kwa neema ya pekee aliyonijalia Mungu kwa uwezo wake mkuu.
8 Oui, à moi, le moindre de tous les saints, cette grâce a été donnée, d'annoncer aux Païens les richesses insondables du Christ,
Mimi ni mdogo kuliko watu wote wa Mungu; lakini amenijalia neema yake, ili niwahubirie watu wa mataifa utajiri wake Kristo usiopimika,
9 et de les éclairer sur cette dispensation du mystère caché de toute éternité en Dieu, le créateur de toutes choses. (aiōn g165)
tena niwaangazie watu wote waone jinsi mpango wa Mungu uliofichika unavyotekelezwa. Mungu aliye Muumba wa vitu vyote alificha siri hiyo yake tangu milele, (aiōn g165)
10 C'est ainsi que, maintenant, la sagesse de Dieu, infiniment diverse, est manifestée par l'Eglise aux dominations et aux puissances dans les lieux célestes,
kusudi, sasa kwa njia ya kanisa, wakuu na wenye enzi wa mbinguni wapate kuitambua hekima ya Mungu iliyo ya namna nyingi.
11 suivant son dessein éternel, qu'il a réalisé en Jésus-Christ, notre Seigneur, (aiōn g165)
Mungu alifanya jambo hilo kufuatana na azimio lake la milele ambalo amelifanya kwa njia ya Kristo Bwana wetu. (aiōn g165)
12 en qui nous avons, par la foi en lui, la liberté de nous approcher de Dieu avec confiance.
Basi, katika kuungana na Kristo, na kwa njia ya imani katika Kristo, sisi tunathubutu kumkaribia Mungu kwa uhodari.
13 Aussi, je vous demande de ne point vous laisser décourager par les afflictions que j'endure pour vous: elles sont votre gloire!
Kwa hiyo, nawaombeni msife moyo kwa sababu ya mateso ninayopata kwa ajili yenu, maana hayo ni kwa ajili ya utukufu wenu.
14 C'est à cause de cela que je fléchis les genoux devant le Père,
Kwa sababu hiyo, nampigia magoti Baba,
15 duquel toute famille, dans les cieux et sur la terre, tire son nom,
aliye asili ya jamaa zote duniani na mbinguni.
16 lui demandant que, selon les richesses de sa gloire, il vous donne d'être puissamment fortifiés par son Esprit dans votre être intérieur;
Namwomba Mungu, kadiri ya utajiri wa utukufu wake, awajalieni kwa uwezo wa Roho wake, nguvu ya kuwa imara ndani yenu,
17 en sorte que le Christ habite dans vos coeurs par la foi, et qu'étant enracinés et fondés dans l'amour,
naye Kristo akae mioyoni mwenu kwa imani. Namwomba mpate kuwa na mzizi na msingi katika mapendo
18 vous puissiez comprendre, avec tous les saints, quelle en est la largeur, la longueur, la profondeur et la hauteur,
kusudi muweze kufahamu pamoja na watu wote wa Mungu jinsi upendo wa Kristo ueneavyo kwa mapana na marefu, kwa kimo na kina.
19 et connaître l'amour du Christ, qui surpasse toute connaissance, afin que vous soyez remplis de toute la plénitude de Dieu.
Naam, mpate kujua upendo wa Kristo upitao elimu yote, mjazwe kabisa utimilifu wote wa Mungu.
20 Or, à Celui qui peut, par la puissance qui opère en nous, faire infiniment au delà de tout ce que nous demandons et pensons,
Kwake yeye ambaye kwa nguvu yake ifanyayo kazi ndani yetu, aweza kufanya mambo makuu zaidi ya yale tuwezayo kuomba au kufikiria;
21 à Lui la gloire dans l'Église et en Jésus-Christ, dans tous les âges, aux siècles des siècles! Amen. (aiōn g165)
kwake Mungu uwe utukufu katika kanisa na katika Kristo Yesu, nyakati zote, milele na milele! Amina. (aiōn g165)

< Éphésiens 3 >